Naibu Waziri wa Viwanda, biashara na Masoko Dk. Cyril A. Chami akimpatia zawadi wa bahati nasibu ndogo ya viatu iliyofanyika katika uzinduzi huo,Bw. Victor Mushi,ambapo watu kadhaa walijinyakulia zawadi hizo za viatu vikiwemo viatu mbalimbali vya usalama..Ni globu ya kijamii inayojihusisha na mambo yote ya kijamii,natumaini jamii yangu ya kitanzania itafaidika sana pindi ichukuapo fursa ya kuperuzi kwenye globu hii,dhamira yangu ni kufikisha ujumbe pamoja na kuiburudisha jamii yangu na furaha yangu ni kuona natimiza dhamira yangu kwako.natumaini kuwa wewe utaniunga mkono kwa kile ambacho nataka kukifanya kwa ajili ya jamii yangu ya kitanzania.NASHUKURU KWA KUNIELEWA.
Aug 25, 2010
UZINDUZI WA KIPINDI CHA ZAMARADI CHA TAKE ONE KILIVYOFANA JANA,
TANGAZO LA MSIBA (BANGALORE INDIA)
KWA NIABA YA FAMILIA YA MAREHEMU BWANA NA BIBI MWAKALASI YA KIJITONYAMA, BW RODRICK MWAMBENE NA BI JULIETH MWAKALASI WANAWATANGAZIA NDUGU NA JAMAA KUWA NDUGU YAO MPENDWA, EDWIN MBONELA MWAKALASI ALIYEKUWA ANASOMA NCHINI INDIA KATIKA CHUO CHA ACHARYA BANGALORE AMEFARIKI AGOSTI 21 BAADA YA KUUGUA KWA MUDA MFUPI.
PIA IBADA YA HESHIMA ZA MWISHO ZITATOLEWA KUANZIA SAA 6.00 MCHANA HAPO HAPO NYUMBANI KWAO.
KWA NIABA YA FAMILIA YA WA WAFIWA, TUNAPENDA KUTOA SHUKRANI ZA DHATI KWA WAFUATAO AMBAO WALIJITAHIDI KUOKOA MAISHA YA MAREHEMU KWA UPANDE WA MATIBABU MPAKA KUSAFIRISHA MWILI WAKE KUJA
SHUKRANI ZA HIZO ZIENDE KWA:-
UBALOZI WA
BWANA AMETOA, BWANA AMETWAA, JINA LA MBWANA LIHIMIDIWE, AMEN.
KWA MAELEZO ZAIDI WASILIANA NA BW RODRICK MWAMBENE KWA SIMU NAMBA 0754 362901, 0713 362901.
OpenSanit wazindua bidhaa zao jijini Dar
Mkurugenzi Mtendaji wa kampun ya Open Sanit,Bw.Octavian Mshiu akifafanua jambo kw a mgeni rasmi Naibu Waziri wa Viwanda, biashara na Masoko Dk. Cyril Chami kabla ya kuzindua bidhaa za kampuni ya Beier Safety Footwear ya Afrika Kusini ikishirikiana na kampuni ya Open Sanit Tanzania jioni ya leo ndani ya hoteli ya Sea Cliff jijini Dar
Mkurugenzi Mkuu wa kampuni ya BEIER SAFETY FOOTWEAR,Bw.Silvio Ceriani akizungumza machache mbele ya wageni waalikwa kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi kuzindua bidhaa za kampuni hiyo.
Naibu Waziri wa Viwanda, biashara na Masoko Dk. Cyril A. Chami akimpatia zawadi wa bahati nasibu ndogo ya viatu iliyofanyika katika uzinduzi huo,Bw. Victor Mushi,ambapo watu kadhaa walijinyakulia zawadi hizo za viatu vikiwemo viatu mbalimbali vya usalama..
Baadhi ya wageni waalikwa wakiangali baadhi ya bidhaa zinazotengenezwa na kampuni hizo mbili,bidhaa hizo za aina mbalimbali zinazotumika katika masuala ya usalama hasa viwandani na kwenye makampuni.
