Oct 20, 2010

MWISHO MWAMPAMBA AREJEA NA KUPOKELEWA NA BABA YAKE!

Mwisho Mwampamba akipokea shada la maua kutoka kwa ndugu zake mara baada ya kuwasili kwenye uwanja wa ndege wa Mwalimu J.K.Nyerere jioni ya leo akitokea Afrika kusini kwa ndege ya shirika la ndege la SAA ambako alishiriki shindano la BigBrother Africa na kushika nafasi ya tatu huku mshiriki Uti kutoka Nigeria akijinyakulia kitita cha Dola laki mbili za Kimarekani.
Mwisho kesho anatarajiwa kutembelea vyombo mbalimbali vya habari na kueleza mambo mbalimbali yaliyojiri kwa muda wote wa miezi mitatu walipokuwa kwenye jumba la Bigbrother na washiriki wenzake na keshokutwa atazungumza na waandishi wa habari jijini Dar es salaam katika picha kushoto ni baba yake mzee Mwampamba.
Mwisho Mwampamba akisindikizwa na ndugu zake pamoja na walinzi wakati alipowasili kwenye uwanja wa ndege wa Mwalimu J.K.Nyerere jioni ya leo akitokea nchini Afrika Kusini alikoshiriki katika shindano la BigBrother Africa Allstars na kushika nafasi ya tatu.
Mwisho mara baada ya kpokelewa akiwa katika usafiri aina ya Lemousine huku akiwa mwenye furaha.
Meneja Masoko wa Multchoice Furaha Samalu kulia akiwa katika pilika za mapokezi na Meneja Utawala wa Kampuni hiyo Tike Mwakitwange.
Mzee Mwampamba kulia ambaye ni baba yake na Mwisho akiwa na baadi ya watoto na ndugu na jamaa wakimsubiri Mwisho huku wakiwa wameshikilia maua.
Anna Kulia na Teddy kutoka Multchoice nao walijumuika katika mapokezi hayo.
Wafanyakazi wa kampuni ya Multchoice wakiwa kwenye uwanja wa ndege wa Mwalimu J.K.Nyerere wakati walipokwenda kumpokea mshiriki wa shindano la Bigbrother All Stars 2010 lililomalizika jumapoili iliyopita huko Afrika Kusini.
(full shangwe)

SERIKALI YAIKEMEA TAMWA YAITAKA KUZINGATIA MASHARTI YA USAJILI!

Ismail Ngayonga na Magreth Kinabo

MAELEZO

Dar-Es-Salaam

SERIKALI imekitaka Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania (TAMWA) kuzingatia masharti ya usajili waliopewa na malengo waliyojipangia pasipo kuingilia masuala ya kisiasa nchini, ikiwemo kuzingatia suala la utawala bora.

Hayo yamesemwa leo Jijini Dar-Es-Salaam na Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni na Michezo, Seth Kahumanda wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na tamko (TAMWA) juu ya taarifa ya vyombo vya ulinzi na usalama lilivyotolewa hivi karibuni na Mnadhimu Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi ya Wananchi wa Tanzania( JWTZ ) Luteni Jenerali Abdulrahman Shimbo, utafiti wa taasisi ya Synovate pamoja na REDET.

Kamuhanda alisema kuwa Serikali inashangazwa na Kauli ya Mkurugenzi wa TAMWA, Analilea Nkya kwa kuwa imekwenda kinyume na majukumu ya taasisi hiyo, ambayo ni pamoja na kusaidia waandishi wanawake kujiendeleza kitaaluma ili kushika hatamu ya uongozi katika vyombo vya habari, kubadilisha mfumo wa habari hasi za wanawake na kuwasaidia wanawake Watanzania kujiletea maendeleo.

Aliongeza kuwa TAMWA ni chama cha kitaaluma kama vilivyo vyama vingine, na iwapo kinahitaji kubadili malengo yake kuwa ya 0kisiasa basi hakina budi kuangalia mustakabali wa chama chao na mwelekeo wao na kufuata utaratibu kwa mujibu wa sheria .

