Ni globu ya kijamii inayojihusisha na mambo yote ya kijamii,natumaini jamii yangu ya kitanzania itafaidika sana pindi ichukuapo fursa ya kuperuzi kwenye globu hii,dhamira yangu ni kufikisha ujumbe pamoja na kuiburudisha jamii yangu na furaha yangu ni kuona natimiza dhamira yangu kwako.natumaini kuwa wewe utaniunga mkono kwa kile ambacho nataka kukifanya kwa ajili ya jamii yangu ya kitanzania.NASHUKURU KWA KUNIELEWA.
Oct 20, 2010
MWISHO MWAMPAMBA AREJEA NA KUPOKELEWA NA BABA YAKE!
SERIKALI YAIKEMEA TAMWA YAITAKA KUZINGATIA MASHARTI YA USAJILI!
Ismail Ngayonga na Magreth Kinabo
MAELEZO
Dar-Es-Salaam
SERIKALI imekitaka Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania (TAMWA) kuzingatia masharti ya usajili waliopewa na malengo waliyojipangia pasipo kuingilia masuala ya kisiasa nchini, ikiwemo kuzingatia suala la utawala bora.
Hayo yamesemwa leo Jijini Dar-Es-Salaam na Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni na Michezo, Seth Kahumanda wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na tamko (TAMWA) juu ya taarifa ya vyombo vya ulinzi na usalama lilivyotolewa hivi karibuni na Mnadhimu Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi ya Wananchi wa Tanzania( JWTZ ) Luteni Jenerali Abdulrahman Shimbo, utafiti wa taasisi ya Synovate pamoja na REDET.
Kamuhanda alisema kuwa Serikali inashangazwa na Kauli ya Mkurugenzi wa TAMWA, Analilea Nkya kwa kuwa imekwenda kinyume na majukumu ya taasisi hiyo, ambayo ni pamoja na kusaidia waandishi wanawake kujiendeleza kitaaluma ili kushika hatamu ya uongozi katika vyombo vya habari, kubadilisha mfumo wa habari hasi za wanawake na kuwasaidia wanawake Watanzania kujiletea maendeleo.
Aliongeza kuwa TAMWA ni chama cha kitaaluma kama vilivyo vyama vingine, na iwapo kinahitaji kubadili malengo yake kuwa ya 0kisiasa basi hakina budi kuangalia mustakabali wa chama chao na mwelekeo wao na kufuata utaratibu kwa mujibu wa sheria .
“Matamko ya Mkurugenzi wa TAMWA yamevuka mipaka na kwenda nje ya malengo ya TAMWA. TAMWA inatakiwa kuheshimu masharti ya usajili wao na kuyatekeleza,” alisema Katibu Mkuu huyo huku akisisitiza kwamba chama hicho pia kinatakiwa kuheshimu masuala ya utawala bora uliopo nchini kwa kuwa suala la kuheshimu misingi ya utawala bora si la Serikali pekee.
Kwa mujibu wa Kamuhanda alisema kuwa chama hicho bado kinakabiliwa na changamoto mbalimbali za utekelezaji wa malengo yake ikiwemo kuwaendeleza waandishi wa habari wanawake kwa ajili ya kuwapatia ujuzi wa kutosha utakaowawezesha kushika nafasi za uongozi katika vyombo vya habari na sehemu nyinginezo za maeneo ya kazi.
Aidha Kamuhanda aliongeza kuwa Serikali itaendelea kushirikiana na chama hicho, katika malengo yao waliojiwekea.
Akizungumzia kuhusu mwenendo wa vyombo vya habari juu ya mchakato wa Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 31,mwaka huu, Kahumanda alivishukuru baadhi ya vyombo vya habari na wahariri wake kwa kukemea matendo na kauli zinazoashiria kuhatarisha uvunjifu wa amani nchini.
“ Vyombo vya habari vinafanyakazi nzuri katika kuhabarisha wananchi juu ya mchakato wa Uchaguzi Mkuu baadhi yake vimepinga na kukemea waziwazi juu ya vitendo vinavyoashria uvunjifu wa amani kwa mfano kwa kuandika tahariri ninavipongeza kwa kuwa vimeonyesha ujasiri na ninaomba viendelee na msimamo huo kwa sababu amani ndio hazina kubwa ya nchi yetu,” alisisitiza Kamuhanda.
