Sep 20, 2010

Eric Shigongo aleta Chuo Kikuu mtaani!!

Mwalimu wa Kimataifa wa somo la Ujasiriamali, Eric James Shigongo amesogeza elimu nyumbani kwako na kukupa mafundisho yenye hadhi ya Chuo Kikuu cha Mtaani.
Shigongo atazindua CD inayoitwa Street University (Chuo Kikuu cha Mtaani) hivi karibuni, lengo likiwa kuwawezesha watu mbalimbali kujifunza somo la Ujasiriamali. Akizungumza na gazeti hili wikiendi iliyopita, Shigongo alisema kuwa ameamua kutoa CD hiyo ili kutoa fursa pana kwa wajasiriamali chipukizi kujifunza mbinu mbalimbali za kunufaika kibiashara. “Ndani ya CD hiyo natoa elimu bora kabisa. Elimu ya kuwawezesha kuwa wafanyabiashara wakubwa. Elimu ya kuwakomboa Watanzania katika mambo ya kiuchumi,” alisema Shigongo na kuongeza: “Nahitaji kuzalisha mabilionea wengi kadiri inavyowezekana, kwahiyo Watanzania wenye kiu ya kutaka kuwa mabilionea, wanaweza kunufaika kupitia CD yangu.” Shigongo aliendelea: “Watu wajiandae kuipata hivi karibuni. Itapatikana kwenye maduka ya Zizzou Fashions.” "Great achievement, involves great risks" Abdallah Mrisho www.abdallahmrisho.blogspot.com

Rais Kikwete Katika mazishi ya Julius Msekwa Dar es Salaam!!

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiweka saini katika kitabu cha maombolezo wakati alipokwenda kuifariji familia ya Marehemu Julius Msekwa ambaye ni mtoto wa Makamu mwenyekiti wa CCM Bara Pius Msekwa nyumbani kwao Bongoyo Oysterbay, jijini Dar es Salaam jana jioni.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akitoa heshima za mwisho kwa marehemu Julius Msekwa ambaye ni mtoto wa Makamu Mwenyekiti wa CCM Bara Pius Msekwa wakati wa ibada ya mazishi iliyofanyika nyumbani kwa wazazi wa marehemu , Bongoyo Oysterbay jijini Dar es Salaam jana jioni.Marehemu Julius Msekwa aliyefariki wiki iliyopita huko Nicosia Cyprus ambapo alikuwa akifanya kazi ya mtaalamu Mshauri bingwa katika fani ya teknolojia ya Mawasiliano, alizikwa jana katika makaburi ya Kinondoni jijini Dar es Salaam.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete,(wapili kushoto) Makamu Mwenyekiti wa CCM Bara Pius Msekwa(kushoto) na mkewe Mama Anna Abdallah(watatu kushoto) pamoja na Rais mstaafu awamu ya tatu Mzee Ali Hassan Mwinyi(kulia) wakishiriki ibada ya mazishi ya kumuombea Marehemu Julius Msekwa aliyefariki huko Nicosia Cyprus wiki iliyopita na kuzikwa jana katika makaburi ya Kinondoni jijini Dar es Salaam.(picha na Freddy Maro).

WILLBROAD SLAA KATIKA KAMPENI WILAYANI SIHA

Mgombea urais wa Tanzania kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Willibrod Slaa, akimnadi mgombea ubunge katika jimbo la Hai kupitia chama hicho, Freeman Mbowe, wakati wa mkutano wa kampeni zilizofanyika Bomang'ombe mjini jana. (Picha na Joseph Senga)
Waendesha pikipiki wakiwa katika maandamano ya msafara wa mghombea urais wa TanzaNia kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Willibrod Slaa, kuelekea katika mikutano yake ya kampeni katika jimbo la Hai mkoani Kilimanjaro jana. (Picha na Joseph Senga)
Mwasisi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Edwin Mtei, akiwahutubia wanachi wa Siha mkoani Kilimanjaro, wakati wa mkutano wa mgombea urais wa Tanzania kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Willibrod Slaa (kulia) juzi. (Picha na Joseph Senga)

PPF Stakeolders Conference cocktail at Naura Springs Arusha!!

