Sep 17, 2010

SERIKALI KUNUNUA MAHINDI YA WAKULIMA- AGIZO LA RAIS JAKAYA KIKWETE!

NA MAGRETH KINABO – MAELEZO

SERIKALI imetoa sh. bilioni 23.8 kwa ajili ya kununua mahindi tani 200,000 kutoka kwa wakulima wa ili kuweza kuyahifadhi katika Hifadhi ya Taifa kwa ajili ya matumizi ya baadae, vikiwemo vifaa vingine kama vile ni mizani , dawa za kufukuzia wadudu na mashine.

Kauli hiyo ilitolewa jana na Waziri wa Kilimo Chakula na Ushirika, Stephen Wasira jijini Da res Salaam jana(leo) ambapo alisema Rais Jakaya Kikwete ameagiza tani 400, 000 za mahindi zinunuliwe ikiwa ni lengo la Serikali katika kuyahifadhi mahindi hayo ambayo uzalishaji wake umeongezeka katika kipindi cha mwaka .

“ Serikali imeshatoa fedha hizo ili kuweza kununua tani hizo katika kipindi cha msimu huu”alisema Waziri Wasira huku akifafanua kwamba tayari serikali imeshanunua tani za mahindi 52,000 katika kipindi cha msimu huu hivyo ifikapo mwisho wa mwezi huu ambazo tani za mahindi 105,000 za mahindi zitakuwa zimenunuliwa na Serikali .

Aliongeza pia Serikali itaomba fedha nyingine sh. bilioni 33 kutoka Hazina kwa ajili ya kununua tani za mahindi nyingine za mahindi 95,000 ili kufikisha lengo la awamu ya kwanza ya ununuaji wa mahindi hayo ambayo jumla yake ni tani 200,000.

Hata hivyo aliongeza kwamba baada ya ununuzi huo watafanya tathimini ili kuweza kufikisha lengo la kununua tani nyingine za mahindi 200,000 zilizobakia kama ilivyoagizwa na Rais Kikwete.

Waziri Wasira alisema hifadhi ya Taifa hivi sasa ya ina tani za 52,000 zilizonunuliwa msimu huu na nyingine tani za mahindi za awali 47,000. Hata hivyo alisema uwezo wake wa kuhifadhi ni tani 240,000.

Akizungumzia kuhusu uzalishaji wa mahindi katika kipindi cha mwaka huu alisema umeongezeka,hivyo hayo ni mafanikio mazuri kutokana na hali ya hewa ilikuwa nzuri.

Alisema katika kipindi cha mwaka huu uzalishaji wa mahindi umeongezeka hadi kufikia tani milioni 4.7 wakati katika kipindi cha mwaka jana ulikuwa tani milioni 3.5.

“ Uzalishaji huu katika kipindi cha mwaka jana ulituwezesha kuwalisha watu milioni mbili wa mikoa yote iiliyokuwa na uhaba wa chakula ya kanda ya Kaskazini bila ya kuagiza chakula toka nje ya nchi au kuomba msaada wa namna hiyo,” alisema Waziri Wasira.

Waziri Wasira alisema tayari wameshafanya maandalizi ya kuagiza mbegu za mahindi tani 20,000, hivyo tani 9000 za mbegu hizo zimeshaagizwa kutoka nchi mbalimbali Tanzania ikiwemo na kampuni zitazipeleka karibu na wakulima. Hhata hivyo alisema mahitaji ya sasa ya mbegu hizo ni tani 30,000.

Kwa upande wa mbolea tani tayari kuna tani 201,000 wakati mahitaji ni tani 385,000, lakini tani nyingine zinaendelea kuagizwa.

Akizungumzia kuhusu ziara aliyoifanya Iran wiki iliyopita, Waziri Wasira alisema itasaidia kutoa ushirikiano katika masuala ya kilimo kati ya nchi hiyo na Tanzania. Hivyo Iran , itawekeza nchini Tanzania kwenye zana na kilimo, umwagiliaji, uongezaji thamani wa mazaokwa kuwekeza viwanda na kufanya utafiti ili kuhamasisha kilimo kwanza katika kukuza viwanda.

No comments:

THE DON HIMSELF

Karibuni sana kwenye blog hii ya kijamii iliyosheheni makila kitu kuanzia siasa uchumi afya na burudani kwa ujumla wake.uingiapo kwenye blog hii ni mengi ambayo utapata nafasi ya kukutana nayo,kumbuka mawazo yako ndo hasa yanayojenga na kunifanya niwe na ufanisi zaidi.kariiiiiiibuuuuuuuuuuuu saaaaaaaaaaaaaaanaaaaaaaaaa.(THE DJ HIMSELF-JIWE)

Followers

BLOG ZA MARAFIKI

Search This Blog

ZILIZOPITA

DUNIA MUZIMA