“Matamko ya Mkurugenzi wa TAMWA yamevuka mipaka na kwenda nje ya malengo ya TAMWA. TAMWA inatakiwa kuheshimu masharti ya usajili wao na kuyatekeleza,” alisema Katibu Mkuu huyo huku akisisitiza kwamba chama hicho pia kinatakiwa kuheshimu masuala ya utawala bora uliopo nchini kwa kuwa suala la kuheshimu misingi ya utawala bora si la Serikali pekee.

Kwa mujibu wa Kamuhanda alisema kuwa chama hicho bado kinakabiliwa na changamoto mbalimbali za utekelezaji wa malengo yake ikiwemo kuwaendeleza waandishi wa habari wanawake kwa ajili ya kuwapatia ujuzi wa kutosha utakaowawezesha kushika nafasi za uongozi katika vyombo vya habari na sehemu nyinginezo za maeneo ya kazi.

Aidha Kamuhanda aliongeza kuwa Serikali itaendelea kushirikiana na chama hicho, katika malengo yao waliojiwekea.

Akizungumzia kuhusu mwenendo wa vyombo vya habari juu ya mchakato wa Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 31,mwaka huu, Kahumanda alivishukuru baadhi ya vyombo vya habari na wahariri wake kwa kukemea matendo na kauli zinazoashiria kuhatarisha uvunjifu wa amani nchini.

“ Vyombo vya habari vinafanyakazi nzuri katika kuhabarisha wananchi juu ya mchakato wa Uchaguzi Mkuu baadhi yake vimepinga na kukemea waziwazi juu ya vitendo vinavyoashria uvunjifu wa amani kwa mfano kwa kuandika tahariri ninavipongeza kwa kuwa vimeonyesha ujasiri na ninaomba viendelee na msimamo huo kwa sababu amani ndio hazina kubwa ya nchi yetu,” alisisitiza Kamuhanda.

Awali akimkaribisha Katibu Mkuu ambaye alikuwa kwenye ziara ya kuitembelea Idara ya Habari(MAELEZO), Mkurugenzi wa Idara hiyo, Clement Mshana alisema ofisi zaidi zinahitajika kwa ajili ya kuhifadhi picha, machapisho mbalimbali na habari, hotuba za viongozi pamoja na vipindi mbalimbali ambavyo ni vya radio na televisheni ili viweze kutumika katika sehemu za baadae endapo janga la moto likitokea.

Mkurugenzi huyo aliongeza kuwa idara hiyo inaratibu shughuli za tovuti ya wananchi ambapo mpaka sasa wananchi kadhaa wwaliokuwa na kero zao zimewezwa kutatuliwa na kupatiwa majibu kutoka mamlaka husika.

NGWE YA LALA SALAMA:KAMPENI ZA MNYIKA UBUNGO KATA YA SINZA MPAKA BAA!

Mgombea Ubunge jimbo la Ubungo kwa kupitia CHADEMA Ndugu John Mnyika akiwahutubia wakazi wa Sinza Palestina jijini Dar ves salaam katika mkutano wake wa kampeni uliofanyika Jumapili iliyopita John Mnyika anagombea ubunge katika jimbo la Ubungo.
Mnyika akiwa katika gari kwenye msafara wake wakati alipopita katika mitaa mbalimbali ya Sinza na kusalimiana na wakazi wa Sinza.
Hapa akisalimiana na watu mbalimbali wakati alipokatiza katika moja ya baa zinazouza pombe huko Sinza.

