Aug 14, 2010

Rais Kikwete aongoza Kikao Cha halmshauri Kuu ya CCm TaIFA MJINI Dodoma jana aagana na Balozi wapya wa Tanzania Ufaransa na Marekani!!

Mwenyekiti wa CCM Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Waziri Mkuu Mizengo Pinda muda mfupi kabla ya kuanza kwa kikao cha Halmshauri Kuu ya CCM Taifa mjini Dodoma leo asubuhi.Katikati ni Katibu mkuu wa CCM Yusuf Makamba. Baadhi ya wajumbe wa Halmashauri kuu ya CCM Taifa wakiwa katika kikao leo mjini Dodoma. Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiagana na Balozi mpya wa Tanzania nchini Ufaransa Mhe. Begum Taj wakati balozi huyo na mwenzake Balozi Mwanaidi Maajar(kulia) walipokwenda kumuaga ikulu ndogo mjini Dodoma leo asubuhi.Balozi Mwanaidi Maajar aliyekuwa balozi wa Tanzania nchini Uingereza anakuwa balozi wa Tanzania nchini Marekani na kituo chake cha kazi kitakuwa Washington. Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiongoza kikao cha halmashauri kuu ya CCm Taifa mjini Dodoma leo asubuhi.Wengine katika picha kutoka kushoto ni Rais Mstaafu awamu ya Tatu Benjamin William Mkapa, Rais Mstaafu awamu ya pili Mzee Ali Hassan Mwinyi,Makamu wa CCM Bara Pius Msekwa na kulia nia katibu mkuu wa CCM Yusuf Makamba.

No comments:

THE DON HIMSELF

Karibuni sana kwenye blog hii ya kijamii iliyosheheni makila kitu kuanzia siasa uchumi afya na burudani kwa ujumla wake.uingiapo kwenye blog hii ni mengi ambayo utapata nafasi ya kukutana nayo,kumbuka mawazo yako ndo hasa yanayojenga na kunifanya niwe na ufanisi zaidi.kariiiiiiibuuuuuuuuuuuu saaaaaaaaaaaaaaanaaaaaaaaaa.(THE DJ HIMSELF-JIWE)

Followers

BLOG ZA MARAFIKI

Search This Blog

ZILIZOPITA

DUNIA MUZIMA