







Ni globu ya kijamii inayojihusisha na mambo yote ya kijamii,natumaini jamii yangu ya kitanzania itafaidika sana pindi ichukuapo fursa ya kuperuzi kwenye globu hii,dhamira yangu ni kufikisha ujumbe pamoja na kuiburudisha jamii yangu na furaha yangu ni kuona natimiza dhamira yangu kwako.natumaini kuwa wewe utaniunga mkono kwa kile ambacho nataka kukifanya kwa ajili ya jamii yangu ya kitanzania.NASHUKURU KWA KUNIELEWA.
Wajumbe
Tom Chilala na wajumbe wengine mkutanoniJuma Pinto na Ibrahim Masudi 'Maestro' kabla ya matokeo kutangazwaMwenyekiti mpya wa TASWA na Kamati yake kuu
Chama cha waandishi wa habari za michezo nchini Tanzania, TASWA, kimefanya uchaguzi wa viongozi wapya baada ya uongozi wa zamani kumaliza muda wake wa miaka mitatu kama katiba inavyoelekeza. Katika uchaguzi huo viongozi wapya waliochaguliwa ni:
MWENYEKITI: JUMA PINTO
MAKAMU MWENYEKITI: MAULID KITENGE
KATIBU MKUU:: AMIR MHANDO
KATIBU MSAIDIZI: GEORGE JOHN
MTUNZA HAZINA: SULTAN SIKIRO
MSAIDIZI: MOHAMED MKANGARAKWA
WAJUMBE: ELIUS KAMBIRI, GRACE HOKA, ZENA CHANDE, ALFRED LUCAS, OSMAN KAPINGA, SALUM JABA
Baada ya jina la Frederick Mwakalebela kuenguliwa katika orodha ya wagombea Ubunge kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi, CCM, baadhi ya watu wamekuwa wakihoji uhalali wa kufanya hivyo il hali wana-CCM wengine wanaogombea viti hivyo katika majimbo mengine nchini wana kesi mahakamani lakini wameruhusiwa kuendelea na kinyang’anyiro hicho. Maswali hayo yaliifikia CCM na hapa ni ufafanuzi wake:
Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Halmashauri Kuu ya CCM (NEC-CCM), Mh. John Chiligati amesema kesi inayomkabili mshindi wa kura za maoni aliyepokwa ‘haki’ ya kuteuliwa kugombea ubunge wa Iringa Mjini kwa tiketi ya chama hicho, Frederick Mwakalebela, haifanani na washindi wengine wa kura za maoni walioteuliwa ambao ni Basil Mramba anayegombea jimbo la Rombo na Andrew Chenge anayegombea jimbo la Bariadi Mashariki licha ya kuwa na kesi mahakamani kama yeye.
Alisema
Mwakalebela ameachwa kwa sababu ya kukosa kwake maadili.
“Suala kwa Mwakalebela ni maadili tu, katika mchakato huu, kakamatwa kwa tuhuma za rushwa na TAKUKURU wamesema wanayo sababu ya kumpeleka mahakamani.” “Lakini alikuwa ndio kwanza kaingia katika mchezo wenyewe na katika mchezo huu huu kabla ya dakika 90, akapigiwa filimbi kuwa amecheza faulo,” alisema Chiligati.
Kuhusu tofauti ya Mramba, Chenge na Mwakalebela Chiligati alisema, “ kisheria wote ni watuhumiwa na hawakutwa na hatia, lakini kimaadili ni tofauti… Mramba anatuhumiwa kutumia vibaya madaraka, tuliita wanasheria wakasema hiyo kesi haimuondolei sifa ya kuwa mgombea.”
Hata hivyo alikiri kuwa Mramba alipitishwa baada ya kufanyika mjadala kati ya wajumbe hao wa NEC.
“Katika Mkoa wa Shinyanga Jimbo la Bariadi Mashariki aliteuliwa Chenge kutetea nafasi yake, anayo kesi ya trafiki, haimkoseshi haki ya kuwa mgombea,” alisema Chiligati.
credit source: http://www.wavuti.com
1.MKOA WA KIGOMA
(i) Mjini: Peter Serukamba,
(ii)Kigoma South: Gulam Hussein Shaaban Kifu,
(iii)Kasulu Urban: Neka Raphael Neka,
(iv)Kasulu Rural: Daniel Nsanzugwanko,
(v)Manyovu: Albert F. Ntabaliba,
(vi)Buyungu: Christopher Chiza,
(vii)Muhambwe: Jamal Abdallah Tamimu,
(viii)Kigoma North: Rabinson, F. Lembo.