NBC Marketing Manager Mr. William Kallaghe speaking during a cocktail hosted in Arusha recently. The Bank hosted the cocktail for the 20th PPF Stakeolders Conference.(left) is NBC MD Mr. Lawrence Mafuru.

NBC MD Mr. Lawrence Mafuru (left) speaking to guests during a cocktail hosted by the bank at Naura Springs Hotel in Arusha during the recently concluded 20th PPF stakeholders’ conference

Participants of the 20th PPF Stakeholders Conference chat during a cocktail hosted by the National Bank of Commerce in Arusha recently.

Participants of the 20th PPF Stakeholders Conference chat during a cocktail hosted by the National Bank of Commerce in Arusha recently.

President Kikwete opens the African Court on Human and Peoples' Rights 18th Session n Dar es Salaam!!

The President of the African Court on Human and People’s Rights Jean Mutsinzi escorts President Jakaya Mrisho Kikwete out of the Golden tulip hotel in Dar es Salaam shorly after President Kikwete opened the 18th Ordinary Session of the African Court on Human and People’s Rights this morning.
President Jakaya Mrisho Kikwete in a group picture with Judges of the African Court On huma and People’s Rights shortly after the opening of the Court’s 18th Ordinary Session held the Golden Tulip Hotel in Dar es Salaam this morning.
President Jakaya Mrisho Kikwete in a group picture with Judges of the African Court On huma and People’s Rights shortly after the opening of the Court’s 18th Ordinary Session held the Golden Tulip Hotel in Dar es Salaam this morning.

BAHATI NASIBU YA KUSISIMUA SUPA PESA YAZINDULIWA RASMI NCHINI!

Bahati nasibu ya kipekee inayojulikana kama SUPA PESA itakayowawezesha watumiaji wa simu kujishindia mamilioni ya pesa kila siku imezinduliwa rasmi nchini jana.

Akiongea kwenye uzinduzi wa bahati nasibu hiyo mkurugenzi wa Supa pesa Bwana Harm Fourie alisema “SUPA PESA ni bahati nasibu inayohusisha ujumbe mfupi wa simu ambayo ni kama mchezo utakaowawezesha wahusika kubahatisha kushinda zawadi za pesa, vocha na nyinginezo nyingi kirahisi tu kwa kutuma ujumbe mfupi wa simu. Kutakuwa na droo na zawadi za kila siku na ya kila wiki itakayowawezesha wateja kushindania zaidi ya tshs milioni 25 kila wiki.

Supa Pesa inahusisha watumiaji wa simu wa mitandao yote ambayo ni Zain, Tigo, Vodacom na Zantel kwa gharama ya Tshs 500 tu. Baada ya kutuma ujumbe mfupi, mhusika atatumiwa ujumbe wa kumuidhinisha kushiriki kwenye droo. Baada ya hapo mitambo ya kisasa kabisa inachagua washindi bila mpangilio maalumu.

Mr Fourie aliongeza kusema “Supa Pesa itajikita kuisaidia jamiii haswa kwenye maswala ya elimu. Tunaelewa kwamba serikali ina changamoto kubwa sana kwenye hili swala na tunaamini kuwa elimu ina mchango mkubwa sana katika maendeleo ya jamii. Tunapenda kujihusisha moja kwa moja kwenye kutoa mchango utakaoleta mabadiliko katika maisha ya watanzania.

Msemaji mkuu wa Supa Pesa Nancy Sumari alinukuliwa akisema “kutakuwa na droo za kila siku kuanzia Jumatatu mpaka Ijumaa ambapo washindi watatu watajinyakulia Tshs milioni 1 kila siku. Washindi hao watajulishwa ushindi wao kupitia ujumbe mfupi wa simu na watatumiwa hela zao ndani ya masaa 24 kupitia huduma ya malipo ya Mpesa kutoka Vodacom. Pia kutakuwa na droo ya kila Ijumaa itakayohusisha wale wote waliotuma zaidi ya SMS nne (4) katika wiki hiyo,mshindi atajinyakulia Tshs. Milioni Kumi. Mshindi huyu wa wiki atapigiwa simu kupitia redio ya Clouds FM kujulishwa kuhusu ushindi wake. Dhumuni kubwa ni kuhakikisha tunawafurahisha wateja wetu kwa kutajirisha maisha ya watu wengi kwa kutoa washindi wengi kila wiki. Bahati nasibu hii ni rahisi sana kushiriki hivyo tunawahimiza watanzania wengi washiriki na kushinda na SUPA PESA!“

