Aug 27, 2010

Timu ya Taifa ya Pool Yaendelea Kujifua Kujiandaa na Mashindano Ya Dunia


Kocha wa timu ya Taifa ya Pool,Denis Lungu akiwaelekeza wachezaji wa timu hiyo namna ya kushika fimbo na kupiga mpira wakati wa mazoezi yao yanayoendelea kufanyika katika klabu ya Break Point,kijitonyama.
Kocha Denis Lungu akiwapa maelekezo wachezaji wa timu ya Taifa ya Pool wanaojiandaa na mashindano ya Dunia yanayotarajiwa kufanyika Novemba,8 2010 huko nchini Ufaransa.timu hii ina wachezaji nane (8) ambani ni Felix Atanas,Abuu Shaban,Godfrey Sway,Mohamed Iddy,Omar Akida,Godfrey Muhando,Aliakber Akberal na Arjuan Lavinja.ikiwa chini ya udamini mkubwa wa bia ya Safari Lager.

NHIF YAWATAKA VIONGOZI TALGWU KUTHIBITISHA MADAI

Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya afya akitoa ufafanuzi kuhusu madai yaliyowasilishwa kwenye vyombo vya habari na viongozi wa Talgwu kuwa wanadai serikali na Mfuko wakati alipokutana na waandishi wa vyombo mbalimbali kwenye ukumbi wa mikutano wa mfuko huo kurasini bendera tatu kushoto kwake ni wakurugenzi wa mfuko.

Na.Paul Marenga NHIF
MFUKO wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) umekitaka Chama cha Wafanyakazi wa Serikali za Mitaa (TALGWU) kutokwepa kueleza ukweli kuhusiana na madai ya makato yaliyokatwa kimakosa kwa wanachama wao wakati wa uanzishaji wa Mfuko huo mwaka 2001.

Kauli hiyo imetolewa na Mkurugenzi Mkuu wa NHIF, Emmanuel Humba wakati akizungumza na waandishi wa habari makao makuu ya Mfuko huo Bendera Tatu, Dar es salaam leo.

“Sisi katika Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya hatutaki malumbano, bali tunapenda kupitia kwenu umma wa Watanzania na wanachama wetu waelewe ukweli kuhusu suala hili ambalo kwanza siyo suala geni,” alisema Humba.

Mfuko huo uliamua kutoa ufafanuzi baada ya baadhi ya vyombo vya habari juzi na jana kutangaza na kuandika kwamba Talgwu itaifikisha mahakamani NHIF kwa kushindwa kulipa wafanyakazi 58,000 wa Tamisemi zaidi ya sh bilioni 3.6 ambazo zilikatwa kinyume cha sheria.

Alisema pamoja na ukweli kwamba madai haya yamekuwa yakitolewa au kuibuka kunapokuwa na uchaguzi ndani ya TALGWU au uchaguzi mkuu wa Serikali, viongozi wa TALGWU wamekuwa hawawaambii wanachama wao maagizo ya serikali kuhusiana na madai yao hayo.

Yapo maagizo ya Serikali katika suala hili, alisema Humba na kuongeza kuwa TALGWU ilipaswa kueleza wazi imefanya nini ili kulimaliza kabisa suala hili ambalo Mfuko tayari ulishatekeleza kwa upande wake, kulingana na maagizo na miongozi ya Serikali.

Kwa mujibu wa Humba, Serikali na NHIF baada ya kubaini kuwa kulikuwa na Watumishi 12,894 waliokatwa kimakosa iliwarejeshea kiasi cha Shilingi 269,563,469.54 watumishi hao.

Alisema kazi ya kuwakabidhi fedha hizo ilifanywa kwa pamoja kati ya Mfuko na Chama cha TALGWU makao makuu na matawi yake mikoani.

Akifafanua zaidi alisema pamoja na hatua hiyo ya kuwalipa watumishi hao, TALGWU ilikuja na madai mapya wakisema bado kuna watumishi 53, 000 ambao hawajalipwa na wanadai kiasi cha Shilingi bilioni 1.8 na sasa wanadai shilingi Bilioni 3.6 kwa watumishi 58,000.

“Kwa taasisi yoyote inayofuata misingi ya fedha taratibu lazima ziwepo na hawa kama wanaona kwamba malipo ya mwanzo hayatoshi basi wafuate maagizo yanayostahili.

“Hakuna wakati wowote ambapo Mfuko huu umekaidi kutekeleza maelezo yoyote halali, kama TALGWU wanavyodai katika taarifa yao iliyotolewa kwa Vyombo vya Habari jana,” alisema.

Mwongozo wa pili wa makato ya wafanyakazi kwenda NHIF kutoka Utumishi uliotolewa Mei 2002, ulifafanua kuwa wanaokatwa ni wale wanaolipwa na Serikali kuu ingawa walikuwa katika Serikali za Mitaa na kubainisha kuwa watumishi ambao hawahusiki na makato ni wale walioajiriwa na Serikali za mitaa na kulipwa kwa kutumia vyanzo vya mapato vya Serikali za Mitaa.

Hata hivyo Serikali, Mwezi Novemba, 2002 illifanyia mapitio Sheria ya Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya ili kuwajumuisha Watumishi wote walioko kwenye Serikali za Mitaa.

