Sep 20, 2010

Tanzania imepewa Tuzo ya Umoja wa Mataifa ya Millenium Development Goals (MDGs) 2010 !!

Tanzania imepewa Tuzo ya Umoja wa Mataifa ya Millenium Development Goals (MDGs) 2010 : The Global Heabeat kutokana na mafanikio makubwa iliyoyapata katika maendeleo ya Elimu katika sherehe zilizofanyiaka kwenye ukumbi wa Waldorf Astoria Grand Ballroom jijini New York Septemba 19, 2010. Pichani Waziri Mkuu Mizengo Pinda akipokea tuzo hiyo na kutoka kwa Mmoja wa wasimamizo wa shughuli hiyo na Msanii maarufu , John Schneder. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Tanzania imepewa Tuzo ya Umoja wa Mataifa ya Millenium Development Goals (MDGs) 2010 The Global Hearbeat kutokana na mafanikio makubwa iliyoyapata katika maendeleo ya Elimu katika sherehe zilizofanyiaka kwenye ukumbi wa Waldorf Astoria Grand Ballroom jijini New York Septemba 19, 2010. Pichani Waziri Mkuu Mizengo Pinda na Balozi wa Tanzania kwenye umoja wa mataifa, Ombeni Sefue wakiwa wameshika tuzo hiyo baada ya kukabidhiwa: . (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akiwa na Naibu Katibu Mkua Umoja wa Mataifa, Dk. Asha Rose Migiro kabla ya mazungumzo yao kwenye hoteli ya Intercontinental jijini New York Septemba 19, 2010. Mheshimiwa Pinda yuko New York kumwakilisha Rais Jakaya Kikwete katika Mkutano wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa linalojali Maendeleo ya Millenia. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

Ridhiwani katika kampeni Masasi na Nanyumbu!!

Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji ya Baraza la Umoja wa Vijana Taifa, Ridhiwani Kikwete, akihutubia wakati wa mapokezi alipokuwa akiingia wilayani Masasi, Mtwara juzi..(PICHA NA RICHARD MWAIKENDA)
Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji ya Baraza la Umoja wa Vijana Taifa, Ridhiwani Kikwete, akiwaongoza baadhi ya makada wa CCM, kusalimiana na wanachama wa chama hicho, walipowasili katika ofisi za CCM, wilayani Nanyumbu,juzi kuanza vikao vya ndani vya kuweka mikakati ya ushindi kwa CCM katika Uchauzi Mkuu Oktoba 31, mwaka huu.Kutoka kushoto ni Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya tawi la CCM, London, Uingereza, Haruna Mbeyu na Omar Matulnga ambaye ni miononi mwa wadau wa chama hicho.
Sehemu ya umati wa watu ulojitokeza kumlaki,Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji ya Baraza la Umoja wa Vijana Taifa, Ridhiwani Kikwete, alipowasili Masasi, Mtwara juzi , kuanza ziara kuhamasisha vijana kupanga mikakati ya ushindi wa kishindo kwa CCM..(PICHA NA RICHARD MWAIKENDA)
Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji ya Baraza la Umoja wa Vijana Taifa, Ridhiwani Kikwete (katikati) akiwa na baadhi ya wanachama wa CCM, alipotembelea juzi nyumba aliyoishi yeye na babake, Rais Jakaya Kikwete mwaka 1988 mjini Masasi, ambaye wakati huo alikuwa Katibu wa CCM wa Wilaya hiyo.
Waendesha pikipiki, wakiwa wamejipanga wakati wa kumlaki,Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji ya Baraza la Umoja wa Vijanawa CCM Taifa, Ridhiwani Kikwete, wakijiandaa kuonoza msafara wa kiongozi huyo wa vijana,alipoanza ziara ya kampeni jana wilaya ya Masasi, Mtwara juzi..(PICHA NA RICHARD MWAIKENDA)

MASHINDANO YA VODACOM LATHAM OPEN 2010 YAFANA HUKO SINDA KISIWANI!!

Washiriki wa mashindano ya kuvua samaki ya Vodacom Lathan Open 2010 waliokuwa wakiendesha boti ya Natasha wakishangilia kwa kunyoosha vidole vyao juu mara baada ya kukabidhiwa zawadi zao za ushindi wa kuvua samaki wengi zaidi, mashindano hayo yamefanyika jana kwenye kisiwa cha Sinde kwenye Bahari ya Hindi, kushoto ni Necta Foya Meneja wa Mawasiliano Vodacom Tanzania.

Bw. David Sutton wa boti ya uvuvi ya Simba kulia akionyesha zawadi yake aliyoipokea kutoka kwa Mkuu wa Udhamini wa Vodacom Tanzania George Rwehumbiza mara baada ya boti yao kuwa miongoni mwa washindi wa jumla walioshinda kuvua samaki wengi zaidi katika mashindano ya Vodacom Lathan Open 2010 yaliyofanyika kwenye kisiwa cha Sinda jana, kushoto ni Necta Foya Meneja wa Mawasiliano Vodacom Tanzania.