MISS PROGRESS INTERNATIONAL KUSAIDIA MAPAMBANO DHIDI YA MAUAJI YA MAALBINO



Katibu Mtendaji wa BASATA Bw.Materego akisisitiza jambo kwenye Jukwaa la Sanaa ambapo alimpongeza Julieth kwa mpango wake wa kupambana na mauaji dhidi ya maalbino.
Mdau akichangia mada kwenye Jukwaa la Sanaa.Alimshauri Julieth kutokutumbukia kwenye skendo ambazo zimekuwa zikiwakumba baadhi ya warembo nchini.
Sehemu ya wadau wa Jukwaa la Sanaa wakimsikiliza Miss Progress International Julieth William (Hayuko pichani)

****************** ******************* *******************
Na Alistide Kwizela

Mshindi wa Shindano la Urembo la Progress International Julieth William amesema kwamba waandaaji wa shindano hilo lililofanyika nchini Italia hivi karibuni na kushirikisha warembo zaidi ya 50 kutoka mataifa mbalimbali wamemtengea kitita cha Euro 20,000 sawa na shilingi milioni 40 za kitanzania kwa ajili ya kupambana na mauaji dhidi ya walemavu wa ngozi (maalbino)

Akizungumza kwenye Jukwaa la Sanaa Jumatatu hii,Julieth alisema kwamba, fedha hizo amezipata kufuatia kuandika andiko la mradi (proposal) la jinsi ya kupambana na mauaji ya walemavu wa ngozi ambalo lilimpa asilimia 50 za ushindi kwenye shindano hilo.

Alisema kwamba, anasikitishwa na kuumizwa na mauaji dhidi ya binadamu wasio na hatia na kusisitiza kwamba,lazima watanzania wabadilike na kujua kwamba utajiri au mafanikio katika shughuli zao hayapatikani kutokana na viungo vya binadamu bali juhudi katika kazi na kujituma.

Alisema kwamba, mradi wake huo ambao atauendesha kwa kushirikiana na wanaharakati wengine utajikita kwenye maeneo ya kanda ya ziwa ambapo atakuwa akitoa elimu kwa umma,uhamasishaji wa jamii dhidi ya vitendo hivyo, kuunda Kamati ndogondogo chini ya walemavu wa ngozi zitakazokuwa zikifanya kazi ya kuielimisha jamii na mambo mengine mengi.

Aliongeza kwamba,ameshaanza mazungumzo na serikali ili kuona ni kwa jinsi gani atashirikiana nayo katika kufanikisha mradi huo ambao alisema kwa kuanzia utalenga maeneo yaliyoathirika zaidi ambayo ni ya Mikoa ya Mwanza na Shinyanga.

Kuhusu ushindi wake kwenye Shindano hilo la Miss Progress International ambapo aliwabwaga warembo zaidi ya 50 kutoka nchi mbalimbali, alisema ulitokana na yeye kutokukata tamaa,kujenga utamaduni wa kutafuta fursa na kuzitumia ipasavyo,kujituma na kujiamini.

Aliwaasa warembo kutokubweteka na kukata tamaa bali kujenga utamaduni wa kujiamini,kusaka fursa mpya na kuzitumia ipasavyo, kuwa mfano katika jamii kwa kuwa na maadili bora na zaidi kujihusisha na masuala mbalimabali ya kijamii.

Kwa upande wake Katibu Mtendaji wa BASATA,Ghonche Materego alimpongeza Julieth William kwa ushindi wake zaidi wazo lake la kushirikiki vita dhidi ya mauaji ya walemavu wa ngozi na kumueleza kwamba BASATA iko pamoja naye kwani ni mlezi wake.

Alisema kwamba, warembo hawana budi kujifunza kutoka kwenye mafanikio ya Julieth kwani kwa muda mrefu Tanzania pamoja na kupeleka warembo kwenye mashindano mbalimbali ya kimataifa wamekuwa hawafanyi vizuri sana ingawa alisema wamekuwa wakiitangaza nchi kwa kiwango kikubwa.

Wachangiaji wengi kwenye Jukwaa la Sanaa walimpongeza Julieth na kumtakia kila la kheri kwenye mradi wake huo ingawa pia hawakusita kumuonya dhidi ya tabia zisizofaa ambazo zimekuwa zikioneshwa na warembo mara wanapopata mafanikio.

Swahili Fashion Week yazinduliwa rasmi leo



Mbunifu wa Mavazi na Muandaaji wa onyesho la mavazi la Swahili Fashion Week,Mustafa Hassanali akifafanua jambo mbele ya wandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusiana na tamasha hilo katika mkutano na wanahabari hao uliofanyika leo katika hoteli ya Southen Sun jijini Dar.


