Sep 22, 2010

KCB BANK YAKABIDHI MSAADA WA VITABU SHULE YA SEKONDARI KINONDONI MUSLIM!!

Mkurugenzi Mtendaji wa KCB Tanzania Joram Kiarie akimkabidhi Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Kinondoni Muslim, Rajabu Mruma msaada wa vitabu vya masomo na samani za ofisini kwa ajili ya walimu vyenye thamani ya Milioni 4/- ili kusaidia kupunguza uhaba wa vifaa unaoikabili pamoja na kuinua kiwango cha elimu. Kushoto ni Kaimu mkuu wa shule hiyo, Mohammed Songo.
Mkurugenzi Mtendaji wa KCB Tanzania Joram Kiarie akiwaeleza jambo wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Kinondoni Muslim Tiba Kalufya na Mayasa Hemed mara baada ya kuikabidhi shule hiyo msaada wa vitabu vya masomo na samani za ofisini kwa ajili ya walimu vyenye thamani ya Milioni 4/- ili kusaidia kupunguza uhaba wa vifaa unaoikabili pamoja na kuinua kiwango cha elimu. Kulia ni mkuu wa idara ya masoko na mahusiano wa benki hiyo Christina Manyenye.
Mkurugenzi Mtendaji wa KCB Tanzania Joram Kiarie akizungumza na baadhi ya wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Kinondoni Muslim, mara baada ya hafla ya kukabidhi msaada wa vitabu vya masomo na samani za ofisini kwa ajili ya walimu vyenye thamani ya Milioni 4/- ili kusaidia kupunguza uhaba wa vifaa unaoikabili pamoja na kuinua kiwango cha elimu iliyofanyika shuleni hapo. (Na Mpigapicha Wetu).
Wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Kinondoni Muslim wakijisomea vitabu vilivyotolewa na benki ya KCB Tanzania mara baada ya hafla ya makabidhiano ya msaada wa vitabu vya masomo na samani za ofisini kwa ajili ya walimu vyenye thamani ya Milioni 4/- ili kusaidia kupunguza uhaba wa vifaa unaoikabili pamoja na kuinua kiwango cha elimu iliyofanyika jana (leo) jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mtendaji wa KCB Tanzania Joram Kiarie akiwapa vitabu wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Kinondoni Muslim, mara baada ya hafla ya kukabidhi msaada wa vitabu vya masomo na samani za ofisini kwa ajili ya walimu vyenye thamani ya Milioni 4/- ili kusaidia kupunguza uhaba wa vifaa unaoikabili pamoja na kuinua kiwango cha elimu.

RASCOM, is an intergovernmental, commercial satellite organization in Africa!!

RASCOM, is an intergovernmental, commercial satellite organization and the expression of the strong willingness of the African Governments to pool their efforts in a view to providing the African continent with telecommunications infrastructure based on space technology.

It is intended not only to give African national networks (countries) the opportunity to interconnect directly

without third party networks, but also to

supplement their existing telecom infrastructure by allowing them to provide services in isolated areas where there is no existing infrastructure, and complement the other technologies in order to provide a total solution to our users.

Besides the above objectives, the Mission of RASCOM is also to provide telecommunications services at affordable costs and supporting the creation of access to remote and underserved areas making universal service a reality in Africa.

RASCOM has a membership of 45 African countries including Tanzania. The headquarters are in Abidjan/Ivory Coast. We are here today for the meeting of Board of Directors of RASCOM following an invitation from TTCL which is one of the members of the Board of RASCOM.

To achieve its mission, RASCOM has established strategic partners in RascomStar-QAF Company, which has, under an Agreement, the responsibility to implement the RASCOM telecommunications satellite system dedicated to the African continent.

Our operating company, RascomStar-QAF is entrusted, among other responsibilities, with the task of the operation, maintenance and marketing of the services offered by the RASCOM satellites.

The first Pan African satellite was launched in December 2007 from Kourou/ French Guyana in South America and commercial operations started in 2008. Due to some technical problems it encountered after the launch which reduced its life time, it became necessary to quickly manufacture and launch a replacement satellite.

The current satellite is still in orbit providing services. We are already providing Band Lease Services (BLS) with the current satellite with a continental connectivity to more than 30 African countries to support the Pan African e-network for e-health and e-learning which is a project promoted by the African Union and the Indian Government.

Those who like sports will no doubt remember the under 17 football world cup which took place in Nigeria. These matches were transmitted live using our satellite.

On 4th August, 2010 the second Pan African satellite was launched from the same launch site. Those who are using the first satellite will have a seamless transfer to the replacement satellite.

All of this has been possible thanks to the partnership with other investors: Libyan African Investment Portfolio (LAIP) and Thales Alenia Space (TAS) of France.

We also had financing from some development banks in Africa which are Libyan Foreign Bank (LFB), African Development Bank (AfDB), West African Development Bank (BOAD) and Central African Development Bank (BDEAC) which participated in this project in a form of loan.

The following services will be provided by the satellite:

Broadband Connectivity Services (BCS) which will make it possible to create direct connectivity among all African countries. We will also have Telephony Services (TES) which will extend access to remote and underserved areas in Africa using a special designed terminal supporting voice, data (internet) and radio/TV reception. Band Lease Services (BLS) will also be available. The satellite will also support the transmission of both radio and television broadcasting services.