Mmgeni rasmi Naibu Waziri wa Viwanda, biashara na Masoko Dk. Cyril Chami (tatu kulia) akioneshwa aina ya bidhaa mbalimbali zitakazokuwa zikitengenezwa na kampuni hizo mbili,ya Beier Safety Footwear ktoka Afrika Kusini ikishirikiana na kampuni ya Open Sanit (Tanzania) jioni ya leo hoteli ya Sea Cliff jijini Dar.
Baadhi ya bidhaa zitakazokuwa zinatengenezwa na kampuni ya Beier Safety Footwear kutoka nchini Afrika ya Kusini ikishirikiana na kampuni ya Open Sanit ya Tanzania.kama vipi ingia http://www.opensanit.com/ kupata maelezo zaidi.Kilimanjaro Lager Kudhamini Bongo Star Search 2010
Na Mwandishi Wetu
Bongo star search ni moja ya kipindi kinacho rushwa na television hapa nchini Tanzania ambacho kime fanikiwa kwa kiwango kikubwa kabisa kuinua vipaji vya wanamuziki wa Tanzania.
Ikumbukwe kuwa mwaka jana kampuni ya kutengeneza bia hapa nchini TBL kwa kupitia kinywaji chake kinachojihusisha na maswala ya muziki,Kilimanjaro premium lager. Ilishiriki kama mmoja wa wadhamini wa shindano hilo.
Uhusiano huu mkubwa wa kampuni hizi mbili umetokana na sababu kuu kwamba BSS inahusika kutafuta na kuinua vipaji vya wanamuziki hasa vijana wa umri wowote ambapo Kilimanjaro premium lager kufuatia kauli mbiu yake ya Kufikisha Muziki wa Tanzania Kilele cha mafanikio kwa upande mwingine ina husika na muziki wa vijana wa Kitanzania.
Kilimanjaro premium lager imekua ikunga mkono juhudi za kuendeleza Muziki hapa Tanzania kwa kiwango cha juu.. Ikiwa mdhamini mkubwa kwenye zoezi la kutoa Tunzo za Muziki Tanzania kila mwaka,Tunzo zinazojulikana kama Kilimanjaro Tanzania Music Awards. Ndio maana Kilimanjaro premium lager imeona hakuna sababu ya wao kutoshirikiana na BSS 2010 katika kuinua vipaji vya wanamuziki wa Tanzania.
Kilimanjaro premium lager imeandikisha mkataba wa kuwa mdhamini wa Bongo star search kwa kipindi cha miaka mitatu ambayo ni BSS 2010, BSS 2011, BSS 2012.
Washiriki wa BSS watashirikishwa katika mambo mbali mbali yakiwemo mashindano yatakayo kua yanafanyika siku hadi siku katika jumba la BSS KILI HOUSE 2010.
BSS 2010 itakuwa ikirusha hewani kila jumapili saa tatu na robo usiku (3:15) kupitia television ya ITV ikishirikiana na Radio one na magazeti ya The Guardian ,Nipashe.unatakia kufuatilia shindano hilo bila kukosa na pia ni muhimu kupiga kura yako ili kuweza kuwachagua watakao weza kushiriki mpaka mwisho .
ziara ya miss tanzania katika ziwa manyara
ZIARA ya warembo 30 wanaoshiriki katika shindano la Vodacom Miss Tanzania 2010 kutembelea vivutio na rasilimali tofauti nchini zilizopo kanda ya kaskazini imeendelea na jana walikuwa Hifadhi ya Taifa ya Ngorongoro (NCA) iliyopo mkoani Arusha.
Wakiwa ndani ya hifadhi hiyo licha ya kujionea moja ya maajabu saba ya dunia yaani bonde la Ngorongoro walipata fursa ya kujionea wanyama na baionuwai za aina mbalimbali kama vile Simba,Tembo,chui na ndege wa aina tofauti.
Mbali na hayo walijionea pia maboma ya Maasai ambayo nayo yanatumika kutangaza utamaduni wa kabila la wamaasai ambao na kuwezesha kuingiza serikali fedha nyingi za kigeni kutoka kwa watalii wanaotembelea hifadhi hiyo.