Muwakilishi wa Hoteli ya Southen Sun,Bi. Judith Muyo akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari kuhusu onyesho la mavazi la Swahili Fashion Week,wengini ni Mustafa Hassanali (katikati),Mratibu wa Mitindo,Bw. Washington (kulia),Afisa habari wa Mustafa Hassanali,Saphia Ngalapi (pili kushoto) na mwisho kabisa ni Alex Galinoma kutoka EATV.


Kwa mara ya tatu sasa Swahili Fashion Week itafanyika Karimjee Hall kuanzi tarehe 4 hadi 6 November 2010, Dar Es Salaam , Tanzania .


Swahili Fashion Week itawaleta pamoja wabunifu wa mavazi 24 kutoka nchi zinazoongea lugha ya Kiswahili ili kuweza kuonyesha ubunifu wao katika kubuni mavazi ya aina mbalimbali kwa kutumia aina mbalimbali za malighafi.


Wabunifu watakaoonesha mavazi katika Swahili Fashion Week kwa mwaka huu ni pamoja na Ailinda Sawe, Manju Msita, Kemi Kalikawe, Christine Mhando, Shellina Ibrahim, Farha Naaz Sultan, Gabriel Mollel, Robi Morro, Asia Idarous, Zamda George, Khadija Mwanamboka, Jamilla Vera Swai and Made by Afrika. wabunifu kutoka Kenya ni Sonu Sharma, Moo Cow, KiKoromeo, John Kavike na Kooroo, na kutoka Uganda ni mbunifu Stella Atal.


“Pamoja na maonyesho ya mavazi, mwaka huu Swahili Fashion Week itakwenda sambamba na tamasha la maonyesho ya bidhaa mbalimbali zenye asili ya mswahili kutoka mwambao wa Afrika mashariki”. Alisema Mustafa Hassanali muaandaaji y tukio la Swahili Fashion Week.


“Tunafungua milango zaidi kwa ajili ya watazamaji wapya wa Swahili Fashion Week, amboa watapata fursa ya kununua bidhaa mbalimbali. Tamasha hili ambalo linazileta pamoja bidhaa mbalimbali za sanaa na utamaduni wa mswahili, pia litahamasisha ubunifu zaidi katika bidhaa zinazokwenda sambamba na maisha halisi ya jamii ya watu wanaoongea lugha ya Kiswahili kwa kukutana pamoja na kubadilisha mawazo na kujifunza uzoefu mpya katika masuala yanayohusiana na sanaa kwa ujumla.” Aliaongeza Hassanali.


Pamoja na maonyesho, pia kutakuwepo aina tofauti za burudani kutoka kwa vikundi


Mbalimbali vya muziki, uchoraji wa hina, usukaji mikeka, sambamba na semina za aina tofauti zitakazo washirikisha wabunifu wa mavazi.


Aidha Swahili fashion Week imeandaa aina tofauti za zawadi zitakazotolewa mwaka huu kwa lengo la kutambua na kuthamini vipaji vya aina mbalimbali vitakavyooneshwa, ikiwa ni pamoja na zawadi ya mwaka kwa mbunifu anaechipukia.


Swahili fashion week 2010 imedhaminiwa na Home of Swahili Fashion week Southern Sun, Origin Africa, USAID Compete, EATV, East Africa Radio, Malaria Haikubaliki, BASATA (Baraza La Sanaa Tanzania) Ultimate Security, Monier 2000, Colour Print ltd, Global Outdoor Ltd, Amarula, Vayle Springs Ltd, ZG Films, Darling Hair, Danish make up designs, Nipashe, Bilicanas, Perfect Machinery LTD, 1 & 1 internet solutions, Sengi Tours, Ifashion na 361 Degrees.