Humba alisema chimbuko la madai ya TALGWU ni kuwa wao hawaikubali tafsiri iliyotolewa na Serikali kuhusu ni nani waliotakiwa kuchangia na vilevile haikubali miongozo ya makato iliyotolewa na Serikali, jambo ambalo liko nje ya uwezo wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya.

“Tunauomba uongozi wa TALGWU kama kuna madai yoyote halali basi wafuate maelekezo waliyopewa ya kuwasilisha orodha ya majina ya watumishi wanaodai kwenye Ofisi ya Waziri Mkuu TAMISEMI na yakishahakikiwa na kuletwa kwetu, sisi tutawalipa mara moja,” Alisema Humba.

Alisema Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya wakati wote unafanya kazi zake kwa kuzingatia Sheria ya kuundwa kwake na kusimamia majukumu yake kwa mujibu wa Sheria. “Fedha hizi ambazo tunazisimamia ni fedha za umma (Public Funds) ambazo zinasimamiwa na kukaguliwa na Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG). Ndiyo maana hata malipo ya awali tuliyalipa kwa kuzingatia taratibu za fedha na idhini kutoka Serikalini.” Alisema.

wanaume kuitambulisha albam yao pamoja na website yao octoba 25


kundi la Wanaume (lililojiengua kutoka kwa kundi la Wanaume Halisi) linatarajia kuitambulisha albamu yake mpya itakayokwenda sambamba na uzinduzi wa Logo pamoja na tovuti yao kwa watu maalumu ndani ya kiota cha maraha kilichopo kati kati ya jiji,Savanah Lodge mnamo Octoba 25.

Akizungumza na blog jirani jijini Dar jioni hii kiongozi wa kundi hilo Rich One amesema kuwa baada kuikamilisha albamu yao yenye jumla ya nyimbo kumi,kwa sasa wanajipanga vyema kuitambulisha albamu hiyo itakayojulikana kwa jana la POA TUA, vile vile utakwenda sambamba na uzinduzi wa Logo na tovuti itakayokuwa na habari zao mbalimbali zikiwemo na kazi zao kama vile vyimbo na video zao.

"Tumeamua kuja na mambo mapya baada ya kimya kidoogo kwa wapenzi wetu,kama nilivyosema hapo awali albamu ina jumla ya nyimbo kumi,ambazo baadhi yake ni Poa Tu, Mapenzi Matamu, Apple, Moyo Wangu, Zaga Zaga na nyingine nyingi," alisema Rich One na kuongeza kuwa albamu hiyo imesheheni mahadhi tofauti tofauti kama vile Zouk, R&B pamoja na Hip Hop.

Rich One amesema kuwa ndani ya albamu hiyo amewashirikisha wasanii kadhaa mahiri katika anga ya muziki wa kizazi kipa,kama vile Chidi Benz,Kitokororo wa FM Academia,Hard Mad,Chiku Keto,Mh Themba na wengineo.

Kundi hilo linaloundwa na wakali akiwemo Athuman Yahya (A.Man), Juma Mbelwa (Juma Jazz), Karim Kaiman (Kakaman), Abdul Ally (Mzimu), Richard Shauri (Rich One) pamoja na David Mpangile (Daz-p).

DR. BILAL AWAASA WASOMI NCHINI

Mgombea mwenza wa nafasi ya urais kupitia tiketi ya Chama cha Mapinduzi, Dk. Mohamed Gharib Bilal, akimnadi mgombea ubunge wa Jimbo la Nachingwea, Mathias Chikawe, baada ya kuingia Wilayani Nachingwea jana jioni Wananchi wa Nachingwa wakimsikiliza Mgombea Mwenza wa nafasi ya urais Dk. Mohamed Gharib Bilal, alipokuwa akiwahutubia wananci wa Wilaya ya Nachingwea katika uwanja wa Sokoine leo mchana kina mama wakiimba.
Mgombea Mwenza Dk. Gharib Bilal, akiongozana na Mgobea Ubunge wa Jimbo la Nachingwea, Mathias Chikawe, baada ya kupokelewa mpakani mwa Wilaya ya Liwale na Nachingwea jana Agost 26, wakati wa zaiara ya mgombea mwenza ya kunadi ilani ya Chama cha Mapinduzi katika kampeni za kukiombea kura Chama hicho katika uchaguzi mkuu ujao unaotarajia kufanyika Oktoba 31 mwaka huu.
Mohamed Gharib Bilal, akipokelewa na Diwani wa Viti maalum, Asina Lutumbo na Mwenyekiti mstaafu wa UWT, Anna Abdalah, baada ya kuwasili kwenye uwanja wa Sokoine wilayani Nachingwea alipofika kufanya mkutano wa kampeni leo
Wananchi wa Kijiji cha Miembeni Wilaya ya Nachingwea wakimzunguka Mgombea Mwenza Dk. Gharib Bilal, baada ya kutanda barabarani na kuwaomba viongozi wa msafara kumruhusu kushuka ili kumuona na kusaliana naye, wakati msafara huo ulipofika mpakanai mwa wilaya ya Nanchingwea ukitokea Wilayani Liwale jana



*Dk Bilal awaasa wasomi nchini

*Awataka kujenga makazi bora na sio kukimbilia magari

*Msafara wake wapata ajali ya gari wilayani Ruangwa


Na mwandishi wetu,lindi

MGOMBEA mwenza wa Chama cha Mapinduzi (CCM),Dk.Mohamed Bilal amewashauri wasomi kote nchini kuanzisha utamaduni wa kujenga makazi yaliyobora ili taifa liweze kupiga hatua katika sekta ya makazi.

