Feb 17, 2011

WAANDAAJI MUZIKI WAILILIA BONGO FLEVA WALALAMIKIA MUELEKEO WA MUZIKI HUO

Katibu Mtendaji wa BASATA, Ghonche Materego (Kushoto) akisisitiza jambo kwenye Jukwaa la Sanaa linalofanyika kila Jumatatu kwenye Ukumbi wa baraza hilo.Wengine kutoka kulia ni Hassan Bumbuli Katibu wa Chama cha Waandishi wa Habari za Sanaa na Utamaduni (CAJAtz) na Ruyembe Mulimba, Mratibu wa program hiyo.
Muandaaji wa Muziki kutoka Studio za MJ, Joachim Kimario ‘Master J’ (Kulia) akichangia mjadala kwenye Jukwaa la Sanaa, BASATA.Kulia kwake ni muandaaji mwenzake Allan Mapigo.
Mtangazaji wa vituo vya redio na TV vya East Africa Anna Peter hakuwa nyuma katika kutoa dukuduku lake kwani lawama zilielekezwa kwa watangazaji kwamba, wamekuwa chanzo cha kudidimia kwa muziki wa kizazi kipya.
Wadau wa Jukwaa la Sanaa la BASATA wakifuatilia kwa makini mjadala kwenye jukwaa hilo mapema wiki hii.

Na Mwandishi Wetu

Waandaaji mahiri wa muziki wa kizazi kipya hapa nchini Joachim Kimario (Master J), Lamar na Allan Mapigo wamedai kwamba,muziki wa kizazi kipya maarufu kwa jina la Bongo Flava umepoteza muelekeo na juhudi za makusudi zinahitajika katika kuurudisha kwenye mstari na kuupa utambulisho wa kitanzania.

Wakizungumza katika mjadala mkali kwenye Jukwaa la Sanaa linalofanyika kila Jumatatu kwenye Ukumbi wa Baraza la Sanaa la Taifa, waandaaji hao wa muziki walitupa lawama kwa watangazaji wa vituo vya redio na TV kwamba ndiyo chanzo kikubwa cha kuporomoka kwa muziki huo kwa kile walichoeleza kwamba, hakuna utaratibu wa kuchuja nyimbo kabla ya kwenda hewani na baadhi hawana utaalam wa kazi zao.

Aidha, waliongeza kwamba pamoja na wao kujitahidi kuandaa midundo kwa kufyonza kutoka jamii za kitanzania, wasanii wa hapa nyumbani wamekuwa ni wa kuiga kila kitu wanapoingia studio na hawako tayari kubadilika wanapoelekezwa hali ambayo imeufanya muziki uhame kutoka kuwa wa jamii ya Tanzania na kuwa ule wenye kunakiri kila kitu kutoka nje hususan Marekani.

“Kwa sasa wasanii wanachokifanya ni kusikiliza muziki wa nje na kuja kuingiza kwenye muziki wao.Wamekuwa wakikopi kila kile msanii wa nje anachofanya kuanzia kuvaa na kuimba, wanataka wafanane na Jay Z hata wakija studio wanataka watengenezewe sound (midundo) kama ile ya nje” alisema Lamar kutoka Studio za FishCrab.

Kwa upande wake Master J ambaye ni mmiliki wa Studio za MJ alisema kwamba,siku hizi wanamuziki hawaangalii mazingira ya jamii za kitanzania tofauti na zamani, wamekuwa ni wa kuimba mambo yasiyofaa na yasiyopatikana katika jamii yetu bali ile ya Marekani hali ambayo imezidi kuutokomeza muziki wa kizazi kipya.

“Zamani tulikuwa na Hip Hop kama za akina 2 Proud ambaye kwa sasa anajiita Mr.Two (Sugu).Walikuwa wanaimba Hip Hop yenye kubeba matatizo halisi ya jamii ya Tanzania , Sugu aliimba nyimbo kama mikononi mwa polisi, miaka chini ya 18 na zote mbali ya kugusa matatizo yaliyopo ya jamii zilipendwa na kufanya vizuri tofauti na sasa” alisisitiza Master J
Aliongeza “Ujio wa redio na televisheni zisizozingatia utaalamu (professionalism) kwa watangazaji wake bali swaga (ujanja ujanja) na vipaji tu vya kuongea ni moja ya sababu ya kupoteza dira kwa muziki na hapo ndipo mambo yalianza kuharibika”.