Oct 19, 2010

YOU ARE RESPONSIBLE FOR YOUR OWN LIFE "PIPI"

She loves life...nobody made the happiness she has,she is responsible for her own life.
The fact that she turned 18 this year....made her feel excited because it would be her first time to vote!!and now she is getting more and more excited about that day, the 31st of October.....

PLEASE TUMIA KURA YAKO PIA TAREHE 31 MWEZI WA KUMI, SIO UKAE UNALALAMIKIA SERIKALI.....

KIDUM, NONINI AND MATONYA LIVE@CLUB VOLTS LONDON FRI 22ND OCT

JUNGLE DREAM / BONGO UK PRESENTS
EAST AFRICAN ARTISTS WITH SWAGGAEST AND FINEST ARTISTS FROM EAST AFRICA..

FEATURING: KIDUM, NONINI, MATONYA

PERFORMANCES FROM UGANDAN UK BASED ARTISTS....ITS KENYA, UGANDA, TANZANIA, BURUNDI, RWANDA....
ON FRIDAY 22 OCTOBER
AT CLUB VOLTS
169-171 FORE STREET EDMONTON, LONDON, N18 2XB

FRO MROE INFO:
07944456643 ED K EDRIS
07533512670 VICTOR

MWALIMU JULIUS KAMBARAGE NYERERE HONORED IN WASHINGTON DC.

The 3rd Annual Celebration in Remembrance of the Life and Work of The Father of the Tanzanian Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere was held at the Howard University Towers Auditorium on October 16th 2010.
This event is hosted annually by the Julius K. Nyerere Commemoration, Inc. of Washington DC. JKNC, Inc. is founded and largely sponsored by an African American couple; Ndugu and Mrs. Rick Tingling-Clemmons, whose love for Mwalimu and admiration for his works and philosophy inspired them to organize this worthy event in his name. The theme this year is in concurrence with Mwalimu's core values… "Fighting Poverty, Ignorance and Disease".
Rick and Mama Michele Tingling
H. E., Ambassador Mwanaidi Maajar - third from right; with the event organizers, together with Mr. Suleiman Saleh; Minister Plenipotentiary Political affairs, Tanzania Embassy - second from left, Ms. Khadija Mwanamboka of Tanzania Mitindo House - 3rd from left and Ms. Belinda Mlingo the Mistress of ceremony and JKNC Inc. partner - second from right.

DR. GHALIB BILAL KATIKA MIKUTANO YA KAMPENI KILIMANJARO.

Mgombea Mwenza wa Urais wa CCM, DK. Mohamed Gharib Bilal, akiwahutubia wananchi wa Kata za Bomambuzi na Pasua wakati alipofanya mkutano wa kampeni katika Wilaya ya Moshi mjini Mkoa wa Kilimanjaro jana okt 17. Picha na Muhidin Sufiani
-Mgombea Mwenza wa urais wa CCM, Dk. Mohamed Gharib Bilal, akimnadi mgombhea ubunge wa Jimbo la Moshi Vijijini, Cyril Chami, wakati wa mkutano wa kampeni uliofanyiika leo Okt 18 kwenye uwanja wa Kijiji cha Chekereni Mkoa wa Kilimanjaro. Pichha na Muhidin Sufiani
Mmoja wa wanachama wa chama cha mapinduzi akishangilia huku wenzake wakimuangalia wakati wa mkutano wa Kampeni wa Dr. Ghalib Bilal.
Wanachama na mashabiki wa CCM wa Mtaa wa Sokoni Kata ya Bomambuzi na Pasua, wakimsikiliza mgombea Mwenza wa urais wa CCM. Dk. Mohamed Gharib Bilal, wakati alipofanya mkutano wa kampeni jana Okt 17 katika uwanja wa Sokoni Pasua Wilaya ya Moshi Mjini Mkoa wa Kilimanjaro na kumnadi mgombea Ubunge wa Jimbo hilo, Justine Salakana. Picha na Muhidin Sufiani

Rais Jakaya Kikwete katika kampeni Mkuranga.