Wafanyakazi wa Yachit Club ya jijini Dar es salaam wakiwapima samaki uzito rekodi mbalimbali za boto zilizoshiriki kwenye mashindano ya uvuvi ya Vodacom Latham Open 2010 yaliyofanyika kwenye kisiwa cha Sinda jana, mara baada ya mashindano Club hiyo huuza samaki hao kwa mnada na fedha zinazopatikana kupelekwa katika kusaidia watu wenye matatizo mbalimbali nchini.
Baadhi wa washiriki wakirejea mara baada ya kufanya uvuvi.
Hizi ni baadhi ya boti za uvuvi zilizoshiriki kwenye mashindano ya Vodacom Latham Open 2010 zikiwa zimeegeshwa ufukweneni mwa bahari ya Hindi huko katika kisiwa cha Sinda.

Sep 18, 2010

Pinda Amwakilisha JK Umoja Wa Mataifa.


Waziri Mkuu Mizengo Pinda na mkewe Mama Tunu Pinda wakizungumza na Balozi wa Tanzania umoja wa Mataifa Ombeni Sefue (kushoto) na Balozi wa Tanzania nchini Marekani Mwanaidi Maajar baada ya kuwasili kwenye uwanja wa ndege wa JFK jijini New York leo kumwakilisha Rais Jakaya Kikwete katika Mkutano wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa kuhusu Maendeleo ya Millenia. (Picha:Ofisi ya Waziri Muu)

TUME YA HAKI ZA BINADAMU NA UTAWALA BORA KUENDELEA KULINDA HAKI ZA WATOTO NCHINI!!

Na. Mary Kweka – MAELEZO.

Dar es Salaam.

Tume ya haki za Binadamu na Utawala bora imesema itaendelea kulinda, kutetea , na kushughulikia malalamiko mbalimbali ya uvunjwaji wa Haki za binadamu kwa watoto nchini.

Kauli hiyo ilitolewa jana Jijini Dar es salaam na Mwenyekiti wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora Jaji Kiongozi Mstaafu Ramadhani Manento wakati akizungumza na viongozi wa mabaraza ya watoto waliofanya ziara ofisi kwake ikiwa ni sehemu ya kongamano lao la mwaka huu linalomalizika leo ( jumamosi) jijini Dar es salaam.

Alisema ili kujenga taifa bora lenye maadili , jamii inao wajibu mkubwa wa kuhakikisha kuwa watoto wanalindwa na kuthaminiwa pamoja na kupatiwa mahitaji mbalimbali yakiwemo Elimu, Malazi bora, haki ya kupendwa, uhuru wa kucheza na kutoa maoni.

Aliongeza kuwa katika kulinda na kutetea haki za watoto, Serikali kupitia tume ya haki za binadamu na Utawala Bora imeanzisha Dawati la watoto ambalo linawajibika na kupokea malalamiko mbalimbali ya uvunjwaji wa haki za biadamu kwa watoto.

“Dawati la watoto linawajibika kulinda na kutetea haki za watoto wanaoishi katika mazingira magumu, walioachishwa shule,matatizo ya miradhi, utekelezaji wa sheria ya ubakaji wa watoto kwa watuhumiwa na mazingira ya watoto walio magerezani “Alifafanua Jaji Manento.

Aliendelea kufafanua kuwa Dawati hilo linatoa elimu kwa watu hasa wazazi kutambua umuhimu wa haki za watoto na kuwa makini pale wanapotoa adhabu kwa watoto huku akitoa angalizo kwa wazazi kuwa makini na adhabu hizo kuwa ziwe na vikomo na si zakuwajeruhi watoto na kuwasababishia ulemavu na kuwapotezea maisha.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Utafiti na Nyaraka wa tume hiyo Bi Epifania Mfundo alisema mwaka huu dawati la watoto limepokea jumla ya malalamiko 114 mpaka sasa, na wamefanikiwa kushughulikia malalamiko 28 kati ya 114 yaliyowasilishwa kwenye tume ya haki za binadamu na utawala bora.

“ Tunapokea malalamiko mbalimbali kupitia watoto wenyewe, taasisi mbalimbali,wazazi, vyombo mbalimbali vya habari,na tunapotembelea na kukagua Magereza na vituo vya Polisi kuangalia hali ya watoto walioko sehemu hizo”, alifafanua Bi Mfundo

Rais Kikwete katika kampeni Mbulu na Babati!!

Mgombea Urais kwa tiketi ya CCM Dr.Jakaya Mrisho Kikwete akiwapungia maelfu ya wakazi wa mji wa Babati wakati wa mkutano mkubwa wa Kampeni uliofanyika mjini Babati jana jioni(Picha na Freddy Maro)
mgombea urais kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi Dr.Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na wananchi wa Haydom, mkoani Manyara muda mara alipowasili katika mkutano wa Kampeni jana mchana,
Mgombea Urais kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi Dr.Jakaya Mrisho Kikwete akiongea na mwanafunzi Nicholaus Haba wa shule ya sekondari Dongobesh muda mfupi baada ya Rais Kikwete kuhutubia wananchi wa Kata ya Dongobesh wilayani Mbulu jana asubuhi.

