Aug 17, 2010

TUME YA TAIFA YA SAYANSI NA TEKNOLOJIA YATOA TUZO


Waziri wa Sayansi na Tek nolojia Prof. Peter Msolla akimkabidhi mfano wa hundi yenye thamani ya shilingi milioni ishirini Prof. Mathew Luhanga wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam kufuatia Taasisi ya Kompyuta ya Chuo Kikuu cha Dar es salaam kushika nafasi ya kwanza leo jijini Dar es salaam wakati wa sherehe ya kutoa tuzo za taifa za ugunduzi na ubunifu na kutoa Mwega kwa ajili ya utafiti mwaka 2010.

Waziri wa Sayansi na Teknolojia Prof. Peter Msolla akimtunuku cheti cha mshindi wa kwanza Prof. Mathew Luhanga wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam kufuatia Taasisi ya Kompyuta ya Chuo Kikuu cha Dar es salaam kushika nafasi ya kwanza leo jijini Dar es salaam wakati wa sherehe ya kutoa tuzo za taifa za ugunduzi na ubunifu na kutoa Mwega kwa ajili ya utafiti mwaka 2010.
Waziri wa Sayansi na Teknolojia Prof. Peter Msolla akiangalia mbegu za mahindi na kupata maelezo kutoka kwa mtaalam wa Kilimo Kutoka kituo cha utafiti Ilonga kilichoko kilosa mkoani Morogoro Dkt. Chaboba Mkangwa. Kulia ni Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Sayansi na Teknolojia Dkt. Hassan Mshindi.
Waziri wa Sayansi na Teknolojia Prof. Peter Msolla (katikati) akipata maelezo kutoka kwa Bw. Godfrey Kimarya mgunduzi wa tanuru la mkaa lenye uwezo wa kutoa mkaa mwingi na wenye ubora kwa gharama nafuu leo jijini Dar es salaam wakati wa sherehe ya kutoa Tuzo za Taifa za Ugunduzi na Ubunifu pamoja na utoaji wa fedha za kusaidia shughuli za utafiti wa elimu, kilimo,ufugaji, ufundi na viwanda kwa taasisi na vikundi mbalimbali nchini.Wataalam kutoka Chuo Kikuu cha Kilimo Sokoine -Morogoro (SUA) Prof. Rhodes Makundi (kulia) na Christophe Cox (kushoto) wakitoa maelezo ya panya buku wenye uwezo kugundua mabomu yaliyotegwa ardhini na vimelea vya ugonjwa wa kifua kikuu (TB) leo jijini Dar es salaam wakati sherehe ya kutoa Tuzo za Taifa za Ugunduzi na Ubunifu pamoja na utoaji wa fedha za kusaidia shughuli za utafiti wa elimu, kilimo,ufugaji, ufundi na viwanda kwa taasisi na vikundi mbalimbali nchini .Profesa Rhodes Makundi kutoka Chuo Kikuu cha Kilimo Sokoine - Morogoro (SUA) akitoa ufafanuzi wa panya buku wenye uwezo wa kugundua mabomu yaliyotegwa ardhini na vimelea vya ugonjwa wa kifua kikuu (TB) kwa Waziri wa Sayansi na Teknolojia Prof. Peter Msolla leo jijini Dar es salaam wakati wa sherehe ya kutoa tuzo za taifa za ugunduzi na ubunifu na kutoa Mwega kwa ajili ya utafiti

(Picha na Aron Msigwa - MAELEZO)

MAADILI KWA VYOMBO VYA HABARI/WASANII YAGONGANISHA VICHWA

Katibu Mtendaji wa Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA),Ghonche Materego (Kulia) akisisitiza jambo wakati akichangia mada kwenye Jukwaa la Sanaa Jumatatu hii.Katikati ni mwasilishaji wa mada, Bi.Mabel Masasi na Katibu wa CAJAtz,Hassan Bumbuli.Mdau wa Sanaa na Mwenyekiti wa Chama cha Wamiliki wa Video Library nchini, Richard Kalinga akichangia mada kuhusu Mchango wa Sekta ya Utangazaji Katika Kulinda Maadili ya Mtanzania.Mkongwe wa Sanaa za Maonyesho,Nkwama Bhalanga akilia na rushwa kwenye vituo vya redio ambapo alisema kwamba ni kikwazo katika maendeleo ya muziki nchini.Alipendekeza vibanwe na TCRA kupitia utoaji leseni.Aliyekaa kulia kwake,ni Mkongwe wa dansi nchini,Kasim Mapili.

Umakini zaidi kwa wadau wa sanaa kwenye Jukwaa.Hapa wakimsikiliza Katibu Mtendaji wa BASATA,Bw.Materego (hayuko pichani) wakati akihitimisha mada ya siku ya leo.


**************** *****************

Wadau, kama kawaida Jukwaa la Sanaa ambalo sasa limekuwa ni mkombozi kwa wasanii wetu na chanzo mahsusi cha habari na kisima cha elimu, Jumatatu hii lilibeba mada ya Mchango wa Sekta ya Utangazaji Katika Kulinda Maadili ya Mtanzania iliyowasilishwa na Bi.Mabel Masasi kutoka Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA).

Akiwasilisha mada yake ambayo ilivuta idadi kubwa ya watu,Bi Masasi aliyataja majukumu ya mamlaka yake ambayo ni pamoja na kulinda haki na maslahi ya wateja, kuchochea kuwepo kwa watoa huduma waliosajiliwa, kutoa leseni kwa watangazaji, posta na mawasiliano ya kielektroniki, kuweka viwango vya huduma katika mawasiliano nk.

Aidha, aligusia suala la maadili katika vyombo vya habari ambapo alisema kwamba, kumekuwa na kazi za sanaa chafu ambazo zimekuwa zikipita kwenye vyombo vya habari na mamlaka imekuwa ikichukua hatua na kuvitoza faini vyombo hivyo kwa kupitisha kazi chafu za sanaa.

Aliongeza kwamba, mamlaka ya mawasiliano imekuwa ikifuatilia kwa makini programu zote katika redio hususan zile zinazorusha muziki na filamu na kuhakikisha kuwa hakuna kazi chafu za sanaa zinazopita.Katika hili wadau wengi walihoji lugha chafu zinazotumiwa na watangazaji katika vituo vya redio hususan vya FM.

Hata hivyo, wadau wengi waliochangia mada hiyo, walilalamikia sana rushwa miongoni mwa watangazaji na Ma DJ wa redio na wamesema kwamba, zimepelekea gemu la muziki kupwaya.Katika hili wadau wameiomba Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) kuanza mkakati wa kuvibana vituo vya redio kwani vimekuwa ni tatizo kwa maendeleo ya muziki.

Suala lingine lililoibuka, ni suala la vituo vya redio kutokuwalipa wasanii mirabaha ambapo ilishauriwa kuwa TCRA iwaze sasa kuvibana vituo vya redio na TV ambavyo havilipi mirabaha kwa wasanii.Wazo hili liliungwa mkono na wadau wengi hasa ikizingatiwa kwamba,TCRA ndiyo wanaotoa leseni kwa vituo hivyo.TCRA walisema kwamba, watalifanyia kazi kwa kushirikiana na COSOTA.

