Mgombea urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia chama cha Mapinduzi CCM Jakaya Mrisho Kikwete akimnadi mgombea ubunge jimbo la Isimani William Lukuvi ambaye amepita bila kupingwa baada ya kukosa mpinzani katika mikutano mbalimbali ya kampeni iliyofanyika jana mkoani Iringa. Uchaguzi mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani unatarajiwa kufanyika Oktoba 31 mwaka huu nchini kote. (Picha kwa hisani ya Akal Issa Michuzi).
Dr. Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na aliyekuwa mgombea ubunge wa Iringa mjini Bw. Frederick Mwakalebela kwa pamoja wakiwasalimia wananchi waliofika kwenye mkutano wa kampeni za chama hicho uliofanyika katika uwanja wa Samora mkoani Iringa. Mwakalebela, huku akishangiliwa na maelfu ya wakazi wa mji huo, aliweka historia ya kuwa mwana CCM aliyenadiwa hadharani pamoja na kushindwa katika kura za maoni ambapo alipopanda jukwaani sio tu alitangaza kuvunja makundi bali pia kuomba wananchi wa Iringa kumpa kura mshindani wake Mh. Monica Mbega na madiwani pamoja na Rais kwenye uchaguzi mkuu Octoba 31.
Aliyekuwa mbunge wa Sumbawanga Mjni mzee Paul Kimiti akiwa katika picha ya pamoja na Mgombea wa jimbo la Iringa Mjini Monica Mbega kushoto na aliyekuwa mgombea wa CCM katika kura za maoni ndani ya chama Fredirick Mwakalebela jana wakati Mgombea urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia CCM Dr. Jakaya Mrisho Kikwete alipofanya ziara mkoani humo na kuhutubia mikutano mbalimbali ya kampeni.
No comments:
Post a Comment