Aug 20, 2010

BAADHI YA WAREMBO WANAO WANIA TAJI LA MISS TANZANIA MWAKA HUU

Wilhemina Etami (Kanda ya Kati)
Alice Lushiku (Kanda ya Kinondoni)
Bahati Chando (Ilala)
Flora Martin (Elimu ya Juu)
Fatma Ibrahim (Kanda ya Ziwa)
Salma Mwakalukwa(Ilala)
Buduri Ibrahim(Kanda ya Ziwa)
Amisuu Malick (Kinondoni)
Britnery Urassa (Temeke) Irene Hezron (Kinondoni)
Genevieve Emmanuel (Teneke) Vodacom Miss Tanzania anayemaliza muda Miriam Gerald akiwa katika kubarizi hkambini hapo.
Vodacom Miss Tanzania katika picha ya pamoja. Moja ya sehemu ya vivutio vilivyopo katika hoteli ya Giraffe View Dar es Salam.
Baadhi ya warembo.
Mlezi wa Miss Tanzania ambaye pia ni Mkurugenzi wa Kituo Cha Uwekezaji nchini (TIC) Emmanuel Ole Naiko,alipowatembelea jana na kambini kwao hoteli ya Giraffe View, Dar es Salaam.

FOMU ZA KUGOMBE URAIS ZARUDISHWA RASMI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akiwashukuru jana jijini Dar es salaam, wanachama wa CCM waliojitokeza kumpongeza kwa hatua ya kurejesha fomu katika Ofisi za Tume ya Uchaguzi na pia kukubaliwa kama Mgombea halali wa CCM katika uchaguzi ujao. Picha na Tiganya Vincent-Dar es salaam
Mgombea Mwenza wa Rais Jakaya Mrisho Kikwete Dkt Mohamed Gharib Bilal akiwashukuru wanachama wa CCM na wapenzi waliofika jana katika viwanja vya Ofisi Ndogo ya CCM jijini Dar es salaam kwa ajili ya kuwapongeza kwa kukubaliwa bila na Tume ya Uchaguzi ya Tanzania kuwa wagombea kwa tiketi ya CCM katika uchaguzi ujao.
Katibu Mkuu wa CCM Yusuph Makamba (kushoto) akiteta na Mwenyekiti wa CCM Dkt Jakaya Kikwete jana nje ya Ofisi Ndogo za CCM jijini Dar es salaam mara baada kurejea kutoka Tume ya Uchaguzi alipokuwa amerudisha Fomu ya kuwania Urais wa Tanzania katika uchaguzi Mkuu ujao.
Msaani Ummy Wenceslaus (Dokii) akitumbuiza jana jijini Dar es salaam baadhi ya wanachama waliofika katika Ofisi Ndogo za CCM kuwalaki wagombea wao mara baada ya Rais Kikwete na Mgombea Mweza Dkt Bilal kurejea kutoka Tume ya Uchaguzi ambapo alikuwa amerudisha fomu kuwania Urais wa Tanzania katika uchaguzi Mkuu ujao.
Wanachama wa Chama Cha Mapinduzi wakiwasikiliza wagombea wao wakati walipokuwa wakihutubia maelfu wa wanachama wao katika ofisi ndogo ya chama CCM Lumumba.

Wagombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha CHADEMA Dr. Wilbroad Slaa kushoto na Mgombea Mwenza Khamis Hamad Khamis mara baada ya kurejesha fomu zao katika ofisi za tume hiyo leo jijini Dar es salaam. Tume ya Taifa ya Uchaguzi ilipanga kuwa Wagombea wote wanatakiwa kuwa wamerudisha fomu leo Agost 19 na kesho Agosti 20 ndiyo kampeni zinaanza rasmi kwa vyama vyote ambapo uchaguzi mkuu unatarajiwa kufanyika Oktoba 31 mwaka huu.
Wanachama wa Chama CHADEMA wakishangilia nje ya ofisi za Tume ya Uchaguzi ya Taifa wakati walipomsindikiza wagombea wa urais kupitia chama hicho wakati waliporejesha fomu katika Tume hiyo leo jijini Dar es salaam.
Mwenyekiti wa NCCR Mageuzi James Mbatia akiwa katika msafara nawanachama wa chama hicho katika maeneo ya Moroco Konondoni jijini Dar es salaam mara baada ya kurejesha fomu ya kugombea ubunge jimbo la Kawe leo.
Wanachama wa chama cha NCCR Mageuzi wakiwa katika msafara katika maeneo ya Moroco Kinondoni mara baada ya mgombea wao wa ubunge jimbo la kawe kurejesha fomu za kugombea ubunge kawe leo.