The RASCOM satellite will be a possible partner for the NEPAD e-school project whose objective is to see internet connectivity in more than 600,000 schools in Africa. We are also working together with Pan African Postal Union (PAPU) and African Telecommunications Union (ATU) in the e-Post project which plans to use ICT in bringing new services within the postal network in Africa.

RASCOM is following with a lot of interests the developments taking place in Africa with the deployment of optical fiber around Africa and across regional networks. This is a great initiative which should be encouraged and the participation of Governments is testimony that the development of the ICT infrastructure is now being given the deserved attention and importance. But I am also convinced that deploying a number of different technologies like fiber and satellite will only complement each other. No technology can singly meet the demands of ICT.

It is a general agreement that Africa needs huge capacities to support development of ICT and to create affordability levels as volumes increase. We also agree that the focus for broadband development should not only be in major towns but should be extended into rural Africa to support a number of e-services. This is why all developments aimed at expanding infrastructure in the continent are most welcome.

We are very thankful to the Leaders of Africa who have continuously been very supportive of the RASCOM project through the African Union.

This is just the beginning

Already we are in the advanced stages in terms of the planning and design for the next generation satellites with very large bandwidths which will respond to the needs of Africa in terms of services, broadband requirement and cost to the users.

The launch event of the second Pan African satellite served to assure the African Continent of RASCOM’s long term commitment to its mission of creating capacities to support Connectivity in Africa and access to information and communication to underserved and remote areas in Africa. For more information on RASCOM, please visit the RASCOM Website

UTURUKI YAANDAA MAONYESHO YA BIDHAA ZAKE JIJINI DAR ES SALAAM!!

NA ZAHRA MAJID- MAELEZO

22/0/2010.

UBALOZI wa Uturuki nchini Tanzania unatarajia umeandaa maonyesho ya pili ya bidhaa za nchi hiyo yatakayoanza Septemba 30 , mwaka huu hadi Oktoba3, mwaka huu kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar-es-salaam.

Hayo yalisemwa jana na balozi wa Uturuki nchini, Tanzania Dk. Sander Gurbuz katika mkutano wake na waandishi wa habari wa ambapo alisema Tanzania na Uturuki zina uhusiano mzuri hivyo , maonyesho hayo kwani yatasaidia kudumisha ushirikiano baina ya nchi hizo.

Alizitaja baadhi ya bidhaa zitakazoonyeshwa ni za nguo, vyakula ujenzi na zana za kilimo.

Dr. Gurbuz pia alibainisha kuwa Uturuki imewekeza katika sekta mbalimbali nchini kama vile kilimo, afya,madini, elimu , nguo na utalii.

“Tumewekeza nchini Tanzania ili tuweze kuzalidha bidhaa mbalimbali kwa ajili ya kuuza ndani ya nchi na nje ya nchi ,” alisema Balozi Gurbuz.

Balozi huyo alisema pia wameandaa mdahalo wa wa wafanyabiashara utakaohusisha nchi za Afrika Mashariki ukaohudhuriwa wajumbe 300 ambao unaotarajiwa kufanyika Ferbuari mwakani mara baada ya uchaguzi mkuu kumalizika. Mdahalo huo unatarajiwa kufanyika jijini Dar es Salaam.

Alielezea pia katika sekta ya elimu wana utaratibu wa kutoa ufadhili wa masomo ya juu huchukua wanafunzi 35 mpaka 45 kwa mwaka.

Aliongeza kuwa wamekuwa wakiwaleta madaktari wenye utaalamu mbalimbali kuja kufanya tiba nchini bure wapatao kati ya 25 hadi 35 jijini Dar es Salaam na wana mpango wa wa kuwaleta wengine ambao watatoa tiba hiyo hadi nje ya mkoa huo.

Balozi huyo alisema pia wana mpango wa kuandaa ziara ya waandishi wa habari kutembela nchi hiyo

Washindi watano wa Shindano la Chemsha Bongo kuzuru China!!

Benjamin Sawe na Vicent Tiganya

Maelezo -Dar es Salaam

Imeelezwa kuwa Serikali ya China na Tanzania zimekuwa na ushirikiano wa muda mrefu katika sekta ya habari ambapo shirika la habari la China (Xinhua News Agency) limekuwepo

nchini kwa miaka mingi likiandika habari za maendeleo.

Hayo yamesemwa jana jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi wa Idara ya Habari,Utamaduni na Michezo Bwana Clement Mshana katika sherehe za kutuoa tuzo kwa washindi wa Chemsha Bongo kuhusu miaka 45 ya uhusiano wa kibalozi kati ya serikali ya China na Tanzania.

Bwana Mshana alisema licha ya kuwa na kukabiliana na propaganda za nchi za magharibi shirika la habari la China (Xinhua News Agency) limekuawa likiandika habari za maendeleo na kuongeza sauti ya nchi zinazoendelea.

Alisema vipindi vinavyotangazwa na shirika hilo kwa lugha ya Kiswahili vimesaidia kuimarisha ushirikiano na udugu uliopo kati ya Tanzania na Serikali ya China.