Supa pesa imepanga kwenda na wakati na kujumuisha mambo mbalimbali ya kufurahisha kwenye kuendesha mchezo huu ili kuhakikisha kuwa inawaridhisha wateja wake kwa kutajirisha na kubadilisha maisha yao.

MWAMVITA MAKAMBA AWAPA SOMO WAHITIMU WA JITEGEMEE SEKONDAR!!

Mkurugenzi wa Mahusiano wa Vodacom Tanzania Mwamvita Makamba akimkabidhi Mwanafunzi Anyelwisye Mwakibinga cheti cha kutambuliwa kama kiongozi bora wa Scout katika shule ya JKT Jitegemee kwenye mahafali ya 26 ya kidato cha nne shuleni hapo, wanaoshuhudia kulia ni Kaimu Mkuu wa shule hiyo Meja Michael Mtenjele na katikati ni Mwenyekiti wa Bodi ya shule Raymond Mpazi.
Baadhi ya wanafunzi wavulana wa JKT Jitegemee wa kidato cha Nne walioshiriki katika mahafali ya 26 yaliyofanyika mwishoni mwa wiki shuleni hapo.
Baadhi ya wanafunzi wasichana wa JKT Jitegemee wa kidato cha Nne walioshiriki katika mahafali ya 26 yaliyofanyika mwishoni mwa wiki shuleni hapo.

Mkurugenzi wa Mahusiano wa Vodacom Tanzania Mwamvita Makamba akimkabidhi Mwanafunzi Mwanahawa Amiry cheti pamoja na zawadi kwa kufanya vizuri katika kipaji cha kucheza ngoma za asili katika shule ya JKT Jitegemee kwenye mahafali ya 26 ya kidato cha nne yaliyofanyika mwishoni mwa wiki shuleni hapo, katikati ni Mwenyekiti wa Bodi ya shule hiyo Raymond Mpazi.

. Mkurugenzi wa Mahusiano wa Vodacom Tanzania Mwamvita Makamba akimkabidhi Mwanafunzi Anyelwisye Mwakibinga cheti cha kutambuliwa kama kiongozi bora wa Scout katika shule ya JKT Jitegemee kwenye mahafali ya 26 ya kidato cha nne shuleni hapo, wanaoshuhudia kulia ni Kaimu Mkuu wa shule hiyo Meja Michael Mtenjele na katikati ni Mwenyekiti wa Bodi ya shule Raymond Mpazi.

Tanzania imepewa Tuzo ya Umoja wa Mataifa ya Millenium Development Goals (MDGs) 2010 !!

Tanzania imepewa Tuzo ya Umoja wa Mataifa ya Millenium Development Goals (MDGs) 2010 : The Global Heabeat kutokana na mafanikio makubwa iliyoyapata katika maendeleo ya Elimu katika sherehe zilizofanyiaka kwenye ukumbi wa Waldorf Astoria Grand Ballroom jijini New York Septemba 19, 2010. Pichani Waziri Mkuu Mizengo Pinda akipokea tuzo hiyo na kutoka kwa Mmoja wa wasimamizo wa shughuli hiyo na Msanii maarufu , John Schneder. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Tanzania imepewa Tuzo ya Umoja wa Mataifa ya Millenium Development Goals (MDGs) 2010 The Global Hearbeat kutokana na mafanikio makubwa iliyoyapata katika maendeleo ya Elimu katika sherehe zilizofanyiaka kwenye ukumbi wa Waldorf Astoria Grand Ballroom jijini New York Septemba 19, 2010. Pichani Waziri Mkuu Mizengo Pinda na Balozi wa Tanzania kwenye umoja wa mataifa, Ombeni Sefue wakiwa wameshika tuzo hiyo baada ya kukabidhiwa: . (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akiwa na Naibu Katibu Mkua Umoja wa Mataifa, Dk. Asha Rose Migiro kabla ya mazungumzo yao kwenye hoteli ya Intercontinental jijini New York Septemba 19, 2010. Mheshimiwa Pinda yuko New York kumwakilisha Rais Jakaya Kikwete katika Mkutano wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa linalojali Maendeleo ya Millenia. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

