Ni globu ya kijamii inayojihusisha na mambo yote ya kijamii,natumaini jamii yangu ya kitanzania itafaidika sana pindi ichukuapo fursa ya kuperuzi kwenye globu hii,dhamira yangu ni kufikisha ujumbe pamoja na kuiburudisha jamii yangu na furaha yangu ni kuona natimiza dhamira yangu kwako.natumaini kuwa wewe utaniunga mkono kwa kile ambacho nataka kukifanya kwa ajili ya jamii yangu ya kitanzania.NASHUKURU KWA KUNIELEWA.
Oct 25, 2010
Oiko Credit Tanzania yakabidhi bilioni 2.6 kwa Saccos mbalimbali jijini dar
Oct 24, 2010
TIMOTHY ABEL MDINKA"ASALI YA ITIGI NDIYO BORA ZAIDI DUNIANI"
Kikwete aiteka Karatu, Maelfu wafurika mkutano wake wa kampeni
Maelfu ya wananchi wa Jimbo la Karatu na vitongoji vyake wamefurika kwenye mkutano wa kampeni wa Mgombea Urais wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete leo jioni hii.
Mkutano huo uliofanyika kwenye uwanja wa michezo Karatu mjini ulifurika wana CCM na wananchi waliokuwa na hamasa kubwa ya kumsikiliza Mheshimiwa Kikwete.
Umati huo kwa ujumla wake ulimueleza Mheshimiwa Kikwete kwamba wananchi wa Karatu wamechoshwa na sera za upinzani ambazo zimeshindwa kuleta maendeleo kwa miaka mingi.
Akiwauliza wananchi hao iwapo wako tayari kuipigia kura CCM na madiwani wake na mbunge, wananchi wao kwa ujumla wao wote walinyanyua mikono na kuonyesha ishara ya kuikubali CCM na kuwa wataipa kura zote.
Mkutano huo uliochangamka na uliokuwa na shamrashamra nyingi, ulihudhuriwa pia na Waziri Mkuu Mstaafu Fredrick Sumai ambaye aliwasalimu wananchi na kuwaomba wachague CCm kwa maendeleo ya kweli.
Mkutano huu ni wa mwisho kwa siku ya leo ambapo Mheshimiwa Kikwete alianzia Kibaya na Matui Mkoani Manyara.
Oct 23, 2010
MWISHO MWAMPAMBA AKARIBISHWA NYUMBANI TANZANIA.
Mwisho Mwapamba akiwasili katika hafla hiyo huku akiwa ameongozana na baadhi ya wageni waalikwa akiingia kwenye Hoteli ya Continental jijini Dar es salaam ambapo hafla ya kumkaribisha mshiriki huyo wa Bigbrother Africa AllStars 2010 aliyerejea hivi karibuni kutoka Afrika Kusini alikokuwa akishiriki katika shindano hilo kwa miezi mitatu shindano hilo lililomalizika wiki iliyopita huku Mnigeria Uti akiibuka mshindi na kujinyakulia kitita cha Dola za Kimarekani laki mbili .
Ukiangalia picha hii watu wote wanaangalia upande mmoja, huu ulikuwa ni wakati wa kuwasili Mwisho Mwampamba katika hafla hiyo iliyohudhuriwa na watu mbalimbali kwenye Hoteli ya Continental jijini Dar es salaam.
