Sep 22, 2010

KALUNDE BAND KUTIKISA JIJI LA MAPUTO OKTOBA 2, 2010!!

BENDI ya muziki wa dansi ya Kalunde imepata mwaliko wa kwenda kutumbuiza Jijini Maputo nchini Msumbiji.

Akizungumza Jijini Dar es Salaam jana Rais wa bendi hiyo Deo Mwanambilimbi alisema itatumbuiza Oktoba 2 mwaka huu.

Aidha aliongeza kwa kusema kuwa bendi hiyo inatarajia kuondoka nchini Oktoba Mosi na wanamuziki wake wote.

“Tumepata mwaliko wa kwenda kutumbuiza kwenye moja ya tamasha ambalo hufanyika kila mwaka hivyo tunatarajia kwenda kupiga nyimbo zote za Kalunde” alisema Mwanambilimbi.

Alisema mwaliko huo umekuja baada ya baadhi ya mashabiki wa bendi hiyo kuvutiwa na nyimbo wanazopiga.

Kalunde kwa sasa inatamba na nyimbo za ‘Itumbangwewe’, ‘Hilda’, ‘Nataka Kuzaa na Wewe’ , ‘Usiniguse’ ,’Fikiria’ na ‘Kilio Kilio’.

Pia imetoa vibao viwili vipya ambavyo ni ‘Fungua’ na ‘Maiwane’ ambazo tayari zimeanza kutamba katika kumbi za burudani ambazo bendi hiyo inapopiga.

Baadhi ya wanamuziki watakaoondoka na bendi hiyo ni Mwanambilimbi mwenyewe, Shehe Mwakichui, Junior Gringo, Deborah Nyangi, Sarafina Mshindo, Mwapwani Yahya, Othman Majuto na Remmy.

No comments:

THE DON HIMSELF

Karibuni sana kwenye blog hii ya kijamii iliyosheheni makila kitu kuanzia siasa uchumi afya na burudani kwa ujumla wake.uingiapo kwenye blog hii ni mengi ambayo utapata nafasi ya kukutana nayo,kumbuka mawazo yako ndo hasa yanayojenga na kunifanya niwe na ufanisi zaidi.kariiiiiiibuuuuuuuuuuuu saaaaaaaaaaaaaaanaaaaaaaaaa.(THE DJ HIMSELF-JIWE)

Followers

BLOG ZA MARAFIKI

Search This Blog

ZILIZOPITA

DUNIA MUZIMA