“Ni jambo la kufurahisha kuona kuwa kutokana na mawasiliano kati ya China na Tanzania katika sekta mbalimbali ,Watanzania wengi wamekuwa na hamu kubwa ya kuelewa mambo ya China hivyo kupelekea watu wengi kujifunza lugha ya Kichina.”.Alisema Mkurugenzi Mshana.

Alisema shindano la Tuzo kwa waandishi wa Chemsha Bongo lililoendeshwa kwa mara ya kwanza kwa mara ya kwanza kwa ushirikiano kati ya vyombo vya Habari vya China na Tanzania limeutangaza,limeelimisha na kudumisha uhusiano kati ya Tanzania na China.

Katika hatua nyingine Balozi wa China nchini Tanzania Liu Xinsheng mashindano ya Chemsha Bongo yalilenga kufuata moyo wa ushirikiano na mawasiliano kati ya China na Afrika katika mambo ya Utamaduni

Alisema katika kuadhimisha miaka 45 ya uhusiano kati ya China na Tanzania Radio za China na Tanzania zimefanikiwa kufanya kufanya ushirikiano katika matangazo ya Chemsha Bongo hiyo zilitangaza vipindi mbalimbali vya utangazaji vya Kiswahili vya kukumbusha mchakato wa kukua kwa urafiki kati ya nchi ya China na Tanzania.

Balozi Xinsheng alifafanua kuwa Chemsha Bongo hiyo imeweka daraja la kuongeza urafiki,maelewano na mawasiliano kati ya wachina na watanzania na kusukuma mbele maendeleo ya uhusiano wa wenzi wa mikakati kati ya China na Tanzania.

Katika mashindano ya ya Chemsha Bongo Radio ya China ya kimataifa (CRI), TBC na Sauti ya Tanzania Zanzibar zilifanya ushirikiano katika kurusha matangazo ya shindano la Chemsha Bongo ambapo wasikilizaji walitakiwa kutoa mapendekezo kwa ajili ya kuendeleza zaidi kati ya China na Tanzania

Aidha mashindano hayo yalishirikisha zaidi ya wasikilizaji 1600 kutoka mikoa 20 ya Tanzania ambapo washindi watano maalum watakwenda kutembelea nchi ya China kwa siku kumi na washindi wa pili walipata zawadi ya Vereheni ambapo washindi wa tatu walipata zawadi ya Luninga za rangi.

FM ACADEMIA KUTOA ZAWADI KWA WAKAZI WA MBAGALA KUU!!

WAANDAJI wa Onesho la Bendi ya FM
Academia wazee wa Ngwasuma wametangaza zawadi kwa
washindi watakaibuka katika shindano
maalum la kucheza mitindo ya bendi hiyo,
kwenye utambulisho wa bendi hiyo
utaofanyika kesho kwenye Ukumbi wa Nawina Mbagala Kuu jijini Dare es laam salaam.
Mratibu wa Onesho hilo Zahor Said, alisema kuwa usiku huo
maalum wa Ngwasuma utakuwa na burudani mbalimbali ambazo
zitausindikiza utambulisho huo.
Said alisema watafanya utambulisho huo kwa kusindikizwa na
vikundi vya unenguaji vya kiduku.
Alisema utambulisho huo wa albamu ya Vuta nikuvute utakuwa
chini ya Rais wa bendi hiyo Nyoshi El Saadat watapiga nyimbo zote 11
zilizopo kwenye Albamu hiyo ikiwa ni pamoja na nyimbo za
zamani.
Alizitaja nyimbo zilizobeba albamu hiyo kuwa ni Heshima kwa
Wanawake ambayo ilipata tunzo mwaka jana,Mwili wangu,
Usiku wa juma tano na Jasmini.
Nyimbo zingine ni Angalia shida yangu,Mgeni,Heiken
Ngwasuma,Moses Katumbi,Fadhila kwa mama Intro Ngwasuma
Mathematics na vuta ni kuvute ambayo imebeba jina la albam.
Usiku huo umedhaminiwa na Henkein Bear, Kampuni ya Inoch,
Blog za JaneJohn5, Mamapipiro na Full Shangwe.

Ridhiwani akemea wanaotumia udini katika kampeni!