Hata hivyo, kumekuwa na tatizo la wasanii wenyewe kusaini mikataba na vituo vya redio ya kutolipwa chochote na badala yake wanaruhusu kazi zao zichezwe bure.Ilielezwa kwamba, wasanii wamekuwa hawajali mikataba na wengine wamekuwa wakisaini kazi zao kupigwa bure bila wao kulipwa.Tatizo hili linaonekana kuwa kubwa na wasanii wamekuwa wakilalama bila kuchukua hatua na kujali kai zao.

Kwa ujumla wadau,Jukwaa la Sanaa ni Mahali ambapo wasanii wanapaswa kufika kwa wingi kila Jumatatu kuanzia saaa 4 hadi saa 6.Ni kupitia Jukwaa hili la Sanaa, tutaweza kufika mbele kutokana na mijadala inayoibuka, elimu inayotolewa na kuwepo kwa masuala ya msingi kuhusu sekta ya sanaa na utamaduni yanayoibuka na kujibiwa.

Jumatatu ijayo yaani Tarehe 23/8/2010, Jukwaa la Sanaa Kama kawaida litakuja na Mada ya URASIMISHAJI WA WASANII,ambayo pamoja na mambo mengine itahusu utambuzi wa wasanii ili kufuta dhana inayojengeka sasa kwamba Msanii ni mtu muongo,mbabaishaji, mchovu na asiye na dili.Tafadhali Usikosekane,Fika.

Aug 16, 2010

WANA CCM IRINGA KESHO KUFANYA MAANDAMANO KUPINGA MAAMUZI YA NEC YA CCM DODOMA KUMTEUA MONICA MBEGA


HASIRA zatawala kwa wanachama wa chama cha mapinduzi (CCM) jimbo la Iringa mjini na Njombe magharibi ambao wanapinga maamuzi ya wajumbe wa halmashauri kuu ya chama cha mapinduzi (CCM) Taifa chini ya mwenyekiti wake Rais Jakaya Kikwete kukata majina ya washindi wa kura za maoni na kuwapa ridhaa wagombea wasiotakiwa ndani ya CCM.


Huku siri zaendelea kuvuja kuhusiana na Mwakalebela na Fadhil Ngijilo kufikishwa mahakamani kwa tuhuma za rushwa ni njama za mfanyabiashara mmoja mkubwa mjini Iringa mwenye asili ya kiasia ambaye anatajwa kuwa ndiye aliyesuka mpango wa kuwafanya wagombea hao kufikishwa mahakamani na wagombea wengine kutoka jimbo la Mufindi kaskazin lengo likiwa ni saidia Mbega aonekane msafi.


Hivyo hatua hiyo imeonekana kuwakwaza zaidi jambo ambalo wamekusudia kesho jumatatu kukutana majira ya asubuhi ofisi za CCM wilaya na mkoa kurejesha kadi zao na kwenda ofisi za Chadema kuchukua kadi za uanachama .


Pamoja na hayo pia diwani mpambanaji wa ufisadi katika CCM kata ya Miyomboni Kitanzini Gravas Kalolo aliyeshindwa kura za maoni na mshindi wa pili wa kura za maoni (CCM) jimbo la Njombe kaskazin Alatanga Nyagawa kutangaza rasmi kujiunga na Chadema akiwemo aliyekuwa mwekahazina wa vijana TLP Taifa Abuu Changawa Majeck huku mshindi wa kura za maoni jimbo la Njombe Magharibi Thomas Nyimbo akiahidi kutoa uamuzi wake wamwisho dhidi ya CCM ndani ya masaa 48 kuanzia leo saa 5 asubuhi.


Maamuzi hayo ya CCM Taifa yameonyesha kuwakwaza zaidi wana CCM hao ambapo hadi majira majira ya saa 6 mchana katika jimbo la Iringa mjini na Njombe Magharibi zaidi ya wana CCM 1000 walitangaza kujiunga rasmi na chama cha demokrasia na maendeleo(Chadema) ikiwa ni pamoja na kurejesha kadi za CCM Chadema huku baadhi yao wakimtangaza rasmi mgombea ubunge wa Chadema Iringa mjini Mchungaji Peter Msingwa kuwa mbunge mteuli wa jimbo hilo.


Mchungaji Msigwa ameonyesha ni chaguo la wana Iringa bila kujali itikadi ya vyama vyao baada ya mmoja kati ya wafanyabiashara wakubwa mjini Iringa ambaye alikuwa msaada mkubwa kwa CCM kumkabidhi pipa moja la mafuta aina ya Dizel kwa ajili ya kampeni za ubunge.


baada ya halmashauri kuu ya CCM Taifa kukata jina la Thomas Nyimbo na Frederick Mwakalebela pamoja na kushinda kwa kishindo katika kura za maoni.


Nyimbo katika kura za maoni CCM jimbo la Njombe Magharibi alishinda kwa kura 6,795 akifuatiwa na aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo Yono Kevela aliyepata kura 3,434 huku mteule wa CCM atakayegombea ubunge jimbo hilo Gerson Lwenge akiambulia kura 2,971 japo mbalo linapingwa na wana CCM jimbo hilo la Njombe Magharibi kuwa ni vema hata wange mchukua mtu wa nne .



Danford Mpumilwa (854) ama msaidizi wa askofu wa kanisa la kiinjili la kilutheri Tanzania (KKKT) dayosisi ya kusini Mch. Isaya Mengele (822) kuliko kumpata mshindi watatu ambaye ndiye aliongoza kwa kucheza rafu katika mchakato huo.


Daud Twengele na Yohana Mussa ambao ni wana CCM wa jimbo hilo la Njombe Magharibi walisema kuwa wanasikitishwa sana na maamuzi ya halmashauri kuu ya CCM kumtema Nyimbo kwa sababu zao wenyewe jambo ambalo walidai kuwa mwenyekiti wa CCM Taifa Rais Kikwete asitegemee kura za wana CCM katika jimbo hilo ambalo wamefanya uchakatuaji mgombea wao .


" CCM yenyewe ilitueleza kuwa Nyimbo ambaye alikuwa amefungiwa kugombea nafasi yoyote ndani ya CCM kuwa amemaliza adhabu yake ..... sasa sisi wana CCM tumemchagua ili arudi kututumikia kama mbunge wetu bungeni wao wanakutana Dodoma na kupinga maamuzi yetu na kumleta mtu wao ambaye sisi tulimkataa ....sasa tunasema wajumbe wa halmashauri kuu ya CCM Taifa waliompendekeza huyu tuliyemtema sisi ndio watakuja kumchagua katika uchaguzi mkuu octoba ila sisi kura zetu ni upinzani na hata kama leo Nyimbo atakwenda chama chenye mwelekeo kama Chadema ajue ushindi alioupata utakuwa mara tano zaidi "



Pamoja na wana CCM hao katika jimbo la Njombe Magharibi kutangaza msimamo wao wa kwenda na Nyimbo popote atakapotangaza kuwania ubunge ,wapambe wa Monica Mbega na wale wa Mwakalebela katika jimbo la Iringa mjini juzi usiku na jana wameshinda wakigombana kupinga maamuzi ya Halmashauri kuu ya CCM Taifa kumpitisha Mbega kugombea tena jimbo hilo.


Walisema kuwa kura 2,989 alizoambulia Mbega katika mchakato huo dhidi ya kura 3,897 zilizompa ushindi Mwakalebela ni ishara tosha kuwa wana CCM jimbo hilo la Iringa mjini walikuwa wamechoka na uwakilishi wa Mbega na ndio sababu ya kumpumzisha kwa kumpa nafasi hiyo Mwakalebela .