Vijana wa Joseph Kusaga kutoka Clouds Television kutoka kulia ni Katunda, Ray, Casto na Ezra nao walikuwepo katika kurekodi tukio zima la kmkaribisha Mwisho Mwampamba. Oct 21, 2010
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete Ziarani Zanzibar
Oct 20, 2010
Wakenya walivyosherehekea kwa mara ya kwanza siku ya mashujaa
Rais Mwai Kibaki akiwasalimia wananchi wa Kenya waliojitokeza katika uwanja wa Nyayo jijini Nairobi kuhudhuria sherehe ya mashujaa. Kwa mara ya Kwanza wakenya wamesherehekea siku ya mashujaa waliopigania uhuru wa nchi hiyo. Miaka ya nyuma walikuwa wanasherehekea siku hiyo kumkumbuka rais wa kwanza wa Nchi hiyo hayati Jommo Kenyatta. (Picha na Anna Nkinda Nairobi)
Askari wa Jeshi la Kenya wakitoa salamu ya heshima kwa Rais Mwai Kibaki (hayupo pichani) wakati wa sherehe za mashujaa zilizofanyika leo katika uwanja wa Nyayo jijini Nairobi . Kwa mara ya Kwanza wakenya wamesherehekea siku ya mashujaa waliopigania uhuru wa nchi hiyo. Miaka ya nyuma walikuwa wanasherehekea siku hiyo kumkumbuka rais wa kwanza wa Nchi hiyo hayati Jommo Kenyatta.
Askari Polisi kikosi cha mbwa wakitoa salamu ya heshima kwa Rais Mwai Kibaki (hayupo pichani) wakati wa sherehe za mashujaa zilizofanyika leo katika uwanja wa Nyayo jijini Nairobi . Kwa mara ya Kwanza wakenya wamesherehekea siku ya mashujaa waliopigania uhuru wa nchi hiyo. Miaka ya nyuma walikuwa wanasherehekea siku hiyo kumkumbuka rais wa kwanza wa Nchi hiyo hayati Jommo Kenyatta.
Wapiganaji wa vita vya Maumau wakipita kwa heshima mbele ya Rais Mwai Kibaki (hayupo pichani) wakati wa sherehe za mashujaa zilizofanyika leo katika uwanja wa Nyayo jijini Nairobi . Kwa mara ya Kwanza wakenya wamesherehekea siku ya mashujaa waliopigania uhuru wa nchi hiyo. Miaka ya nyuma walikuwa wanasherehekea siku hiyo kumkumbuka rais wa kwanza wa Nchi hiyo hayati Jommo Kenyatta.
Wapiganaji wa vita vya Maumau wakipita kwa heshima mbele ya Rais Mwai Kibaki (hayupo pichani) wakati wa sherehe za mashujaa zilizofanyika leo katika uwanja wa Nyayo jijini Nairobi . Kwa mara ya Kwanza wakenya wamesherehekea siku ya mashujaa waliopigania uhuru wa nchi hiyo. Miaka ya nyuma walikuwa wanasherehekea siku hiyo kumkumbuka rais wa kwanza wa Nchi hiyo hayati Jommo Kenyatta.
Wanariadha wa Kenya ambao pia ni mashujaa walioshiriki michezo ya Jumuia ya Madola iliyomalizika hivi karibuni Nchini India na kuipatia nchi yao medali 32 ambazo 12 zilikuwa za dhahabu, 10 za Shaba na 10 za fedha wakipita kwa heshima mbele ya Rais Mwai Kibaki (hayupo pichani) wakati wa sherehe za mashujaa zilizofanyika leo katika uwanja wa Nyayo jijini Nairobi . Kwa mara ya Kwanza wakenya wamesherehekea siku ya mashujaa waliopigania uhuru wa nchi hiyo. Miaka ya nyuma walikuwa wanasherehekea siku hiyo kumkumbuka rais wa kwanza wa Nchi hiyo hayati Jommo Kenyatta.
Wananchi wa Kenya wakiwa wamejitokeza kwa wingi kuhudhuria siku ya mashujaa iliyofanyika leo katika uwanja wa Nyayo jijini Nairobi. Kwa mara ya Kwanza wakenya wamesherehekea siku ya mashujaa waliopigania uhuru wa nchi yao. Miaka ya nyuma walikuwa wanasherehekea siku hiyo kumkumbuka rais wa kwanza wa Nchi hiyo hayati Jommo Kenyatta.(kwa msaada wa blog jirani)
MWISHO MWAMPAMBA AREJEA NA KUPOKELEWA NA BABA YAKE!