Awali akimkaribisha Katibu Mkuu ambaye alikuwa kwenye ziara ya kuitembelea Idara ya Habari(MAELEZO), Mkurugenzi wa Idara hiyo, Clement Mshana alisema ofisi zaidi zinahitajika kwa ajili ya kuhifadhi picha, machapisho mbalimbali na habari, hotuba za viongozi pamoja na vipindi mbalimbali ambavyo ni vya radio na televisheni ili viweze kutumika katika sehemu za baadae endapo janga la moto likitokea.
Mkurugenzi huyo aliongeza kuwa idara hiyo inaratibu shughuli za tovuti ya wananchi ambapo mpaka sasa wananchi kadhaa wwaliokuwa na kero zao zimewezwa kutatuliwa na kupatiwa majibu kutoka mamlaka husika.
NGWE YA LALA SALAMA:KAMPENI ZA MNYIKA UBUNGO KATA YA SINZA MPAKA BAA!
MISS PROGRESS INTERNATIONAL KUSAIDIA MAPAMBANO DHIDI YA MAUAJI YA MAALBINO
Swahili Fashion Week yazinduliwa rasmi leo
Swahili Fashion Week itawaleta pamoja wabunifu wa mavazi 24 kutoka nchi zinazoongea lugha ya Kiswahili ili kuweza kuonyesha ubunifu wao katika kubuni mavazi ya aina mbalimbali kwa kutumia aina mbalimbali za malighafi.
Wabunifu watakaoonesha mavazi katika Swahili Fashion Week kwa mwaka huu ni pamoja na Ailinda Sawe, Manju Msita, Kemi Kalikawe, Christine Mhando, Shellina Ibrahim, Farha Naaz Sultan, Gabriel Mollel, Robi Morro, Asia Idarous, Zamda George, Khadija Mwanamboka, Jamilla Vera Swai and Made by Afrika. wabunifu kutoka Kenya ni Sonu Sharma, Moo Cow, KiKoromeo, John Kavike na Kooroo, na kutoka Uganda ni mbunifu Stella Atal.
“Pamoja na maonyesho ya mavazi, mwaka huu Swahili Fashion Week itakwenda sambamba na tamasha la maonyesho ya bidhaa mbalimbali zenye asili ya mswahili kutoka mwambao wa Afrika mashariki”. Alisema Mustafa Hassanali muaandaaji y tukio la Swahili Fashion Week.
“Tunafungua milango zaidi kwa ajili ya watazamaji wapya wa Swahili Fashion Week, amboa watapata fursa ya kununua bidhaa mbalimbali. Tamasha hili ambalo linazileta pamoja bidhaa mbalimbali za sanaa na utamaduni wa mswahili, pia litahamasisha ubunifu zaidi katika bidhaa zinazokwenda sambamba na maisha halisi ya jamii ya watu wanaoongea lugha ya Kiswahili kwa kukutana pamoja na kubadilisha mawazo na kujifunza uzoefu mpya katika masuala yanayohusiana na sanaa kwa ujumla.” Aliaongeza Hassanali.
Pamoja na maonyesho, pia kutakuwepo aina tofauti za burudani kutoka kwa vikundi
Mbalimbali vya muziki, uchoraji wa hina, usukaji mikeka, sambamba na semina za aina tofauti zitakazo washirikisha wabunifu wa mavazi.
Aidha Swahili fashion Week imeandaa aina tofauti za zawadi zitakazotolewa mwaka huu kwa lengo la kutambua na kuthamini vipaji vya aina mbalimbali vitakavyooneshwa, ikiwa ni pamoja na zawadi ya mwaka kwa mbunifu anaechipukia.
Swahili fashion week 2010 imedhaminiwa na Home of Swahili Fashion week Southern Sun, Origin Africa, USAID Compete, EATV, East Africa Radio, Malaria Haikubaliki, BASATA (Baraza La Sanaa Tanzania) Ultimate Security, Monier 2000, Colour Print ltd, Global Outdoor Ltd, Amarula, Vayle Springs Ltd, ZG Films, Darling Hair, Danish make up designs, Nipashe, Bilicanas, Perfect Machinery LTD, 1 & 1 internet solutions, Sengi Tours, Ifashion na 361 Degrees.