Akizungumzia kuhusiana na aliyojifunza ndani ya Ngorongoro mmoja wa warembo Angelina Ndege kutoka Mkoa wa Lindi kanda ya mashariki alisema amejifunza kwamba kuna hifadhi zingine siyo lazima waishi wanyama pori tu bali hata binadamu nao wanaishi.
“Tangia nizaliwe miaka 19 iliyopita sikuwahi kufikiri kama wanyamapori hawawezi kuishi na binadamu, lakini ndani ya bonde la Ngorongoro nimeshuhudia wanyama wakiishi na binadamu tena bila rabsha yoyote,” alisema Ndege.
Aidha alibainisha kuwa ameweza kujifunza kwamba wanyama huwa hawakai katika hifadhi moja bali huwa wanahama na kwenda sehemu zingine kutafuta malisho kuendana na hali ya hewa.
Kutokana na hilo aliwaomba Watanzania kujenga tabia ya kutembelea hifadhi za taifa zilizopo nchini na kuachana na fikra kwamba wanaopaswa kwenda katika maeneo hayo ya rasilimali za taifa ni watalii kutoka nje tu ili kusaidia kuinua uchumi wa nchi kupitia sekta ya utalii.
Mary Magali ambaye ni mrembo anaewakilisha mkoa wa Iringa aliwashukuru wadhamini wakuu wa mashindano haya ambao ni Vodacom Tanzania kwa kudhamini mashindano haya pamoja na gharama zote za kutembelea hifadhi za taifa kanda ya kaskazini ili kujionea na kujifunza kuhusiana na rasilimali za taifa.
“La muhimu nililojifunza baada ya kutembelea hifadhi za taifa ya Kinapa na Ngorongoro ni kufahamu kuhusiana na Simba wanaopanda miti wanaopatikana ndani ya kreta ikiwemo maji yam to wa mbu na kirurumo kukutana sehemu moja inayotumiwa na viboko kulala na kusambaa ziwani,” alisema Magali.
Naye Mlezi wa warembo hao ambae alikuwa mshiriki wa Vodacom Miss Tanzania 2009,Gladys Shao, alisema warembo wote wanaendelea vizuri na maandalizi na hawana matatizo yoyote ya kiafya na kwamba wanafurahia na kujifunza mambo mbalimbali ya utalii wa ndani kwani unaanza na Mtanzania mwenyewe.
bongocelebrity yafanya mahojiano na Madaraka Nyerere
Mwaka jana mwezi wa nne(April) yeye na Jaffar Amin(mtoto wa Iddi Amin-Rais wa zamani wa Uganda) waliingia katika vitabu vya kumbukumbu vya wapenda amani duniani walipokutana kwa mara ya kwanza ikiwa ni ishara ya amani na usuluhisho barani Afrika na kwingineko.
Dr. Bilali aanza kampeni mkoani Pwani
Mgombea Ubunge wa Jimbo la Kilwa Kusini, Ramadhan Madabida (kulia) akiteta jambo na Mgombea Mwenza, Mohamed Gharib Bilal, wakati wakimpokea kutoka Wilaya ya Rufiji kuingia Wilaya ya Kilwa Masoko akiwa katika safara ya Kampeni kwenye Mkoa huo wa Pwani.
Mkuu wa Wialaya ya Kilwa Masoko, Nurdin Babu akiongozana na Mgombea Mwenza wa Urais, Dr. Mohamed Gharib Bilali wakati alipompokea mpakani mwa Wilaya ya Rufiji kuingia kwenye Wilaya yake kuendelea na mkutano wa Kampen
Mgombea Mwenza wa urais,Dr. Mohamed Gharib Bilal, akimnadi mgombea Ubunge wa Jimbo la Rufiji kupitia tiketi ya Chama cha Mapinduzi, Dk. Seif Rashid, wakati wa mkutano wa Kampeni uliofanyika kwenye Viwanja vya Shule ya Msingi Muhoro, Tarafa na Kata ya Muhoro, Wilaya ya Rufiji Mkoa wa Pwani.