2.MKOA WA KILIMANJARO
(I) Moshi Mjini:Justin Salakana,
(ii) Moshi Vijijini: Dk. Cyril Agust Chami,
(iii)Rombo: Basil Pesambili Mramba,
(iv)Same Mashariki): Anne Kilango Malecela,
(v)Same Magharibi: Dk. David Mathayo David,
(vi)Hai: Fuya Godwin Kimbita,
(vii) Vunjo: Chrispin Theobald Meela,
(viii) Mwanga: Profesa Jumanne Maghembe,
(ix)Siha, Aggrey D.J. Mwanri.
3.MKOA WA MANYARA:
(i)Babati mjin:Kisyeri Werema Chambiri,
(ii)Babati Vijini: Jitu Vrajil Soni,
(iii)Hanang: Dk. Mary Michael Nagu,
(iv)Kiteto: Benedict Ole Nangoro
(v) Mbulu:Philip Sang’ake Marmo,
(vi)Simanjiro:Christopher Ole Sendeka.
4.MKOA WA MARA
(i) Musoma mjini: Vedasto Manyinyi,
(ii)Musoma vijijini:Nimrod Elirehema Mkono,
(iii)Mwibara: Alphaxard Kangi Lugola,
(iv)Bunda: Stephen Masatu Wasira,
(v)Rorya: Lameck Okambo Airo,
(vi)Tarime, Nyambari Chacha Nyangwine,
(vii)Serengeti: Dk. Stephene Kebwe Kebwe.
5.MKOA WA MBEYA
(i) Mbeya Mjini: Benson Mwailugula Mpesya,
(ii) Mbeya Vijijini: Luckson Ndage Mwanjala,
(iii) Kyela: Dk Harrison George Mwakyembe,
(iv)Mbarali: Dickson Modestus Kilufi,
(v)Lupa: Victor Kilasile Mwambalaswa,
(vi) Songwe:Philipo Augustino Mulugo,
(vii) Rungwe Mashariki: Profesa Mark James Mwandosya,
(viii) Rungwe Magharibi: Profesa David Homeli Mwakyusa,
(ix) Ileje: Aliko Nikusuma Kibona,
(x)Mbozi Mashariki: Godfrey Weston Zambi,
(xi)Mbozi Magharibi: Dk. Luka Jelasa Siame.
6. MKOA WA MOROGORO
(i)Morogoro Mjini:Aziz Mohamed Abood,
(ii)Morogoro Kaskazini: Dk. Lucy Sawera Nkya,
(iii)Morogoro Kusini: Innocent Kalogeris,
(iv)Mvomero: Amos Gabriel Makala
(v) Ulanga Mashariki: Celina Ompeshi Kombani,
(vi)Ulanga Magharibi: Haji Hussein Mponda,
(vii)Gairo: Ahmed Mubukhut Shabiby
(viii)Kilosa, Mustafa Heidi Mkulo,
(ix)Mikumi: Abdulsalaam Suleiman,
(x)Kilombero: Abdul Rajab Mteketa.
