Ni globu ya kijamii inayojihusisha na mambo yote ya kijamii,natumaini jamii yangu ya kitanzania itafaidika sana pindi ichukuapo fursa ya kuperuzi kwenye globu hii,dhamira yangu ni kufikisha ujumbe pamoja na kuiburudisha jamii yangu na furaha yangu ni kuona natimiza dhamira yangu kwako.natumaini kuwa wewe utaniunga mkono kwa kile ambacho nataka kukifanya kwa ajili ya jamii yangu ya kitanzania.NASHUKURU KWA KUNIELEWA.
Sep 22, 2010
Ridhiwani akemea wanaotumia udini katika kampeni!
Na Richard Mwaikenda,Tunduru. MJUMBE wa Kamati ya Utekelezaji ya Baraza Kuu la Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa, Ridhiwani Kikwete, amekemea tabia ya baadhi waumini wa dini ya kiislamu kudhihaki dini zingine kwa kuwaita makafiri baadhi ya wagombea katika kampeni za Uchaguzi Mkuu zinazoendelea nchini. Ridhiwani,alikemea tabia hiyo katika mkutano wa kampeni juzi mjini Tunduru, baada ya kupata taarifa kuwa kuna baadhi ya viongozi wa Chama cha Wananchi (CUF) wanatumia udini katika mikutano yao ya kampeni kwa kuwaambia wananchi kuwa wasimchague Mgombea ubunge wa Jimbo la Tunduru Kaskazini kupitia Chama Cha Mapinguzi (CCM), Injinia Ramo Makani kwa kumuita kafiri, kwa vile yeye ni mkristo. "Jamani mimi pia ni mwislamu, si vizuri kumwita mwenzio kafiri, si neno zuri, kwani kila mmoja anayo haki ya kufuata imani ya dini anayoitaka na isitoshe katika uchaguzi huu hatutafuti Imamu wala Sheikh wa kutuongoza bali tunatafuta kiongozi imara wa kuleta maendeleo ya jimbo na nchi kwa ujumla,"alisema Ridhiwani huku akishangiliwa na umati wa watu katika mkutano uliofanyika Lindi mjini. Alisema kuwa hata wakiamua kumchagua Imamu ama Sheikh kuwa mbunge, kwa hali ya kawaida hatokuwa na muda wa kwenda kuswalisha msikitini, kwani muda wake mwingi ikiwezekana hata kufikia miezi sita ataupoteza kwa kuhudhuria vikao vya bunge Dodoma, hivyo kwenda tofauti na maadili ya kazi hiyo ya kiroho.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
ME MYSELF & I
THE DON HIMSELF
Karibuni sana kwenye blog hii ya kijamii iliyosheheni makila kitu kuanzia siasa uchumi afya na burudani kwa ujumla wake.uingiapo kwenye blog hii ni mengi ambayo utapata nafasi ya kukutana nayo,kumbuka mawazo yako ndo hasa yanayojenga na kunifanya niwe na ufanisi zaidi.kariiiiiiibuuuuuuuuuuuu saaaaaaaaaaaaaaanaaaaaaaaaa.(THE DJ HIMSELF-JIWE)
No comments:
Post a Comment