Na Richard Mwaikenda,Tunduru.
MJUMBE wa Kamati ya Utekelezaji ya Baraza Kuu la Umoja wa Vijana
wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa, Ridhiwani Kikwete, amekemea
tabia ya baadhi waumini wa dini ya kiislamu kudhihaki dini zingine
kwa kuwaita makafiri baadhi ya wagombea katika kampeni za Uchaguzi
Mkuu zinazoendelea nchini.
Ridhiwani,alikemea tabia hiyo katika mkutano wa kampeni juzi mjini
Tunduru, baada ya kupata taarifa kuwa kuna baadhi ya viongozi wa
Chama cha Wananchi (CUF) wanatumia udini katika mikutano yao ya
kampeni kwa kuwaambia wananchi kuwa wasimchague Mgombea ubunge wa
Jimbo la Tunduru Kaskazini kupitia Chama Cha Mapinguzi (CCM),
Injinia Ramo Makani kwa kumuita kafiri, kwa vile yeye ni mkristo.
"Jamani mimi pia ni mwislamu, si vizuri kumwita mwenzio kafiri, si
neno zuri, kwani kila mmoja anayo haki ya kufuata imani ya dini
anayoitaka na isitoshe katika uchaguzi huu hatutafuti Imamu wala
Sheikh wa kutuongoza bali tunatafuta kiongozi imara wa kuleta
maendeleo ya jimbo na nchi kwa ujumla,"alisema Ridhiwani huku
akishangiliwa na umati wa watu katika mkutano uliofanyika Lindi
mjini.
Alisema kuwa hata wakiamua kumchagua Imamu ama Sheikh kuwa mbunge,
kwa hali ya kawaida hatokuwa na muda wa kwenda kuswalisha
msikitini, kwani muda wake mwingi ikiwezekana hata kufikia miezi
sita ataupoteza kwa kuhudhuria vikao vya bunge Dodoma, hivyo kwenda
tofauti na maadili ya kazi hiyo ya kiroho.

KALUNDE BAND KUTIKISA JIJI LA MAPUTO OKTOBA 2, 2010!!

BENDI ya muziki wa dansi ya Kalunde imepata mwaliko wa kwenda kutumbuiza Jijini Maputo nchini Msumbiji.

Akizungumza Jijini Dar es Salaam jana Rais wa bendi hiyo Deo Mwanambilimbi alisema itatumbuiza Oktoba 2 mwaka huu.

Aidha aliongeza kwa kusema kuwa bendi hiyo inatarajia kuondoka nchini Oktoba Mosi na wanamuziki wake wote.

“Tumepata mwaliko wa kwenda kutumbuiza kwenye moja ya tamasha ambalo hufanyika kila mwaka hivyo tunatarajia kwenda kupiga nyimbo zote za Kalunde” alisema Mwanambilimbi.

Alisema mwaliko huo umekuja baada ya baadhi ya mashabiki wa bendi hiyo kuvutiwa na nyimbo wanazopiga.

Kalunde kwa sasa inatamba na nyimbo za ‘Itumbangwewe’, ‘Hilda’, ‘Nataka Kuzaa na Wewe’ , ‘Usiniguse’ ,’Fikiria’ na ‘Kilio Kilio’.

Pia imetoa vibao viwili vipya ambavyo ni ‘Fungua’ na ‘Maiwane’ ambazo tayari zimeanza kutamba katika kumbi za burudani ambazo bendi hiyo inapopiga.

Baadhi ya wanamuziki watakaoondoka na bendi hiyo ni Mwanambilimbi mwenyewe, Shehe Mwakichui, Junior Gringo, Deborah Nyangi, Sarafina Mshindo, Mwapwani Yahya, Othman Majuto na Remmy.

UZINDUZI WA TAMKO LA WANAHARAKATI WASIO WA KISERIKALI 2010; “WAKATI NA BAADA YA UCHAGUZI2010"

Asasi ya Agenda Participation 2000 asasi isiyo ya kiserikali inayofanya kazi ya kuhamasisha utamaduni wa utawala bora na demokrasia ndani ya Tanzania. Asasi pamoja na mambo mengine inatoa elimu ya uraia, mafunzo na kuhifadhi masuala ambayo yanaweza kuimarisha ushiriki wa wananchi katika utawala, demokrasia na michakato ya maendeleo.

AP2000, ikiongozwa na Dira ya; “Kuona jamii ya kidemokrasia na yenye amani na dola au nchi inayoendeshwa na utamaduni wa misingi au kanuni za kidemokrasia”. AP2000 imekuwa ikiratibu tangu mwaka 2005 na pia mwaka huu 2010 mchakato wa kukusanya na kuboresha maoni ya wanaharakati wasio wa kiserikali katika masuala mbali mbali nyeti kwa maslahi ya Taifa letu.

Kuelekea Uchaguzi Mkuu Oktoba 31, 2010, AP2000 imehusika kuratibu uandaaji wa Tamko la Wanaharakati Wasio wa Kiserikali kwa msaada wa mashirika mbalimbali kwa taarifa na ushauri. Sambamba na mashirika hayo, kwa namna ya pekee Shirika la Kijerumani la Friedrich Ebert Stiftung, wamehusika kufadhili uchapaji, uzinduzi na usambazaji wa tamko hili.

Tamko la Wanaharakati Wasio wa Kiserikali tunalolizindua leo kupitia mgeni rasmi Mhe. Jaji Mstaafu Lameck Mfalila, 21.09.2010 katika Hoteli ya Blue Pearl, Ubungo Plaza, Dar-es-Salaam likishuhudiwa na wanaharakati toka Asasi za kiraia, Balozi, Mashirika ya Kimataifa, Wanahabari, na wananchi wote kwa ujumla toka kila pembe ya Tanzania limegusa maeneo makuu yafuatayo;

  1. Tathmini ya Maendeleo Kiuchumu na Haki
  2. Ajira
  3. Mazingira na Maliasili
  4. Kilimo, Uvuvi na Ufugaji
  5. Huduma za Jamii
  6. Uongozi na Utawala
  7. Rushwa
  8. Maisha na Usalama wa Binadamu
  9. Maadili ya Uchaguzi

Vipaumbele hivi vilivyofafanuliwa kwa kina sana katika chapisho la Tamko hili, vinaangaliwa na Wanaharakati Wasio Wakiserikali kama msingi wa kupiga kura wagombea kutoka vyama vya siasa. Sambamba, kuwataka wagombea ngazi za Udiwani, Ubunge na Urais pia viongozi na watumishi wa umma kuzingatia maazimio hayo wakati na baada ya Uchaguzi Mkuu mwaka huu 2010.

