






Ni globu ya kijamii inayojihusisha na mambo yote ya kijamii,natumaini jamii yangu ya kitanzania itafaidika sana pindi ichukuapo fursa ya kuperuzi kwenye globu hii,dhamira yangu ni kufikisha ujumbe pamoja na kuiburudisha jamii yangu na furaha yangu ni kuona natimiza dhamira yangu kwako.natumaini kuwa wewe utaniunga mkono kwa kile ambacho nataka kukifanya kwa ajili ya jamii yangu ya kitanzania.NASHUKURU KWA KUNIELEWA.
Na Hillary Shoo,Singida.
HATIMAE sakata la Mgombea Ubunge wa Jimbo la Singida mjini kupitia chama cha CHADEMA, Josephat Isango kudai kuwa mgombea mwenzake wa CCM, Mohammed Dewji amelikodi gari alilokuwa akitumia mgombea huyo kwenye kampeni,limeingia katika sura mpya baada ya mmiliki wa gari hilo kudai kuwa alimnyang’anya kutokana na usumbufu wa malipo na kwenda kinyume na makubaliano.
Akizungumza na gazeti hili nyumbani kwake jana mmiliki wa gari hilo Saidi Madeira alisema kuwa gari hilo lilikodiwa na ofisi ya CCM mkoa wa singida na wala Dwewji hahusiki na hilo.
"Mimi niwe muwazi kwa kweli Dewji sijawahi kuzungumza nae kuhusu suala la gari langu na wala mtu yoyote kutoka katika ofisi yake, mimi gari nimelikodi kwa Katibu wa CCM Mkoa wa Singida baada ya kuona hawa jamaa wa CHADEMA ni wababaishaji katika suala la malipo.
"Awali tulikubaliana kuwa kila siku gari hilo litalipiwa shilingi 20,000 ikiwa ni pamoja na kuwaziwa mafuta na kumlipa dreva lakini nilikaa karibu wiki nzima sijalipwa fedha zangu na mbaya zaidi gari lilikuwea linakwenda hadi Ikungi sehemu ambayo haikuwa katika makubaliano namia." Alisisitiza Madeira na kuongeza.
"Malipo yalivyokuja na kushauriana na familia yangu tukaona tusiwape tena hili gari hawa jamaa wa Chadema maana linakwenda kinyume na makubaliano ndipo alifika Katibu wa CCM mkoa Naomi Kapambala na kulihitaji gari hilo kwa ajili ya shughuli zao za chama.
Alisema baada ya kuafikiana na katibu juu ya utaratibu mzima wa kazi aliamua kuwapa gari hilo aina ya Suzuki Vitara lenye namba za usajili T 663 ASZ na alilipwa fedha zake zote hadi mwisho wa uchaguzi mkuu kwisha Oktoba 31 mwaka huu.
Aidha Madeira alisema hivi sasa gari hilo liko chini ya ofisi ya CCM mkoa na wala halipo kwenye kampeni za Dewji kama inavyodaiwa na watu.
"Mimi sijawahi kuzungumza na mwandishi wa habari juu ya hili gari zaidi yako leo wewe unayenihoji, nashangaa sana kuasikia kuwa mimi nimezunguza na vyombo vya habari hii sio kweli uhandishi wa namna hii ni wa kunichonganisha mimi pamoja na familia yangu kwa ujumla."Alisisitiza.
Hata hivyo Madeira amesema kuwa anandaa utaratibu wa kisheria ili aweze kmfikisha mwandishi wa habari aliyeandika habari hiyo mahakamani ili aweze kuthibitisha madai hayo, kuwa Dewji alikodi gari hilo.
Kwa upande wake Dewji alisema anasikitishwa sana na taarifa hizo na kwamba hajawahi kukodi gari la mtu yoyote binafsi kwa ajili ya shughuli zake za kampeni.
"Mimi nina magari yangu matatu ambayo ndiyo nayatumia katika kampeni sasa nikodi gari jingine la nini, siwajawahi kufanya hivyo na wala sina haja ya magari mengine haya niliyonayo yananitosheleza kufika kila eneo na kuzungumza na wapiga kura wangu." Alisema Dewji kwa masikitiko makubwa.
Hata hivyo Dewji aliwataka wananchi pamaoja na wanachama wa CCM hivi sasa kuwa watulivu na kuachana na siasa za kuchafuana na badala yake wasubiri siku ya kupiga kura ili wamalize kazi.
Katibu wa CCM mkoa wa singida Naomi Kapambala amesema kuwa gari hilo wamelikodi wao kwa ajli ya shughuli za chama na wala Dewji hahusiki kwa lolote.