Sep 17, 2010

Mrembo Julieth kuwakilisha Tanzania katika shindano la Miss Progress Italia!


Na Mwandishi Wetu MREMBO Julieth William aliyeshika nafasi ya tatu katika mashindano ya Miss Tanzania 2009, ameteuliwa kuiwakilisha Tanzania katika mashindano ya dunia ya Miss Progress International yatakayofanyika nchini Italia Septemba 26 mwaka huu. Mrembo huyo aliyetarajiwa kuondoka nchini jana jioni kuelekea nchini Italia kwa ajili ya kinyang’anyiro hicho alikabidhiwa bendera jana na Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) Aloyce Nzuki. Akizungumza baada ya kukabidhiwa bendera, mrembo huyo alisema aliteuliwa na waandaaji wa mashindano hayo kupitia mtandao wa mashindano ya Miss Tanzania na kwamba Tanzania inashiriki mchuano huo kwa mara ya kwanza mwaka huu. Alisema kabla ya kushiriki watakuwa kambini kwa wiki mbili na yeye kama mwakilishi wa Tanzania ana jukumu la kuutangaza utalii wa ndani ya nchi kupitia Utamaduni. “Nimefarijika kuwakilisha nchi kupitia mashindano haya kwani hii ni mara ya kwanza kwetu kushiriki hivyo ni changamoto kubwa kwangu binafsi na nchi kwa ujumla,” alisema. Alisema ana imani ataiwakilisha vyema Tanzania na ushiriki wake katika mashindano hayo utaweza kuchangia kwa kiasi kikubwa ongezeko la watalii na pato la taifa kwa ujumla. Kwa upande wake Nzuki alisema TTB inajivunia ushiriki wa mrembo huyo katika mashindano hayo ya utalii ya ngazi ya kidunia kwani pamoja na mambo mengine mrembo husika atakuwa balozi mzuri wa kazi za bodi hiyo katika kuutangaza utalii wa ndani. Alisema waandaaji wameifanya Tanzania iendelee kusomeka vizuri katika soko la utalii duniani na kwamba kuchaguliwa kwa mwakilishi huyo ni kitu cha kujivunia kwani ni nchi chache za kiafrika zinazoshiriki mashindano hayo. Mashindano hayo ambayo yanaandaliwa na Taasisi ya Miss Progress International ya Italia yanafanyika kwa mara ya tatu tangu kuanzishwa kwake na yanashirikisha warembo kutoka nchi 60 tofauti duniani zikiwemo sita za Afrika ambazo ni Tanzania, Kenya, Uganda, Ethiopia,Algeria na Nigeria

Nape Nape Nnauye ateuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Masasi

Benjamin Sawe

Maelezo

Dar es Salaam

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amemteua ndugu Nape Moses Nnauye kuwa Mkuu wa Wilaya ya Masasi Mkoani Mtwara.

Bwana Nnauye amechukua nafasi ya aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Masasi Said Ali Amanzi ambaye amebadilishiwa kituo chake cha kazi na kuhamishiwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana mkoani Mwanza.

Kabla ya uteuzi huo Ndugu Nnauye alikuwa ni Katibu Msaidizi Idara ya Siasa na Mahusiano ya Kimataifa CCM Makuu Dar es Salaam wakati Bwana Said Ali Amanzi amechukua nafasi ya Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana Ndugu Cleopas Rugarabamu ambaye alifariki mwezi Julai mwaka huu akiwa kwenye matibabu nchini India.

SERIKALI KUNUNUA MAHINDI YA WAKULIMA- AGIZO LA RAIS JAKAYA KIKWETE!

NA MAGRETH KINABO – MAELEZO

SERIKALI imetoa sh. bilioni 23.8 kwa ajili ya kununua mahindi tani 200,000 kutoka kwa wakulima wa ili kuweza kuyahifadhi katika Hifadhi ya Taifa kwa ajili ya matumizi ya baadae, vikiwemo vifaa vingine kama vile ni mizani , dawa za kufukuzia wadudu na mashine.

Kauli hiyo ilitolewa jana na Waziri wa Kilimo Chakula na Ushirika, Stephen Wasira jijini Da res Salaam jana(leo) ambapo alisema Rais Jakaya Kikwete ameagiza tani 400, 000 za mahindi zinunuliwe ikiwa ni lengo la Serikali katika kuyahifadhi mahindi hayo ambayo uzalishaji wake umeongezeka katika kipindi cha mwaka .

“ Serikali imeshatoa fedha hizo ili kuweza kununua tani hizo katika kipindi cha msimu huu”alisema Waziri Wasira huku akifafanua kwamba tayari serikali imeshanunua tani za mahindi 52,000 katika kipindi cha msimu huu hivyo ifikapo mwisho wa mwezi huu ambazo tani za mahindi 105,000 za mahindi zitakuwa zimenunuliwa na Serikali .