Katika Jukwaa hilo la Sanaa pamoja na waandaaji wa muziki hao kutoa michango yao kuhusu mwenendo wa muziki wa kizazi kipya nchini, Mtaalam wa muziki John Ndumbaro alitoa maelezo ya kina kuhusu sekta hiyo ya sanaa ambapo mada ilikuwa ni Changamoto Katika Kutengeneza Muziki wenye Utambulisho wa Tanzania.

Explosions at munitions depot rock district near Dar es Salaam airport


Witnesses who heard explosions in Tanzania's largest city Wednesday night said they first thought the blasts were thunderclaps, until they saw the night sky glowing red and orange.

Sandip Patel grabbed his camera and ran to the top of his apartment building. He snapped away as a series of explosions shook neighborhoods around Dar es Salaam's Julius Nyerere International Airport.

Eyewitnesses from the Kimara district, north of the airport, told CNN they could see fireballs from their homes in the hills. "Particles from the explosion hit where we live. We took cover by laying down," one observer recounted.

"It looked like a sunrise in the dark," another eyewitness said. "Windows were rattling, you could feel the vibrations ... there were continuous explosions."

Blasts were first reported just after 9 p.m. (1 p.m. ET) and continued intermittently for about an hour and a half. Shock waves could be felt in neighborhoods more than six miles (10 kilometers) away from the airport, according to eyewitnesses.

Patel told CNN that his first impression, upon hearing the noise and feeling his apartment tremble, was that storms were coming. He and his wife studied the sky for proof of bad weather -- or detonations -- and it didn't take long to notice a "red-red, orange-orange thing in the sky." Wanting a better view, he and his wife ran to the 11th floor of their apartment building and Patel began taking pictures.

His photos show the night sky over Dar es Salaam lit with an eerie orange fireball. Munitions streak away from the center of the red-orange globe at crazy, looping angles. Patel told CNN that ammunition was "going up like firecrackers. A number of them went off every second ... over a long time. Every second or two, you'd hear some sort of explosion."

In a travel summary issued late Wednesday, Britain's High Commission said an army munitions bunker exploded in the Mbagala district near the international airport. Police have set up an evacuation center at Saba Saba grounds on Kilwa road, according to the summary, and are asking residents with in a 10-kilometer radius to evacuate.

Multiple witnesses have confirmed hearing similar announcements on the radio, warning residents of Dar es Salaam to avoid the area and asking residents to evacuate.

Patel spoke about the ammunition depository near the airport with CNN. He said residents have long been concerned about the facility, and that a deadly accident happened at the same storehouse two years ago. Patel said he thought chaos and panic caused a significant number of casualties in that incident, and expressed fear that something similar could happen again.

The U.K. travel summary said two children died in September 2009 as a result of the clearance of unexploded ordnance at the Mbagala ammunition storage depot. The summary warned anyone visiting the area not to pick up metal objects and to report any strange items they see to local authorities.

An airport employee confirmed for CNN that explosions were heard near the airport, but would not comment on time or location.

THE DON HIMSELF

Karibuni sana kwenye blog hii ya kijamii iliyosheheni makila kitu kuanzia siasa uchumi afya na burudani kwa ujumla wake.uingiapo kwenye blog hii ni mengi ambayo utapata nafasi ya kukutana nayo,kumbuka mawazo yako ndo hasa yanayojenga na kunifanya niwe na ufanisi zaidi.kariiiiiiibuuuuuuuuuuuu saaaaaaaaaaaaaaanaaaaaaaaaa.(THE DJ HIMSELF-JIWE)

Followers

BLOG ZA MARAFIKI

Search This Blog

ZILIZOPITA

DUNIA MUZIMA