Akizungumza kwa niaba ya wana CCM waliofika ofisi za Chadema kurejesha kadi na kujiunga na chama hicho Sarehe Ngole alisema kuwa kama wajumbe hao wa NEC waliona kuwa Mbega anafaa kuendelea kuwa mbunge wa jimbo hilo wasingeruhusu wana CCM wengine kuchukua fomu za kuwania nafasi hiyo bali wangempitisha mgombea wao.


" CCM inataka kutufanya sisi ni hayawani tusiojua chochote ...kwani kama wana CCM tuliacha shughuli zetu na kwenda katika kampeni za kura za maoni na kuacha kwenda makanisani na kushiriki kuchagua mgombea wetu Mwakalebela iweje wao Dodoma wampitishe Mbega.....tunasema Mbega ni mbunge wa NEC Dodoma sio jimbo la Iringa mjini ....sisi jimbo la Iringamjini mbunge wetu ni Frederick Wilfredy Mwakalebela ndie ambaye tunamtaka asimame katika uchaguzi mkuu vinginevyo mgombea wa Chadema jimbo hilo mchungaji Peter Msigwa kuanzia sasa tunamkatanga rasmi kama mbunge wetu asubiri kuapishwa baada ya uchaguzi"


Hata hivyo alipinga sababu za NEC kumuengua Mwakalebela kwa tuhuma za Rushwa kwani walisema kuwa ndani ya CCM hakuna ambaye mgombea ambaye ameingia bila kutoa rushwa labda walioshika nafasi za mwisho ndio ambao walishindwa kwa kukosa pesa na kuwa katika jimbo hilo wote wasingepitishwa nafasi hiyo wangemteua John Kiteve ambaye kati ya wagombea 12 alikuwa wa mwisho kwa kupata kura 136 kuwa huyo ndiye mgombea safi na hakutumia rushwa ya aina yoyote kuomba kura zaidi ya maelezo yake.


Kwa upande wake mgombea ubunge wa Chadema jimbo la Iringa mjini mchungaji Msingwa akiwapokea wana CCM hao alisema kuwa wana CCM wanajidanganya wenyewe kwa kupinga rushwa wakiwa ndani ya CCM huku na kuwa watanzania wamechoshwa na CCM sasa wanahitaji mageuzi ya kweli bila CCM.


Msigwa alisema kuwa inashangaza kuona watanzania wanaendelea kudanganywa na fulana za wagombea wa CCM huku wakiendelea kupata viongozi wabovu wasiojali maendeleo zaidi ya kuangalia maslahi yao .


Hata hivyo alisema baraka idadi ya wana CCM wakiwemo wale walioshindwa udiwani na ubunge ambao wametangaza kujiunga Chadema ni kielelezo tosha kuwa CCM jimbo la Iringa mjini haina chake na badala yake viongozi wake kuendelea kutoa ushirikiano kwa Chadema ambacho ni chama mbadala kwa CCM.


Pia Msigwa alisema tayari wana CCM wakiwemo wafanyabiashara ambao walikuwa wakikisaidia chama cha mapinduzi wameanza kuomba kukisaidia chadema kwa nguvu zote na hadi sasa pipa moja la mafuta ya kampeni limepatikana.

WAREMBO WA EASTERN ZONE 2010 WAAGWA

MREMBO ANGERINA NGEGE AKIWA AMEPOZI KWA PICHA
MKURUGENZI WA KAMPUNI YA KIMKEV ENTERTAINMENT AMBAO NI WAANDAJI
WA MISS EASTERN ZONE),BW.KIM KIMENYA AKIONGEA NA WAREMBO PAMOJA NA WAGENI WAALIKWA WAKATI AKIWAKARIBISHA DINNER ALIYOWAANDALIA WAREMBO WA EASTERN ZONE KWA AJILI YA KUWAAGA KABLA YA KUJIUNGA NA KAMBI YA MISS VODACOM TANZANIA KWENYE HOTELI YA CITY STYLE SIKU YA JUMAMOSI TAREHE 14.08.2010.KAMBI YA MISS TANZANIA INATARAJI KUANZA TAREHE 16.08.2010MKURUGENZI WA KAMPUNI YA KIMKEV ENTERTAINMENT, BW.KIM KIMENYA AKIMKABIDHI POSHO YA KUJIKIMU MREMBO ANGELINA NDEGE.
MREMBO ANGELINA NDEGE AKIONGEA JAMBO WAKATI WA DINNER YA KUWAAGA WAREMBO WA EASTERN ZONE 2010 NDANI YA HOTELI YA CITY STYLE SINZA
VILAJI VIKIGONGANISHWA
PICHA YA PAMOJA NA WAREMBO,UOGOZI WA HOTELI YA CITY STYLE NA WADAU.

VODACOM TANZANIA YAFUTURISHA WATOTO YATIMA JIJINI DAR ES SALAAM!!

Mgeni rasmi Sheikh Mkuu wa Tanzania Sheikh Issa Shaabani Simba akisoma hotuba yake katika viwanja vya Karimjee leo jioni wakati wa Futari iliyoandaliwa na Kampuni ya simu za mkononi Vodacom Tanzania kupitia kitengo chake cha Vodacom Foundation maalum kwa watoto yatima wa vituo mbalimbali vya jijini Dar es salaam katika mfungo huu wa mwezi mtukufu wa (Ramadhan) ambapo waislamu kote duniani hufunga kama utekelezaji wa nguzo muhimu katika kumcha mwenyezi mungu.
Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Tanzania Bw. Dietlof Mare akizungumza wakati akikaribisha watoto yatima kutoka vituo mbalimbali vya jijini Dar es salaam na wageni waalikwa wakati wa futari kwenye viwanja vya karimjee leo jioni kushoto ni mkurugenzi wa kitengo cha Teknohama Vodacoma Tanzania Maharage Chande.
Sheikh Mkuu wa Tanzania Sheikh I ssa Shaabani Simba kushoto akipokea ndoo ya mafuta ya kula kutoka kwa Mkurugenzi wa Vodacom Tanzania Dietlof Mare kwa niaba ya watoto hao kama moja ya zawadi ambazo kampuni hiyo imetoa kwa vituo hivyo ili mkusaidia kwa ajili ya futari kulia nia Mkurugenzi Vodacom Foundation Mwamvita Makamba na katikati ni mmoja wa wasaidizi wa Sheikh Mkuu wa Tanzania Sheikh Issa Shaaban Simba.
Wafanyakazi mbalimbali wa vodacom wakiwa katika picha ya pamoja na watoto hao.
Sheikh Mkuu wa Tanzania Sheikh Issa Shaabani Simba kushoto akiwasili kwenye viwanja vya Karimjee kama mgeni rasmi katika futari iliyoandaliwa na Vodacom Tanzania kulia ni Mkurugenzi wa kampuni hiyo Dietlof Mare.
Mkurugenzi wa Vodacom Foundation Mwamvita Makamba akiwaongoza wageni walioonozana na Sheikh Mkuu Issa Shaaban Simba wakati walipowasili kwenye viwanja vya Karimjee.
Mkurugenzi wa Vodacom Foundation akiwa katika picha ya pamoja na watoto kwa ajili ya kupokea zawadi kutoka Vodacom.
Meneja wa Vodacom Foundation Yessaya Mwakifulefule kulia akiwa na wadau wa Vodacom Edwin Temba kati na mdau mwingine Mohamed Kalambo wa Vodacom.
.Afisa Uhusiano wa Vodacom Mwamvua Mlangwa kushoto, Afisa wa Vodacom Foundation Grace Lyon katikati na Meneja Mawasiliano wa Vodacom Tanzania Necta Foya wakijiandaa kupokea wageni mbalimbali katika futari hiyo.
Hapa watoto wakiimba kaswida kabla ya muda wa kufuturu kuwadia.
Hapa watoto wakisuburi kufuturu vituo mbalimbali vya kulelea watoto villialikwa na mkuleta watoto kwa ajili ya kupata futari na wenzao ktoka maeneo mbalimbali ya jiji la Dar es salaam.

