Na Alistide Kwizela.
Hatimaye Shirikisho la Wanamuziki Tanzania leo (Jumatano) limepata viongozi wake wa muda katika uchaguzi uliofanyika kwenye Ukumbi wa BASATA na kusimamiwa na Afisa Mtendaji Mkuu wa COSOTA,Bw.Yunus Mkinga.
Katika uchaguzi huo uliokuwa wa vuta ni kuvuta,Bw.Ibra Washokera aliweza kuibuka kidedea kwenye nafasi ya urais baada ya kupata kura 12 na kumbwaga Mkongwe wa muziki wa dansi,Hamza Kalala ‘Komandoo’ aliyeambulia kura 2 tu.
Kwa upande wa nafasi ya Makamu wa Rais,Mwanamuziki wa muziki wa asili,Che Mundugwao aliibuka kidedea kwa kupata kura 9 na kuwaacha mbali wapinzani wake ambao ni Mkongwe Kassim Mapili na Gwalugano Ayoub walioambulia kura 3 kila mmoja.
Nafasi ya Katibu ilichukuliwa na Salum Mwinyi huku nafasi ya Mkurugenzi wa Fedha na Mipango ikikamatiwa na Samwel Semkuto.Aidha, wajumbe waliochaguliwa ni Samatha Rajab, Said Mukandara na George Mbata.
Wakiongea kwa kwa nyakati tofauti baada ya uchaguzi, Katibu Mtendaji wa BASATA,Ghonche Materego,Bw.Yustus Mkinga na Mlezi wa Mashirikisho ya wasanii,Mzee Rashid Masimbi walisema kwamba, kazi iliyopo mbele ni kwa viongozi hao kupanga mikakati ya muda mfupi na muda mrefu ya kuwaendeleza wasanii na kupigania maslahi yao.
Aidha, walisisitiza kwamba, kwa sasa wasanii wa muziki wanatakiwa kusimama imara chini ya shirikisho lao na kuwa na msimamo thabiti katika masuala mbalimbali yanayowahusu.
Kesho itakuwa ni zamu ya uchaguzi wa Shirikisho la Sanaa za Ufundi na keshokutwa ni shirikisho la Sanaa Jongevu (Filamu),Wadau wote mnakaribishwa kwenye chaguzi hizo ambazo ni maendeleo makubwa kwa wasanii na sekta ya sanaa kwa ujumla.
Ni globu ya kijamii inayojihusisha na mambo yote ya kijamii,natumaini jamii yangu ya kitanzania itafaidika sana pindi ichukuapo fursa ya kuperuzi kwenye globu hii,dhamira yangu ni kufikisha ujumbe pamoja na kuiburudisha jamii yangu na furaha yangu ni kuona natimiza dhamira yangu kwako.natumaini kuwa wewe utaniunga mkono kwa kile ambacho nataka kukifanya kwa ajili ya jamii yangu ya kitanzania.NASHUKURU KWA KUNIELEWA.
Aug 12, 2010
SHIRIKISHO LA MUZIKI NALO LAPATA VIONGOZI WAO!!!
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
ME MYSELF & I
THE DON HIMSELF
Karibuni sana kwenye blog hii ya kijamii iliyosheheni makila kitu kuanzia siasa uchumi afya na burudani kwa ujumla wake.uingiapo kwenye blog hii ni mengi ambayo utapata nafasi ya kukutana nayo,kumbuka mawazo yako ndo hasa yanayojenga na kunifanya niwe na ufanisi zaidi.kariiiiiiibuuuuuuuuuuuu saaaaaaaaaaaaaaanaaaaaaaaaa.(THE DJ HIMSELF-JIWE)
No comments:
Post a Comment