Mgombea urais kwa tiketi ya CCM Rais Jakaya Mrisho Kikwete
akiwahutubia wananchi wa jimbo la Mkuranga huko Kimanzichana leo mchana.
Rais Dr.Jakaya Mrisho Kikwete akimnadi mgombea ubunge jimbo la Mkuranga kwa tiketi ya CCM Adam Kighoma Malima wakati wa Mkutano wa kampeni uliofanyika huko Kimanzichana, wilayani Mkuranga leo mchana (picha na Freddy Maro
Mgombea urais kwa tiketi ya CCM akiwa ambeba mtoto wa miaka miwili Asia Ndomondo muda mfupi baada ya kuwasili katika mji wa Kibiti na kuhutubia katika mkutano wa kampeni mjini hap leo
mgombea Urais kwa tiketi ya CCM Dr.Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na wananchi wa eneo la Kimanzichana jimbo la Mkuranga wakati wa mkutano wa Kampeni uliofanyika leo mchana.

WAANGALIZI WA UCHAGUZI MKUU KUTOKA SADC WAWASILI NCHINI.

Mwenyekiti wa waangalizi wa uchaguzi mkuu kutoka Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za kusini mwa Afrika (SADC) ambaye pia ni Waziri wa Mambo ya Nje wa Zambia Kabinga Pande (kulia) akizungumza na wadau mbalimbali wakiwemo viongozi wa siasa, waandishi wa habari na waangalizi wa uchaguzi kutoka SADC juu ya ujio wa ujumbe wa waangalizi hao na majukumu yao wakati wa uchaguzi mkuu utakaofanyika tarehe 31 mwezi huu leo jijini Dar es salaam. Pamoja na mambo mengine ametoa wito kwa watanzania kudumisha amani na kuonyesha ukomavu wa kisiasa uliopo nchini hasa kabla na baada ya uchaguzi. (Picha Aron Msigwa na Fullshagwe Crew)
Baadi yAAa Wanasheria kutoka Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa nao pia walikuwepo.
Baadhi ya Mabalozi na wageni waalikwa mbalimbali waliohudhuria mkutano huo.
Mchungaji Christopher Mtikila ambaye ni Mwenyekiti wa Chama cha Democratic Party DP akiuliza swali kwa waangalizi wa kimataifa wa uchaguzi mkuu kutoka SADC ambao walikutana na waandishi wa habari leo kwenye Hoteli ya Movenpick jijini Dar es salaam.
Washiriki wa mkutano wa ujumbe wa waangalizi wa uchaguzi mkuu kutoka nchi za SADC wakifuatilia masuala mbalimbali leo jijini Dar es salaam.

Oct 18, 2010

Ziara ya Mama Salma Kikwete- Rukwa

Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akiongea 17-10-2010 na wanachama wa UWT jimbo la Nkasi Kusini na Nkasi Kaskazini Moani Rukwa katika mkutano wa ndani wa Kampeni za Uchaguzi Mkuu Oktoba 31 mwaka huu . (Picha na Mwanakombo Jumaa Maelezo)
Wanachama wa UWT Majimbo ya Mpanda Mjini na Vijijini Mkoa Mpya wa Katavi wakimshangilia Mke wa Rais Mama Salma Kikwete 17-10-2010 katika mkutao wa ndani wa Kampeni za Uchaguzi Mkuu Mwaka huu .
Align CenterKikundi cha utamaduni cha kinamama wa Mkoani Rukwa wakimuonyesha umahiri wa kucheza ngoma ya asili katika mkoa huo.(17-10-2010)
Wanacha wa UWT Mkoa wa Rukwa wakimsikliza Mke wa Rais Mama Salma Kikwete katika mkutano wa ndani wa Kampeni za Uchaguzi Mkuu Oktoba 31, Mwaka huu.

MAISHA BILA UONI YANAWEZEKANA!