Mwisho Mwampamba akipokea shada la maua kutoka kwa ndugu zake mara baada ya kuwasili kwenye uwanja wa ndege wa Mwalimu J.K.Nyerere jioni ya leo akitokea Afrika kusini kwa ndege ya shirika la ndege la SAA ambako alishiriki shindano la BigBrother Africa na kushika nafasi ya tatu huku mshiriki Uti kutoka Nigeria akijinyakulia kitita cha Dola laki mbili za Kimarekani.
Mwisho Mwampamba akisindikizwa na ndugu zake pamoja na walinzi wakati alipowasili kwenye uwanja wa ndege wa Mwalimu J.K.Nyerere jioni ya leo akitokea nchini Afrika Kusini alikoshiriki katika shindano la BigBrother Africa Allstars na kushika nafasi ya tatu.
Meneja Masoko wa Multchoice Furaha Samalu kulia akiwa katika pilika za mapokezi na Meneja Utawala wa Kampuni hiyo Tike Mwakitwange. SERIKALI YAIKEMEA TAMWA YAITAKA KUZINGATIA MASHARTI YA USAJILI!
Ismail Ngayonga na Magreth Kinabo
MAELEZO
Dar-Es-Salaam
SERIKALI imekitaka Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania (TAMWA) kuzingatia masharti ya usajili waliopewa na malengo waliyojipangia pasipo kuingilia masuala ya kisiasa nchini, ikiwemo kuzingatia suala la utawala bora.
Hayo yamesemwa leo Jijini Dar-Es-Salaam na Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni na Michezo, Seth Kahumanda wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na tamko (TAMWA) juu ya taarifa ya vyombo vya ulinzi na usalama lilivyotolewa hivi karibuni na Mnadhimu Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi ya Wananchi wa Tanzania( JWTZ ) Luteni Jenerali Abdulrahman Shimbo, utafiti wa taasisi ya Synovate pamoja na REDET.
Kamuhanda alisema kuwa Serikali inashangazwa na Kauli ya Mkurugenzi wa TAMWA, Analilea Nkya kwa kuwa imekwenda kinyume na majukumu ya taasisi hiyo, ambayo ni pamoja na kusaidia waandishi wanawake kujiendeleza kitaaluma ili kushika hatamu ya uongozi katika vyombo vya habari, kubadilisha mfumo wa habari hasi za wanawake na kuwasaidia wanawake Watanzania kujiletea maendeleo.
Aliongeza kuwa TAMWA ni chama cha kitaaluma kama vilivyo vyama vingine, na iwapo kinahitaji kubadili malengo yake kuwa ya 0kisiasa basi hakina budi kuangalia mustakabali wa chama chao na mwelekeo wao na kufuata utaratibu kwa mujibu wa sheria .
“Matamko ya Mkurugenzi wa TAMWA yamevuka mipaka na kwenda nje ya malengo ya TAMWA. TAMWA inatakiwa kuheshimu masharti ya usajili wao na kuyatekeleza,” alisema Katibu Mkuu huyo huku akisisitiza kwamba chama hicho pia kinatakiwa kuheshimu masuala ya utawala bora uliopo nchini kwa kuwa suala la kuheshimu misingi ya utawala bora si la Serikali pekee.
Kwa mujibu wa Kamuhanda alisema kuwa chama hicho bado kinakabiliwa na changamoto mbalimbali za utekelezaji wa malengo yake ikiwemo kuwaendeleza waandishi wa habari wanawake kwa ajili ya kuwapatia ujuzi wa kutosha utakaowawezesha kushika nafasi za uongozi katika vyombo vya habari na sehemu nyinginezo za maeneo ya kazi.
Aidha Kamuhanda aliongeza kuwa Serikali itaendelea kushirikiana na chama hicho, katika malengo yao waliojiwekea.
Akizungumzia kuhusu mwenendo wa vyombo vya habari juu ya mchakato wa Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 31,mwaka huu, Kahumanda alivishukuru baadhi ya vyombo vya habari na wahariri wake kwa kukemea matendo na kauli zinazoashiria kuhatarisha uvunjifu wa amani nchini.