Aliongeza pia Serikali itaomba fedha nyingine sh. bilioni 33 kutoka Hazina kwa ajili ya kununua tani za mahindi nyingine za mahindi 95,000 ili kufikisha lengo la awamu ya kwanza ya ununuaji wa mahindi hayo ambayo jumla yake ni tani 200,000.

Hata hivyo aliongeza kwamba baada ya ununuzi huo watafanya tathimini ili kuweza kufikisha lengo la kununua tani nyingine za mahindi 200,000 zilizobakia kama ilivyoagizwa na Rais Kikwete.

Waziri Wasira alisema hifadhi ya Taifa hivi sasa ya ina tani za 52,000 zilizonunuliwa msimu huu na nyingine tani za mahindi za awali 47,000. Hata hivyo alisema uwezo wake wa kuhifadhi ni tani 240,000.

Akizungumzia kuhusu uzalishaji wa mahindi katika kipindi cha mwaka huu alisema umeongezeka,hivyo hayo ni mafanikio mazuri kutokana na hali ya hewa ilikuwa nzuri.

Alisema katika kipindi cha mwaka huu uzalishaji wa mahindi umeongezeka hadi kufikia tani milioni 4.7 wakati katika kipindi cha mwaka jana ulikuwa tani milioni 3.5.

“ Uzalishaji huu katika kipindi cha mwaka jana ulituwezesha kuwalisha watu milioni mbili wa mikoa yote iiliyokuwa na uhaba wa chakula ya kanda ya Kaskazini bila ya kuagiza chakula toka nje ya nchi au kuomba msaada wa namna hiyo,” alisema Waziri Wasira.

Waziri Wasira alisema tayari wameshafanya maandalizi ya kuagiza mbegu za mahindi tani 20,000, hivyo tani 9000 za mbegu hizo zimeshaagizwa kutoka nchi mbalimbali Tanzania ikiwemo na kampuni zitazipeleka karibu na wakulima. Hhata hivyo alisema mahitaji ya sasa ya mbegu hizo ni tani 30,000.

Kwa upande wa mbolea tani tayari kuna tani 201,000 wakati mahitaji ni tani 385,000, lakini tani nyingine zinaendelea kuagizwa.

Akizungumzia kuhusu ziara aliyoifanya Iran wiki iliyopita, Waziri Wasira alisema itasaidia kutoa ushirikiano katika masuala ya kilimo kati ya nchi hiyo na Tanzania. Hivyo Iran , itawekeza nchini Tanzania kwenye zana na kilimo, umwagiliaji, uongezaji thamani wa mazaokwa kuwekeza viwanda na kufanya utafiti ili kuhamasisha kilimo kwanza katika kukuza viwanda.

uingereza kuipiga tanzania katika bajeti


Waziri wa Fedha na Uchumi Mustafa Mkulo( kulia) akitangaza uamuzi wa Serikali ya Uingereza wa kuchangia katika Bajeti ya Taifa(GBS) kiasi cha bilioni 240 leo mjini Zanzibar . Kushoto ni Naibu Waziri wa Idara inayoshughulikia Misaada ya Kimataifa ya Uingereza (DFID) Stephen O’Brian.Tiganya Vincent-MAELEZO- Zanzibar


Na Tiganya Vincent-MAELEZO- Zanzibar

Serikali ya Uingereza imetoa kiasi cha bilioni 240 sawa na Paundi milioni 103.5 kwa ajili ya kuchangia Bajeti ya Tiafa (GBS) kwa mwaka wa fedha wa 2010/2011.

Kauli hiyo imetolewa leo mjini Zanzibar na Waziri wa Fedha na Uchumi Mustafa Mkulo na Naibu Waziri wa Idara inayoshughulikia Misaada ya Kimataifa ya Uingereza (DFID) Stephen O’Brien.

wakati wakitoa ufafanuzi huo kwa waandishi wa habari mjini Zanibar.

Mkulo alisema kuwa fedha hizo zitasaidia kutekeleza vipaumbele katika kutekeleza maeneo muhimu katika Mpango wa Kukuza Uchumi na Kupunguza Umaskini Tanzania(MKUKUTA).

Kufuatia hali hiyo ameishukuru Uingereza kwa niaba ya Serikali na wananchi wa Tanzania kwa kuendelea kuunga mkono juhudi za kuleta maendeleo ya Watanzania.

Alisema kuwa hali hiyo imejidhihirisha katika miradi mbalimbali ya maendeleo ambayo imekuwa ikifadhiliwa na Uingereza kwa ajili ya kuboresha maisha ya Watanzania wengi.

Mkulo alitaja wafadhili wengine walichangia Bajeti ya mwaka 2010/2011 kuwa ni Denmark Dola milioni 16.3, Finland Dola milioni 18.8, Norway Dola milioni 31.4 na Ireland Dola milioni 14.2.

Aidha aliwahakikishia wafadhili wote wa Tanzania kuwa Serikali itahakikisha kuwa kuna usimamizi mzuri wa misaada na fedha zote zinazotoka kwa wahisani ili kuendelea kujenga imani kwao.