Katibu Mkuu wa Chama cha Wasioona Tanzania bwana.Emanuel Saimon akichapa risala ya chama chake katika maonesho ya maadhimisho ya siku ya fimbo nyeupe yaliyofanyika kwenye viwanja vya Shycom-Shimyanga.
Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga bi. Amina Masenza akiangalia fundi cherehani bw. Abdala toka wilaya ya Temeke akikata nguo.
Fundi simu ambaye ni mlemavu asiyeoona toka wilaya ya Temeke akitengeneza simu katika maadhimisho hayo.
Fundi simu akiingiza nyimbo katika simu kwa kutumia kompyuta yake .

JAKAYA KIKWETE ALIPOITEKA KAWE

-Kaongozana na Juma Othman Juma

- Waiaga CUF na kuchukua kadi za CCM

- Waahidi wengi zaidi wanakuja nyuma yao visiwani humo

Wakongwe wawili wa siasa za vyama vingi visiwani Zanzibar Mheshimiwa Fatma Maghimbi na Juma Othman Juma wamerudisha kadi zao za CUF na kuchukua za CCM leo jimboni Kawe jijini Dar es salaam na kuahidi wenzao wengi watafuata nyayo zao kutoka CUF.

Akielezea sababu zake za kurudi CCM, Juma Othman Juma amesema ameguswa kwa kazi kubwa aliyofanya Mheshimiwa Kikwete Tanzania Bara na Visiwani hususan aliporejesha amani na utulivu visiwani Unguja na Pemba kipindi cha uchaguzi mkuu wa mwaka huu.

Alisema tangu historia ya vyama vingi ianze Tanzania, kila wakati wa uchaguzi wananchi wengi wa visiwa vya Unguja na Pemba hulazimika kukimbia visiwani humo kwa kuhofia hali ya kutokuwa na usalama katika kipindi hicho.

"Lakini sasa napenda kumshukuru sana Mheshimiwa Kikwete kwa kurudisha heshima ya nchi yetu duniani kwani mwaka huu wa kampeni, hakuna hata mmoja aliyehama visiwani humo kukimbia uchaguzi" alimaliza Juma Othman akishangiliwa na umati mkubwa wa wana CCM waliojitokeza kwenye mkutano huo wa kampeni.

Mama Fatma Maghimbi amewahi kuwa waziri kivuli wa Katiba na Sheria ndani ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akiwa kama mbunge wa Chama Cha Wananchi CUF. Naye Juma Othman Juma amewahi kuwa muanzilishi wa Chama Cha Siasa visiwani kabla ya kujiunga na Chama cha Wananchi CUF.

Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama cha Mapinduzi CCM Mh. Jakaya Kikwete akimnadi Mama Kizigha, mgombea ubunge wa CCM jimbo la kawe leo kwenye mkutano wa kampeni uliofanyika kwenye viwanja vya Tanganyika Parkers jijini Dar es salaam.
Uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge, na Madiwani unatarajiwa kufanyika Oktoba 31 mwaka huu nchini kote. (Picha na Muhidin Issa Michuzi)
Bw. Juma Othman Juma akiwa na Mama Fatma Maghimbi baada ya kurejesha kadi za CUF na kupewa za CCM leo.
Msanii wa Bongo Fleva Diamond akitumbuiza leo Kawe kwenye mkutano wa kampeni wa Jakaya Kikwete
Nyomi uwanja wa Tanganyika Packers kwenye mkutano wa kampeni wa Jjakaya Kikwete leo.
sehemu ya nyomi uwanja wa Tanganyika Packers, Kawe, jijini Dar leo

THE DON HIMSELF

Karibuni sana kwenye blog hii ya kijamii iliyosheheni makila kitu kuanzia siasa uchumi afya na burudani kwa ujumla wake.uingiapo kwenye blog hii ni mengi ambayo utapata nafasi ya kukutana nayo,kumbuka mawazo yako ndo hasa yanayojenga na kunifanya niwe na ufanisi zaidi.kariiiiiiibuuuuuuuuuuuu saaaaaaaaaaaaaaanaaaaaaaaaa.(THE DJ HIMSELF-JIWE)

Followers

BLOG ZA MARAFIKI

Search This Blog

ZILIZOPITA

DUNIA MUZIMA