“ Vyombo vya habari vinafanyakazi nzuri katika kuhabarisha wananchi juu ya mchakato wa Uchaguzi Mkuu baadhi yake vimepinga na kukemea waziwazi juu ya vitendo vinavyoashria uvunjifu wa amani kwa mfano kwa kuandika tahariri ninavipongeza kwa kuwa vimeonyesha ujasiri na ninaomba viendelee na msimamo huo kwa sababu amani ndio hazina kubwa ya nchi yetu,” alisisitiza Kamuhanda.
Awali akimkaribisha Katibu Mkuu ambaye alikuwa kwenye ziara ya kuitembelea Idara ya Habari(MAELEZO), Mkurugenzi wa Idara hiyo, Clement Mshana alisema ofisi zaidi zinahitajika kwa ajili ya kuhifadhi picha, machapisho mbalimbali na habari, hotuba za viongozi pamoja na vipindi mbalimbali ambavyo ni vya radio na televisheni ili viweze kutumika katika sehemu za baadae endapo janga la moto likitokea.
Mkurugenzi huyo aliongeza kuwa idara hiyo inaratibu shughuli za tovuti ya wananchi ambapo mpaka sasa wananchi kadhaa wwaliokuwa na kero zao zimewezwa kutatuliwa na kupatiwa majibu kutoka mamlaka husika.
NGWE YA LALA SALAMA:KAMPENI ZA MNYIKA UBUNGO KATA YA SINZA MPAKA BAA!
MISS PROGRESS INTERNATIONAL KUSAIDIA MAPAMBANO DHIDI YA MAUAJI YA MAALBINO
Swahili Fashion Week yazinduliwa rasmi leo

Swahili Fashion Week itawaleta pamoja wabunifu wa mavazi 24 kutoka nchi zinazoongea lugha ya Kiswahili ili kuweza kuonyesha ubunifu wao katika kubuni mavazi ya aina mbalimbali kwa kutumia aina mbalimbali za malighafi.
Wabunifu watakaoonesha mavazi katika Swahili Fashion Week kwa mwaka huu ni pamoja na Ailinda Sawe, Manju Msita, Kemi Kalikawe, Christine Mhando, Shellina Ibrahim, Farha Naaz Sultan, Gabriel Mollel, Robi Morro, Asia Idarous, Zamda George, Khadija Mwanamboka, Jamilla Vera Swai and Made by Afrika. wabunifu kutoka Kenya ni Sonu Sharma, Moo Cow, KiKoromeo, John Kavike na Kooroo, na kutoka Uganda ni mbunifu Stella Atal.
“Pamoja na maonyesho ya mavazi, mwaka huu Swahili Fashion Week itakwenda sambamba na tamasha la maonyesho ya bidhaa mbalimbali zenye asili ya mswahili kutoka mwambao wa Afrika mashariki”. Alisema Mustafa Hassanali muaandaaji y tukio la Swahili Fashion Week.
“Tunafungua milango zaidi kwa ajili ya watazamaji wapya wa Swahili Fashion Week, amboa watapata fursa ya kununua bidhaa mbalimbali. Tamasha hili ambalo linazileta pamoja bidhaa mbalimbali za sanaa na utamaduni wa mswahili, pia litahamasisha ubunifu zaidi katika bidhaa zinazokwenda sambamba na maisha halisi ya jamii ya watu wanaoongea lugha ya Kiswahili kwa kukutana pamoja na kubadilisha mawazo na kujifunza uzoefu mpya katika masuala yanayohusiana na sanaa kwa ujumla.” Aliaongeza Hassanali.
Pamoja na maonyesho, pia kutakuwepo aina tofauti za burudani kutoka kwa vikundi
Mbalimbali vya muziki, uchoraji wa hina, usukaji mikeka, sambamba na semina za aina tofauti zitakazo washirikisha wabunifu wa mavazi.