Kauli hiyo ya Dk Bilal aliitoa wakati akihutubia mamia ya wakazi wa Manisapaa ya Lindi ambapo pia alitumia nafasi hiyo kumnadi mgombea ubunge kupitia CCM, Mohamed Abdulaziz.

“Zamani tukisoma chuo kikuu na kuhitimu hatukumudu hata kununua simu. Siku hizi kila mwananchi anayo fursa ya kupata simu. Vijana wetu siku hizi wanahitimu vyiuo vikuu na baada ya mwaka mmoja wanaweza kununua magari. Nadhani sasa ni wakati muafaka kwa wao kuanza mkakati wa kujenga makazi bora,” alisema na kuongeza;


“Tunao mpango madhubuti wa kuhakikisha kuwa kila mwananchi anapata makazi bora. Mpango huu upo katika ilani yetu na ni imani yangu kuwa wananchi wakimchagua Rais Kikwete katika uchaguzi ujao, basi itakuwa kazi rahisi kwetu kufanikisha azma hii muhimu katika maendeleo ya wananchi wetu.”

Dk Bilal bado anaendelea na kampeni katika mkoa wa Lindi ambapo jana alifanikiwa kufanya kampeni katika wilaya za Ruangwa, Liwale na Nachingwea. Katika kapmeni hizo, Dk Bilal alisisitiza umuhimu wa wananchi kutambua kuwa serikali ya CCM imejipanga vema na kwamba ina kila sababu za kutaka kuwapa maendeleo zaidi ya hapo wali[po.

Msomi huyu wa masuala ya Nyuklia alifafanua pia kuwa, serikali ya CCM inatambua kero za barabara zinazoikabili mikoa ya Kusini na kwamba hatua za kukabiliana na hali hiyo zinaonekana kwa kuwa barabara nyingi zinafanyiwa kazi kwa sasa.


Pia alisisitiza umuhimu wa wananchi kuchangamkia fursa za Kilimo Kwanza kwa kuhakikisha kuwa wanawatumia wataalam wachache waliopo sambamba na fursa kama mbegu na mbolea zinazohamasishwa na wananchi kutolewa. Tena alifafanua kuwa, anayo taarifa ya kero kuhusu zao la Korosho na akawaeleza wananchi kwamba tiba ya kero hiyo ipo na rais Kikwete ameshafanya kila awezalo kuhakikisha vyama vya ushirika vinaimarishwa sambamba na kuwapa bei bora wakulima wa Korosho.

Mgombea Mweza, Dk Bilal alifafanua pia umuhimu wa wazazi kuwajali watoto wao na kuhakikisha wanawapeleka katika shule za awali kwa kuwa ilani ya CCM inatamka wazi kuwa, ifikapo mwaka 2015, kila shule ya Msingi itatakiwa kuwa na shule hizo, hivyo wazazi wachangamkie fursa hiyo iliyopo mbele yao.

Sambamba na hilo, gari mmoja lilokuwa ndani ya msafara wa mgombea huyo liliacha njia na kupinduka katika kijiji cha Nangumbo wilaya ya Ruangwa mkoani majira ya saa nne, asubuhi, wakati magari hayo yakiwa katika njia ya kwenda makao makuu ya wilaya ya Ruangwa kwa ajili ya mkutano wa kampeni.

Shuhuda wetu aliyekuwepo katika tukio hilo alieleza kuwa, gari hilo lilipata ajari kufuatia vumbi kali liliolosababisha dereva wa gari kutoona mbele huku akitakiwa kupita katika eneo lililo[kuwa na tuta kubwa.

Gari hilo lilikuwa na abiria wane, lakini wote walisalimika na baada ya jitihada za kuwatioa katika gari hilo kukamilika, msafara uliendelea kama kawaida.

Aug 26, 2010

KAMPENI ZA KIKWETE NGARA


Mkutano wa kampeni kwa mgombea wa CCM uliokuwa ufanyike mjini Ngara jana jioni ulilazimika kuahirishwa baada ya helkopta aliyokuwa akitumia kushindwa kumpeleka mjini humo kutokana na hali mbaya ya hewa.
Hata hivyo ilimlazimu Rais Kikwete kutumia barabara ambapo aliwasiri mjini humo usiku jkwajili ya kuongea na wananchi, hivyo mkutano huo umeahirishwa hadi leo mapema asubuhi.
Wananchi waliofurika katika viwanja vya posta ya zamani kwa ajili yasikiliza hotuba hiyo, waliambiwana Mwenyekiti wa CCM Hellen Adrian, baadae jana saa 11 jioni kuwa mkutano huo usingekuwepo hadi leo.
Baadae usiku Rais aliwasiri kwas njia ya barabara na kuandaliwa futari na kinamama wa wilayani humo kama inavyoonekana alipopokelewa kwa jili ya masafa zaidi kwajili ya kampeni

HILI NDILO BANGO LA DR.SLAA

Haya wakati kampeni za Chadema zinakaribia bango hili limeandaliw akumnadi mgombea!

