Aug 27, 2010

wanaume kuitambulisha albam yao pamoja na website yao octoba 25


kundi la Wanaume (lililojiengua kutoka kwa kundi la Wanaume Halisi) linatarajia kuitambulisha albamu yake mpya itakayokwenda sambamba na uzinduzi wa Logo pamoja na tovuti yao kwa watu maalumu ndani ya kiota cha maraha kilichopo kati kati ya jiji,Savanah Lodge mnamo Octoba 25.

Akizungumza na blog jirani jijini Dar jioni hii kiongozi wa kundi hilo Rich One amesema kuwa baada kuikamilisha albamu yao yenye jumla ya nyimbo kumi,kwa sasa wanajipanga vyema kuitambulisha albamu hiyo itakayojulikana kwa jana la POA TUA, vile vile utakwenda sambamba na uzinduzi wa Logo na tovuti itakayokuwa na habari zao mbalimbali zikiwemo na kazi zao kama vile vyimbo na video zao.

"Tumeamua kuja na mambo mapya baada ya kimya kidoogo kwa wapenzi wetu,kama nilivyosema hapo awali albamu ina jumla ya nyimbo kumi,ambazo baadhi yake ni Poa Tu, Mapenzi Matamu, Apple, Moyo Wangu, Zaga Zaga na nyingine nyingi," alisema Rich One na kuongeza kuwa albamu hiyo imesheheni mahadhi tofauti tofauti kama vile Zouk, R&B pamoja na Hip Hop.

Rich One amesema kuwa ndani ya albamu hiyo amewashirikisha wasanii kadhaa mahiri katika anga ya muziki wa kizazi kipa,kama vile Chidi Benz,Kitokororo wa FM Academia,Hard Mad,Chiku Keto,Mh Themba na wengineo.

Kundi hilo linaloundwa na wakali akiwemo Athuman Yahya (A.Man), Juma Mbelwa (Juma Jazz), Karim Kaiman (Kakaman), Abdul Ally (Mzimu), Richard Shauri (Rich One) pamoja na David Mpangile (Daz-p).

No comments:

THE DON HIMSELF

Karibuni sana kwenye blog hii ya kijamii iliyosheheni makila kitu kuanzia siasa uchumi afya na burudani kwa ujumla wake.uingiapo kwenye blog hii ni mengi ambayo utapata nafasi ya kukutana nayo,kumbuka mawazo yako ndo hasa yanayojenga na kunifanya niwe na ufanisi zaidi.kariiiiiiibuuuuuuuuuuuu saaaaaaaaaaaaaaanaaaaaaaaaa.(THE DJ HIMSELF-JIWE)

Followers

BLOG ZA MARAFIKI

Search This Blog

ZILIZOPITA

DUNIA MUZIMA