“Napenda kuwahakikishia kuwa wafadhili na wahisani katika Bajeti ya Taifa kuwa fedha zitakazotolewa na wahisani zitatumika katika miradi na malengo yaliyokusudiwa ili kuhakikisha thamani halisi ya fedha zinazotolewa na wahisani”alisistiza Mkulo.

Kwa upande Naibu Waziri wa Idara inayoshughulikia Misaada ya Kimataifa ya Uingereza (DFID) Stephen O’Brien alitoa wito kwa Serikali ya Tanzania kuhakikisha kila kiasi cha fedha zinazotolewa na Uingereza zinatumika katika malengo yaliyokusudiwa ili matokeo yake yaweze kupimika.

US Ambassador visited to the TWENDE platform at Diamond Jubilee yestarday


Ambassador Alfonso Lenhadt delivering his massage to women entrepreneurs
Mustafa Hassanali, founder of TWENDE showing the US ambassador a basket created by a women entrepreneur.
Ambassador Alfonso looking at a batik shirt created by Farha Sultan
American Ambassador, Alfonso Lenhhard listerning to Ms Caroline Kessy during his visit to the TWENDE platform at Diamond Jubilee yestarday
The Ambassador discussing the quality of products among the women participating to TWENDE
Ms Teresia Mistry from Zanzibar disussing with Ambassador Alfonso Lenhardt.
US Amassador Alfonso Lenhardt (Right) and his Wife, Jacqueline Lenhardt in picture with some women entrepreneurs participating in TWENTE platfrom.
Tanzanian women entrepreneurs as they listnen to the Ambassador's speech
US Ambassor Alfonso Lenhardt, listerning to contrubutions from women entrepreneurs.(mtaa kwa mtaa-blogspot)

MANENO YA NAKAAYA BAADA YA KUICHAGUA CCM.

Changes from within. Lots of guys are quick to judge, If I could do something where I was, I would.
The support system was very low. its easy to talk about what you don't know... but I did what I had to do.
sikutegemea nyote mtafurahia but #this is politics#
(djchoka.blogspot.com)

BASATA LAWAFUNDA VIONGOZI WA MASHIRIKISHO YA WASANII NCHINI!!


Na Mwandishi Wetu
Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) limewataka viongozi wa mashirikisho ya wasanii kuhakikisha wanakuwa imara na thabiti ili kuleta ufanisi kwenye mashirikisho ya wasanii nchini yaliyoundwa na kupata viongozi wake hivi karibuni. Hayo yamesisitizwa na Wakufunzi kutoka BASATA wakati wakitoa semina kwa viongozi wa mashirikisho ya wasanii nchini iliyofanyika wiki hii kwenye ukumbi wa Baraza hilo na kuhudhuriwa na viongozi wote wa mashirikisho ya wasanii na wajumbe wao. Mashirikisho yaliyohusika kwenye semina hiyo ni pamoja na lile la Sanaa ya Muziki,Maonyesho,Ufundi na Filamu ambapo mada mbili zilizotolewa kwa viongozi hao ambazo ni Wajibu na Maadili ya Uongozi wa Mashirikisho ya Sanaa iliyowasilishwa na Mkurugenzi wa Idara ya Mfuko na Uwezeshaji wa BASATA,Bw.Ruyembe Mulimba na na ile ya Mchakato wa Kuandaa Mpango Mkakati wa Shirikisho iliyowasilishwa na Mwalimu Rashid Masimbi kutoka Kituo cha Sanaa za Maonyesho Tanzania. Akizungumza kwenye semina hiyo,Ruyembe alisema kwamba, viongozi wa mashirikisho ya wasanii hawana budi kuwa mstari wa mbele katika kutetea maslahi ya wasanii,kuwa na mwenendo mwema, kuzingatia maadili ya uongozi, kuzingatia dhana ya kutangulia na kuelekeza huku mtangulizi akiwa anafahamu anakowapeleka watu anaowaongoza. “Kiongozi mzuri lazima aelewe majukumu na mwenendo mwema katika kazi ya kusimamia watu ambao wanahusika na utendaji wa shughuli husika kwa ushirikiano na kwa pamoja kulingana na Katiba iliyopo” alisisitiza Ruyembe. Aliongeza kwamba, historia inaonesha vyama vingi na shirika za wasanii zimekuwa kwenye migogoro isiyoisha kutokana na viongozi kutokuwa na utashi wa kuongoza., kutanguliza maslahi binafsi na kushindwa kabisa kuwa na maono ya kutekeleza mikakati inayokuwa imewekwa. Alizidi kufafanua kwamba, wasanii wanakumbwa na changamoto nyingi sana zikiwemo za wao kuibiwa kazi zao, kunyonywa kupitia mikataba, kulipwa malipo kidogo na ukosefu wa masoko hivyo viongozi wa mashirikisho hawana budi kuwa mstari wa mbele kuhakikisha changamoto hizo zinawekewa mikakati ya kupunguzwa kama si kumalizwa kabisa. Naye Mwalimu Rashid Masimbi alisema kwamba, moja ya kazi ya viongozi hao wa mashirikisho ya wasanii ni kuhakikisha wanakuja na Mpango Mkakati wa muda mfupi na mrefu ambao utalenga kujenga dira ya utendaji na mafanikio ya mashirikisho. Aliongeza kwamba, viongozi hawana budi kuwa na mpango mkakati ambao utaeleza nini kitafanyika,nani atakifanya, kwa namna gani na kwa muda gani. “Mpango Mkakati ndiyo dira, dhamira, malengo, shughuli na matokeo ya utendaji wa shirikisho lolote hivyo lazima nyinyi viongozi mtuoneshe ni kwa jinsi gani tutayafikia haya” alisisitiza. Baadhi ya viongozi waliohudhuria semina hiyo waliishukuru BASATA kwa mpango huo na kusisitiza kwamba, semina kama hizo ziandaliwe mara kwa mara ili kujenga ufanisi wa mashirikisho ya wasanii na sekta ya sanaa kwa ujumla.