Umati wa watu, Wakazi wa Somanga wakimzunguka Mgombea Mwenza na kufunga barabara kwa muda ili kumpokea mgombea huyo alipokuwa akipita eneo hilo kuelekea Wilaya ya Kilwa Masoko. Na Mwandishi Wetu,Pwani
MGOMBEA mwenza wa Urais kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi(CCM),Dr. Mohamed Bilal amesema ifikapo mwaka 2015 kila shule ya msingi kote nchini itapaswa kuwa na darasa moja la wa chekechea.
Dk.Bilali aliyasema hayo jana wakati akiwahutubia wananchi wa wilaya ya Rufiji katika mkutano wa adhara uliofanyika katika uwanja wa Shule ya Msingi ya Mhoro Kata ya Chumbi mkoani Pwani sambamba na kumnadi mgombea ubunge wa Jimbo la Rufiji Dk. Seif Rashid na mgombea ubunge wa Jimbo la KIbiti,Abdul Marombwa,alisema mpango huo mkakata umeainishwa katika Ilani ya CCM ya mwaka 2010-2015.
Dk.Bilali ambaye jana ndiyo alianza ziara ya kampeni yake rasmi mkoani hapa alisema lengo la mpango huo kuingizwa kwenye ilani hiyo ya CCM, ni chama hicho kupitia serikali yake inataka kuona wanafunzi wa shule wanaomaliza shule za awali wanajiunga na shule za msingi na sekondari na kisha kujiunga na vyuo vikuu.
“Hivi sasa taifa lisilo na wasomi ni dhahiri halitaweza kupiga hatua za kimaendeleo kwa wakati hivyo kwakuwa inapenda kuona wananchi wake wakubwa kwa wadogo wakipita elimu ndiyo maana ilani ya mwaka 2010-2015 imewekea mkazo suala la ukuzwaji wombea sekta ya elimu kwa ngazi zote hivyo nawasii sana wazazi na wananchi kote nchini muwaruhusu watoto wenu waende mashuleni kupata elimu kwani hakuna ulithi usiooza kama elimu.
Huku hotuba yake ikikatishwa mara kwa mara na vibwagizo vya nyimbo za kukisifu chama na kumpongeza rais Jakaya Kikwete kumchagua Dk.Bilali kuwa mgombea mwenza, alisema ili mpango huo utimie wananchi wa kada zote hawana budi kuinga mkono serikali ya ccm ilikuweza ujenzi huo wa madarasa ya wananfunzi wa shule za awali yanajengwa na kuongeza kwa kuwataka wananchi wote wanampatia kura za ndiyo mgombea urais wa ccm,Kikwete Leo mgombea mwenza ataendelea na ziara yake ya kampeni mkoani Kilwa.
Aug 24, 2010
vodacom miss tanzania watembelea mbuga ya ngorongoro
Rais Kikwete Akiwa Sengerema
MKALI AMBAYE KIDUMU AMEKOPY NA KUPEST STYLE YA MELODY NA SAUTI YAKE.(LINEX - LINENGA)
O ten akiwa na LINEX wakiingia ndani ya uwanja wa taifa kuhudhuria moja ya matamasha ya muziki wa kizazi kipya siku za hivi karibuni.
anajulikana kama LINEX SUNDAY wengi humuita LINENGA ambaye kwa sasa anasumbua kwa ngoma yake inayokwenda kwa jina la MAMA HALIMA.
LINEX & O TEN wakiwa kwenye moja ya matamasha yao
linexAug 23, 2010
Aug 22, 2010
ZIARA YA WAREMBO WA VODACOM MISS TANZANIA (KINAPA)
DEWJI APITA BILA KUPINGWA, PINGAMIZI DHIDI YAKE ZATUPWA.
Na Hillary Shoo,
Singida.
Mgombea Ubunge kwa tiketi ya (CCM) jimbo la Singida mjini (pichani) Mohammed Dewji ameteuliwa kuwa mgombe pekee wa jimbo hilo baada ya pingamizi lililotolewa na wapinzani wake kutupwa na msimamizi wa uchaguzi jimbo hilo.
