Timu ya Taifa ya Morocco imeweza kujipatia pointi muhimu na goli la ugenini baada ya kuifunga Taifa Stars bao 1-0 katika mchezo wao uliopita katika Uwanja wa Taifa jijini Dar. Alikuwa mshambuliaji Mounir El-Hamdaou wa Morocco aliyefunga bao hilo pekee la mchezo kwa shuti kali toka mguu wa kushoto, lililomshinda mlinda mlango Juma Kaseja, dakika mbili tu kabla ya kumalizika kwa kipindi cha kwanza. Hii ilikuwa ni mwendelezo wa ratiba ya mechi za kufuzu kucheza fainali ya kombe la Mataifa ya Afrika ambapo katika mechi iliyotangulia iliyochezwa nchini Algeria hapo Septemba 3, 2010, Tanzania walipata pointi muhimu ya ugenini japo walitoka sare ya bao 1 - 1 dhidi ya wenyeji wao. Tanzania imepangwa kundi moja la D, na timu za Algeria, Morocco na Jamhuri ya Afrika ya Kati. Mgeni rasmi katika mechi hiyo alikuwa Raisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na mdau mkubwa wa michezo, Jakaya Mrisho Kikwete ambaye alisitisha kampeni za uchaguzi mkuu ili kuhudhuria mechi hiyo. credit source: http://www.wavuti.com
Ni globu ya kijamii inayojihusisha na mambo yote ya kijamii,natumaini jamii yangu ya kitanzania itafaidika sana pindi ichukuapo fursa ya kuperuzi kwenye globu hii,dhamira yangu ni kufikisha ujumbe pamoja na kuiburudisha jamii yangu na furaha yangu ni kuona natimiza dhamira yangu kwako.natumaini kuwa wewe utaniunga mkono kwa kile ambacho nataka kukifanya kwa ajili ya jamii yangu ya kitanzania.NASHUKURU KWA KUNIELEWA.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
ME MYSELF & I
THE DON HIMSELF
Karibuni sana kwenye blog hii ya kijamii iliyosheheni makila kitu kuanzia siasa uchumi afya na burudani kwa ujumla wake.uingiapo kwenye blog hii ni mengi ambayo utapata nafasi ya kukutana nayo,kumbuka mawazo yako ndo hasa yanayojenga na kunifanya niwe na ufanisi zaidi.kariiiiiiibuuuuuuuuuuuu saaaaaaaaaaaaaaanaaaaaaaaaa.(THE DJ HIMSELF-JIWE)
No comments:
Post a Comment