Aug 13, 2010

BAADA YA 'MACHO KODO' DR LEADER SASA KUJA NA 'KAGOMA KWENDA'

MSANII wa muziki wa kizazi kipya nchini Lucas Silas "Dr.Leader" amewataka mashabiki wake wakae tayari kwa ajili ya ujio wake mpya na wimbo wake mwengine ambao unakwenda kwa jina la "Kagoma Kwenda" anayotarajia kuiachia hivi karibuni.

Msanii huyo ambaye kwa sasa anatamba na wimbo wake Macho Kodokodo ambao unafanya vizuri katika vituo mbalimbali vya redio hapa nchini,na Kueleza kuwa na wimbo huo ambao anatarajia kuuachia utakuwa mzuri zaidi.

Akizungumza na blog hii Dr.Leader alisema kuwa kwa sasa anacho angalia ni kitu gani ambacho mashabiki wake wanakuwa wanakiitaji ili kuweza kuwaridhisha pia kuweza kutambilika kimataifa kupitia mziki huo.

Dr.Leader alisema kuwa wasanii ambao ni chipukizi hawapaswi kukata tamaa hivyo waendeleee kufanya kazi zao vizuri na kwa kuzingatia maadili ya kazi zao pamoja na kujituma ili waweze kutambulika na kupata mafaniko.

Msanii huyo pia alielezea kuwa changamoto zinazowakabili wasanii wa mikoani ni kutokuwa na watu ambao wanakuwa wakiwasapoti katika kazi zao hivyo kuufanya mziki huo kuwa mgumu kwa kwa wasanii wa mikoani.

No comments:

THE DON HIMSELF

Karibuni sana kwenye blog hii ya kijamii iliyosheheni makila kitu kuanzia siasa uchumi afya na burudani kwa ujumla wake.uingiapo kwenye blog hii ni mengi ambayo utapata nafasi ya kukutana nayo,kumbuka mawazo yako ndo hasa yanayojenga na kunifanya niwe na ufanisi zaidi.kariiiiiiibuuuuuuuuuuuu saaaaaaaaaaaaaaanaaaaaaaaaa.(THE DJ HIMSELF-JIWE)

Followers

BLOG ZA MARAFIKI

Search This Blog

ZILIZOPITA

DUNIA MUZIMA