MTV & BHARTI AIRTEL SIGN PARTNERSHIP TO BRING MTV AFRICA MUSIC AWARDS TO LAGOS IN DECEMBER 2010.


25 August 2010: MTV Networks Africa (MTVNA) and Bharti Airtel have confirmed that they will be holding the 2010 MTV Africa Music Awards (MAMA) in Lagos, Nigeria.
MTVNA’s jubilant celebration of contemporary African music and creativity will be held at the EKO EXPO Hall, Lagos on 11 December 2010, focusing the spotlight on Africa’s most outstanding musicians, from the heart of one of the continent’s most vibrant cities.
The 2010 MTV Africa Music Awards with Airtel will take the form of a stunning live music event and global television spectacular, featuring performances from contemporary African and international music giants and hosted by a major music celebrity. Artists from around the continent will battle to win a coveted MAMA trophy in one of twelve award categories including: Best Male, Best Female, Best Video, Best Group, Artist of the Year, Best Lusophone Act, Best Anglophone Act, Best Francophone Act, Song of the Year, Brand: New Act, Best International Act and MAMA Legend.

Telecommunications giant Airtel comes on board as the headline sponsor of the MTV Africa Music Awards 2010, signalling the telco’s profound commitment to African music and youth culture following its purchase of Zain Africa’s business operations earlier this year. The sponsorship was announced by Andre Beyers, Chief Marketing Officer, Airtel Africa and Alex Okosi, Senior Vice President & Managing Director, MTV Networks Africa.

Sponsorship of the MAMA will provide Airtel with unique brand exposure across multiple platforms including live event activations across the continent. A key component of the partnership will be the development of exclusive mobile and data content for the Airtel subscribers in sub-Saharan Africa including wallpapers and various downloads. The campaign will also be fully activated in the digital space with a bespoke mobi-site (mtvmama.mobi) and a dynamic website (www.mama.mtvbase.com). Multiple SMS voting and interactive mechanics will be integrated into the campaign, to provide Airtel customers with unique access to the MAMA initiative.

Commented Alex Okosi, Senior Vice President & Managing Director, MTV Networks Africa, “We are thrilled to be partnering with Airtel to bring the MTV Africa Music Awards with Airtel to Lagos for the first time and look forward to delivering the most exciting MAMA yet on 11 December.”
Said Mr. Beyers, “Airtel is proud to be at the forefront in nurturing talent in Africa and connecting the passions of millions of youth across the continent through music. Our support for the MAMA awards is founded on our commitment to empower the youth through initiatives that will help Africa to identify and celebrate talent.”
Conceived in 2008 as the ultimate celebration of African contemporary music talent, the MTV Africa Music Awards with Airtel provides a major promotional platform for the African music industry, championing, supporting and empowering African talent by broadcasting their music around the world via MTV’s global multimedia network.
The awards celebrate contemporary African and international genres loved by the youth and young adults across sub-Saharan Africa including Hip Hop, Hip Life, R&B, Afro Pop, Afro House, Kwaito, Boomba, Bongo Flava, Coupé Décalé, Dancehall, Soul and Rock.
The inaugural MAMA was held at the Velodrome, Abuja in 2008, while October 2009 saw the awards move to Nairobi, Kenya, with performances from 2Face (Nigeria), Amani (Kenya), A.Y. (Tanzania), Blu3 (Uganda), Brickz (South Africa), Da LES (South Africa), D’Banj (Nigeria), Fally Ipupa (DRC), HHP (South Africa), Lizha James (Mozambique), M.I. (Nigeria), Mo’ Hits Allstars (Nigeria), Nameless (Kenya), Pype (Nigeria), Samini (Ghana), STL (Kenya), Lira (South Africa), Wahu (Kenya) and Zebra & Giraffe (South Africa), alongside international stars Wyclef Jean and Akon.
Past winners have included 2-FACE (Nigeria), Nameless (Kenya), Samini (Ghana), Wahu (Kenya), HHP (South Africa), D’Banj (Nigeria) and Patricke-Stevie Moungondo (Congo Brazzaville).
-ENDS-

Notes to Editors
The MTV Africa Music Awards with Airtel is open to all soloists or groups who have received airplay on MTV base or MTV during the qualifying period (30 June 2009 to 31 August 2010) including artists from: Angola, Benin, Botswana, Burkina Faso, Burundi, Cameroon, Cape Verde, Central Africa Republic, Chad, Comores, Congo, Cote d’Ivoire, Djibouti, DRC, Equatorial Guinea, Eritrea, Ethiopia, Gabon, Gambia, Ghana, Guinea, Guinea Bissau, Kenya, Liberia, Madagascar, Malawi, Mali, Mauritania, Mauritius, Mozambique, Namibia, Niger, Nigeria, Rwanda, Sao Tome & Principe, Senegal, Seychelles, Sierra Leone, South Africa, St Helena, Sudan, Swaziland, Tanzania, Togo, Uganda, Zambia and Zimbabwe.