Ridhiwani katika kampeni Masasi na Nanyumbu!!

Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji ya Baraza la Umoja wa Vijana Taifa, Ridhiwani Kikwete, akihutubia wakati wa mapokezi alipokuwa akiingia wilayani Masasi, Mtwara juzi..(PICHA NA RICHARD MWAIKENDA)
Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji ya Baraza la Umoja wa Vijana Taifa, Ridhiwani Kikwete, akiwaongoza baadhi ya makada wa CCM, kusalimiana na wanachama wa chama hicho, walipowasili katika ofisi za CCM, wilayani Nanyumbu,juzi kuanza vikao vya ndani vya kuweka mikakati ya ushindi kwa CCM katika Uchauzi Mkuu Oktoba 31, mwaka huu.Kutoka kushoto ni Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya tawi la CCM, London, Uingereza, Haruna Mbeyu na Omar Matulnga ambaye ni miononi mwa wadau wa chama hicho.
Sehemu ya umati wa watu ulojitokeza kumlaki,Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji ya Baraza la Umoja wa Vijana Taifa, Ridhiwani Kikwete, alipowasili Masasi, Mtwara juzi , kuanza ziara kuhamasisha vijana kupanga mikakati ya ushindi wa kishindo kwa CCM..(PICHA NA RICHARD MWAIKENDA)
Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji ya Baraza la Umoja wa Vijana Taifa, Ridhiwani Kikwete (katikati) akiwa na baadhi ya wanachama wa CCM, alipotembelea juzi nyumba aliyoishi yeye na babake, Rais Jakaya Kikwete mwaka 1988 mjini Masasi, ambaye wakati huo alikuwa Katibu wa CCM wa Wilaya hiyo.
Waendesha pikipiki, wakiwa wamejipanga wakati wa kumlaki,Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji ya Baraza la Umoja wa Vijanawa CCM Taifa, Ridhiwani Kikwete, wakijiandaa kuonoza msafara wa kiongozi huyo wa vijana,alipoanza ziara ya kampeni jana wilaya ya Masasi, Mtwara juzi..(PICHA NA RICHARD MWAIKENDA)

MASHINDANO YA VODACOM LATHAM OPEN 2010 YAFANA HUKO SINDA KISIWANI!!

Washiriki wa mashindano ya kuvua samaki ya Vodacom Lathan Open 2010 waliokuwa wakiendesha boti ya Natasha wakishangilia kwa kunyoosha vidole vyao juu mara baada ya kukabidhiwa zawadi zao za ushindi wa kuvua samaki wengi zaidi, mashindano hayo yamefanyika jana kwenye kisiwa cha Sinde kwenye Bahari ya Hindi, kushoto ni Necta Foya Meneja wa Mawasiliano Vodacom Tanzania.

Bw. David Sutton wa boti ya uvuvi ya Simba kulia akionyesha zawadi yake aliyoipokea kutoka kwa Mkuu wa Udhamini wa Vodacom Tanzania George Rwehumbiza mara baada ya boti yao kuwa miongoni mwa washindi wa jumla walioshinda kuvua samaki wengi zaidi katika mashindano ya Vodacom Lathan Open 2010 yaliyofanyika kwenye kisiwa cha Sinda jana, kushoto ni Necta Foya Meneja wa Mawasiliano Vodacom Tanzania.