"Sisi ndio tumelikodi hili gari, Dewji hahusiki kabisa,yeye ana magari yake anayotumia katika kampeni zake, sasa hili la nini tena kwake alihoji Kapambala."Alisema
Trade and commerce in Africa has received a major boost with the introduction of two trade related products; AfriCash and Afritrade by United Bank for Africa (UBA) Tanzania Limited. These unique products have been designed by UBA to facilitate trade transactions across the continent.
The two products which were launched in Dar es Salaam on Wednesday October 27, 2010 will leverage on the
growing continental presence of UBA, currently in nineteen African countries.
While launching the products in Dar es Salaam, Managing Director /CEO for United Bank for Africa (UBA) Tanzania Limited, Mr. Ayobola Abiola said that the products were conceived to ease the stress associated with business transactions and payment processes across borders within Africa.
Abiola said the Afritrade product is designed to give customers convenience in payments to third party in any part of the continent. According to him, “Customers of Afritrade are required to apply for trade transaction at any UBA business office with necessary documents while the initiating UBA location advises the benefiting UBA location in the country of the beneficiary and on receipt of transaction message, beneficiary is notified immediately via phone/e-mail and official written notification is sent within 24hours enclosing original copy of the transaction instrument where applicable, and goods are shipped (or services rendered) by beneficiary.
Documents are presented by beneficiary and examined by UBA staff for regulatory compliance. Claim for value of documents is sent to initiating UBA location and documents sent by courier. Payment is made to beneficiary within 24hours of submission of compliant claim.”
He listed benefits of the Afritrade to the customer to include; significant cost savings to the customer as it provides lower charges than normal local tariff for trade transactions, Real-Time trade payments into accounts within East African Community (EAC), Union Economique et Monétaire Ouest Africaine (UEMOA) and Central African Economic and Monetary Community (CEMAC) regions, faster resolution of discrepancies, same Day completion of Intra-African Transactions by leveraging on our business offices across Africa and not international correspondent banks among others.
In addition, he noted that the previously introduced ‘AfriCash’ has been repositioned to target financial remittances from individuals and groups within Africa which have increased dramatically over the past decade. He emphasized that the UBA AfriCash is available in all the 19 countries where the bank has presence including, Kenya, Ghana, Sierra Leone, Cote d’Ivoire, Liberia, Cameroon, Uganda, Chad, Burkina Faso, Senegal, Benin, Gabon, Guinea, Nigeria, Zambia, Tanzania, Mozambique, Congo Brazzaville, Democratic Republic of Congo and still counting.
The bank’s Chairman – Board of Directors, Gen Robert Mboma in his remark noted that the introduction of the new products is premised on the value proposition by UBA as it consolidates its operations in the continent. “Our continent is full of potentials and intra-country trade within the continent will see the potentials translating into growth and development, and that is exactly what these products bring to African trade and commerce,” said Mboma.
United Bank for Africa Plc is one of Africa’s leading financial institutions offering universal banking services to more than 7.5 million customer accounts from over 850 branches across Africa.
With presence in New York, London, and Paris as well as other major financial hubs, UBA combines strong local knowledge of Africa and global expertise to connect people and businesses across Africa and the world through retail and corporate banking, innovative cross-border payments, trade finance and investment banking making it the bank of choice for Africans and African-related businesses globally.
Maelfu ya wananchi wa Jimbo la Karatu na vitongoji vyake wamefurika kwenye mkutano wa kampeni wa Mgombea Urais wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete leo jioni hii.
Mkutano huo uliofanyika kwenye uwanja wa michezo Karatu mjini ulifurika wana CCM na wananchi waliokuwa na hamasa kubwa ya kumsikiliza Mheshimiwa Kikwete.
Umati huo kwa ujumla wake ulimueleza Mheshimiwa Kikwete kwamba wananchi wa Karatu wamechoshwa na sera za upinzani ambazo zimeshindwa kuleta maendeleo kwa miaka mingi.
Akiwauliza wananchi hao iwapo wako tayari kuipigia kura CCM na madiwani wake na mbunge, wananchi wao kwa ujumla wao wote walinyanyua mikono na kuonyesha ishara ya kuikubali CCM na kuwa wataipa kura zote.
Mkutano huo uliochangamka na uliokuwa na shamrashamra nyingi, ulihudhuriwa pia na Waziri Mkuu Mstaafu Fredrick Sumai ambaye aliwasalimu wananchi na kuwaomba wachague CCm kwa maendeleo ya kweli.
Mkutano huu ni wa mwisho kwa siku ya leo ambapo Mheshimiwa Kikwete alianzia Kibaya na Matui Mkoani Manyara.