WAZIRI MKUU MIZENGO PINDA KUSHUHUDIA SHEREHE ZA KUMUAPISHA RAIS NKURUNZINZA BUJUMBURA LEO

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akiwapungia wananchi wa Burundi waliofika kwenye uwanja wa ndege Bujumbura Augosti 25, 2010 jana ambako leo atamwakilisha Rais Jaky Kikwete katika sherehe za kumwapisha Rais wa Burundi, Pierre Nkurnzinza. Kulia ni Spika wa Bunge la Nchi hiyoPie Ntavyohanyuma na wapili kushoto ni mkewe Tunu. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akisalimiana na watanzania waishio Burundi baada ya kuwasili kwenye uwanja wa ndege wa Bujumbura Augost 25 jana Waziri mkuu leo atamwakilisha Rais Jakaya Kikwete katika sherehe za kuapishwa kwa rais wa chi hiyo, Pierre Nkurunzinza
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda kiongozwa na Spika wa Bunge la Burundi baada ya kuwasili kwenye uwanja wa ndege wa Bujumbura Augosti 25 ambako leo atamwakilisha Rais Jakaya Kikwete katika sherehe za kumwapisha Rais wa Nchi hiyo, Pierre Nkurunzinza. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

warembo wa vodacom miss tanzania 2010 wakiwa mkoani manyara


Baadhi ya warembo wa Vodacom Miss Tanzania 2010 wakiwa wameshikilia vyandarua kabla ya kugawa vyandarua kwa baadhi ya wakazi wa mto wa Mbu mkoani Manyara jana. Warembo hao wapo Kanda ya Kaskazini kutembelea vivutuio vya Utalii na kuhamasisha Utalii wa ndani ya nchini.
Mshiriki wa Shindano la Vodacom Miss Tanzania 2010,Geneviver Emmanuel akigawa chandarua kwa mmoja wa wakazi wa Mto wa Mbu Mkoani Manyara jana katika utekelezaji wa Kapeni ya malaria. Warembo hao wapo Kanda ya Kaskazini kutembelea vivutuio vya Utalii na kuhamasisha Utalii wa NMdani Nchini.
Paulina Lowasa dada wa Mbunge wa Monduli na Waziri Mkuu wa Zamani, Edward Lowasa, akiwapa mkono wa kuwatakia heri Warembo wa Vodacom Miss Tanzania alipokutana nao Wilayani Monduli mkoni Arusha jana na kuwapa zawadi ya vikoi vya kimaasai warembo wote 30. Warembo hao wanatembelea Kanda ya Kaskazini kuangalia vivutio vya Utalii nchini.
Baadhi ya Warembo wa Vodacom Miss Tanzania wakiwa katika picha ya pamoja na wanafunzi wa Shule ya Sekondari Wasichana Maasai iliyopo Monduli Mkoani Arusha wakati wa rembo hao walipotembelea shule hiyo jana wakiwa katika ziara yao ya kutembelea vivutio vya utalii na kuhamasisha utalii wa ndani nchini.
Washiriki wa Shindano la Vodacom Miss Tanzania 2010 wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Viongozi wa UWT Wilayani Monduli pamoja na Viongozi wa Kamati ya Miss Tanzania baada ya akina mama hao kuwapa zawadi ya vikoi vya kimasai na kuwatakia kila la heri katika mashindano hayo yatakayo fikia Kilele Septemba 11 mwaka huu jijini Dar es Salaam.

Wateja wa Zain sasa Kupeta Kinamna hii..!

FREE CALLS, FREE SMS, FREE INTERNET

Zain Tanzania the most respected company, today has announced a Customer rewarding promotion, with free calls during the holy month of Ramadan.

The offer adds-up on the company’s championship in rewarding their customers and today it continues to re enforce its commitment by providing unmatched offer to their customers.

Speaking on the promotion, the company’s Managing Director, Sam Elangalloor said “we are happy to announce this promotion for the holy month of Ramadan to reward our customers”.
“We wish our customers Ramadhan Karim and hope they will communicate with their families, friends and loved ones more. Our aim is to continue making all communications services in Tanzania more affordable and make your Zain phone a must have”, he said.

He further added that the promotion will give our customers free calls, free sms and free internet access. “We are confident Tanzania will see more affordability in the months to come guaranteed by the widest coverage and quality network from Zain”.

This promotion will enable Zain customers to have free calls after the first minute, 100 free sms and 200mb/s free Internet Access all from midnight to 6 in the morning and hence continues to enjoy the only true 1 Tshs tariff.

The offer will be for Zain prepaid customers only and will not require any registration

Aug 25, 2010

UZINDUZI WA KIPINDI CHA ZAMARADI CHA TAKE ONE KILIVYOFANA JANA,

Muhongo mchungu na baba hapo wakijadili jambo
Claud na mkewe walikuwepo jana.

Bi mwenda nae hakubaki nyuma

Zamaradi,dina na Dj Fetty...

Natasha na Bi mwenda
Kutoka kitengo chetu cha habari mwenye shati jeupe anaitwa Lazaro Matalange na Philip Mwihava..

Stella wa hapa clouds upande wa masoko na Wakuvanga wakishow love jana.


Singe Mtambalike a.k.a Richie richie hakubaki nyuma maana hili jambo ni lao pia.


