Wanaume wa Tanzania sasa wanachokitu cha kujivunia kutokana kuanzishwa kwa Jarida la Man ambalo lilianza kuonekana mitaani mwishoni mwa mwaka jana.
Jarida hili limekuwa likigusa mambo mbalimbali yanayohusu wanaume kuanza kwenye afnya, biashara na maisha ya kawaida.
Mtendaji Mkuu wa kampuni ya Euro Consultancy Limited, Dismas Masawe alisema Jarida la Man linachapishwa na wazawa ambapo kwa sasa linapatikana nchini kote na likiwa katika toleo lake la nne.
Akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari jana uliofanyika kwenye hoteli ya New Africa, Dar es Salaam, Masawe alisema jarida hilo litakuwa linatoka kila baada ya miezi miwili na limeanzishwa ili kuziba pengo lililokuwepo katika sekta ya majarida kutokana na yale yaliyopo kuandika zaidi habari za wanawake.
“Jarida letu linachimbua mambo mbalimbali ambayo msomaji angependa kuyajua kuanzia magari, mambo ya ujenzi, taasisi za fedha, mambo ya uchukuzi, michezo, teknolojia, mitindo, uhusiano na kupitia mambo mbalimbali yanayotuzunguka katika jamii,” alisema.
Massawe, alisema jarida la Man linachapishwa katika kiwanda cha Jamana Dar es Salaam, na kwamba ni sehemu ambayo wanawake wanaweza kutumia kama jiwe muhimu la kuwatambua wanaume na kufahamu nini jinsia nyingine.
Alisema katika matoleo manne ambayo yamekwishatoka mpaka sasa Man limewahoji watu mbalimbali maarufu nchini. Katika toleo la kwanza Man, ilimfanyia mahojiano ndugu Azim Jamal ambaye ni mhamasishaji mkubwa, mchambuzi na mzungumzaji mkubwa. Toleo la pili Nehemiah Kyando Mchechu ambaye alikuwa Mtendaji Mkuu wa Benki ya Biashara ya Afrika na sasa ni Mtendaji Mkuu wa Shirika la Nyumba Tanzania (NHC).
Katika jarida la tatu Man, ilimhoji Ofisa Mtendaji Mkuu wa Mohamed Enterprises Tanzania Limited, ambaye pia ni Mbunge wa Singida, Mohamed Dewji, na katika toleo la mwisho Man lilimhoji Mwenyekiti na Mtendaji Mkuu wa kampuni ya Executive Solutions Limited, NduguAggrey Marealle. Marealle aafahamika kwa uwezo wake mkubwa katika kazi za Uhusiano wa Umma na Serikali kwa ujumla.
Massawe alisema Jarida la Man hivi karibuni litafungua milango kwa nchi za jirani za Kenya na Uganda na baadaye Kusini mwa Afrika kutokana na kuwepo kwa soko zuri la katika eneo hilo.
Pia katika siku zijazo, Jarida hili litakuwa likipatikana kwenye mtandao ambapo wasomaji watakuwa na uwezo wa kulipia ili waweze kulisoma.
Kwa mujibu wa Mtendaji huyo, Jarida hilo linawachangiaji wengi ambao wako katika ngazi juu katika serikali na taasisi mbalimbali mpaka raia wa kawaida. Massawe alisema wachangiaji wengine pia ni wanawake.
Aliwataka watanzania kujenga utamaduni wa kusoma ili kuweza kujua mambo mbalimbali yanayotokea duniani na pia kujua vitu mbalimbali.
“Watu wengi hawapendi kujisomea, lakini kusoma ni mojawapo ya njia ya kufanya mtu asiwe na muda kupoteza na pia kujifunza mambo mengi zaidi yanayotokea duniani,” alisema.
Amesema japokuwa Jarida hilo linahusu wanaume, lakini imeonekana wanawake wengi wameonekana kuvutiwa nalo na kulisoma.
Kwa maelezo zaidi wasiliana na
Dismas Massawe
CEO, Euro Consultancy Limited.
Mobile: 0784407475/0655407475
Email: dismas@eurocom.co.tz
au
Taji Liundi
Chief Editor, Man Magazine,
Mobile: 0787888799
No comments:
Post a Comment