Maazimio haya yanabeba uzito na masuala nyeti yanayoikandamiza Taifa na kuzidi kuliweka katika hali ngumu na kikwazo kuelekea ustawi na maendeleo endapo hayatashughulikiwa kwa haraka na kiukamilifu

Uchaguzi Mkuu unatoa nafasi adhimu kwa wapiga kura na wagombea kukumbuka malengo ya msingi ya mfumo wa uchaguzi, yaani kuweka mbele na kulinda maslahi ya Taifa hili. Kwa mantiki hiyo, tunasisitiza uwepo wa mchakato wa uchaguzi wenye uwazi, haki na amani.Lakini pia, tunapinga vikali aina yoyote ya vitisho, rushwa, mizengwe au hila kupindisha ushindi utokanao na kura halali za wananchi.Tunasisitiza katika siasa safi zenye kuzingatia misingi ya kidemokrasia.

Haya ndiyo tunayoyaamini, tunayoyasimamia, tuna amini yana msingi sasa na hata baada ya Uchaguzi Mkuu 2010. Wagombea watakaoingia madarakani, viongozi wa umma wote wanapaswa kuyasimamia kwa vitendo kwa maslahi na ustawi wa Taifa letu.

Tanzania tunayotaka kuiona ni Taifa lenye amani na maendeleo ambalo linaheshimu haki za wananchi

wake wote bila kujali jinsia, hadhi, dini, kabila, imani ya kundi fulani na uwezo kimwili ama kiuchumi. Tunataka Tanzania ambayo licha ya kutokuwa na wala rushwa, inaendeshwa na viongozi wenye uvumilivu na uadilifu, wenye kutumia ipasavyo maliasili na rasilimali hususan watu. Tunataka Tanzania inayojitosheleza kwa chakula; yenye miundombinu bora yenye misingi ya kiteknolojia; na yenye kutafsiri maendeleo ya kitaifa kwa kuangalia afya, elimu na ustawi wa jamii. Tunaomba wananchi wote wayasimamie haya na kuyafatilia, kwa sababu Tanzania tunayotaka inawezekana.

Ninawashukuru sana kwa kufika kwenu katika uzinduzi huu. Ni matumaini yangu makubwa mtaupasha umma vizuri juu ya haya tuliyowasilisha kwa umma kupitia tamko hili.

Mungu Ibariki Tanzania!

Imetolewa na;

Your browser may not support display of this image. Prof. Max Mmuya,

Mwenyekiti, Agenda Participation 2000.

Mwenyekiti wa WAMA Mama Salma Kikwete mkoani Kilimanjaro

Mwenyekiti wa WAMA Mama Salma Kikwete wa pili(kulia) akisalimia wakati alipowasili Jimbo la Mwanga mkoani Kilimanjaro na kufanya mkutano wa ndani kwa wanachama wa UWT jimboni kuhusu umuhimu wa kujitokeza kwa wingi ifikapo Oktoba 31, mwaka huu kupiga kura katika Uchaguzi Mkuu. (kulia) Mgombea Ubunge Jimbo la Mwanga Prpf. Jumanne Magembe, akifuatiwa na Mwenyekiti wa UWT Mkoa Kilimnjaro Regina Chonjo. Picha na Mwanakombo Jumaa.
Mama Salma Kikwete akimnadi mgombea ubunge jimbo la Mwanga Mkoa Kilimanjaro Prof. jumanne Magembe
Mama Salma Kikwete akimnadi Mgombea ubunge (CCM) Jimbo la Same Magharibi David Mathayo
Wakina mama wa UWT mjini Moshi wakishangilia wakati mama Salma alipoongea nao katika mkutano wa ndani
Wakina Mama wa Wilaya ya Mwanga wakimsikiliza mama Salma Kikwete wakati alipowahutubua kwenye mkutano wa ndani akielezea umuhimu wa kupiga kura kwa mwanamke.