Uchaguzi mkuu wa TASWA wafana

Sehemu ya wanachama wa Taswa wakati wa uchaguzi mkuu huoWagombea wakisubiri matokeo

Wajumbe

Tom Chilala na wajumbe wengine mkutanoniJuma Pinto na Ibrahim Masudi 'Maestro' kabla ya matokeo kutangazwaMwenyekiti mpya wa TASWA na Kamati yake kuu

Vicheko wakati wa kusubiri matokeo

'Takukuru' nao walikuwepo kuangalia mambo....

Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi TASWA akitangaza matokeo

Mwenyekiti mpya wa TASWA Juma Pinto na viongozi wenzie

Wana TASWA mkutanoni

wana TASWA

Wajumbe wa TASWA mkutanoniUongozi wa TASWA uliomaliza muda wake katika picha ya pamoja

Chama cha waandishi wa habari za michezo nchini Tanzania, TASWA, kimefanya uchaguzi wa viongozi wapya baada ya uongozi wa zamani kumaliza muda wake wa miaka mitatu kama katiba inavyoelekeza. Katika uchaguzi huo viongozi wapya waliochaguliwa ni:

MWENYEKITI: JUMA PINTO
MAKAMU MWENYEKITI:
MAULID KITENGE
KATIBU MKUU:
: AMIR MHANDO
KATIBU MSAIDIZI:
GEORGE JOHN
MTUNZA HAZINA:
SULTAN SIKIRO
MSAIDIZI:
MOHAMED MKANGARAKWA
WAJUMBE: ELIUS KAMBIRI, GRACE HOKA, ZENA CHANDE, ALFRED LUCAS, OSMAN KAPINGA, SALUM JABA

Ufafanuzi wa CCM juu ya sakata la kuenguliwa Mwakalebela kugombea Ubunge Iringa mjini

Baada ya jina la Frederick Mwakalebela kuenguliwa katika orodha ya wagombea Ubunge kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi, CCM, baadhi ya watu wamekuwa wakihoji uhalali wa kufanya hivyo il hali wana-CCM wengine wanaogombea viti hivyo katika majimbo mengine nchini wana kesi mahakamani lakini wameruhusiwa kuendelea na kinyang’anyiro hicho. Maswali hayo yaliifikia CCM na hapa ni ufafanuzi wake:

Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Halmashauri Kuu ya CCM (NEC-CCM), Mh. John Chiligati amesema kesi inayomkabili mshindi wa kura za maoni aliyepokwa ‘haki’ ya kuteuliwa kugombea ubunge wa Iringa Mjini kwa tiketi ya chama hicho, Frederick Mwakalebela, haifanani na washindi wengine wa kura za maoni walioteuliwa ambao ni Basil Mramba anayegombea jimbo la Rombo na Andrew Chenge anayegombea jimbo la Bariadi Mashariki licha ya kuwa na kesi mahakamani kama yeye.

Alisema

Mh. Andrew Chenge

Mh. Basil Mramba

Bw. Frederick Mwakalebela

Mwakalebela ameachwa kwa sababu ya kukosa kwake maadili.

“Suala kwa Mwakalebela ni maadili tu, katika mchakato huu, kakamatwa kwa tuhuma za rushwa na TAKUKURU wamesema wanayo sababu ya kumpeleka mahakamani.” “Lakini alikuwa ndio kwanza kaingia katika mchezo wenyewe na katika mchezo huu huu kabla ya dakika 90, akapigiwa filimbi kuwa amecheza faulo,” alisema Chiligati.

Kuhusu tofauti ya Mramba, Chenge na Mwakalebela Chiligati alisema, “ kisheria wote ni watuhumiwa na hawakutwa na hatia, lakini kimaadili ni tofauti… Mramba anatuhumiwa kutumia vibaya madaraka, tuliita wanasheria wakasema hiyo kesi haimuondolei sifa ya kuwa mgombea.”

Hata hivyo alikiri kuwa Mramba alipitishwa baada ya kufanyika mjadala kati ya wajumbe hao wa NEC.
“Katika Mkoa wa Shinyanga Jimbo la Bariadi Mashariki aliteuliwa Chenge kutetea nafasi yake, anayo kesi ya trafiki, haimkoseshi haki ya kuwa mgombea,” alisema Chiligati.

credit source: http://www.wavuti.com

Aug 15, 2010

WALIOTEULIWA KUGOMBEA UBUNGE KATIKA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA KWA KUPITIA CHAMA CHA MAPINDUZI KATIKA UCHAGUZI MKUU 2010

1.MKOA WA KIGOMA
(i) Mjini: Peter Serukamba,
(ii)Kigoma South: Gulam Hussein Shaaban Kifu,
(iii)Kasulu Urban: Neka Raphael Neka,
(iv)Kasulu Rural: Daniel Nsanzugwanko,
(v)Manyovu: Albert F. Ntabaliba,
(vi)Buyungu: Christopher Chiza,
(vii)Muhambwe: Jamal Abdallah Tamimu,
(viii)Kigoma North: Rabinson, F. Lembo.

2.MKOA WA KILIMANJARO
(I) Moshi Mjini:Justin Salakana,
(ii) Moshi Vijijini: Dk. Cyril Agust Chami,
(iii)Rombo: Basil Pesambili Mramba,
(iv)Same Mashariki): Anne Kilango Malecela,
(v)Same Magharibi: Dk. David Mathayo David,
(vi)Hai: Fuya Godwin Kimbita,
(vii) Vunjo: Chrispin Theobald Meela,
(viii) Mwanga: Profesa Jumanne Maghembe,
(ix)Siha, Aggrey D.J. Mwanri.

3.MKOA WA MANYARA:
(i)Babati mjin:Kisyeri Werema Chambiri,
(ii)Babati Vijini: Jitu Vrajil Soni,
(iii)Hanang: Dk. Mary Michael Nagu,
(iv)Kiteto: Benedict Ole Nangoro
(v) Mbulu:Philip Sang’ake Marmo,
(vi)Simanjiro:Christopher Ole Sendeka.

4.MKOA WA MARA
(i) Musoma mjini: Vedasto Manyinyi,
(ii)Musoma vijijini:Nimrod Elirehema Mkono,
(iii)Mwibara: Alphaxard Kangi Lugola,
(iv)Bunda: Stephen Masatu Wasira,
(v)Rorya: Lameck Okambo Airo,
(vi)Tarime, Nyambari Chacha Nyangwine,
(vii)Serengeti: Dk. Stephene Kebwe Kebwe.

