Aug 16, 2010

VODACOM TANZANIA YAFUTURISHA WATOTO YATIMA JIJINI DAR ES SALAAM!!

Mgeni rasmi Sheikh Mkuu wa Tanzania Sheikh Issa Shaabani Simba akisoma hotuba yake katika viwanja vya Karimjee leo jioni wakati wa Futari iliyoandaliwa na Kampuni ya simu za mkononi Vodacom Tanzania kupitia kitengo chake cha Vodacom Foundation maalum kwa watoto yatima wa vituo mbalimbali vya jijini Dar es salaam katika mfungo huu wa mwezi mtukufu wa (Ramadhan) ambapo waislamu kote duniani hufunga kama utekelezaji wa nguzo muhimu katika kumcha mwenyezi mungu.
Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Tanzania Bw. Dietlof Mare akizungumza wakati akikaribisha watoto yatima kutoka vituo mbalimbali vya jijini Dar es salaam na wageni waalikwa wakati wa futari kwenye viwanja vya karimjee leo jioni kushoto ni mkurugenzi wa kitengo cha Teknohama Vodacoma Tanzania Maharage Chande.
Sheikh Mkuu wa Tanzania Sheikh I ssa Shaabani Simba kushoto akipokea ndoo ya mafuta ya kula kutoka kwa Mkurugenzi wa Vodacom Tanzania Dietlof Mare kwa niaba ya watoto hao kama moja ya zawadi ambazo kampuni hiyo imetoa kwa vituo hivyo ili mkusaidia kwa ajili ya futari kulia nia Mkurugenzi Vodacom Foundation Mwamvita Makamba na katikati ni mmoja wa wasaidizi wa Sheikh Mkuu wa Tanzania Sheikh Issa Shaaban Simba.
Wafanyakazi mbalimbali wa vodacom wakiwa katika picha ya pamoja na watoto hao.
Sheikh Mkuu wa Tanzania Sheikh Issa Shaabani Simba kushoto akiwasili kwenye viwanja vya Karimjee kama mgeni rasmi katika futari iliyoandaliwa na Vodacom Tanzania kulia ni Mkurugenzi wa kampuni hiyo Dietlof Mare.
Mkurugenzi wa Vodacom Foundation Mwamvita Makamba akiwaongoza wageni walioonozana na Sheikh Mkuu Issa Shaaban Simba wakati walipowasili kwenye viwanja vya Karimjee.
Mkurugenzi wa Vodacom Foundation akiwa katika picha ya pamoja na watoto kwa ajili ya kupokea zawadi kutoka Vodacom.
Meneja wa Vodacom Foundation Yessaya Mwakifulefule kulia akiwa na wadau wa Vodacom Edwin Temba kati na mdau mwingine Mohamed Kalambo wa Vodacom.
.Afisa Uhusiano wa Vodacom Mwamvua Mlangwa kushoto, Afisa wa Vodacom Foundation Grace Lyon katikati na Meneja Mawasiliano wa Vodacom Tanzania Necta Foya wakijiandaa kupokea wageni mbalimbali katika futari hiyo.
Hapa watoto wakiimba kaswida kabla ya muda wa kufuturu kuwadia.
Hapa watoto wakisuburi kufuturu vituo mbalimbali vya kulelea watoto villialikwa na mkuleta watoto kwa ajili ya kupata futari na wenzao ktoka maeneo mbalimbali ya jiji la Dar es salaam.

No comments:

THE DON HIMSELF

Karibuni sana kwenye blog hii ya kijamii iliyosheheni makila kitu kuanzia siasa uchumi afya na burudani kwa ujumla wake.uingiapo kwenye blog hii ni mengi ambayo utapata nafasi ya kukutana nayo,kumbuka mawazo yako ndo hasa yanayojenga na kunifanya niwe na ufanisi zaidi.kariiiiiiibuuuuuuuuuuuu saaaaaaaaaaaaaaanaaaaaaaaaa.(THE DJ HIMSELF-JIWE)

Followers

BLOG ZA MARAFIKI

Search This Blog

ZILIZOPITA

DUNIA MUZIMA