DR. JAKAYA KIKWETE AENDELEA NA KAMPENI MKOANI IRINGA

Mgombea urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia chama cha Mapinduzi CCM Jakaya Mrisho Kikwete akimnadi mgombea ubunge jimbo la Isimani William Lukuvi ambaye amepita bila kupingwa baada ya kukosa mpinzani katika mikutano mbalimbali ya kampeni iliyofanyika jana mkoani Iringa. Uchaguzi mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani unatarajiwa kufanyika Oktoba 31 mwaka huu nchini kote. (Picha kwa hisani ya Akal Issa Michuzi).
Dr. Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na aliyekuwa mgombea ubunge wa Iringa mjini Bw. Frederick Mwakalebela kwa pamoja wakiwasalimia wananchi waliofika kwenye mkutano wa kampeni za chama hicho uliofanyika katika uwanja wa Samora mkoani Iringa. Mwakalebela, huku akishangiliwa na maelfu ya wakazi wa mji huo, aliweka historia ya kuwa mwana CCM aliyenadiwa hadharani pamoja na kushindwa katika kura za maoni ambapo alipopanda jukwaani sio tu alitangaza kuvunja makundi bali pia kuomba wananchi wa Iringa kumpa kura mshindani wake Mh. Monica Mbega na madiwani pamoja na Rais kwenye uchaguzi mkuu Octoba 31.
Aliyekuwa mbunge wa Sumbawanga Mjni mzee Paul Kimiti akiwa katika picha ya pamoja na Mgombea wa jimbo la Iringa Mjini Monica Mbega kushoto na aliyekuwa mgombea wa CCM katika kura za maoni ndani ya chama Fredirick Mwakalebela jana wakati Mgombea urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia CCM Dr. Jakaya Mrisho Kikwete alipofanya ziara mkoani humo na kuhutubia mikutano mbalimbali ya kampeni.
Umati mkubwa ukiwa umjeaa kwenye uwanja wa Samora mkoani Iringa wakati Dr. Jakaya Kikwete alipohutubia kutano mjini humo.
Huu ndiyo umati wa baadhi ya watu aliohudhuria kwenye mkutano mgombea wa CCM Dr. Jakaya Mrisho Kikwete jana kwenye uwanja wa Samora.

HUU NDIYO USAFIRI WA MOHAMMED DEWJI MGOMBEA UBUNGE SINGIDA MJINI!!

Huu ndiyo usafiri wa mgombea ubunge wa jimbo la Singida Mjini Bw. Mohammed Dewji hapa kama unavyomuona akiwa amepozi kwa picha mbele ya usafiri wake. (Picha kwa hisani ya Mo Blog)
Mchuma ukiwa tayari kwa kazi moja tu ya kumsafirisha mgombea wa ubunge jimbo la Singida kupitia Chama cha Mapinduzi CCM kila kona ya jimbo hilo katika mikutano yake ya kampeni.

Buriani Dk. Ernest Mashimba!!

Na Barnabas Lugwisha

Jumapili usiku, mida ya saa mbili hivi Mwandishi mwenzangu wa Habari , Mbaraka Islam, alinipigia simu na kuniuliza, “kaka umesikia kwamba Dk.Mashimba amefariki,” nikamwabia sijui kwa kweli, akasema hebu fuatilia, nikawapigia simu Wahariri watatu Absolom Kibanda, John Mapinduzi na Jackson Manyerere nikapata hakikisho.

Ni kweli ametutoka msomi huyu na kazi ya Mungu haina makosa, alikuwa mtu asiye na majivuno, mpenda utani na pande la baba kama ilivyo kwa wanaume wengi wa kisukuma.

Kabla ya umauti kumfika, alinusurika kifo mwanzoni mwa miaka ya 2000 maeneo ya Chango’mbe ambapo dereva wake alifariki hapo hapo, ilikuwa ni ajali ya kugongana na nadhani na daladala.

Alitibiwa na akapona, alivyokuwa muhimbili amelezwa alipata fahamu na kuagiza wasaidizi wake wanipe maelekezo kwamba niandike stori ambayo itaonyesha kwamba anaendelea pia nilizungumza naye kwa simu na akaniambia “Lugwisha, waambie wananchi sijafa, niko hai, kaandike hivyo poti,” kweli nikaandika hivyo akafurahi sana, baadaye alipelekwa Afrika Kusini kwa matibabu zaidi na akapona.

Dk. Mashimba hakuwa na mbwembe kama ilivyo kwa wasomi wengi wa ngazi yake, ambao wengi wao huwa na mikogo na kujifanya Miungu watu kana kwamba hawatauonja umauti.

We fikiria wakati mwingine nilikuwa nakunywa naye supu ya utumbo pale Chuo Cha Usimamisi wa Fedha (IFM), nani mwenye nafasi kama yake atafanya hivyo, wengi hujiona miungu watu, kwa Dk Mashimba haikuwa hivyo na simpambi kwa kuwa ametangulia mbele ya haki, alikuwa ni mtu wa watu ,ni nadra sana kumuona amevaa suti, labda kuwe na ugeni mzito kwake.

Mwaka 2005 niliandika makala yake moja yenye kichwa “Mkemia Mkuu Asiyevaa” suti, nilidhani atakasirika lakini, kumbe alifurahi sana , akaikata ile makala na kuibandika kwenye ubao wa matangazo pale nje ya ofisi yake.

Nilifahamiana naye kwa mara ya kwanza mwaka 1997 nikiwa Mwandishi wa The African maeneo ya Idara ya Habari Maelezo nakutana, nakumbuka ilikuwa ni kwenye mkutano wa Waandishi wa Habari, wakati huo Dr Mashimba alikuwa ameambatana na Waziri wa Afya wa wakati huo, Dr Aron Chiduo.