7.MKOA WA TABORA
(i)Urambo Mashariki: Samwel John Sitta
(ii)Urambo Magahribi: Juma Athuman Kapuya,
(iii)Tabora Mjini: Ismail Aden Rage,
(iv)Igunga: Rostam Abdulsasu Aziz,
(v)Sikonge: Said Juma Nkumba
(vi) Igagula: Athuman Rashid Mfutakamba
(vii) Tabora: Sumar Shaffin Mamlo,
(viii)Bukene: Seleman Jumanne Zedi
(ix)Nzega:Dr. Hamisi Andrea Kigwangala
8.MKOA WA TANGA
(i)Tanga mjini: Omari Rashid Nundu
(ii)Kilindi: Beatrice Matumbo Shelukind
(iii)Muheza: Herbert James Mntangi
(iv)Mkinga: Danstan Luka Kitandula
(v)Pangani: Salehe Ahmed Pamba
(vi)Lushoto: Henry Daffa Shekifu
(vii)Bumbuli: January Makamba
(viii)Korogwe Mjini:Yusuph Nasri
(ix)Mlalo:Brig. Gen. Hassan Athuman Ngwilizi
(x)Korogwe Vijijini: Stephen Ngonyani
(xi)Handeni: Dr. Abdalah Omari Kigoda
10.MKOA WA DAR ES SALAAM
(i).Kinondoni: Idd Mohamed AZAN
(ii).Ubungo: Hawa Mgonja NG’UMBI
(iii).Kawe: Angella Charles KIZIGHA
(iv).Ilala: Musa Azan ZUNGU
(v).Ukonga: Eugen Elishirima MWAIPOSA
(vi).Segerea:Dr. Milton Makongoro MAHANGA
(vii).Temeke: Abbas Zuber MTEMVU
(viii).Kigamboni:Dr. Faustine NDUGULILE
11.MKOA WA LINDI
(i)Lindi Mjini:Ndugu Mohamed ABDULAZIZ
(ii)Mtama:Ndugu Bernard Kamillius MEMBE
(iii)Mchinga:Ndugu Said M. MTANDA
(iv)Nachingwea:Ndugu Mathias Meinrad CHIKAWE
(v)Ruangwa:Ndugu Kassim MAJALIWA
(vi)Kilwa kaskazini:Ndugu Murtaza Ali MANGUNGU
(vii)Kilwa Kusini:Ndugu Ramadhan Rashid MADABIDA
(viii)Liwale:Ndugu Faith Mohamed MITAMBO
12.MKOA WA PWANI
(i)Bagamoyo: Dr. Shukuru J. Kawambwa
(ii)Chalinze: Saidi Athuman Bwanamdogo
(iii)Kisarawe: Seleman Saidi Jafo
(iv)Kibiti: Abdul J. Marombwa
(v)Kibaha Vijijini: Mahamud Abuu Jumaa
(vi)Kibaha Mjini: Silvestery F. Koka
(vii)Mkuranga: Adam Kighoma Malima
(viii)Rufiji: Dr. Seif Seleman Rashid
(ix)Mafia: Abdulkarim E. Shaha
13.MKOA WA RUKWA
(i)Kwela: Malocha Aloyce Ignace
(ii)Kalambo: Kandege Sinkamba Josephat
(iii)Nkasi Kaskazini: Ally Mohamed Kessy
(iv)Nkasi Kusini:Deusderius Mipata
(v)Mlele: Mizengo Kayanza Peter Pinda
(vi)Mpanda Kati (mjini): Sebastian Simon Kapufi
(vii)Sumbawanga Mjini: Aeshi Khalfan Hilaly
(viii)Mpanda Vijijini: Moshi S. Kakoso
14.MKOA WA SHINYANGA
(i)Shinyanga Mjini: Steven Julius Masele
(ii)Kishapu: Nchambi Seleman Masoud
(iii)Kahama: James Daud Lembeli
(iv)Msalala: Maige Ezekiel Magolyo
(v)Solwa: AhmeD Ally Salum
(vi)Bukombe: Emanuel Jumanne Luhahula
(vii)Mbogwe: Masele Agustino Manyanda
(viii)Bariadi Mashariki: Makondo Martine Kaunda
(ix)Bariadi Magharibi: Chenge Andrew John
(x)Maswa Mashariki: Bunyongoli Peter Edward
(xi)Maswa Magharibi: Kisena Robert Simon
(xii)Meatu:Salum Khamis Salum
(xiii)Kisesa: Joelson Luhaga Mpina.