Wafanyakazi wa Yachit Club ya jijini Dar es salaam wakiwapima samaki uzito rekodi mbalimbali za boto zilizoshiriki kwenye mashindano ya uvuvi ya Vodacom Latham Open 2010 yaliyofanyika kwenye kisiwa cha Sinda jana, mara baada ya mashindano Club hiyo huuza samaki hao kwa mnada na fedha zinazopatikana kupelekwa katika kusaidia watu wenye matatizo mbalimbali nchini.
Baadhi wa washiriki wakirejea mara baada ya kufanya uvuvi.
Hizi ni baadhi ya boti za uvuvi zilizoshiriki kwenye mashindano ya Vodacom Latham Open 2010 zikiwa zimeegeshwa ufukweneni mwa bahari ya Hindi huko katika kisiwa cha Sinda.

Sep 18, 2010

Pinda Amwakilisha JK Umoja Wa Mataifa.


Waziri Mkuu Mizengo Pinda na mkewe Mama Tunu Pinda wakizungumza na Balozi wa Tanzania umoja wa Mataifa Ombeni Sefue (kushoto) na Balozi wa Tanzania nchini Marekani Mwanaidi Maajar baada ya kuwasili kwenye uwanja wa ndege wa JFK jijini New York leo kumwakilisha Rais Jakaya Kikwete katika Mkutano wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa kuhusu Maendeleo ya Millenia. (Picha:Ofisi ya Waziri Muu)

TUME YA HAKI ZA BINADAMU NA UTAWALA BORA KUENDELEA KULINDA HAKI ZA WATOTO NCHINI!!

Na. Mary Kweka – MAELEZO.

Dar es Salaam.

Tume ya haki za Binadamu na Utawala bora imesema itaendelea kulinda, kutetea , na kushughulikia malalamiko mbalimbali ya uvunjwaji wa Haki za binadamu kwa watoto nchini.

Kauli hiyo ilitolewa jana Jijini Dar es salaam na Mwenyekiti wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora Jaji Kiongozi Mstaafu Ramadhani Manento wakati akizungumza na viongozi wa mabaraza ya watoto waliofanya ziara ofisi kwake ikiwa ni sehemu ya kongamano lao la mwaka huu linalomalizika leo ( jumamosi) jijini Dar es salaam.

Alisema ili kujenga taifa bora lenye maadili , jamii inao wajibu mkubwa wa kuhakikisha kuwa watoto wanalindwa na kuthaminiwa pamoja na kupatiwa mahitaji mbalimbali yakiwemo Elimu, Malazi bora, haki ya kupendwa, uhuru wa kucheza na kutoa maoni.

Aliongeza kuwa katika kulinda na kutetea haki za watoto, Serikali kupitia tume ya haki za binadamu na Utawala Bora imeanzisha Dawati la watoto ambalo linawajibika na kupokea malalamiko mbalimbali ya uvunjwaji wa haki za biadamu kwa watoto.

“Dawati la watoto linawajibika kulinda na kutetea haki za watoto wanaoishi katika mazingira magumu, walioachishwa shule,matatizo ya miradhi, utekelezaji wa sheria ya ubakaji wa watoto kwa watuhumiwa na mazingira ya watoto walio magerezani “Alifafanua Jaji Manento.

Aliendelea kufafanua kuwa Dawati hilo linatoa elimu kwa watu hasa wazazi kutambua umuhimu wa haki za watoto na kuwa makini pale wanapotoa adhabu kwa watoto huku akitoa angalizo kwa wazazi kuwa makini na adhabu hizo kuwa ziwe na vikomo na si zakuwajeruhi watoto na kuwasababishia ulemavu na kuwapotezea maisha.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Utafiti na Nyaraka wa tume hiyo Bi Epifania Mfundo alisema mwaka huu dawati la watoto limepokea jumla ya malalamiko 114 mpaka sasa, na wamefanikiwa kushughulikia malalamiko 28 kati ya 114 yaliyowasilishwa kwenye tume ya haki za binadamu na utawala bora.

“ Tunapokea malalamiko mbalimbali kupitia watoto wenyewe, taasisi mbalimbali,wazazi, vyombo mbalimbali vya habari,na tunapotembelea na kukagua Magereza na vituo vya Polisi kuangalia hali ya watoto walioko sehemu hizo”, alifafanua Bi Mfundo

Rais Kikwete katika kampeni Mbulu na Babati!!