Ndani ya Mkutano huo nilimbana bana na maswali Dr Mashimba ambaye alikuwa akimsaidia Dk Chuduo kutoa ufafanuzi masuala mbalimbali.

Tulipomaliza Mkutano huo Dr Mashimba alinialika Ofisini kwake pale jirani na Hospitali ya Ocean Road na kuanza kufahamiana naye na kasha nikawa nafanya kazi za Uhusiano wa Umma za Wakala wa Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali kwa takriban miaka saba hivi.

Kilichonivutia katika historia ya Dk Mashimba ambaye leo hatunaye ni historia ya maisha yake , ni Msukuma wa Ngudu, Kwimba lakini amesomea Zanzibar kuanzia Darasa la kwanza hadi alipojiunga na chuo kikuu Cha Dar es Salaam mwazoni mwa miaka 1980, kabla serikali ya Mapinduzi Zanzibar haijampeleka nchini Australia kwa masomo ya ya shahada ya Pili na shahada ya Uzamivu (PHD).

Alivyorudi nchini kutoka ughaibuni mwaka 1995 , alipandishiwa cheo na kuwa Mkemia Mkuu wa Zanzibar, japo alikuwa amekaa Zanzibar tangu utoto wake lafudhi yake haikubadilika, ilikuwa ni ya Kisukuma tu, mwaka 1996 iliwahi kuripotiwa na vyombo vya habari kuwa Mkemia Mkuu wa Zanzibar alikuwa akiendesha daladala, nilimuuliza kuhusu ukweli huo alikubali.

“Ndiyo poti kwani nikiendesha daladala kuna nini, si ya kwangu bwana”, alisema huku akicheka.

Tukiaachana na hayo, atakumbukwa kwa kufanya mambo mengi pale Maabara ya Mkemia Mkuu, chini ya utawala wake, maabara iliboreshwa, aliwezesha mashine ya DNA kununuliwa na alijenga Maabara ya Kanda pale Mwanza.Alikuwa ni mchapa kazi kwelikweli.

Alitupeleka kozi mbalimbali baadhi ya Waandishi wa Habari zihusuzo maswala ya Maabara yake na kwa kweli huduma mbalimbali ziliboreshwa na kuuzingatia Mkataba wa Huduma kwa Mteja ambao kwake yeye ndiyo ilikuwa ilani ya utendaji wake.

Aliiboresha Maabara kwa vifaa mbalimbali vya kisasa muda mwingi alikuwa akiwahurumia wachimbaji madini wadogo wadogo wanaotumia madini ya Mercury kusafishia madini yao .

Alianzisha huduma za elimu kwa Umma juu ya umuhimu wa kupima maji ya visima kwenye maabara yake kwali aliamini kwamba visima vingi vya maji ya kunywa hapa jijini si salama,.

Nilimshawishi kuanzisha jarida la Elimu ya Ukemia kwa Umma, alikubali na nikapata bahati ya kuwa muhariri wa kwanza jarida hilo , kwa kufanya kazi kwa karibu na Dk.Mashimba nilipata nafasi ya kujifunza mambo mengi ya yahusiyo tasnia hiyo muhimu ya Ukemia hapa nchini.

Nakumbuka kuna wakati ilitokea mvutano baina ya serikali ya mapinduzi Zanzibar na Muungano, Zanzibar walitaka akafanye kazi kwao kwa kuzingatia kwamba serikali ya mapinduzi ndiyo iliyomsomesha.

Amefariki akiwa usingizini, ilikuwa ni mipango ya Mungu, ametangulia na sisi tuko nyuma yake.

Ulale Mahale pema peponi Dk. Mashimba.

Tume ya Kuratibu Udhibiti wa Dawa za Kulevya yatoa msaada wa kompyuta kwa Asasi ya Guluka Kwalala leo jijini dar


Mkemia Mwandamizi wa wa Tume,Bw. Yovin Ivo (kulia) akiongea na vyombo vya habari katika ukumbi wa mikutano wa tume hiyo wakati wa kukabidhi msaada wa Kompyuta ikiwa pamoja na Hp Laser jet P2055 Printer, APC Back-ups 650VA na Kasperky Antivirus 2010 Licensed, yenye thamani ya Tsh. 2,643,500/=.kwa Asasi ya Guluka Kwalala inayoshirikiana na Tume kukabiliana na kudhibiti matumizi wa dawa za kulevya nchini. kushoto ni Afisa Mtumishi Mkuu wa Tume ya Kuratibu Udhibiti wa Dawa za Kulevya,Bi. Aida Tesha
Katibu Mtendaji wa Asasi ya Guluka Kwalala,Bw. Bernard Ndunguru akitoa maelezo kwa vyombo vya habari namna wanavyokabiliana na matumizi ya dawa za kulevya pia alitoa shukrani kwa tume juu ya msaada walioupata na kusema hivyo vifaa walivyopewa vitasaidia sana kuchapisha nyaraka muhimu wakati wa utendaji.kulia ni Afisa Mtumishi Mkuu wa Tume ya Kuratibu Udhibiti wa Dawa za Kulevya,Bi. Aida Tesha.
Afisa Mtumishi Mkuu wa Tume ya Kuratibu Udhibiti wa Dawa za Kulevya,Bi. Aida Tesha (pili kushoto) akifungua moja ya box la kompyuta tayari kwa kukabidhi kwa Katibu Mtendaji wa Asasi ya Guluka Kwalala,Bw. Bernard Ndunguru (kushoto) ukiwa ni msaada uliotolewa na tume kwa Asasi hiyo.(pili kulia) ni Mkemia Mwandamizi wa wa Tume,Bw. Yovin Ivo na kulia kabisa ni Afisa Maendeleo ya Jamii wa Tume,Bi. Salome Mbonile.
Baadhi ya wanahabari wakifuatilia kwa makini maelezo yaliyokuwa yakitolewa na Mkemia Mwandamizi wa Tume,Bw. Yovin Ivo leo.