Wasanii jana walipata pia nafasi ya kubadilishana mawazo,kwa mbali unamuona Dr.Cheni.


Utani ulikuwepo mwingi sanaYvone Sherry a.k.a Monalisa nampendaga sana huyu dada

Ben Kinyaiya


TANGAZO LA MSIBA (BANGALORE INDIA)

KWA NIABA YA FAMILIA YA MAREHEMU BWANA NA BIBI MWAKALASI YA KIJITONYAMA, BW RODRICK MWAMBENE NA BI JULIETH MWAKALASI WANAWATANGAZIA NDUGU NA JAMAA KUWA NDUGU YAO MPENDWA, EDWIN MBONELA MWAKALASI ALIYEKUWA ANASOMA NCHINI INDIA KATIKA CHUO CHA ACHARYA BANGALORE AMEFARIKI AGOSTI 21 BAADA YA KUUGUA KWA MUDA MFUPI.

MWILI WA MAREHEMU UMEKWISHA WASILI NCHINI NA IBADA YA KUMUOMBEA ITAFANYIKA NYUMBANI KWAO, KIJITONYAMA (KARIBU NA SHULE YA MSINGI KIJITONYAMA) NA BAADAYE MAZISHI KUFANYIKA KATIKA MAKABURI YA KINONDONI ENEO LA MWEMBENI 25 .8.2010 SAA 10.00 ALASIRI.

PIA IBADA YA HESHIMA ZA MWISHO ZITATOLEWA KUANZIA SAA 6.00 MCHANA HAPO HAPO NYUMBANI KWAO.

KWA NIABA YA FAMILIA YA WA WAFIWA, TUNAPENDA KUTOA SHUKRANI ZA DHATI KWA WAFUATAO AMBAO WALIJITAHIDI KUOKOA MAISHA YA MAREHEMU KWA UPANDE WA MATIBABU MPAKA KUSAFIRISHA MWILI WAKE KUJA TANZANIA.

SHUKRANI ZA HIZO ZIENDE KWA:-

UBALOZI WA TANZANIA NCHINI INDIA KUPITIA KWA AFISA WAKE BW. MWAMANENGE AMBAYE PIA NI MSHAURI WA WANAFUNZI WA TANZANIA NCHINI HUMO, TANZANIA STUDENT ASSOCIATION OF ACHARYA (TASAA) CHINI YA MWENYEKITI WAKE BW. HAMIS FUPI, TANZANIA STUDENT ASSOCIATION OF MYSORE (TASAM), KAMPUNI ILIYOSAFIRISHA MWILI, KUMAR AMBULANCE CO. & INTERNATIONAL, RAMAYA HOSPITAL NA NRR HOSPITAL ZOTE ZA BANGALORE.

BWANA AMETOA, BWANA AMETWAA, JINA LA MBWANA LIHIMIDIWE, AMEN.

KWA MAELEZO ZAIDI WASILIANA NA BW RODRICK MWAMBENE KWA SIMU NAMBA 0754 362901, 0713 362901.

OpenSanit wazindua bidhaa zao jijini Dar


Mkurugenzi Mtendaji wa kampun ya Open Sanit,Bw.Octavian Mshiu akifafanua jambo kw a mgeni rasmi Naibu Waziri wa Viwanda, biashara na Masoko Dk. Cyril Chami kabla ya kuzindua bidhaa za kampuni ya Beier Safety Footwear ya Afrika Kusini ikishirikiana na kampuni ya Open Sanit Tanzania jioni ya leo ndani ya hoteli ya Sea Cliff jijini Dar
Mkurugenzi Mkuu wa kampuni ya BEIER SAFETY FOOTWEAR,Bw.Silvio Ceriani akizungumza machache mbele ya wageni waalikwa kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi kuzindua bidhaa za kampuni hiyo.
Naibu Waziri wa Viwanda, biashara na Masoko Dk. Cyril A. Chami akimpatia zawadi wa bahati nasibu ndogo ya viatu iliyofanyika katika uzinduzi huo,Bw. Victor Mushi,ambapo watu kadhaa walijinyakulia zawadi hizo za viatu vikiwemo viatu mbalimbali vya usalama..
Baadhi ya wageni waalikwa wakiangali baadhi ya bidhaa zinazotengenezwa na kampuni hizo mbili,bidhaa hizo za aina mbalimbali zinazotumika katika masuala ya usalama hasa viwandani na kwenye makampuni.
Mmgeni rasmi Naibu Waziri wa Viwanda, biashara na Masoko Dk. Cyril Chami (tatu kulia) akioneshwa aina ya bidhaa mbalimbali zitakazokuwa zikitengenezwa na kampuni hizo mbili,ya Beier Safety Footwear ktoka Afrika Kusini ikishirikiana na kampuni ya Open Sanit (Tanzania) jioni ya leo hoteli ya Sea Cliff jijini Dar. Baadhi ya bidhaa zitakazokuwa zinatengenezwa na kampuni ya Beier Safety Footwear kutoka nchini Afrika ya Kusini ikishirikiana na kampuni ya Open Sanit ya Tanzania.kama vipi ingia http://www.opensanit.com/ kupata maelezo zaidi.