15.MKOA WA SINGINDA
(i)Singida Mjini:Mohamed Gulam Dewji
(ii) Manyoni Mashariki:Capt.(mstaafu) John Chiligati
(iii)Manyoni Magharibi: John Paul Lwanji
(v)Iramba Magharibi: Mwigulu Lameck Nchemba Matelu
(vi)Iramba Mashariki:Salome David Mwambu
(vii)Singida Kaskazini:Lazaro Samwel Nyalandu
(viii)Singida Magharibi:Alhaj Mohamed Misanga
(ix)Singida Mashariki:Jonathan Andrew Njau
16.MKOA WA ARUSHA
(i)Arusha:Dr. Batilda BURIANI
(ii)Arumeru Mashariki: Jeremiah Solomon SUMARI
(iii)Arumeru Magharibi: Goodluck Joseph Ole MEDEYE
(iv)Karatu: Dr. Wilbald Slaa LORRI
(v)Longido: Michael Lekule LAIZER
(vi)Monduli: Edward Ngoyai LOWASSA
(vii)Ngorongoro: Saning’o Kaika Ole TELELE
17.MKOA WA IRINGA
(i)Iringa Mjini: Monica Ngenzi MBEGA
(ii)Isimani: William Vangimembe LUKUVI
(iii)Kalenga: William Augustino MGIMWA
(iv)Kilolo:Prof. Peter Mahamudu MSOLLA
(v)Ludewa: Deo Haule FILIKUNJOMBE
(vi)Makete:Dr. Binilith Satano MAHENGE
(vii)Mufindi Kaskazini: Mohamed Hassan MGIMWA
(viii)Mufindi Kusini: Menrad Lutengano KIGOLA
(ix)Njombe Kaskazini:Deo Kasenyenda SANGA (Jah People)
(x)Njombe Kusini: Anne Semamba MAKINDA
(xi)Njombe Magharibi: Gerson Hosea LWENGE
18.MKOA WA KAGERA
(i)Nkenge: Assumpter Nshunju MSHAMA
(ii)Bukoba Mjini: Khamis S. KAGASHEKI
(iii)Bukoba Vijijini:Ndugu Jasson S. RWEIKIZA
(iv)Muleba Kaskazini: Charles J. MWIJAGE
(v)Muleba Kusini: Anna K. TIBAIJUKA
(vi)Chato: John Pombe MAGUFULI
(vii)Kyerwa: Eustace O. KATAGIRA
(viii)Karagwe: Gosbert B. BLANDES
(ix)Biharamulo: Oscar R. MUKASA
(x)Ngara: Deogratias Aloys NTUKAMAZINA
Na Alistide Kwizela.
Hatimaye Shirikisho la Wanamuziki Tanzania leo (Jumatano) limepata viongozi wake wa muda katika uchaguzi uliofanyika kwenye Ukumbi wa BASATA na kusimamiwa na Afisa Mtendaji Mkuu wa COSOTA,Bw.Yunus Mkinga.
Katika uchaguzi huo uliokuwa wa vuta ni kuvuta,Bw.Ibra Washokera aliweza kuibuka kidedea kwenye nafasi ya urais baada ya kupata kura 12 na kumbwaga Mkongwe wa muziki wa dansi,Hamza Kalala ‘Komandoo’ aliyeambulia kura 2 tu.
Kwa upande wa nafasi ya Makamu wa Rais,Mwanamuziki wa muziki wa asili,Che Mundugwao aliibuka kidedea kwa kupata kura 9 na kuwaacha mbali wapinzani wake ambao ni Mkongwe Kassim Mapili na Gwalugano Ayoub walioambulia kura 3 kila mmoja.
Nafasi ya Katibu ilichukuliwa na Salum Mwinyi huku nafasi ya Mkurugenzi wa Fedha na Mipango ikikamatiwa na Samwel Semkuto.Aidha, wajumbe waliochaguliwa ni Samatha Rajab, Said Mukandara na George Mbata.
Wakiongea kwa kwa nyakati tofauti baada ya uchaguzi, Katibu Mtendaji wa BASATA,Ghonche Materego,Bw.Yustus Mkinga na Mlezi wa Mashirikisho ya wasanii,Mzee Rashid Masimbi walisema kwamba, kazi iliyopo mbele ni kwa viongozi hao kupanga mikakati ya muda mfupi na muda mrefu ya kuwaendeleza wasanii na kupigania maslahi yao.
Aidha, walisisitiza kwamba, kwa sasa wasanii wa muziki wanatakiwa kusimama imara chini ya shirikisho lao na kuwa na msimamo thabiti katika masuala mbalimbali yanayowahusu.
Kesho itakuwa ni zamu ya uchaguzi wa Shirikisho la Sanaa za Ufundi na keshokutwa ni shirikisho la Sanaa Jongevu (Filamu),Wadau wote mnakaribishwa kwenye chaguzi hizo ambazo ni maendeleo makubwa kwa wasanii na sekta ya sanaa kwa ujumla.