Rais Dr.Jakaya Mrisho Kikwete akimnadi mgombea ubunge jimbo la Mkuranga kwa tiketi ya CCM Adam Kighoma Malima wakati wa Mkutano wa kampeni uliofanyika huko Kimanzichana, wilayani Mkuranga leo mchana (picha na Freddy Maro Ni globu ya kijamii inayojihusisha na mambo yote ya kijamii,natumaini jamii yangu ya kitanzania itafaidika sana pindi ichukuapo fursa ya kuperuzi kwenye globu hii,dhamira yangu ni kufikisha ujumbe pamoja na kuiburudisha jamii yangu na furaha yangu ni kuona natimiza dhamira yangu kwako.natumaini kuwa wewe utaniunga mkono kwa kile ambacho nataka kukifanya kwa ajili ya jamii yangu ya kitanzania.NASHUKURU KWA KUNIELEWA.
Oct 19, 2010
Rais Jakaya Kikwete katika kampeni Mkuranga.
Rais Dr.Jakaya Mrisho Kikwete akimnadi mgombea ubunge jimbo la Mkuranga kwa tiketi ya CCM Adam Kighoma Malima wakati wa Mkutano wa kampeni uliofanyika huko Kimanzichana, wilayani Mkuranga leo mchana (picha na Freddy Maro WAANGALIZI WA UCHAGUZI MKUU KUTOKA SADC WAWASILI NCHINI.
Mwenyekiti wa waangalizi wa uchaguzi mkuu kutoka Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za kusini mwa Afrika (SADC) ambaye pia ni Waziri wa Mambo ya Nje wa Zambia Kabinga Pande (kulia) akizungumza na wadau mbalimbali wakiwemo viongozi wa siasa, waandishi wa habari na waangalizi wa uchaguzi kutoka SADC juu ya ujio wa ujumbe wa waangalizi hao na majukumu yao wakati wa uchaguzi mkuu utakaofanyika tarehe 31 mwezi huu leo jijini Dar es salaam. Pamoja na mambo mengine ametoa wito kwa watanzania kudumisha amani na kuonyesha ukomavu wa kisiasa uliopo nchini hasa kabla na baada ya uchaguzi. (Picha Aron Msigwa na Fullshagwe Crew) Oct 18, 2010
Ziara ya Mama Salma Kikwete- Rukwa
MAISHA BILA UONI YANAWEZEKANA!
JAKAYA KIKWETE ALIPOITEKA KAWE
-Kaongozana na Juma Othman Juma
- Waiaga CUF na kuchukua kadi za CCM
- Waahidi wengi zaidi wanakuja nyuma yao visiwani humo
Wakongwe wawili wa siasa za vyama vingi visiwani Zanzibar Mheshimiwa Fatma Maghimbi na Juma Othman Juma wamerudisha kadi zao za CUF na kuchukua za CCM leo jimboni Kawe jijini Dar es salaam na kuahidi wenzao wengi watafuata nyayo zao kutoka CUF.
Akielezea sababu zake za kurudi CCM, Juma Othman Juma amesema ameguswa kwa kazi kubwa aliyofanya Mheshimiwa Kikwete Tanzania Bara na Visiwani hususan aliporejesha amani na utulivu visiwani Unguja na Pemba kipindi cha uchaguzi mkuu wa mwaka huu.
Alisema tangu historia ya vyama vingi ianze Tanzania, kila wakati wa uchaguzi wananchi wengi wa visiwa vya Unguja na Pemba hulazimika kukimbia visiwani humo kwa kuhofia hali ya kutokuwa na usalama katika kipindi hicho.
"Lakini sasa napenda kumshukuru sana Mheshimiwa Kikwete kwa kurudisha heshima ya nchi yetu duniani kwani mwaka huu wa kampeni, hakuna hata mmoja aliyehama visiwani humo kukimbia uchaguzi" alimaliza Juma Othman akishangiliwa na umati mkubwa wa wana CCM waliojitokeza kwenye mkutano huo wa kampeni.
Mama Fatma Maghimbi amewahi kuwa waziri kivuli wa Katiba na Sheria ndani ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akiwa kama mbunge wa Chama Cha Wananchi CUF. Naye Juma Othman Juma amewahi kuwa muanzilishi wa Chama Cha Siasa visiwani kabla ya kujiunga na Chama cha Wananchi CUF.
Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama cha Mapinduzi CCM Mh. Jakaya Kikwete akimnadi Mama Kizigha, mgombea ubunge wa CCM jimbo la kawe leo kwenye mkutano wa kampeni uliofanyika kwenye viwanja vya Tanganyika Parkers jijini Dar es salaam. Uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge, na Madiwani unatarajiwa kufanyika Oktoba 31 mwaka huu nchini kote. (Picha na Muhidin Issa Michuzi) |
Bw. Juma Othman Juma akiwa na Mama Fatma Maghimbi baada ya kurejesha kadi za CUF na kupewa za CCM leo. | sehemu ya nyomi uwanja wa Tanganyika Packers, Kawe, jijini Dar leo |
Oct 17, 2010
CHAMA CHA MAWAKILI TANZANIA KUSHIRIKI UANGALIZI UCHAGUZI MKUU OKTOBA 31 2010
YANGA WATUA DAR KWA SHANGWE
Beki mahiri wa timu ya Yanga na timu ya Taifa Taifa Stars Nadir Haroub (Cannavaro) akihojiwa na vyombo mbalimbali vya habari kwenye uwanja wa ndege wa Mwalimu J.K.Nyerere leo mara baada ya timu hiyo kuwasili ikitokea mkoani Mwanza ambako ilicheza mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom kati yake na watani wao wa jadi timu ya Simba zote za jijini Dar es salaam. Katika mchezo huo Mchezaji Jerrison Tegete ndiye aliyefunga goli katika dakika ya 71 kipindi cha pili ambapo kwa mujibu wa mtangazaji wa TBCEnock Bwigane aliyekuwa akitangaza mchezo huo Jerry Tegete akiwa na mpira alimuita golikipa wa Simba Juma K. Juma na kumwambia "Poooooooooooooooooooooo!!!!" wakati kaseja akishanga jina hilo ndipo tegete akafunga goli safi lililoipa ushindi timu hiyo ya Jangwani na matokeo kuwa Yanga 1-Simba 0. Oct 16, 2010
DK BILAL ALIPOUNGURUMA BABATI, MBULU NA KARATU





WAZIRI MKUU MIZENGO PINDA ATEMBELEA HOSPITALI ZA MUHIMBILI NA OCEAN ROAD.
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akimtazama Winter Isaac (3) ambaye ni mmoja wa watoto waliolazwa kwenye Taasisi ya Saratani ya Ocean Road jijini Dar es salaam wakati alipotembelea Taasisi hiyo Oktoba 15, 2010. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akisalimiana na waganga na wauguzi wa wodi ya watoto kwenye hospitali ya taifa ya Muhimbili pamja na baadhi ya watumishi wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii wakati alipotembelea hospitali hiyo kukagua wodi ya wazazi na watoto Oktoba 15, 2010. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu) MAPACHA WA3 WAZINDUA "JASHO LA MTU" KWA MBWEMBWE TRAVELTINE!
Mkurugenzi wa ASET Asha Baraka ambaye alikuwa mgeni rasmi akizindua rasmi albam ya kundi la Mapacha WA3 inayoitwa Jasho la Mtu katika uzinduzi wa nguzu uliofanyika kwenye hoteli ya Traveltine Magomeni jijini Dar es salaam, kundi la Mapacha WA3 linaundwa na Mwanamuziki Josse Marra kutoka FM Academia, Kalala Junior na Harid Chokoraa. Katika picha kulia ni Bw. Ahmed Magoma na kushoto mwisho ni Bw. Bitusi Mkurugenzi wa B2C Transport katikati ni Masoud Wanani Mkurugenzi wa CDS wakishuhudia uzinduzi huo.
Mwimbaji Harid Chokoraa akionyesha uwezo wake katika kucheza wakati wa onesho la uzinduzi wa albam yao inayoitwa Jasho la Mtu kundi hilo la Mapacha wa3 lilikonga nyoyo za mashabiki na kuwakuna vilivyo usiku wa kuamkia leo kwenye hoteli ya Travltine Magomeni jijini Dar es salaam kulia ni Kalala Junio na kushoto ni Josse Marra.
Mzee Yusuf mwimbaji wa muziki wa Taarab na Kiongozi wa bendi ya taarab ya Jahazi Molden Taarab akiimba huku akiwa amezungukwa na vimwana jukwaani wakati aliposhiriki katika uzinduzi wa albam ya Mapacha wa3 inayoitwa Jasho la Mtu.
Mamaa Monica kushoto naye akajimwaga stejini na rafiki yake huku mzee akiwa jukwaani akifanya mambo makubwa.
Vijana Twende Kazi! Mwanamuziki wa FM Academia Josse Mara akiongoza wanenguaji pamoja na wanamuziki wenzake wanaounda kundi la Mapacha wa3 katika kuzindua albam yao ya Jasho la Mtu ulifanyika usiku wa kuamkia leo kwenye hoteli ya Traveltine Magomeni jijini Dar es salaam ukisindikizwa na bendi ya African Stars na Mzee Yusuf kutoka Jahazi Molden Taarab.
Huyu alikuwa mjamzito lakini yeye akaamua kuja kwenye onesho la mapacha watatu na hatimaye akawazaa mapacha watatu palepale Traveltine Magomeni ambao ni Josse Mara wa FM Academia, Harid Chokoraa na Kalala Jujior ambao jana walizindua albam yao ya Jasho la Mtu.
Rapa wa bendi ya Frican Stars anayeitwa Furgason akicheza na mmoja wa wanenguaji wa bendi ya African Stars jana usiki wakati wa onesho la uzinduzi wa albam ya Jasho la Mtu. 















