Benjamin Sawe
Maelezo
Dar es Salaam
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amemteua ndugu Nape Moses Nnauye kuwa Mkuu wa Wilaya ya Masasi Mkoani Mtwara.
Bwana Nnauye amechukua nafasi ya aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Masasi Said Ali Amanzi ambaye amebadilishiwa kituo chake cha kazi na kuhamishiwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana mkoani Mwanza.
Kabla ya uteuzi huo Ndugu Nnauye alikuwa ni Katibu Msaidizi Idara ya Siasa na Mahusiano ya Kimataifa CCM Makuu Dar es Salaam wakati Bwana Said Ali Amanzi amechukua nafasi ya Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana Ndugu Cleopas Rugarabamu ambaye alifariki mwezi Julai mwaka huu akiwa kwenye matibabu nchini India.
No comments:
Post a Comment