Aidha Swahili fashion Week imeandaa aina tofauti za zawadi zitakazotolewa mwaka huu kwa lengo la kutambua na kuthamini vipaji vya aina mbalimbali vitakavyooneshwa, ikiwa ni pamoja na zawadi ya mwaka kwa mbunifu anaechipukia.
Swahili fashion week 2010 imedhaminiwa na Home of Swahili Fashion week Southern Sun, Origin Africa, USAID Compete, EATV, East Africa Radio, Malaria Haikubaliki, BASATA (Baraza La Sanaa Tanzania) Ultimate Security, Monier 2000, Colour Print ltd, Global Outdoor Ltd, Amarula, Vayle Springs Ltd, ZG Films, Darling Hair, Danish make up designs, Nipashe, Bilicanas, Perfect Machinery LTD, 1 & 1 internet solutions, Sengi Tours, Ifashion na 361 Degrees.
Oct 19, 2010
YOU ARE RESPONSIBLE FOR YOUR OWN LIFE "PIPI"
The fact that she turned 18 this year....made her feel excited because it would be her first time to vote!!and now she is getting more and more excited about that day, the 31st of October.....
PLEASE TUMIA KURA YAKO PIA TAREHE 31 MWEZI WA KUMI, SIO UKAE UNALALAMIKIA SERIKALI.....
KIDUM, NONINI AND MATONYA LIVE@CLUB VOLTS LONDON FRI 22ND OCT
EAST AFRICAN ARTISTS WITH SWAGGAEST AND FINEST ARTISTS FROM EAST AFRICA..
FEATURING: KIDUM, NONINI, MATONYA
PERFORMANCES FROM UGANDAN UK BASED ARTISTS....ITS KENYA, UGANDA, TANZANIA, BURUNDI, RWANDA....
ON FRIDAY 22 OCTOBER
AT CLUB VOLTS
169-171 FORE STREET EDMONTON, LONDON, N18 2XB
FRO MROE INFO:
07944456643 ED K EDRIS
07533512670 VICTOR
MWALIMU JULIUS KAMBARAGE NYERERE HONORED IN WASHINGTON DC.
H. E., Ambassador Mwanaidi Maajar - third from right; with the event organizers, together with Mr. Suleiman Saleh; Minister Plenipotentiary Political affairs, Tanzania Embassy - second from left, Ms. Khadija Mwanamboka of Tanzania Mitindo House - 3rd from left and Ms. Belinda Mlingo the Mistress of ceremony and JKNC Inc. partner - second from right. DR. GHALIB BILAL KATIKA MIKUTANO YA KAMPENI KILIMANJARO.
Mgombea Mwenza wa Urais wa CCM, DK. Mohamed Gharib Bilal, akiwahutubia wananchi wa Kata za Bomambuzi na Pasua wakati alipofanya mkutano wa kampeni katika Wilaya ya Moshi mjini Mkoa wa Kilimanjaro jana okt 17. Picha na Muhidin Sufiani
-Mgombea Mwenza wa urais wa CCM, Dk. Mohamed Gharib Bilal, akimnadi mgombhea ubunge wa Jimbo la Moshi Vijijini, Cyril Chami, wakati wa mkutano wa kampeni uliofanyiika leo Okt 18 kwenye uwanja wa Kijiji cha Chekereni Mkoa wa Kilimanjaro. Pichha na Muhidin Sufiani
Mmoja wa wanachama wa chama cha mapinduzi akishangilia huku wenzake wakimuangalia wakati wa mkutano wa Kampeni wa Dr. Ghalib Bilal.
Wanachama na mashabiki wa CCM wa Mtaa wa Sokoni Kata ya Bomambuzi na Pasua, wakimsikiliza mgombea Mwenza wa urais wa CCM. Dk. Mohamed Gharib Bilal, wakati alipofanya mkutano wa kampeni jana Okt 17 katika uwanja wa Sokoni Pasua Wilaya ya Moshi Mjini Mkoa wa Kilimanjaro na kumnadi mgombea Ubunge wa Jimbo hilo, Justine Salakana. Picha na Muhidin Sufiani 