Kongamano la Viongozi Vitana wa Tanzania


Washiriki wa Kongamano la Viongozi Vijana wa Tanzania lililofanyika jijini Dar es Salaam tarehe 18 Septemba, 2010.


Wawakilishi wa Tanzania katika mkutano kati ya Rais Obama na viongozi vijana wa Afrika waandaa kongamano kwa viongozi vijana wa Tanzania

Hapo tarehe 18 Septemba wawakilishi watatu wa Tanzania katika mkutano kati ya Rais Barack Obama na Viongozi Vijana wa Afrika uliofanyika huko Washington DC kuanzia tarehe 3 hadi 5 Agosti 2010 waliandaa Kongamano kwa Viongozi Vijana wa Tanzania lililofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Dar es Salaam.

Masoud Mohamed, Mwenyekiti wa Mtandao wa Vijana Zanzibar, Malula Nkanyemka, mshauri wa uendeshaji miradi mkoani Mwanza na Modesta Mahiga, Mkurugenzi Mtendaji wa Professional Approach Limited, Inc., waliwaalika vijana 50 kutoka mikoa yote ya Tanzania katika kongamano hilo lililojadili malengo ya Rais Obama kwa vijana wa Afrika.

Malengo hayo yanahimiza uwazi, uwajibikaji, jumuiya imara ya kiraia, kuendelezwa vijana katika ujasiriamali, matumizi ya teknolojia katika kuleta maendeleo ya kiuchumi na kuongeza nafasi za ajira.

Bi. Mahiga alisema: "Leo ni mwanzo wa kile tunachotumaini kitakuwa kutaniko la kila robo mwaka la kikundi chetu kipya cha viongozi vijana. Tunataka kukuza elimu na kuchagiza kuwepo kwa mazingira mazuri ya biashara na uwekezaji yatakayowezesha kuongezeka kwa fursa za ajira kwa vijana.

Kwa kupitia michango yao kwa shughuli za kijamii, viongozi wa sekta binafsi wanaweza kuwainua na kuwajengea uwezo wanawake, watoto na vijana nchini Tanzania. Tutashirikiana nao, pamoja na wadau wengine katika kutekeleza malengo haya na kufikisha ujumbe kwa wawekezaji wa ndani na wa nje kwamba Tanzania ipo tayari na wazi kwa biashara."

Akitambua nguvu kubwa ya vijana katika bara hili kutokana na idadi na uwezo wao. Rais Obama alikutana na takriban viongozi vijana 115 kutoka katika mashirika na taasisi za kiraia na sekta binafsi kutoka katika zaidi ya nchi 40 za Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara ili kukuza maendeleo na kujenga ubia na vijana wa Afrika.

Katika hotuba yake wakati wa Kongamano hilo, Afisa Uhusiano wa Umma wa Ubalozi wa Marekani, Bw. Ilya Levin aliwapongeza vijana hao kwa dira na uongozi wao katika kukabili changamoto zinazowakabili Watanzania hivi leo.

Aliwataka kutumia vyema fursa iliyopatikana kutokana na kongamano hili kupanua mtandao wao na kutumia uwezo mkubwa uliopo baina yao ili kuwezesha maendeleo makubwa zaidi.

"Kutokana na moyo mliouonyesha na kujitoa kwenu kikamilifu katika kutekeleza malengo yenu, kuna uwezekano mkubwa wa kupata msaada kutoka sekta binafsi na wadau wengine na hivyo kuwezesha mabadiliko ya kweli ambayo ndio kiu ya vijana wa Kitanzania hivi sasa,"alisema Levin.

Kongamano hili la viongozi vijana wa Kitanzania lilidhaminiwa na Watu wa Marekani kwa kupitia Ubalozi wa Marekani jijini Dar es Salaam.

THE DON HIMSELF

Karibuni sana kwenye blog hii ya kijamii iliyosheheni makila kitu kuanzia siasa uchumi afya na burudani kwa ujumla wake.uingiapo kwenye blog hii ni mengi ambayo utapata nafasi ya kukutana nayo,kumbuka mawazo yako ndo hasa yanayojenga na kunifanya niwe na ufanisi zaidi.kariiiiiiibuuuuuuuuuuuu saaaaaaaaaaaaaaanaaaaaaaaaa.(THE DJ HIMSELF-JIWE)

Followers

BLOG ZA MARAFIKI

Search This Blog

ZILIZOPITA

DUNIA MUZIMA