Academia wazee wa Ngwasuma wametangaza zawadi kwa
washindi watakaibuka katika shindano
maalum la kucheza mitindo ya bendi hiyo,
kwenye utambulisho wa bendi hiyo
utaofanyika kesho kwenye Ukumbi wa Nawina Mbagala Kuu jijini Dare es laam salaam.
Mratibu wa Onesho hilo Zahor Said, alisema kuwa usiku huo
maalum wa Ngwasuma utakuwa na burudani mbalimbali ambazo
zitausindikiza utambulisho huo.
Said alisema watafanya utambulisho huo kwa kusindikizwa na
vikundi vya unenguaji vya kiduku.
Alisema utambulisho huo wa albamu ya Vuta nikuvute utakuwa
chini ya Rais wa bendi hiyo Nyoshi El Saadat watapiga nyimbo zote 11
zilizopo kwenye Albamu hiyo ikiwa ni pamoja na nyimbo za
zamani.
Alizitaja nyimbo zilizobeba albamu hiyo kuwa ni Heshima kwa
Wanawake ambayo ilipata tunzo mwaka jana,Mwili wangu,
Usiku wa juma tano na Jasmini.
Nyimbo zingine ni Angalia shida yangu,Mgeni,Heiken
Ngwasuma,Moses Katumbi,Fadhila kwa mama Intro Ngwasuma
Mathematics na vuta ni kuvute ambayo imebeba jina la albam.
Usiku huo umedhaminiwa na Henkein Bear, Kampuni ya Inoch,
Blog za JaneJohn5, Mamapipiro na Full Shangwe.
No comments:
Post a Comment