Oct 19, 2010
YOU ARE RESPONSIBLE FOR YOUR OWN LIFE "PIPI"
The fact that she turned 18 this year....made her feel excited because it would be her first time to vote!!and now she is getting more and more excited about that day, the 31st of October.....
PLEASE TUMIA KURA YAKO PIA TAREHE 31 MWEZI WA KUMI, SIO UKAE UNALALAMIKIA SERIKALI.....
KIDUM, NONINI AND MATONYA LIVE@CLUB VOLTS LONDON FRI 22ND OCT
EAST AFRICAN ARTISTS WITH SWAGGAEST AND FINEST ARTISTS FROM EAST AFRICA..
FEATURING: KIDUM, NONINI, MATONYA
PERFORMANCES FROM UGANDAN UK BASED ARTISTS....ITS KENYA, UGANDA, TANZANIA, BURUNDI, RWANDA....
ON FRIDAY 22 OCTOBER
AT CLUB VOLTS
169-171 FORE STREET EDMONTON, LONDON, N18 2XB
FRO MROE INFO:
07944456643 ED K EDRIS
07533512670 VICTOR
MWALIMU JULIUS KAMBARAGE NYERERE HONORED IN WASHINGTON DC.
DR. GHALIB BILAL KATIKA MIKUTANO YA KAMPENI KILIMANJARO.
Rais Jakaya Kikwete katika kampeni Mkuranga.
WAANGALIZI WA UCHAGUZI MKUU KUTOKA SADC WAWASILI NCHINI.
Oct 18, 2010
Ziara ya Mama Salma Kikwete- Rukwa
MAISHA BILA UONI YANAWEZEKANA!
JAKAYA KIKWETE ALIPOITEKA KAWE
- Waiaga CUF na kuchukua kadi za CCM
- Waahidi wengi zaidi wanakuja nyuma yao visiwani humo
Wakongwe wawili wa siasa za vyama vingi visiwani Zanzibar Mheshimiwa Fatma Maghimbi na Juma Othman Juma wamerudisha kadi zao za CUF na kuchukua za CCM leo jimboni Kawe jijini Dar es salaam na kuahidi wenzao wengi watafuata nyayo zao kutoka CUF.
Akielezea sababu zake za kurudi CCM, Juma Othman Juma amesema ameguswa kwa kazi kubwa aliyofanya Mheshimiwa Kikwete Tanzania Bara na Visiwani hususan aliporejesha amani na utulivu visiwani Unguja na Pemba kipindi cha uchaguzi mkuu wa mwaka huu.
Alisema tangu historia ya vyama vingi ianze Tanzania, kila wakati wa uchaguzi wananchi wengi wa visiwa vya Unguja na Pemba hulazimika kukimbia visiwani humo kwa kuhofia hali ya kutokuwa na usalama katika kipindi hicho.
"Lakini sasa napenda kumshukuru sana Mheshimiwa Kikwete kwa kurudisha heshima ya nchi yetu duniani kwani mwaka huu wa kampeni, hakuna hata mmoja aliyehama visiwani humo kukimbia uchaguzi" alimaliza Juma Othman akishangiliwa na umati mkubwa wa wana CCM waliojitokeza kwenye mkutano huo wa kampeni.
Mama Fatma Maghimbi amewahi kuwa waziri kivuli wa Katiba na Sheria ndani ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akiwa kama mbunge wa Chama Cha Wananchi CUF. Naye Juma Othman Juma amewahi kuwa muanzilishi wa Chama Cha Siasa visiwani kabla ya kujiunga na Chama cha Wananchi CUF.
Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama cha Mapinduzi CCM Mh. Jakaya Kikwete akimnadi Mama Kizigha, mgombea ubunge wa CCM jimbo la kawe leo kwenye mkutano wa kampeni uliofanyika kwenye viwanja vya Tanganyika Parkers jijini Dar es salaam. Uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge, na Madiwani unatarajiwa kufanyika Oktoba 31 mwaka huu nchini kote. (Picha na Muhidin Issa Michuzi) |
sehemu ya nyomi uwanja wa Tanganyika Packers, Kawe, jijini Dar leo |