MTANGAZAJI WA RFA KID BWAY' AVAMIWA NA ALIYEJITAMBULISHA KUWA NI MSANII, APOTEZA FAHAMU, HAJITAMBUI HADI SASA.

MTANGAZAJI WA RADIO FREE AFRIKA AMBAYE VILEVILE YU PRODUCER WA KUREKODI MUZIKI WA KIZAZI KIPYA NDANI YA TETEMESHA PRODUCTION SANDU GEORGE MPANDA MAARUFU KWA JINA LA KID BWAY AMELAZWA HOSPITALI YA BUGANDO MARA BAADA YA KUVAMIWA NA KUPIGWA NA KITU KIZITO KICHWANI NA JAMAA ASIYEFAHAMIKA.

TAARIFA ZINASEMA KUWA KID BWAY AKIWA NYUMBANI KWAKE LUMALA JIJINI MWANZA, JAMAA ALIYEMVANIA ALIFIKA NYUMBANI HAPO MAJIRA YA SAA 2:30 USIKU NA KUJITAMBULISHA KAMA MSANII AKIHITAJI KUFANYA RECORDING, BAADA YA MAZUNGUMZO NA KUJITAMBULISHA ALIKARIBISHWA NDANI HADI CHUMBA CHA KUREKODIA STUDIO.

NYUMBANI KWA MTANGAZAJI HUYO ANAISHI NA JAMAA ZAKE WAWILI AMBAO WAKATI KID AKIMKARIBISHA MTENDA UHALIFU HUO NYUMBANI HAPO JAMAA HAO WALIMWONA KIJANA HUYO KISHA KILA MMOJA AKAINGIA CHUMBANI KWAKE. DAKIKA KADHAA WAKASIKIA KWA KIPINDI KIREFU SPIKA ZA STUDIO ZIKIKOROMA ISIVYO KAWAIDA NA KUANZA KUDADISI HUKU WAKIMWITA KID BWAY KUWA INAKUWAJE! WAKAITA NA KUITA NDIPO WALIPO AMUA KUINGIA STUDIO NA KUMKUTA SAKAFUNI KAANGUKA DABU ZIKIMTOKA MASIKIONI, PUANI NA KWENYE MAJERAHA SEHEMU ZA KICHWA.

KWA HIVI SASA KID YUPO HOSPITALI YA RUFAA BUGANDO AKIWA HOI HAJITAMBUI YAANI KAPOTEZA FAHAMU, ALITUNDIKIWA DRIPU YA MAJI IKIWA NI HUDUMA YA KWANZA AMBAYO AMEPATIWA JANA MARA BAADA YA KUFIKA HOSPITALINI HAPO AKISUBIRI KIPIMO CHA T SCAN KUONA KWA UNDANI ZAIDI SEHEMU ALIZODHURIKA. HAKUNA TAARIFA YOYOTE YA UPOTEVU WA MALI HALI INAYOPELEKEA WADADISI WA MAMBO KUDHANI KUWA YAWEZEKANA KULIKUWA NA VITA YA KICHINI CHINI AKA BIFU(AMBAYO HAIJAFAHAMIKA).

UCHUNGUZI KWA KUSHIRIKIANA NA JESHI LA POLISI UNAENDELEA KUFANYWA ILI KUJUA NINI SABABU ZA UVAMIZI HUO.

TAARIFA ZAIDI TUTAENDELEA KUKUJULISHA.
TWAMWOMBA MWENYEZI MUNGU AKUPE NGUVU BROTHER UPATE PONA.

Ridhiwani Kikwete atinga na kameni Liwale, Nachingwea!