Mgombea Urais kwa tiketi ya CCM Dr.Jakaya Mrisho Kikwete akiwapungia maelfu ya wakazi wa mji wa Babati wakati wa mkutano mkubwa wa Kampeni uliofanyika mjini Babati jana jioni(Picha na Freddy Maro)
mgombea urais kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi Dr.Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na wananchi wa Haydom, mkoani Manyara muda mara alipowasili katika mkutano wa Kampeni jana mchana,
Mgombea Urais kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi Dr.Jakaya Mrisho Kikwete akiongea na mwanafunzi Nicholaus Haba wa shule ya sekondari Dongobesh muda mfupi baada ya Rais Kikwete kuhutubia wananchi wa Kata ya Dongobesh wilayani Mbulu jana asubuhi.

Sep 17, 2010

Mrembo Julieth kuwakilisha Tanzania katika shindano la Miss Progress Italia!


Na Mwandishi Wetu MREMBO Julieth William aliyeshika nafasi ya tatu katika mashindano ya Miss Tanzania 2009, ameteuliwa kuiwakilisha Tanzania katika mashindano ya dunia ya Miss Progress International yatakayofanyika nchini Italia Septemba 26 mwaka huu. Mrembo huyo aliyetarajiwa kuondoka nchini jana jioni kuelekea nchini Italia kwa ajili ya kinyang’anyiro hicho alikabidhiwa bendera jana na Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) Aloyce Nzuki. Akizungumza baada ya kukabidhiwa bendera, mrembo huyo alisema aliteuliwa na waandaaji wa mashindano hayo kupitia mtandao wa mashindano ya Miss Tanzania na kwamba Tanzania inashiriki mchuano huo kwa mara ya kwanza mwaka huu. Alisema kabla ya kushiriki watakuwa kambini kwa wiki mbili na yeye kama mwakilishi wa Tanzania ana jukumu la kuutangaza utalii wa ndani ya nchi kupitia Utamaduni. “Nimefarijika kuwakilisha nchi kupitia mashindano haya kwani hii ni mara ya kwanza kwetu kushiriki hivyo ni changamoto kubwa kwangu binafsi na nchi kwa ujumla,” alisema. Alisema ana imani ataiwakilisha vyema Tanzania na ushiriki wake katika mashindano hayo utaweza kuchangia kwa kiasi kikubwa ongezeko la watalii na pato la taifa kwa ujumla. Kwa upande wake Nzuki alisema TTB inajivunia ushiriki wa mrembo huyo katika mashindano hayo ya utalii ya ngazi ya kidunia kwani pamoja na mambo mengine mrembo husika atakuwa balozi mzuri wa kazi za bodi hiyo katika kuutangaza utalii wa ndani. Alisema waandaaji wameifanya Tanzania iendelee kusomeka vizuri katika soko la utalii duniani na kwamba kuchaguliwa kwa mwakilishi huyo ni kitu cha kujivunia kwani ni nchi chache za kiafrika zinazoshiriki mashindano hayo. Mashindano hayo ambayo yanaandaliwa na Taasisi ya Miss Progress International ya Italia yanafanyika kwa mara ya tatu tangu kuanzishwa kwake na yanashirikisha warembo kutoka nchi 60 tofauti duniani zikiwemo sita za Afrika ambazo ni Tanzania, Kenya, Uganda, Ethiopia,Algeria na Nigeria

Nape Nape Nnauye ateuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Masasi

Benjamin Sawe

Maelezo

Dar es Salaam

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amemteua ndugu Nape Moses Nnauye kuwa Mkuu wa Wilaya ya Masasi Mkoani Mtwara.

Bwana Nnauye amechukua nafasi ya aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Masasi Said Ali Amanzi ambaye amebadilishiwa kituo chake cha kazi na kuhamishiwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana mkoani Mwanza.