Kilimanjaro Lager Kudhamini Bongo Star Search 2010

Meneja wa bia ya Kilimanjaro,George Kavishe akiongea jambo wakati wa utambulisho wa udhamini wa miaka mitatu kwa Bongo Star Search uliofanyika leo katika ukumbi wa mikutano wa hoteli ya Paradise uliopo ndani ya jengo la Benjamin Mkapa,jijini Dar.kulia ni Mkurugenzi wa BenchMark Production,Madame Ritha Paulsen.
Mkurugenzi wa BenchMark Production,Madame Ritha Paulsen akiongea leo katika ukumbi wa hoteli ya Paradise uliopo ndani ya jengo la Benjamin Mkapa wakati wa utambulisho wa mdhamini mkuu mpya wa Bongo Star Search ambaye ni kampuni ya bia Tanzania (TBL) kupitia kinywaji chak cha Kilimanjaro premium lager.kulia ni Afisa masoko na mafunzo wa TBL,Edith Bebwa.

Na Mwandishi Wetu

Bongo star search ni moja ya kipindi kinacho rushwa na television hapa nchini Tanzania ambacho kime fanikiwa kwa kiwango kikubwa kabisa kuinua vipaji vya wanamuziki wa Tanzania.

Ikumbukwe kuwa mwaka jana kampuni ya kutengeneza bia hapa nchini TBL kwa kupitia kinywaji chake kinachojihusisha na maswala ya muziki,Kilimanjaro premium lager. Ilishiriki kama mmoja wa wadhamini wa shindano hilo.

Uhusiano huu mkubwa wa kampuni hizi mbili umetokana na sababu kuu kwamba BSS inahusika kutafuta na kuinua vipaji vya wanamuziki hasa vijana wa umri wowote ambapo Kilimanjaro premium lager kufuatia kauli mbiu yake ya Kufikisha Muziki wa Tanzania Kilele cha mafanikio kwa upande mwingine ina husika na muziki wa vijana wa Kitanzania.

Kilimanjaro premium lager imekua ikunga mkono juhudi za kuendeleza Muziki hapa Tanzania kwa kiwango cha juu.. Ikiwa mdhamini mkubwa kwenye zoezi la kutoa Tunzo za Muziki Tanzania kila mwaka,Tunzo zinazojulikana kama Kilimanjaro Tanzania Music Awards. Ndio maana Kilimanjaro premium lager imeona hakuna sababu ya wao kutoshirikiana na BSS 2010 katika kuinua vipaji vya wanamuziki wa Tanzania.

Kilimanjaro premium lager imeandikisha mkataba wa kuwa mdhamini wa Bongo star search kwa kipindi cha miaka mitatu ambayo ni BSS 2010, BSS 2011, BSS 2012.

Washiriki wa BSS watashirikishwa katika mambo mbali mbali yakiwemo mashindano yatakayo kua yanafanyika siku hadi siku katika jumba la BSS KILI HOUSE 2010.

BSS 2010 itakuwa ikirusha hewani kila jumapili saa tatu na robo usiku (3:15) kupitia television ya ITV ikishirikiana na Radio one na magazeti ya The Guardian ,Nipashe.unatakia kufuatilia shindano hilo bila kukosa na pia ni muhimu kupiga kura yako ili kuweza kuwachagua watakao weza kushiriki mpaka mwisho .


shiriki nasi ili kuweza kukamilisha ndoto za wanamuziki wetu.

ziara ya miss tanzania katika ziwa manyara


Baadhi ya warembo wanao shiriki shindano la Vodacom Miss Tanzania 2010 wakimsikiliza mmoja wa waongoza watalii katika Hifadhi ya Ziwa Manyara alipokuwa akiwapa maelezo juu ya hifadhi hiyo.
Baadhi ya warembo wa Vodacom Miss Tanzania 2010 wakizungumza na watalii waliokutana nao jana katika hifadhi ya Ziwa Manyara.
Baadhi ya warembo wa Vodacom Miss Tanzania wakipiga picha ndani ya hifadhi ya Ziwa Manyara wakati warembo hao walipotembelea ziwa hilo ikiwa ni sehemu ya ziara yao ya kuangalia vivutio vya utalii katika mikoa ya Kaskazini.
Baadhi ya warembo wanao shiriki shindano la Vodacom Miss Tanzania 2010 wakimsikiliza mmoja wa waongoza watalii (hayupo pichani) katika Hifadhi ya Ziwa Manyara alipokuwa akiwapa maelezo juu ya hifadhi hiyo.
Warembo wa Vodacom Miss Tanzania wakiwa katika picha ya pamoja na watalii waliotoka Chuo Kikuu cha Calfonia Los Angels Marekani waliotembelea Hifadhi ya Ziwa Manyara.



ZIARA ya warembo 30 wanaoshiriki katika shindano la Vodacom Miss Tanzania 2010 kutembelea vivutio na rasilimali tofauti nchini zilizopo kanda ya kaskazini imeendelea na jana walikuwa Hifadhi ya Taifa ya Ngorongoro (NCA) iliyopo mkoani Arusha.

Wakiwa ndani ya hifadhi hiyo licha ya kujionea moja ya maajabu saba ya dunia yaani bonde la Ngorongoro walipata fursa ya kujionea wanyama na baionuwai za aina mbalimbali kama vile Simba,Tembo,chui na ndege wa aina tofauti.