5.MKOA WA MBEYA
(i) Mbeya Mjini: Benson Mwailugula Mpesya,
(ii) Mbeya Vijijini: Luckson Ndage Mwanjala,
(iii) Kyela: Dk Harrison George Mwakyembe,
(iv)Mbarali: Dickson Modestus Kilufi,
(v)Lupa: Victor Kilasile Mwambalaswa,
(vi) Songwe:Philipo Augustino Mulugo,
(vii) Rungwe Mashariki: Profesa Mark James Mwandosya,
(viii) Rungwe Magharibi: Profesa David Homeli Mwakyusa,
(ix) Ileje: Aliko Nikusuma Kibona,
(x)Mbozi Mashariki: Godfrey Weston Zambi,
(xi)Mbozi Magharibi: Dk. Luka Jelasa Siame.


6. MKOA WA MOROGORO

(i)Morogoro Mjini:Aziz Mohamed Abood,
(ii)Morogoro Kaskazini: Dk. Lucy Sawera Nkya,
(iii)Morogoro Kusini: Innocent Kalogeris,
(iv)Mvomero: Amos Gabriel Makala
(v) Ulanga Mashariki: Celina Ompeshi Kombani,
(vi)Ulanga Magharibi: Haji Hussein Mponda,
(vii)Gairo: Ahmed Mubukhut Shabiby
(viii)Kilosa, Mustafa Heidi Mkulo,
(ix)Mikumi: Abdulsalaam Suleiman,
(x)Kilombero: Abdul Rajab Mteketa.

7.MKOA WA TABORA
(i)Urambo Mashariki: Samwel John Sitta
(ii)Urambo Magahribi: Juma Athuman Kapuya,
(iii)Tabora Mjini: Ismail Aden Rage,
(iv)Igunga: Rostam Abdulsasu Aziz,
(v)Sikonge: Said Juma Nkumba
(vi) Igagula: Athuman Rashid Mfutakamba
(vii) Tabora: Sumar Shaffin Mamlo,
(viii)Bukene: Seleman Jumanne Zedi
(ix)Nzega:Dr. Hamisi Andrea Kigwangala

8.MKOA WA TANGA
(i)Tanga mjini: Omari Rashid Nundu
(ii)Kilindi: Beatrice Matumbo Shelukind
(iii)Muheza: Herbert James Mntangi
(iv)Mkinga: Danstan Luka Kitandula
(v)Pangani: Salehe Ahmed Pamba
(vi)Lushoto: Henry Daffa Shekifu
(vii)Bumbuli: January Makamba
(viii)Korogwe Mjini:Yusuph Nasri
(ix)Mlalo:Brig. Gen. Hassan Athuman Ngwilizi
(x)Korogwe Vijijini: Stephen Ngonyani
(xi)Handeni: Dr. Abdalah Omari Kigoda

10.MKOA WA DAR ES SALAAM
(i).Kinondoni: Idd Mohamed AZAN
(ii).Ubungo: Hawa Mgonja NG’UMBI
(iii).Kawe: Angella Charles KIZIGHA
(iv).Ilala: Musa Azan ZUNGU
(v).Ukonga: Eugen Elishirima MWAIPOSA
(vi).Segerea:Dr. Milton Makongoro MAHANGA
(vii).Temeke: Abbas Zuber MTEMVU
(viii).Kigamboni:Dr. Faustine NDUGULILE

11.MKOA WA LINDI
(i)Lindi Mjini:Ndugu Mohamed ABDULAZIZ
(ii)Mtama:Ndugu Bernard Kamillius MEMBE
(iii)Mchinga:Ndugu Said M. MTANDA
(iv)Nachingwea:Ndugu Mathias Meinrad CHIKAWE
(v)Ruangwa:Ndugu Kassim MAJALIWA
(vi)Kilwa kaskazini:Ndugu Murtaza Ali MANGUNGU
(vii)Kilwa Kusini:Ndugu Ramadhan Rashid MADABIDA
(viii)Liwale:Ndugu Faith Mohamed MITAMBO

12.MKOA WA PWANI
(i)Bagamoyo: Dr. Shukuru J. Kawambwa
(ii)Chalinze: Saidi Athuman Bwanamdogo
(iii)Kisarawe: Seleman Saidi Jafo
(iv)Kibiti: Abdul J. Marombwa
(v)Kibaha Vijijini: Mahamud Abuu Jumaa
(vi)Kibaha Mjini: Silvestery F. Koka
(vii)Mkuranga: Adam Kighoma Malima
(viii)Rufiji: Dr. Seif Seleman Rashid
(ix)Mafia: Abdulkarim E. Shaha

13.MKOA WA RUKWA
(i)Kwela: Malocha Aloyce Ignace
(ii)Kalambo: Kandege Sinkamba Josephat
(iii)Nkasi Kaskazini: Ally Mohamed Kessy
(iv)Nkasi Kusini:Deusderius Mipata
(v)Mlele: Mizengo Kayanza Peter Pinda
(vi)Mpanda Kati (mjini): Sebastian Simon Kapufi
(vii)Sumbawanga Mjini: Aeshi Khalfan Hilaly
(viii)Mpanda Vijijini: Moshi S. Kakoso

14.MKOA WA SHINYANGA
(i)Shinyanga Mjini: Steven Julius Masele
(ii)Kishapu: Nchambi Seleman Masoud
(iii)Kahama: James Daud Lembeli
(iv)Msalala: Maige Ezekiel Magolyo
(v)Solwa: AhmeD Ally Salum
(vi)Bukombe: Emanuel Jumanne Luhahula
(vii)Mbogwe: Masele Agustino Manyanda
(viii)Bariadi Mashariki: Makondo Martine Kaunda
(ix)Bariadi Magharibi: Chenge Andrew John
(x)Maswa Mashariki: Bunyongoli Peter Edward
(xi)Maswa Magharibi: Kisena Robert Simon
(xii)Meatu:Salum Khamis Salum
(xiii)Kisesa: Joelson Luhaga Mpina.

15.MKOA WA SINGINDA
(i)Singida Mjini:Mohamed Gulam Dewji
(ii) Manyoni Mashariki:Capt.(mstaafu) John Chiligati
(iii)Manyoni Magharibi: John Paul Lwanji
(v)Iramba Magharibi: Mwigulu Lameck Nchemba Matelu
(vi)Iramba Mashariki:Salome David Mwambu
(vii)Singida Kaskazini:Lazaro Samwel Nyalandu
(viii)Singida Magharibi:Alhaj Mohamed Misanga
(ix)Singida Mashariki:Jonathan Andrew Njau

16.MKOA WA ARUSHA
(i)Arusha:Dr. Batilda BURIANI
(ii)Arumeru Mashariki: Jeremiah Solomon SUMARI
(iii)Arumeru Magharibi: Goodluck Joseph Ole MEDEYE
(iv)Karatu: Dr. Wilbald Slaa LORRI
(v)Longido: Michael Lekule LAIZER
(vi)Monduli: Edward Ngoyai LOWASSA
(vii)Ngorongoro: Saning’o Kaika Ole TELELE

