Aug 25, 2010

Dr. Bilali aanza kampeni mkoani Pwani


Mgombea Ubunge wa Jimbo la Kilwa Kusini, Ramadhan Madabida (kulia) akiteta jambo na Mgombea Mwenza, Mohamed Gharib Bilal, wakati wakimpokea kutoka Wilaya ya Rufiji kuingia Wilaya ya Kilwa Masoko akiwa katika safara ya Kampeni kwenye Mkoa huo wa Pwani.
Mkuu wa Wialaya ya Kilwa Masoko, Nurdin Babu akiongozana na Mgombea Mwenza wa Urais, Dr. Mohamed Gharib Bilali wakati alipompokea mpakani mwa Wilaya ya Rufiji kuingia kwenye Wilaya yake kuendelea na mkutano wa Kampen
Mgombea Mwenza wa urais,Dr. Mohamed Gharib Bilal, akimnadi mgombea Ubunge wa Jimbo la Rufiji kupitia tiketi ya Chama cha Mapinduzi, Dk. Seif Rashid, wakati wa mkutano wa Kampeni uliofanyika kwenye Viwanja vya Shule ya Msingi Muhoro, Tarafa na Kata ya Muhoro, Wilaya ya Rufiji Mkoa wa Pwani.
Umati wa watu, Wakazi wa Somanga wakimzunguka Mgombea Mwenza na kufunga barabara kwa muda ili kumpokea mgombea huyo alipokuwa akipita eneo hilo kuelekea Wilaya ya Kilwa Masoko.
(Picha na Muhidin Sufiani)


Na Mwandishi Wetu,Pwani

MGOMBEA mwenza wa Urais kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi(CCM),Dr. Mohamed Bilal amesema ifikapo mwaka 2015 kila shule ya msingi kote nchini itapaswa kuwa na darasa moja la wa chekechea.

Dk.Bilali aliyasema hayo jana wakati akiwahutubia wananchi wa wilaya ya Rufiji katika mkutano wa adhara uliofanyika katika uwanja wa Shule ya Msingi ya Mhoro Kata ya Chumbi mkoani Pwani sambamba na kumnadi mgombea ubunge wa Jimbo la Rufiji Dk. Seif Rashid na mgombea ubunge wa Jimbo la KIbiti,Abdul Marombwa,alisema mpango huo mkakata umeainishwa katika Ilani ya CCM ya mwaka 2010-2015.

Dk.Bilali ambaye jana ndiyo alianza ziara ya kampeni yake rasmi mkoani hapa alisema lengo la mpango huo kuingizwa kwenye ilani hiyo ya CCM, ni chama hicho kupitia serikali yake inataka kuona wanafunzi wa shule wanaomaliza shule za awali wanajiunga na shule za msingi na sekondari na kisha kujiunga na vyuo vikuu.

“Hivi sasa taifa lisilo na wasomi ni dhahiri halitaweza kupiga hatua za kimaendeleo kwa wakati hivyo kwakuwa inapenda kuona wananchi wake wakubwa kwa wadogo wakipita elimu ndiyo maana ilani ya mwaka 2010-2015 imewekea mkazo suala la ukuzwaji wombea sekta ya elimu kwa ngazi zote hivyo nawasii sana wazazi na wananchi kote nchini muwaruhusu watoto wenu waende mashuleni kupata elimu kwani hakuna ulithi usiooza kama elimu.

Huku hotuba yake ikikatishwa mara kwa mara na vibwagizo vya nyimbo za kukisifu chama na kumpongeza rais Jakaya Kikwete kumchagua Dk.Bilali kuwa mgombea mwenza, alisema ili mpango huo utimie wananchi wa kada zote hawana budi kuinga mkono serikali ya ccm ilikuweza ujenzi huo wa madarasa ya wananfunzi wa shule za awali yanajengwa na kuongeza kwa kuwataka wananchi wote wanampatia kura za ndiyo mgombea urais wa ccm,Kikwete Leo mgombea mwenza ataendelea na ziara yake ya kampeni mkoani Kilwa.

No comments:

THE DON HIMSELF

Karibuni sana kwenye blog hii ya kijamii iliyosheheni makila kitu kuanzia siasa uchumi afya na burudani kwa ujumla wake.uingiapo kwenye blog hii ni mengi ambayo utapata nafasi ya kukutana nayo,kumbuka mawazo yako ndo hasa yanayojenga na kunifanya niwe na ufanisi zaidi.kariiiiiiibuuuuuuuuuuuu saaaaaaaaaaaaaaanaaaaaaaaaa.(THE DJ HIMSELF-JIWE)

Followers

BLOG ZA MARAFIKI

Search This Blog

ZILIZOPITA

DUNIA MUZIMA