Mbali na hayo walijionea pia maboma ya Maasai ambayo nayo yanatumika kutangaza utamaduni wa kabila la wamaasai ambao na kuwezesha kuingiza serikali fedha nyingi za kigeni kutoka kwa watalii wanaotembelea hifadhi hiyo.

Akizungumzia kuhusiana na aliyojifunza ndani ya Ngorongoro mmoja wa warembo Angelina Ndege kutoka Mkoa wa Lindi kanda ya mashariki alisema amejifunza kwamba kuna hifadhi zingine siyo lazima waishi wanyama pori tu bali hata binadamu nao wanaishi.

“Tangia nizaliwe miaka 19 iliyopita sikuwahi kufikiri kama wanyamapori hawawezi kuishi na binadamu, lakini ndani ya bonde la Ngorongoro nimeshuhudia wanyama wakiishi na binadamu tena bila rabsha yoyote,” alisema Ndege.

Aidha alibainisha kuwa ameweza kujifunza kwamba wanyama huwa hawakai katika hifadhi moja bali huwa wanahama na kwenda sehemu zingine kutafuta malisho kuendana na hali ya hewa.

Kutokana na hilo aliwaomba Watanzania kujenga tabia ya kutembelea hifadhi za taifa zilizopo nchini na kuachana na fikra kwamba wanaopaswa kwenda katika maeneo hayo ya rasilimali za taifa ni watalii kutoka nje tu ili kusaidia kuinua uchumi wa nchi kupitia sekta ya utalii.


Mary Magali ambaye ni mrembo anaewakilisha mkoa wa Iringa aliwashukuru wadhamini wakuu wa mashindano haya ambao ni Vodacom Tanzania kwa kudhamini mashindano haya pamoja na gharama zote za kutembelea hifadhi za taifa kanda ya kaskazini ili kujionea na kujifunza kuhusiana na rasilimali za taifa.

“La muhimu nililojifunza baada ya kutembelea hifadhi za taifa ya Kinapa na Ngorongoro ni kufahamu kuhusiana na Simba wanaopanda miti wanaopatikana ndani ya kreta ikiwemo maji yam to wa mbu na kirurumo kukutana sehemu moja inayotumiwa na viboko kulala na kusambaa ziwani,” alisema Magali.

Naye Mlezi wa warembo hao ambae alikuwa mshiriki wa Vodacom Miss Tanzania 2009,Gladys Shao, alisema warembo wote wanaendelea vizuri na maandalizi na hawana matatizo yoyote ya kiafya na kwamba wanafurahia na kujifunza mambo mbalimbali ya utalii wa ndani kwani unaanza na Mtanzania mwenyewe.

bongocelebrity yafanya mahojiano na Madaraka Nyerere


Jina la Madaraka Nyerere (pichani) sio geni miongoni mwa watanzania.
Ukiachilia mbali ukweli kwamba yeye ni mtoto wa sita wa Hayati Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere (kitu ambacho bila shaka kinampa automatic celebrity status), yeye pia ni mwandishi,mfanyabiashara na mtu ambaye huwa hasiti kuelezea hisia zake kuhusu mambo mbalimbali iwe ni katika nyanja za kisiasa,kijamii na hata kiuchumi kila mara fursa ya kufanya hivyo inapojitokeza.

Mwaka jana mwezi wa nne(April) yeye na Jaffar Amin(mtoto wa Iddi Amin-Rais wa zamani wa Uganda) waliingia katika vitabu vya kumbukumbu vya wapenda amani duniani walipokutana kwa mara ya kwanza ikiwa ni ishara ya amani na usuluhisho barani Afrika na kwingineko.

Hivi karibuni nilipata nafasi ya kuzungumza naye kuhusu mambo kadhaa yakiwemo ya kifamilia na pia kupata maoni yake kuhusu mambo mbalimbali.Je,ni kwanini mpaka leo hii hajajiingiza katika masuala ya siasa au uongozi?Anamuelezeaje Hayati Baba wa Taifa kama baba yake na kama kiongozi?

Ana ushauri gani kwa wapiga kura katika mwaka huu wa uchaguzi? Ana mtizamo gani kuhusu viongozi mbalimbali ambao hupenda kumuenzi Baba wa Taifa kwa maneno huku vitendo vyao vikiwa tofauti kabisa? Unataka kujua kwanini alipewa jina la “Madaraka”? Ana ushauri gani kwa vijana kuhusu suala zima la kujiletea maendeleo? Fuatana nasi katika mahojiano yafuatayo kwa ku
BOFYA HAPA

THE DON HIMSELF

Karibuni sana kwenye blog hii ya kijamii iliyosheheni makila kitu kuanzia siasa uchumi afya na burudani kwa ujumla wake.uingiapo kwenye blog hii ni mengi ambayo utapata nafasi ya kukutana nayo,kumbuka mawazo yako ndo hasa yanayojenga na kunifanya niwe na ufanisi zaidi.kariiiiiiibuuuuuuuuuuuu saaaaaaaaaaaaaaanaaaaaaaaaa.(THE DJ HIMSELF-JIWE)

Followers

BLOG ZA MARAFIKI

Search This Blog

ZILIZOPITA

DUNIA MUZIMA