17.MKOA WA IRINGA
(i)Iringa Mjini: Monica Ngenzi MBEGA
(ii)Isimani: William Vangimembe LUKUVI
(iii)Kalenga: William Augustino MGIMWA
(iv)Kilolo:Prof. Peter Mahamudu MSOLLA
(v)Ludewa: Deo Haule FILIKUNJOMBE
(vi)Makete:Dr. Binilith Satano MAHENGE
(vii)Mufindi Kaskazini: Mohamed Hassan MGIMWA
(viii)Mufindi Kusini: Menrad Lutengano KIGOLA
(ix)Njombe Kaskazini:Deo Kasenyenda SANGA (Jah People)
(x)Njombe Kusini: Anne Semamba MAKINDA
(xi)Njombe Magharibi: Gerson Hosea LWENGE

18.MKOA WA KAGERA
(i)Nkenge: Assumpter Nshunju MSHAMA
(ii)Bukoba Mjini: Khamis S. KAGASHEKI
(iii)Bukoba Vijijini:Ndugu Jasson S. RWEIKIZA
(iv)Muleba Kaskazini: Charles J. MWIJAGE
(v)Muleba Kusini: Anna K. TIBAIJUKA
(vi)Chato: John Pombe MAGUFULI
(vii)Kyerwa: Eustace O. KATAGIRA
(viii)Karagwe: Gosbert B. BLANDES
(ix)Biharamulo: Oscar R. MUKASA
(x)Ngara: Deogratias Aloys NTUKAMAZINA

Aug 14, 2010

Rais Kikwete aongoza Kikao Cha halmshauri Kuu ya CCm TaIFA MJINI Dodoma jana aagana na Balozi wapya wa Tanzania Ufaransa na Marekani!!

Mwenyekiti wa CCM Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Waziri Mkuu Mizengo Pinda muda mfupi kabla ya kuanza kwa kikao cha Halmshauri Kuu ya CCM Taifa mjini Dodoma leo asubuhi.Katikati ni Katibu mkuu wa CCM Yusuf Makamba. Baadhi ya wajumbe wa Halmashauri kuu ya CCM Taifa wakiwa katika kikao leo mjini Dodoma. Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiagana na Balozi mpya wa Tanzania nchini Ufaransa Mhe. Begum Taj wakati balozi huyo na mwenzake Balozi Mwanaidi Maajar(kulia) walipokwenda kumuaga ikulu ndogo mjini Dodoma leo asubuhi.Balozi Mwanaidi Maajar aliyekuwa balozi wa Tanzania nchini Uingereza anakuwa balozi wa Tanzania nchini Marekani na kituo chake cha kazi kitakuwa Washington. Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiongoza kikao cha halmashauri kuu ya CCm Taifa mjini Dodoma leo asubuhi.Wengine katika picha kutoka kushoto ni Rais Mstaafu awamu ya Tatu Benjamin William Mkapa, Rais Mstaafu awamu ya pili Mzee Ali Hassan Mwinyi,Makamu wa CCM Bara Pius Msekwa na kulia nia katibu mkuu wa CCM Yusuf Makamba.

Aug 13, 2010

BAADA YA 'MACHO KODO' DR LEADER SASA KUJA NA 'KAGOMA KWENDA'

MSANII wa muziki wa kizazi kipya nchini Lucas Silas "Dr.Leader" amewataka mashabiki wake wakae tayari kwa ajili ya ujio wake mpya na wimbo wake mwengine ambao unakwenda kwa jina la "Kagoma Kwenda" anayotarajia kuiachia hivi karibuni.

Msanii huyo ambaye kwa sasa anatamba na wimbo wake Macho Kodokodo ambao unafanya vizuri katika vituo mbalimbali vya redio hapa nchini,na Kueleza kuwa na wimbo huo ambao anatarajia kuuachia utakuwa mzuri zaidi.

Akizungumza na blog hii Dr.Leader alisema kuwa kwa sasa anacho angalia ni kitu gani ambacho mashabiki wake wanakuwa wanakiitaji ili kuweza kuwaridhisha pia kuweza kutambilika kimataifa kupitia mziki huo.

Dr.Leader alisema kuwa wasanii ambao ni chipukizi hawapaswi kukata tamaa hivyo waendeleee kufanya kazi zao vizuri na kwa kuzingatia maadili ya kazi zao pamoja na kujituma ili waweze kutambulika na kupata mafaniko.

Msanii huyo pia alielezea kuwa changamoto zinazowakabili wasanii wa mikoani ni kutokuwa na watu ambao wanakuwa wakiwasapoti katika kazi zao hivyo kuufanya mziki huo kuwa mgumu kwa kwa wasanii wa mikoani.

MAMLAKA YA BANDARI TANZANIA YATAKIWA KUWALIPA FIDIA WAKAZI WA NDUMI TANGA!

WAZIRI wa miundombinu Dkt Shukuru Kawamba ameitaka mamlaka ya Bandari kuharakisha malipo ya wananchi waliochukuliwa maeneo yao kwa ujenzi wa Bandari mpya wa eneo la Ndumi ambapo hekta 82 zinahitaji kufidiwa ili kuepusha migogoro.

Dkt Kawambwa alikuwa jijini Tanga kwa ajli ya uzinduzi wa sera ya Taifa ya usalama barabarani na wiki ya nenda kwa usalama iliyofanyika kitaifa mkoani Tanga,alisema ili kuondoa dhana ya ujenzi bandari ya Tanga ni hadithi wananchi wanapaswa kufidiwa.

Pamoja na agizo hilo kwa mamlaka ya bandari,Waziri Kawambwa alisema yeye na wizara yake itahakikisha kwamba inalisimamia suala hilo ili kuweza kuharakisha ulipwaji wa wananchi sambamba na mchakato wa ujenzi wa bandari hiyo ya Ndumi.

"Mimi kama waziri mwenye dhamana nitahakikisha utekelezaji unakuwepo zoezi la ujenzi wa bandari hii mpya,pia nitahakikisha ujenzi wa miundombinu mingine kama ya reli ya Tanga Arusha na Arusha Musoma unatekelezwa"alisema Waziri Kawambwa.

Hata hivyo waziri Kawambwa alisema kwamba utekelezwaji wa miradi hiyo ni mpango wa serikali katika kutekeleza ilani ya chama cha mapinduzi CCM katika sehemu ya ahadi zake ilizowaahidi wananchi ambapo wamedhamiria kwa dhati kukamilisha suala hilo.

Pia aliwataka wananchi kuwa na subira kuhusiana na ujenzi wa bandari mpya kuhusiana na upitikanaji wa michakato mbalimbali ili kuweza kuwa na umakini wa suala zima la jenzi wa Bandari ya Ndumi sambamba na uimarishaji wa miundombinu ya reli nchini.

Kaimu mkurugenzi mkuu wa mamlaka ya bandari nchini,Julius Mfuko alisema mchakato wa ulipaji umeshaandaliwa na miezi mitatu kuanzia sasa utaanza kulipwa na miezi mitatu kuanzia sasa wananchi wataanza kulipwa na Bil 1.7 zimetengwa kwa ajili ya malipo.

Alisisitiza kuwa mamlaka ya bandari tayari imeandaa upembuzi yakinifu ambapo dola mil 695.5 zimetengwa ili kufanikisha ujezi wa bandari mpya na mil 500 ndizo zilizofanya upembuzi yakinifu ambapo yanasubiriwa maelekezo ya wizara ya miundombinu.