Kabla ya uteuzi huo Ndugu Nnauye alikuwa ni Katibu Msaidizi Idara ya Siasa na Mahusiano ya Kimataifa CCM Makuu Dar es Salaam wakati Bwana Said Ali Amanzi amechukua nafasi ya Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana Ndugu Cleopas Rugarabamu ambaye alifariki mwezi Julai mwaka huu akiwa kwenye matibabu nchini India.

SERIKALI KUNUNUA MAHINDI YA WAKULIMA- AGIZO LA RAIS JAKAYA KIKWETE!

NA MAGRETH KINABO – MAELEZO

SERIKALI imetoa sh. bilioni 23.8 kwa ajili ya kununua mahindi tani 200,000 kutoka kwa wakulima wa ili kuweza kuyahifadhi katika Hifadhi ya Taifa kwa ajili ya matumizi ya baadae, vikiwemo vifaa vingine kama vile ni mizani , dawa za kufukuzia wadudu na mashine.

Kauli hiyo ilitolewa jana na Waziri wa Kilimo Chakula na Ushirika, Stephen Wasira jijini Da res Salaam jana(leo) ambapo alisema Rais Jakaya Kikwete ameagiza tani 400, 000 za mahindi zinunuliwe ikiwa ni lengo la Serikali katika kuyahifadhi mahindi hayo ambayo uzalishaji wake umeongezeka katika kipindi cha mwaka .

“ Serikali imeshatoa fedha hizo ili kuweza kununua tani hizo katika kipindi cha msimu huu”alisema Waziri Wasira huku akifafanua kwamba tayari serikali imeshanunua tani za mahindi 52,000 katika kipindi cha msimu huu hivyo ifikapo mwisho wa mwezi huu ambazo tani za mahindi 105,000 za mahindi zitakuwa zimenunuliwa na Serikali .

Aliongeza pia Serikali itaomba fedha nyingine sh. bilioni 33 kutoka Hazina kwa ajili ya kununua tani za mahindi nyingine za mahindi 95,000 ili kufikisha lengo la awamu ya kwanza ya ununuaji wa mahindi hayo ambayo jumla yake ni tani 200,000.

Hata hivyo aliongeza kwamba baada ya ununuzi huo watafanya tathimini ili kuweza kufikisha lengo la kununua tani nyingine za mahindi 200,000 zilizobakia kama ilivyoagizwa na Rais Kikwete.

Waziri Wasira alisema hifadhi ya Taifa hivi sasa ya ina tani za 52,000 zilizonunuliwa msimu huu na nyingine tani za mahindi za awali 47,000. Hata hivyo alisema uwezo wake wa kuhifadhi ni tani 240,000.

Akizungumzia kuhusu uzalishaji wa mahindi katika kipindi cha mwaka huu alisema umeongezeka,hivyo hayo ni mafanikio mazuri kutokana na hali ya hewa ilikuwa nzuri.

Alisema katika kipindi cha mwaka huu uzalishaji wa mahindi umeongezeka hadi kufikia tani milioni 4.7 wakati katika kipindi cha mwaka jana ulikuwa tani milioni 3.5.

“ Uzalishaji huu katika kipindi cha mwaka jana ulituwezesha kuwalisha watu milioni mbili wa mikoa yote iiliyokuwa na uhaba wa chakula ya kanda ya Kaskazini bila ya kuagiza chakula toka nje ya nchi au kuomba msaada wa namna hiyo,” alisema Waziri Wasira.

Waziri Wasira alisema tayari wameshafanya maandalizi ya kuagiza mbegu za mahindi tani 20,000, hivyo tani 9000 za mbegu hizo zimeshaagizwa kutoka nchi mbalimbali Tanzania ikiwemo na kampuni zitazipeleka karibu na wakulima. Hhata hivyo alisema mahitaji ya sasa ya mbegu hizo ni tani 30,000.

Kwa upande wa mbolea tani tayari kuna tani 201,000 wakati mahitaji ni tani 385,000, lakini tani nyingine zinaendelea kuagizwa.

