
Mwisho Mwapamba akiwasili katika hafla hiyo huku akiwa ameongozana na baadhi ya wageni waalikwa akiingia kwenye Hoteli ya Continental jijini Dar es salaam ambapo hafla ya kumkaribisha mshiriki huyo wa Bigbrother Africa AllStars 2010 aliyerejea hivi karibuni kutoka Afrika Kusini alikokuwa akishiriki katika shindano hilo kwa miezi mitatu shindano hilo lililomalizika wiki iliyopita huku Mnigeria Uti akiibuka mshindi na kujinyakulia kitita cha Dola za Kimarekani laki mbili .

Ukiangalia picha hii watu wote wanaangalia upande mmoja, huu ulikuwa ni wakati wa kuwasili Mwisho Mwampamba katika hafla hiyo iliyohudhuriwa na watu mbalimbali kwenye Hoteli ya Continental jijini Dar es salaam.

Wageni waalikwa mbalimbali wakipiga story huku wakipata kinywaji.

Vijana wa Joseph Kusaga kutoka Clouds Television kutoka kulia ni Katunda, Ray, Casto na Ezra nao walikuwepo katika kurekodi tukio zima la kmkaribisha Mwisho Mwampamba.

Mshindi wa BigBrother mwaka 2008 Richard akiwa na rafiki yake kushoto katika hafla hiyo.

Wadau kutoka vyombo mbalimbali vya habari wakipozi kwa picha huku wakigonga bata zao katika hafla hiyo.

Wadau kutoka Multchoice Tanzania wakijimwaga katika hafla ya kumkaribisha Mwisho Mwampamba kwenye Hoteli ya Continentol jana usiku.
No comments:
Post a Comment