
Chamakh Mchezaji wa timu ya Asenal FC inayoshinriki Ligi Kuu Uingereza aliyekaa kulia ni akiwa na mchezaji mwenzaka mmoja wa wachezaji hatari wa timu hiyo aliyewasili pamoja na wachezaji wengine wa timu ya Taifa ya Moroco Kwenye uwanja wa ndege wa Mwalimu J.K.Nyerere , Moroco iliyokuja kwa ndege ya Shirika la ndege la (KLM)inatarajiwa kuumana na timu ya taifa ya Tanzania Taifa Stars kwenye uwanja wa Taifa siku ya jumamosi.
Mchezo huo ambao ni wa kufuzu kucheza fainali za kombea la mataifa ya Afrika mwaka 2012 utaonyeshwa moja kwa moja na kituo cha Televisheni cha SuperSpot cha Afrika Kusini na watanzania wakae mkao wa kula siku ya jumamosi kwani tunaweza kuona burudani nzuri kama ilivyokuwa kwa Timu ya taifa ya Brazil,

hawa wakipiga stori mara baada ya kuwasili uwanja wa ndege wa Mwalimu J.K.Nyerere

Hapa wakislimiana na mmoja wa maafisa kutoka Ubalozi wa Moroco.

wachezaji wengine wakiendelea kutoka nje.

Mchezaji Chamakh wa timu ya Ligi Kuu ya Uingereza Asenal FC wa pili kuoka kulia akiongozana na wachezaji mwenzake kuingia kwenye basi tayari kwa kuelekea hotelini mara baada ya kuwasili jijini Dar es salaam usiku huu.

wakiendelea kutoka na kuingia kwenye basi lao.

Wachezaji mwa timu ya taifa ya Moroco wakipanda kwenye basi lililowachukua mara baada ya kuwasili kwenye uwanja wa ndege wa J.K.Nyerere usiku wa jana
No comments:
Post a Comment