Wagombea Urais kupitia Chama Cha Wananchi CUF Prof. Ibrahim Lipumba kushoto na Mgombea mwenza Duni Haji Duni wakipunga mikono yao mara baada ya kurejesha fomu zao katika Ofisi za Tume ya Taifa ya Uchaguzi Jijini Dar es salaam leo ambapo wagombea kutoka vyama vyote vyote wanatarajia kuanza kampeni kesho nchini kote.
Viongozi wa Chama Wanachi CUF wakinyanyua juu mikono yao kuwapungia wanachama wa Chama hicho waliowasindikiza wagombea wao wakati waliporejesha fomu leo jijini Dar es salaam.
Wanachama wa chama cha CUF wakishangilia katika ofisi za Tume ya Uchaguzi leo wakati wagombea urais wa chama chao waliporejesha fomu Tume ya Uchaguzi leo.

Zitto Kabwe asks for your contributions

Dear Friends,

I would like to express my heartfelt gratitude for all your support.
Today we mark the start of a new journey.

This morning I submitted my nominations forms for re-election for the Kigoma North parliamentary seat ready to serve again the people of Kigoma North and my country TANZANIA.In order to make it happen am humbly asking for your support; if you would like to see Zitto back in Parliament and serving our nation I ask for your support.
I am ready to serve you once again.

DONATE:
Help Zitto keep fighting for our future and our country. Join the campaign by making a donation today.
Your contribution and support will help us in our campaign.

To donate, please:Make a Deposit to Our Campaign Account:

NAME: ZITTO KABWE ZUBERI
BANK: CRDB BANK
ACCOUNT NUMBER: 01J2082022500

Contact Details:
Contact Person: Mhonga Ruhwanya
Mobile Number: +255 0758 000 111
E-mail Address: zitto2010@gmail.com
FACEBOOK: http://www.facebook.com/zittokabwe
Blog: http://www.zittokabwe.wordpress.com/
Follow me on my Twitter Account: http://www.twitter.com/zittokabwe
On FLICKER(PICTURES): http://www.flickr.com/photos/zittokabwe

ZITTO KABWE CAMPAIGN

Aug 18, 2010

UJUMBE WA SAJNA KWA MAFANZ WAKE


Hello, asante sana kwa mchango wako wa aina yoyote uliotupatia katika kuifanikisha album ya Sajna mpaka kukamilika na sasa ikiwa tayari kuingia sokoni Alhamisi hii tarehe 19 Agosti 2010, ASANTE SANA..


ALBUM TITLE: IVETA
ARTIST: SAJNA
RELEASE DATE: 19TH AUGUST 2010
EXECUTIVE PRODUCER: KID BWOY
DISTRIBUTOR: GMC & UMOJA AUDIO VISUAL
ALBUM DETAILS:
Album ya IVETA ya msanii SAJNA ina jumla ya nyimbo 10, ambayo ilianza kutengenezwa Mwezi January 2010 na kukamilika mwezi July 2010. Wasanii waliopata nafasi ya kushirikishwa katika album hii ni Belle 9, Linah wa THT, Josefly kutoka Musoma Mara pamoja na Pipi. Lengo la kutoshirikisha wasanii wengi sana ni kutaka kuonesha uwezo wake na kuthibitisha kwamba msanii mchanga si lazima atoke kwa kupitia mgongo wa wasanii wakubwa.
Studio na producers waliohusika kutengeneza nyimbo katika album hii ni pamoja na TETEMESHA RECORDZ chini ya KID BWOY, AB RECORDS chini ya AMBA, A2P chini ya SAM TIMBER, IMMORTAL MUSIC chini ya TRIS na M LAB chini ya DUKE.
Single ya pili kutoka bado haijaamuliwa ila ni kati ya SITAKI KUUMIZWA na MBALAMWEZI, moja kati ya hizo itakayopendekezwa na wadau wengi ndio itakayofuata baada ya IVETA.