Hatua hiyo imekuja siku chache baada ya wagombe wa vyama vingine vya upinzani, Josephat Isango wa CHADEMA na Omary Sombi wa chama cha AFP kuwasilisha pingamizi kwa msimamizi kuwa Dewji alikiuka sheria ya gharama za chaguzi.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari na msimamizi wa uchaguzi Jimbo la Singida mjini Yona Lucas Maki ambaye pia ni Mkurugenzi wa Manispaa ya Singida ilieleza kuwa baada ya kupitia kwa kina pingamizi hizo, imeonekana kuwa Dewji hakukiuka sheria ya gharama za uchaguzi kama walivyodai wapinzani wake.
Kwa mujibu wa barua yenye kumb Na. HM/SI/U.10/16/VOL.1/140 ya Agosti 21 mwaka huu kwa wagombea hao ilieleza kuwa ninawaletea uamuzi wa pingamizi hizo, mimi Yona Lucas Maki ambaye ni msimamizi wa uchaguzi jimbo la Singida, baada ya kupata maelezo ya utetezi uliyoyatoa dhidi ya pingamizi uliyowekewa ya kupinga uteuzi wa wewe Mohammed Dewji.
“Ninakataa pingamizi zilizotolewa kwa sababu haujatenda vitendo vinavyokataza chini ya sheria ya gharama za uchaguzi.”alisema Maki.
Aidha alisema kwa mujibu wa maeleekezo kwa wasimamizi wa uchaguzi , uchaguzi wa Rais , wabunge na madiwani , 2010 aya ya 5.16 kifungu cha 44 kinasema, “Kwa mujibu wa kifungo cha 44 cha sheria ya uchaguzi Na.1 ya mwaka 1985( sura ya 343) endepo mgombea aliyeteuliwa ni mmoja , baada ya kukamilisha hatua ya pingamizi atatangazwa kuwa amepita bila kupingwa , na uchaguzi hautafanyika katikaaa jimbo hilo. Tume ya Taifa ya uchaguzi itatangaza katika gazeti la serikali kuwa mgombea huyo amechaguliwa kuwa Mbunge.
“ Kwa nukuu hii hapa juu nakutangaza rasmi kuwa mgombea Ubunge ambaye umepita bila kupingwa katika uchaguzi mkuu kwa mwaka 2010 katika jinbo la singida mjini.”ilisema taarifa hiyo ya Maki.
Hata hivyo Dewji alitoa maelezo yake kwa msimamizi huyo kuwa kwamba pingamizi lililotolewa chini ya sheria ya gharama za uchaguzi ni lazima lielezee matendo yasiyoendana na kifungu cha 9 cha sheria ambacho kinatamka mgombea aeleze fedha na vyanzo vingine vya fedha atakazotumia wakati wa kampeni kwa chama chake ndani ya siku 7 zitakazotamkwa na sheria.
Dewji alisema si hivyo tu sehemu ya tano ya sheria ya gharama za uchaguzi ya mwaka 2010 iko wazi kwa kutamka wazi matendo ambayo yanaweza kubatilisha haki ya mtanzania kuwa mgombea ubunge.
“Kutokana na na sheria hiyo ninaomba pingamizi lililotolewa na Josephat Isango wa Chadema na Omary Sombi wa AFP yatupiliwe mbali kwa sababu limetokana na sheria isiyokuwepo hapa Tanzania.” Alisema Dewji.
Rais Kikwete Atua Mwanza na Kumnadi Mgombea Ubunge wa Jimbo la Misungwi
Rais Jakaya Kikwete akikagua gwaride la chipukizi mara baada ya kutua jijini Mwanza leo kwa kampeni mkoa huo wa kanda ya ziwa
Rais Jakaya Kikwete akisalimiana na Mbunge wa Nyamagana Mh. Lawrence Masha ambaye kapita bila kupingwa katika jimbo lake. Anayemfuata ni Mh. William Ngeleja mbunge wa Sengerema ambaye naye kapita bila kupingwa
Wagombea ubunge wa CCM kanda ya ziwa wakimsubiri Rais Jakaya Kikwete alipotua jijini Mwanza leo.
Viongozi mbali mbali walijitokeza kumpokea Rais Jakaya Kikwete leo jijini Mwanza
Viongozi wa dini wa madhehebu mbalimbali wakisubiri kumlaki Rais Jakaya Kikwete jijini Mwanza leo kwa kampeni mkoa huo wa kanda ya ziwa.