Akizungumzia kuhusu ziara aliyoifanya Iran wiki iliyopita, Waziri Wasira alisema itasaidia kutoa ushirikiano katika masuala ya kilimo kati ya nchi hiyo na Tanzania. Hivyo Iran , itawekeza nchini Tanzania kwenye zana na kilimo, umwagiliaji, uongezaji thamani wa mazaokwa kuwekeza viwanda na kufanya utafiti ili kuhamasisha kilimo kwanza katika kukuza viwanda.

uingereza kuipiga tanzania katika bajeti


Waziri wa Fedha na Uchumi Mustafa Mkulo( kulia) akitangaza uamuzi wa Serikali ya Uingereza wa kuchangia katika Bajeti ya Taifa(GBS) kiasi cha bilioni 240 leo mjini Zanzibar . Kushoto ni Naibu Waziri wa Idara inayoshughulikia Misaada ya Kimataifa ya Uingereza (DFID) Stephen O’Brian.Tiganya Vincent-MAELEZO- Zanzibar


Na Tiganya Vincent-MAELEZO- Zanzibar

Serikali ya Uingereza imetoa kiasi cha bilioni 240 sawa na Paundi milioni 103.5 kwa ajili ya kuchangia Bajeti ya Tiafa (GBS) kwa mwaka wa fedha wa 2010/2011.

Kauli hiyo imetolewa leo mjini Zanzibar na Waziri wa Fedha na Uchumi Mustafa Mkulo na Naibu Waziri wa Idara inayoshughulikia Misaada ya Kimataifa ya Uingereza (DFID) Stephen O’Brien.

wakati wakitoa ufafanuzi huo kwa waandishi wa habari mjini Zanibar.

Mkulo alisema kuwa fedha hizo zitasaidia kutekeleza vipaumbele katika kutekeleza maeneo muhimu katika Mpango wa Kukuza Uchumi na Kupunguza Umaskini Tanzania(MKUKUTA).

Kufuatia hali hiyo ameishukuru Uingereza kwa niaba ya Serikali na wananchi wa Tanzania kwa kuendelea kuunga mkono juhudi za kuleta maendeleo ya Watanzania.

Alisema kuwa hali hiyo imejidhihirisha katika miradi mbalimbali ya maendeleo ambayo imekuwa ikifadhiliwa na Uingereza kwa ajili ya kuboresha maisha ya Watanzania wengi.

Mkulo alitaja wafadhili wengine walichangia Bajeti ya mwaka 2010/2011 kuwa ni Denmark Dola milioni 16.3, Finland Dola milioni 18.8, Norway Dola milioni 31.4 na Ireland Dola milioni 14.2.

Aidha aliwahakikishia wafadhili wote wa Tanzania kuwa Serikali itahakikisha kuwa kuna usimamizi mzuri wa misaada na fedha zote zinazotoka kwa wahisani ili kuendelea kujenga imani kwao.

“Napenda kuwahakikishia kuwa wafadhili na wahisani katika Bajeti ya Taifa kuwa fedha zitakazotolewa na wahisani zitatumika katika miradi na malengo yaliyokusudiwa ili kuhakikisha thamani halisi ya fedha zinazotolewa na wahisani”alisistiza Mkulo.

Kwa upande Naibu Waziri wa Idara inayoshughulikia Misaada ya Kimataifa ya Uingereza (DFID) Stephen O’Brien alitoa wito kwa Serikali ya Tanzania kuhakikisha kila kiasi cha fedha zinazotolewa na Uingereza zinatumika katika malengo yaliyokusudiwa ili matokeo yake yaweze kupimika.

THE DON HIMSELF

Karibuni sana kwenye blog hii ya kijamii iliyosheheni makila kitu kuanzia siasa uchumi afya na burudani kwa ujumla wake.uingiapo kwenye blog hii ni mengi ambayo utapata nafasi ya kukutana nayo,kumbuka mawazo yako ndo hasa yanayojenga na kunifanya niwe na ufanisi zaidi.kariiiiiiibuuuuuuuuuuuu saaaaaaaaaaaaaaanaaaaaaaaaa.(THE DJ HIMSELF-JIWE)

Followers

BLOG ZA MARAFIKI

Search This Blog

ZILIZOPITA

DUNIA MUZIMA