Mfuko alibainisha kuwa kwa upande wa mamlaka ya bandari mchakato unaendelea vizuri ambapo wanasubiri serikali kupitia wizara yake ya miundombinu kuwapatia maelekezo ili ujenzi huo wa bandari uweze kufanyika haraka na kwa ufanisi na tija
(kwa msaada wa blog jirani)

SHIRIKISHO LA SANAA ZA MAONYESHO WAPATA VIONGOZI


Viongozi waliochaguliwa wakiwa kwenye picha ya pamoja na wajumbe mbalimbali wa mkutano huo pia wasimamizi wa uchaguzi huo.Katikati waliokaa kwenye viti ni Msimamizi Mkuu wa Uchaguzi huo,Dkt.Hebert Makoye.


Picha/Habari na Afisa Habari wa BASATA,Alistide Kwizela.


Mkakati wa kuyawezesha na kuyapa nguvu mashirikisho ya wasanii nchini leo umeendelea tena ambapo shirikisho la Wasanii wa Sanaa za Maonyesho limefanya uchaguzi na kujipatia viongozi wake wa muda watakaoliongoza jahazi kwa mwaka mmoja.

Katika uchaguzi wa leo uliofanyika kwenye Ukumbi wa Baraza la Sanaa,BASATA na kusimamiwa na Mkuu wa Idara ya Sanaa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam,Dkt.Hebert Makoye,Bi.Agnes Lukanga aliibuka kidedea katika kiti cha urais baada ya kuwashinda wapinzani wake ambao ni Alex Mwakabama (6) na Denis Mango (6).

Ushindani mwingine ulikuwa kwenye kiti cha Makamu wa Rais ambapo, Bw.Abraham Bawadhil ambaye ni Mkufunzi katika Taasisi ya Sanaa Bagamoyo TaSUBA aliibuka mshindi baada ya kumuangusha Alex Mwakabama aliyeambulia kura 6 pekee.

Aidha,nafasi ya Katibu Mtendaji ilinyakuliwa na Denis Mango aliyepata kura 15 dhidi ya tatu za Irene Sanga huku nafasi ya mweka hazina ikichukuliwa na Mary Mwangato aliyepata kura 9.Nafasi za ujumbe zilienda kwa Alex Mwakibinga, Nkwama Bhalanga na Mahadia Ally.

Baada ya uchaguzi kumalizika, jopo la usimamizi likiongozwa na Dkt.Makoye lilitoa nasaha kwa viongozi kwa kuwataka kuja na mikakati ya muda mfupi na mrefu ya kulifanya shirikisho hilo kusimama na kuwa na nguvu pia kujenga umoja miongoni mwa wasanii wa sanaa za maonyesho kwa ajili ya utetezi wa haki na maslahi yao.

Katibu Mtendaji wa BASATA,Ghonche Materego aliwaeleza viongozi kwamba, kazi kubwa ya shirikisho hilo ni kufufua nguvu ya sanaa za maonyesho ambazo katika siku za hivi karibuni imefifia kutokana na ujio wa teknolojia mpya.Alisema kwamba, leo hii hakuna sehemu mtu anaweza Kwenda kuangalia ngoma, maigizo, sarakasi nk. na hii ni kutokana na wadau kulala,hivyo shirikisho halina budi kuja na mikakati ya kukuza sanaa hiyo adhimu.

Naye Mlezi wa Mashirikisho ya Wasanii,Mzee Rashid Masimbi ambaye pia ni Mjumbe wa Bodi ya BASATA alisema kwamba, kazi iliyoko mbele ya shirikisho hilo ni kuja na mpango kazi kabambe, kuandaa kanuni za kuliongoza shirikisho, kutafuta ofisi, kuongoza wanachama wapya na kusaka fedha kwa ajili ya kuendesha rasmi shughuli za shirikisho.

Kesho ni zamu ya Shirikisho la Sanaa Jongevu (Filamu) ambapo litapata rasmi viongozi wake na kuanza safari ya kuandika historia mpya katika tasnia ya sanaa nchini.Wadau wote mnakaribishwa sana kushiriki.Matokeo yatatangazwa kwenye vyombo vya habari

Matukio ya Kikao cha Kamati Kuu ya CCM Ddodoma Jana


Baadhi ya Wajmbe wa Kamati Kuu ya CCM wakikusanya makabrasha ya agenda za Kikao
cha Kamati Kuu ya CCM,mara baada ya kuahirishwa leo huko Dodoma Makao Makuu ya
Chama hicho.


Wajumbe wa wakimsikiliza katibu Mkuu wa CCM Rajab Yussuf Makamba akitoa taarifa
ya kuahirishwa kikao cha kamati kuu ya CCM leo Dodoma.picha kwa hisani ya Ramadhan Othman Abdalla.


Wajumbe wa Kamati Kuu ya CCM wakijadili jambo,wakiwa nje ya Ukumbi wa Mkutano
wa Mako Makuu ya CCM Dodoma leo.

HALI TETE CCM, CC YAAHIRISHWA


Sadick Mtulya, Dodoma

UKIUKWAJI mkubwa wa taratibu wakati wa kura za maoni, tuhuma za rushwa na wanachama kupinga maamuzi ya baadhi ya kamati za siasa za mikoa kugeuza matokeo, ni mambo ambayo yanaendelea kuisumbua CCM kiasi cha kamati kuu kulazimika kuahirisha kikao ambacho kilitakiwa kufanyika jana.

Ratiba ya awali ilionyesha kuwa kamati hiyo ingefanya kikao chake jana na leo kujadili ajenda za halmashauri kuu baada ya kamati ya maadili kumaliza kuzipitia ajenda hizo.

Lakini, taarifa zilizolifikia gazeti hili jana zilieleza kuwa kamati ya maadili ilishindwa kumaliza kazi ya kupitia ajenda hizo kutokana na wingi wa malalamiko yaliyowasilishwa na wagombea na baadhi ya wanachama kupinga matokeo ya kura ya maoni na maamuzi ya kamati za siasa.

Katibu mkuu wa CCM, Yusuf Makamba aliwaambia wajumbe wa kamati kuu jana akisema: “... kikao chetu cha leo cha CC kimepata udhuru kidogo, hivyo tumekiahirisha hadi kesho saa 3:00 asubuhi.

“Sababu kuu ni kamati ya maadili ya chama hadi sasa (saa 9:26 alasiri) bado haijamaliza kazi yake.”

Kikao cha kamati ya maadili kilianza jana majira ya 5:00 asubuhi mara baada ya sekretarieti ya CCM kumaliza kikao cha kuandaa ajenda za kamati kuu. Sekretarieti ilikuwa na kikao chake kuanzia juzi.

Hata hivyo, vyanzo vyetu vilisema uzito wa malalamiko yaliwayosilishwa kuhusu mchakato mzima wa kura ya maoni ya kuchagua wagombea ubunge na udiwani ulivyofanyika Agosti mosi, hasa vitendo vya rushwa, ndio sababu kubwa ya kamati ya maadili kushindwa kumaliza kikao chake kwa wakati.

“Kwa asilimia kubwa karibu wagombea wote waliojitokeza kwa ajili ya kuchaguliwa katika kura za maoni ya CCM, walivunja maadili ya chama, hasa kwa kujihusisha na vitendo vya rushwa," alisema mmoja wa watu walio karibu na kamati kuu.

“Suala hili ndilo limesababisha kamati kushindwa kumaliza kikao chake kulingana na ratiba.”

