Ni globu ya kijamii inayojihusisha na mambo yote ya kijamii,natumaini jamii yangu ya kitanzania itafaidika sana pindi ichukuapo fursa ya kuperuzi kwenye globu hii,dhamira yangu ni kufikisha ujumbe pamoja na kuiburudisha jamii yangu na furaha yangu ni kuona natimiza dhamira yangu kwako.natumaini kuwa wewe utaniunga mkono kwa kile ambacho nataka kukifanya kwa ajili ya jamii yangu ya kitanzania.NASHUKURU KWA KUNIELEWA.
Aug 21, 2010
'ARI ZAIDI,KASI ZAIDI NA NGUVU ZAIDI-PAMOJA TUTASHINDA'KAULI MBIU ILIYOZINDULIWA RASMI HAPO JANA
LIBENEKE JIPYA LA JK HILI HAPA!

www.kikwete2010.co.tz
Libeneke hili maalumu la Mgombea Uraisi na Mgombea Mwenza kwa tiketi ya CCM mwaka 2010 limesheheni habari mbalimbali kama:
· Wasifu wa Wagombea – Mhe. Jakaya M. Kikwete na Dr. Mohammed Gharib Bilal.
· Mafanikio katika sekta mbalimbali.
· Sera na Malengo 2010 – 2015.
· Ratiba za kampeni.
· Hotuba maalumu.
· Matoleo ya Habari.
· Video na picha.
· Mitandao ya Facebook,Twitter na Youtube.
Kupitia tovuti hii na mitandao yake utaweza kupata taarifa mbalimbali na kutoa maoni yako.
“ PAMOJA TUZIDI KUSONGA MBELE”
SIMBA YAIBANJUA AFRICA LYON 2-0, YANGA YAIPA ADABU POLISI DODOMA 1-0!!

WAREMBO VODACOM MISS TANZANIA WATOA MSAADA WA VYANDARUA MOSHI!!
Mchungaji Mtikila Aenguliwa Katika Uchaguzi Mkuu 2010
Na Mwandishi Wetu
WAKATI kampeni za uchaguzi mkuu zikifunguliwa rasmi leo hii, Tume ya Taifa ya Uchaguzi nchini (NEC) imemuengua aliyekuwa mgombea urais kupitia Chama cha Democratic (DP), Mchungaji Christopher Mtikila, kutokana na kutotimiza masharti yaliyowekwa kwa wagombea urais.
Mtikila aliyefika jana katika ofisi za NEC akiwa na mgombea mwenza wake Kibwana Said Kibwana, alienguliwa mara baada ya tume kubahini kwamba hakuwa ametimiza idadi ya wadhamini waliojitokeza kumdhamini.
Jaji Lewis Makame alisema kwamba NEC imefikia uamuzi wa kukitoa chama cha DP, baada ya Mtikila kupata wadhamini
mikoa 10, ingawa kati ya mikoa hiyo katika Mkoa wa Pwani wamepatikana wadhamini 220 wakiwamo 25 wenye kasoro.
Pia Jaji Makame alisema kwamba Mtikila pia alipata wadhamini 220 katika mkoa wa Kilimanjaro kati ya hao 27 wakiwa na kasoro.
Alisema kwamba katika Mkoa wa Dodoma kati ya wadhamini 220, wadhamini 29 walionekana kuwa na kasoro jambo liloifanya tume kuona kuwa Mtikial ahakukidhi vigezo vya kuwania urais.
Si Mtikila pekee ambaye alienguliwa, mgombea mwingine ambaye naye alikutwa na yaliyomkuta Mtikila ni Paul Kyara wa chama cha Sauti ya Umma (SAU) aliyeenguliwa baada ya kutokidhi idadi ya mikoa kumi ambayo mgombea urais anatakiwa kupata udhamini.
Baada ya kuenguliwa, Mtikila alikiri kuwa hasikitiki wala kuhudhunika kutokana na kutolewa huko, kwamadai kwamba hakuwa ameweka uhai wake katika kinyang’anyiro cha kugombea urais.
Alisema kwamba atapitia kwa makini nakala za fomu zake pamoja na viambatanisho vya udhamini, hili aweze kujua
kama atachukua hatua gani.
Vyama vingine vya Demokrasia Makini, Jahazi Asilia na NRA, vilijitoa vyenyewe baada ya kushindwa kufika leo hii katika ofisi za NEC kwaajili ya kurudisha fomu.
Aug 20, 2010
BAADHI YA WAREMBO WANAO WANIA TAJI LA MISS TANZANIA MWAKA HUU
FOMU ZA KUGOMBE URAIS ZARUDISHWA RASMI




Zitto Kabwe asks for your contributions
Dear Friends,
I would like to express my heartfelt gratitude for all your support.
Today we mark the start of a new journey.
This morning I submitted my nominations forms for re-election for the Kigoma North parliamentary seat ready to serve again the people of Kigoma North and my country TANZANIA.In order to make it happen am humbly asking for your support; if you would like to see Zitto back in Parliament and serving our nation I ask for your support.
I am ready to serve you once again.
DONATE:
Help Zitto keep fighting for our future and our country. Join the campaign by making a donation today.
Your contribution and support will help us in our campaign.
To donate, please:Make a Deposit to Our Campaign Account:
NAME: ZITTO KABWE ZUBERI
BANK: CRDB BANK
ACCOUNT NUMBER: 01J2082022500
Contact Details:
Contact Person: Mhonga Ruhwanya
Mobile Number: +255 0758 000 111
E-mail Address: zitto2010@gmail.com
FACEBOOK: http://www.facebook.com/zittokabwe
Blog: http://www.zittokabwe.wordpress.com/
Follow me on my Twitter Account: http://www.twitter.com/zittokabwe
On FLICKER(PICTURES): http://www.flickr.com/photos/zittokabwe
Aug 18, 2010
UJUMBE WA SAJNA KWA MAFANZ WAKE

ALBUM TITLE: IVETA