Mjumbe wa kamati ya Utekelezaji Halmashauri ya baraza la umoja wa vijana wa CCM Ridhiwani Kikwete aliyevaa skafu) akikagua gwaride la viaja wa CCM, baada ya
kulakiwa eneo la eneo la Ngunichile akitokea kufanya kampeni za ndani Liwale kwenda
Nachingwea mkoani Lindi juzi, ambapo katika mkoa huo amefanya mikutano ya kuweka mikakati ya
ushindi wa chama hicho. (PICHA NA RICHARD MWAIKENDA)
Kikundi cha Kwaya cha vijana wa CCM kikitumbuiza wakati wa kampeni za ndani za chama hicho uliohutubiwa na Mjumbe wa kamati ya Utekelezaji ya Baraza Kuu la Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Ridhiwani Kikwete, mjini Liwale juzi
Mjumbe wa kamati ya Utekelezaji ya Baraza Kuu la Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi
(CCM), Ridhiwani Kikwete akiwahutubia wafuasi Wanachama na wafuasi wa chama hicho, wakati
wa mapokezi eneo la Ngunichile akitokea kufanya kampeni za ndani Liwale kwenda Nachingwea
mkoani Lindi jUZI, ambapo katika mkoa huo amefanya mikutano ya kuweka mikakati ya ushindi wa
chama hicho.

VODACOM SASA NI BWERERE

Vodacom Tanzania imepunguza gharama zake katika huduma ya kupiga simu, ambapo wateja wa Vodacom wataweza kupiga simu kwenda mitandao mingine nchini kwa punguzo la zaidi ya asilimia 50.Hii ni katika jitihada za kampuni hii kuhakikisha kuwa mawasiliano yanapatikana kwa gharama nafuu, nchi nzima.

Gharama hizi mpya zitamruhusu mteja wa Vodacom kuweza kupiga kwenda mitandao mingine kwa kiasi kidogo cha shilingi tatu tu za kitanzania kwa sekunde, wakati hapo awali gharama ya kupiga simu kwenda mitandao mingine ilikuwa shilingi sita na nusu.

Huduma hii imekuja miezi michache tu baada ya Vodacom kuzindua huduma nyingine ya shilingi moja kwa sekunde , maarufu kama HABARI NDIO HII.

Ikiwa na wateja milioni nane nchini, kampuni ya Vodacom imeendelea kutoa bidhaa na huduma kwa wateja wake,na kuwawezesha kupata mawasiliano kwa gharama nafuu.

Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Vodacon Tanzania, Mwamvita Makamba alisema jana kwamba kuwa gharama hizi mpya zimeleta mapinduzi katika sekta ya mawasiliano ya simu nchini.

“Kama tulivyozindua huduma ya Habari Ndio Hii, tumejikita kuhakikisha kuwa mtandao wetu unatoa bidhaa na huduma bora kwa wateja wetu ili kuwajenga kiuchumi.”

Kampuni ya Vodacom imekuwa nchini kwa miaka kumi sasa na inatabiri kukua zaidi katika sekta hii mwaka huu na miaka mingine ijayo.

“Tutamatumaini makubwa juu ya utendaji wetu hapo mbeleni na tunashauku kubwa kuweza kutoa huduma zetu zenye ubora wa hali ya juu kwa gharama nafuu.”

Huduma zingine za Vodacom kama Vodajamaa na Cheka Time zitabaki kama zilivyo.

“Vodacom inawahakikishia wateja wake kuwa itaendelea kutoa huduma zenye ubora wa hali ya juu hapo mbeleni” Bi Pendaeli alihitimisha kusema.

JARIDA LA MAN LAZINDULIWA RASMI JIJINI DAR ES SALAAM!!

Wanaume wa Tanzania sasa wanachokitu cha kujivunia kutokana kuanzishwa kwa Jarida la Man ambalo lilianza kuonekana mitaani mwishoni mwa mwaka jana.

Jarida hili limekuwa likigusa mambo mbalimbali yanayohusu wanaume kuanza kwenye afnya, biashara na maisha ya kawaida.

Mtendaji Mkuu wa kampuni ya Euro Consultancy Limited, Dismas Masawe alisema Jarida la Man linachapishwa na wazawa ambapo kwa sasa linapatikana nchini kote na likiwa katika toleo lake la nne.

Akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari jana uliofanyika kwenye hoteli ya New Africa, Dar es Salaam, Masawe alisema jarida hilo litakuwa linatoka kila baada ya miezi miwili na limeanzishwa ili kuziba pengo lililokuwepo katika sekta ya majarida kutokana na yale yaliyopo kuandika zaidi habari za wanawake.

“Jarida letu linachimbua mambo mbalimbali ambayo msomaji angependa kuyajua kuanzia magari, mambo ya ujenzi, taasisi za fedha, mambo ya uchukuzi, michezo, teknolojia, mitindo, uhusiano na kupitia mambo mbalimbali yanayotuzunguka katika jamii,” alisema.

Massawe, alisema jarida la Man linachapishwa katika kiwanda cha Jamana Dar es Salaam, na kwamba ni sehemu ambayo wanawake wanaweza kutumia kama jiwe muhimu la kuwatambua wanaume na kufahamu nini jinsia nyingine.