Song list as appeared on Cd cover
1. IVETA
2. Sitaki Kuumizwa ft. Linah
3. Binadamu
4. Mbalamwezi
5. Udehule
6. Mganga ft. Josefly
7. Nadhifa
8. Roho Mbaya ft. Belle 9 & Pipi
9. Subira
10.Ishara ya Msalaba
ALBUM ITATOKA KATIKA CD NA AUDIO CASSETTE

Regardz
Executive Producer
Kid bwoy
Tetemesha Recordz

dr shein ahutubia wagombea wa ubunge uwakilishi zanzibar

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mgombea wa Urais wa Zanzibar kwa tiketi ya CCM Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein, akiwahutubia Wagombea wa Viti vya Ubunge, Uwakilishi na Udiwani pamoja na Wananchi mbalimbali katika ukumbi wa salama Hoteli ya Bwawani Zanzibar leo.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mgombea wa Urais wa Zanzibar kwa tiketi ya CCM Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein, akisalimiana na wananachama wa Chama cha Mapinduzi na Wananchi wa Zanzibar, baada ya kuwahutubia kwenye mkutano wa Hadhara uliofanyika leo katika ukumbi wa Salama Hoteli ya Bwawani Zanzibar.

Wagombea wa Viti vya Ubunge, Uwakilishi, Udiwani pamoja na Wananchi mbalimbali wa Zanzibar, kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi Wakimsikiliza Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mgombea Urais wa Zanzibar Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein, alipokuwa akiwahutubia kwenye mkutano wa Hadhara katika ukumbi wa Salama Hoteli ya Bwawani Zanzibar leo.

(Amour Nassor -VPO)

HILI NDO LIBENEKE JIPYA LA MDAU MUHIDINI ISSA MICHUZI.

Asalaam Aleikhum Wadau, Kwa furaha, heshima na taadhima naomba kutangaza rasmi libeneke jipya la www.michuzipost.com ambalo wikiendi ilopita lilipaa hewani katika kile kiitwacho uzinduzi laini (soft launch). Kunradhi kwa kutowataarifu mapema, kwani ilibidi mambo kadhaa yawekwe sawa kwanza kabla ya kuthubutu kutia neno kama nifanyavyo sasa. Wadau wa Globu ya Jamii naomba baraka zenu pamoja na maoni juu ya libeneke hili ambalo azma ya kulianzisha ni ile ile ya Kuendeleza Libeneke kwa njia ya kisasa zaidi na kwa upana mkubwa. Hivyo nakaribisha maoni, ushauri pamoja na neno lolote lile litalonkisaidia kuboresha libeneke hili. Kama nilivyotamka awali, bado niko katika uzinduzi laini, kwani kama ujuavyo libeneke kama hili halitaki papara. Linahitaji subira, sikion sikivu la neno toka kwa wadau ambao sapoti yao naithamini kama lulu kwa muda wote huu. Globu ya Jamii itaendelea kuwepo hewani kama kawaida, na itaenda sambamba na Libeneke hili la www.michuzipost.com pamoja na lile la www.michuzi-matukio.blogspot.com. Hivyo wadau Globu ya Jamii itaendelea kudunda kama kawaida, ikiwa ni chapuo la Libeneke jipya ambalo kama utavyoliona, litakuwa na habari na taarifa motomoto kwa mapana na undani zaidi. Inshaallah panapo majaaliwa Libeneke hili jipya litazinduliwa rasmi mnamo September 8, mwaka huu - ikiwa ni siku ya kuadhimisha miaka mitano kamili ya kuzaliwa kwa Globu ya Jamii kama link hii inavyojionesha http://issamichuzi.blogspot.com/2005/09/michuzi-and-ndesanjo.html#comments. Namshukuru Muumba wa Yote kwa kunipa nguvu na uwezo kufikia hapa nilikofikia. Pia natoa shukrani kwa kila mdau ambaye amekuwa akinipa sapoti ya nguvu kila siku kwa kutembelea Globu ya Jamii. Ni mategemeo yangu kwamba baada ya kwikwi ya kuwa na Libeneke jipya wakati fulani huko nyuma, sasa mambo yanaonekana kuwa mswano na Libeneke litaendelea kama kawa. Libeneke hili jipya la www.michuzi.post.com limewezekana kwa ushauri na msaada pamoja na ushirikiano mkubwa wa Bw. Zubeir Masabo na Bw. Alistair Horsburgh, washirika wangu walio Uingereza ambao kwa pamoja tutaendesha Michuzi Post Ltd. kampuni rasmi itayosimamia uzalishaji wa bidhaa za www.michuzipost.com. Sambamba nasi pia kuna kikosi kazi kikubwa ambacho kitakuwa kinashughulika katika kuendeleza Libeneke hili. Muhidin Issa Michuzi Mkurugenzi Michuzi Post Ltd.

Tume ya Kurekebisha Sheria Yaanza Kupitia Ripoti Ya Sheria Za Mila!!