Baada ya kauli ya Makamba, baadhi ya wajumbe wa kamati ya maadili, akiwamo rais mstaafu wa serikali ya awamu ya pili, Alhaji Ali Hassan Mwinyi na wa awamu ya tatu, Benjamin Mkapa walitoka katika kikao cha ndani cha kamati hiyo na kuchukua nyaraka zao zilizokuwepo katika meza kuu ya ukumbi wa White House na kurudi nazo ndani, kuashiria kuendelea na kikao cha kamati ya maadili.

Kampeni na kura za maoni za CCM zilitawaliwa na vitendo vya rushwa na kusababisha wagombea wengi na viongozi wa matawi na kata wa chama hicho kukamatwa na kuhojiwa na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru). Hadfi sasa ni wagombea watatu tu ambao wameshafikishwa mahakamani.

Mbali na vitendo vya rushwa, upigaji kura za maoni ulitawaliwa na ukiukwaji mkubwa wa taratibu uliosababisha vurugu kwenye baadhi ya vituo na hivyo kusababisha wagombea wengi kukata rufaa baada ya matokeo kutangazwa wakidai kuwa kulikuwa na rafu nyingi.

Vikao vya kamati za siasa za mkoa ambazo hutoa alama kwa wagombea navyo viliamsha tatizo jingine kutokana na wanachama karibu katika kila mkoa kufanya maandamano kwenda kwenye ofisi za chama hicho kupinga taarifa zilizokuwa zimezagaa kuwa washindi kwenye kura hizo wamepewa alama za chini zinazomaanisha kuwa hawastahili kupitishwa na chama kugombea.

Kamati ya maadili inaongozwa na Rais Jakaya Kikwete ambaye pia ni mwenyekiti CCM, na wajumbe wengine ni pamoja na makamu mwenyekiti wa CCM Bara, Pius Msekwa, na makamu mwenyekiti wa CCM Zanzibar, Amani Abeid Karume ambaye pia ni rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.

Wengine ni Makamba, marais wastaafu, Mwinyi na Mkapa.

Katika hatua nyingine, wajumbe wote wa kamati kuu jana walihudhuria kikao isipokuwa mwanasiasa mkongwe, John Samuel Malecela pamoja na waziri mkuu wa zamani, Edward Lowassa.

Haikuweza kufahamika sababu ya wajumbe hao kukosekana katika kikao hicho muhimu cha chama.

Baadhi ya wajumbe waliohudhuria ni spika wa Bunge anayemaliza muda wake, Samuel Sitta, na naibu wake, Anne Makinda, spika wa Baraza la Wawakilishi, Pandu Amir Kificho, mgombea mwenza wa urais kwa tiketi ya CCM, Dk Ghalib Bilal pamoja na Abdallah Kinana.

Katika hatua nyingine, wanachama 40 wa CCM Kata ya makulu jana walikamatwa wakati walipokuwa wakiandamana kwenye kundi la wanachama 100 kupinga kubadilishwa kwa jina la Ally Bilingi aliyeshinda katika kura za maoni za udiwani katika kata hiyo.

Mwenyekiti wa Kitongoji cha Bilingi, Steven Ngogo aliliambia Mwananchi kuwa waliamua kwenda ofisi ya CCM ya Wilaya ya Dodoma Mjini kuhakikisha kama kweli ushindi wa Bilingi ulibatilishwa.

“Tulikuwa zaidi ya 90, lakini wenzetu zaidi ya 40 wamekamatwa na Polisi majira ya saa 6:00 mchana wakati tulipokuwa tunakuja huku kama kweli jina la Bilingi ambaye alishinda kwa kura 190, limeondolewa,’’ alisema Ngogo.

Ngogo alifafanua kwamba taarifa ya kubadilishwa kwa ushindi wa Bilingi ziliwafikia mapema na kwamba ilisemekana uamuzi huo ulitokana na kamati ya siasa ya kata kumpa alama ya D.

Hata hivyo, mwenyekiti wa wilaya hiyo, Denis Bendera aliwahakikisha wanachasma hao kuwa hakuna matokeo yeyote yaliyobatilishwa.
“Hakuna matokeo yeyote ya kata na viti maalum hadi sasa yaliobatilishwa. Lakini Agosti 15, ndio majibu yatatolewa rasmi na mtapewa siku tatu za kupinga,’’ alisema Bendera.

Kamanda wa polisi wa Dodoma, Steven Zelothe alisema: "Kwa sasa siwezi kuzungumzia kukamatwa kwa hao watu... wewe si unajua kwamba kwa sasa Dodoma ina ugeni mkubwa wa rais, makamu, mawaziri,” alisema Zelothe.

CHANZO: MWANANCHI

UTAFUTAJI WA WABUNIFU UMEANZA SASA


Ubunifu wa Vera Swao katika Swahili Fashion week 2009
Modo akiwa katika vazi la Kemi Kalikawe Swahili Fashion week 2009

Modo wa kiume katika vazi la Manju Msita Swahili Fashion Week 2009


Kwa mara nyingine tena sekta ya ubunifu Tanzania inatoa fursa kwa wabunifu wote wenye ndoto za kuwa wabunifu bora kushikiri katika shindano la kuibua vipaji vya wabunifu hapa Tanzania . Shindano hili la mwaka limekua likifanyika chini ya mwanvuli wa jukwaa kuu la Africa Mashariki Swahili Fashion Week.

“Tunaangalia wabunifu ambao wana malengo ya kuwa wabunifu bora wa mavazi hapa Tanzania ” Alisema Mustafa Hassanali, mbunifu maaruvfu wa mitindo ambaye ndiye mwandaaji wa shughuli hiyo .

"Shindano hili linafanyika kwa mwaka wa tatu sasa, halina kikwazo cha umri, na linatoa fursa kwa watu wote wanaoamini kwamba wana kipaji cha ubunifu, na wanataka kuwa wabunifu. “Swahili Fashion Week ni jukwaa bora kwa wabunifu kuonyesha uwezo wao wa ubunifu na kuibua sindano la wabunifu wapya, ni jukwaa linalowawezesha watu kufikia malengo yao ”, aliongeza Mustafa Hassanali, ambaye pia ndiye mwasisi wa Swahili Fashion Week.

Shindano hili linatoa fursa kwa wabunifu kutoka pande zote za Tanzania . Mwisho wa kujisajili ni tarehe 30th ya mwezi wa August 2010. “Mwaka 2008 Edwin Musiba alishinda, na mwaka 2009 alishinda 2jenge Afrika Matalay, najiuliza nani atashinda mwaka huu?”, alimalizia Hassanali.

Kwa maelezo zaidi kuhusiana na shindano la ubunifu, tafadhali wasilina na Mratibu wa Swahili Fashion Week bwana
Washington Benbella,
simu namba
0717 547792

au
kupitia barua pepe ,

designers@swahilifashionweek.com

THE DON HIMSELF

Karibuni sana kwenye blog hii ya kijamii iliyosheheni makila kitu kuanzia siasa uchumi afya na burudani kwa ujumla wake.uingiapo kwenye blog hii ni mengi ambayo utapata nafasi ya kukutana nayo,kumbuka mawazo yako ndo hasa yanayojenga na kunifanya niwe na ufanisi zaidi.kariiiiiiibuuuuuuuuuuuu saaaaaaaaaaaaaaanaaaaaaaaaa.(THE DJ HIMSELF-JIWE)

Followers

BLOG ZA MARAFIKI

Search This Blog

ZILIZOPITA

DUNIA MUZIMA