Mkemia Mwandamizi wa wa Tume,Bw. Yovin Ivo (kulia) akiongea na vyombo vya habari katika ukumbi wa mikutano wa tume hiyo wakati wa kukabidhi msaada wa Kompyuta ikiwa pamoja na Hp Laser jet P2055 Printer, APC Back-ups 650VA na Kasperky Antivirus 2010 Licensed, yenye thamani ya Tsh. 2,643,500/=.kwa Asasi ya Guluka Kwalala inayoshirikiana na Tume kukabiliana na kudhibiti matumizi wa dawa za kulevya nchini. kushoto ni Afisa Mtumishi Mkuu wa Tume ya Kuratibu Udhibiti wa Dawa za Kulevya,Bi. Aida Tesha
Katibu Mtendaji wa Asasi ya Guluka Kwalala,Bw. Bernard Ndunguru akitoa maelezo kwa vyombo vya habari namna wanavyokabiliana na matumizi ya dawa za kulevya pia alitoa shukrani kwa tume juu ya msaada walioupata na kusema hivyo vifaa walivyopewa vitasaidia sana kuchapisha nyaraka muhimu wakati wa utendaji.kulia ni Afisa Mtumishi Mkuu wa Tume ya Kuratibu Udhibiti wa Dawa za Kulevya,Bi. Aida Tesha.
Afisa Mtumishi Mkuu wa Tume ya Kuratibu Udhibiti wa Dawa za Kulevya,Bi. Aida Tesha (pili kushoto) akifungua moja ya box la kompyuta tayari kwa kukabidhi kwa Katibu Mtendaji wa Asasi ya Guluka Kwalala,Bw. Bernard Ndunguru (kushoto) ukiwa ni msaada uliotolewa na tume kwa Asasi hiyo.(pili kulia) ni Mkemia Mwandamizi wa wa Tume,Bw. Yovin Ivo na kulia kabisa ni Afisa Maendeleo ya Jamii wa Tume,Bi. Salome Mbonile.
Baadhi ya wanahabari wakifuatilia kwa makini maelezo yaliyokuwa yakitolewa na Mkemia Mwandamizi wa Tume,Bw. Yovin Ivo leo.
No comments:
Post a Comment