Alisema katika matoleo manne ambayo yamekwishatoka mpaka sasa Man limewahoji watu mbalimbali maarufu nchini. Katika toleo la kwanza Man, ilimfanyia mahojiano ndugu Azim Jamal ambaye ni mhamasishaji mkubwa, mchambuzi na mzungumzaji mkubwa. Toleo la pili Nehemiah Kyando Mchechu ambaye alikuwa Mtendaji Mkuu wa Benki ya Biashara ya Afrika na sasa ni Mtendaji Mkuu wa Shirika la Nyumba Tanzania (NHC).

Katika jarida la tatu Man, ilimhoji Ofisa Mtendaji Mkuu wa Mohamed Enterprises Tanzania Limited, ambaye pia ni Mbunge wa Singida, Mohamed Dewji, na katika toleo la mwisho Man lilimhoji Mwenyekiti na Mtendaji Mkuu wa kampuni ya Executive Solutions Limited, NduguAggrey Marealle. Marealle aafahamika kwa uwezo wake mkubwa katika kazi za Uhusiano wa Umma na Serikali kwa ujumla.

Massawe alisema Jarida la Man hivi karibuni litafungua milango kwa nchi za jirani za Kenya na Uganda na baadaye Kusini mwa Afrika kutokana na kuwepo kwa soko zuri la katika eneo hilo.

Pia katika siku zijazo, Jarida hili litakuwa likipatikana kwenye mtandao ambapo wasomaji watakuwa na uwezo wa kulipia ili waweze kulisoma.

Kwa mujibu wa Mtendaji huyo, Jarida hilo linawachangiaji wengi ambao wako katika ngazi juu katika serikali na taasisi mbalimbali mpaka raia wa kawaida. Massawe alisema wachangiaji wengine pia ni wanawake.

Aliwataka watanzania kujenga utamaduni wa kusoma ili kuweza kujua mambo mbalimbali yanayotokea duniani na pia kujua vitu mbalimbali.

“Watu wengi hawapendi kujisomea, lakini kusoma ni mojawapo ya njia ya kufanya mtu asiwe na muda kupoteza na pia kujifunza mambo mengi zaidi yanayotokea duniani,” alisema.

Amesema japokuwa Jarida hilo linahusu wanaume, lakini imeonekana wanawake wengi wameonekana kuvutiwa nalo na kulisoma.

Kwa maelezo zaidi wasiliana na

Dismas Massawe

CEO, Euro Consultancy Limited.

Mobile: 0784407475/0655407475

Email: dismas@eurocom.co.tz

au

Taji Liundi

Chief Editor, Man Magazine,

Mobile: 0787888799

mbio za pool table zaanza jini arusha



Mchezaji wa pool kutoka timu ya mkoa wa Ilala, Evansi Mushi akipiga mpira wakati wa ufunguzi wa mashindano ya taifa ya mchezo huo yaliyoanza kutimua vumbi huko jijini Arusha.mashindano haya yanaendelea kwa udhamini mkubwa wa bia ya Safari Lager.
baadhi ya wachezaji wa mchezo wa pool toka katika timu za mikoa mbali mbali zinazoshiriki katika mashindano hayo,wakiendelea kufuatilia mechi zilizokuwa zikiendelea wakati huo.

jide na machozi band ndani ya savannah lounge usiku huu



Lady Jay Dee a.k.a Binti Komando akiwajibika leo katika kiwanja chake cha kila alhamisi cha Savannah Lounge kilichopo ndani ya jengo la Benjamin Mkapa Tower.
timu nzima ya Machozi Band ikiongozwa na mwanadada Lady Jay Dee ikitoa burudani la kufa mtu usiku huu katika kiota cha Savannah lounge ndani ya Benjamin Mkapa Tower.
Sam,Mau na Joniko wakienda sambamba katika kuimba usiku huu.
mie na mdau Husna ndani ya Savannah Lounge usiku huu.
Detah na Don wakiwakilisha ndani ya Savannah Lounge usiku huu.
Detah (kulia) akigawa zawadi kwa mdau aliekuwa anapata kilaji cha Savannah usiku huu.
Detah (kulia) akiendelea na zoezi la kutoa zawadi kwa wadau waliokuwa wakijipatia kilaji cha Savanna kilichokuwa kikinyweka kwa kasi ya ajabu usiku huu.

Wadau wa Savannah Lounge wakiwa katika libeneke lao usiku huu.
wadau wakiserebuka na mapini ya Machozi Band yaliyokuwa yakiangushwa usiku huu ndani ya Savannah Lounge

THE DON HIMSELF

Karibuni sana kwenye blog hii ya kijamii iliyosheheni makila kitu kuanzia siasa uchumi afya na burudani kwa ujumla wake.uingiapo kwenye blog hii ni mengi ambayo utapata nafasi ya kukutana nayo,kumbuka mawazo yako ndo hasa yanayojenga na kunifanya niwe na ufanisi zaidi.kariiiiiiibuuuuuuuuuuuu saaaaaaaaaaaaaaanaaaaaaaaaa.(THE DJ HIMSELF-JIWE)

Followers

BLOG ZA MARAFIKI

Search This Blog

ZILIZOPITA

DUNIA MUZIMA