Katibu Tawala wa Wilaya ya Ulanga Bw. Alfred Shayo aliyesimama akizungumza kabla ya kuanza kiako cha kupitiwa ripoti ya Rasimu ya Sheria za Mila zinazofuata mkondo wa ukoo wa mama, katikati ni Ofisa Sheria wa Tume Shadrack Makongoro.

(Picha zote na Ofisa Habari wa Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania Munir Shemweta)

Ofisa Sheria wa Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania Shadrack Makongoro (kulia )akimkabidhi Mkuu wa Wilaya ya Ulanga Bw. Francis Miti baadhia ya vifaa kwa ajili ya kuitangaza Tume katika Wilaya yake, wa kwanza kushoto ni Katibu Twala wa Wilaya ya Ulanga Bw. Alfred Shayo.

Ofisa Sheria wa Tume Shadrack Makongoro akisikiliza maoni ya washiriki wa kikao hicho.
Baadhi ya Washiriki wa kikao cha kujadili rasimu ya Sheria za Mila zinazofuata mkondo wa ukoo wa mama katika wilaya ya Ulanga mkoani Morogoro.

Rais Kikwete azindua mnara wa Mashujaa wa Majimaji, Azindua mtambo wa kuzalisha umeme kutumia Gesi Asilia huko Somanga-Kilwa!!

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akibonyeza kitufe kuzindua mradi wa Umeme unaotumia gesi ya aslia huko Somanga Fungu jana jioni.Huko waziri wa Nishati na madini William Ngeleja(watatu kushoto) na Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO Wiliam Mhando(wane kushoto) wakiangalia.Wa kwanza kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Lindi Said Meck Sadiq.(picha na Freddy Maro)
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akifunua kitambaa kuashiria kuzindua mradi wa umeme wa gesi ya asilia huko kijiji cha Somanga Fungu, mkoani Lindi jana jioni.Kushoto ni Waziri wa Nishati na madini William Ngeleja na kulia ni Mkurugenzi mtendaji wa TANESCO William Mhando.
Amiri Jeshi mkuu Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiweka silaha za kijadi katika mnara wa Kumbukumbu ya Mashujaa wa vita vya Majimaji katika kijiji cha Nandete, kata ya Kipatimu wilayani Kilwa jana mchana.(kwa msaada wa blog jirani(full shangwe))

Mwakalebela ajisalimisha, asomewa mashitaka, yuko nje kwa dhamana

Na www.wavuti.com

Frederick Mwakalebela na mkewe, Celina, kizimbani Iringa

Aliyekuwa mshindi wa kura za maoni jimbo la Iringa mjini Bw Frederick Mwakalebela na (suti nyeusi ) akiwa na mkewe (suti nyeupe) wakisindikizwa na marafiki kuingia mahakamani.

Umati mkubwa wa wananchi wa mji wa Iringa na vitongoji vyake ulifurika kusikiliza kesi ya tuhuma za rushwa iliyofunguliwa na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa, TAKUKURU, dhidi ya aliyekuwa mgombea wa Ubunge wa Jimbo la Iringa Mjini kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi, CCM, bwana Frederick Mwakalebela.

Kesi hiyo ndivyo iliyotamkwa na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM kuwa Kamati Kuu ya Chama Cha Mapinduzi, NEC-CCM kama kigezo kikuu cha kuliengua jina la Frederick Mwakalebela katika nafasi hiyo hata ikiwa alishinda katika kura ya maoni, na badala yake nafasi hiyo kupewa mbunge aliyemaliza muda wake na anayewania tena nafasi hiyo, bi Monica Mbega.

Inasimuliwa na Francis Godwin kupitia blogu yake kuwa umati mkubwa wa wananchi wa jimbo la Iringa waliacha shughuli zao na kufika kusikiliza kesi ya Mwakalebela kiasi cha watu kukosa nafasi za kuketi ndani na hivyo kuifuatilia kesi hiyo wakiwa nje ya chumba cha Mahakama ilikokuwa ikiendelea kesi hiyo.

Anasema kuwa baadhi ya wananchi walikuwa na barua zao tayari kwa ajili ya kumdhamini bwana Mwakalebela endapo ingehitajika kufanya hivyo, vile vile, “…mahakimu wasema haijapata kutokea toka kuanzishwa kwa mahakama hiyo umati mkubwa kama huo kuja mahakamani kusikiliza kesi”.

Mwalalebela, ambaye alikuwa kajiandaa kikamilifu, alipataa dhamana iliyosainiwa ya shilingi Milioni 5 na wadhamini wawili.

Mwakalebela akisubiri kusomewa shitaka mahakamani Iringa

Aug 17, 2010

rais karume amwakilisha rais kikwete mkutano wa sadc nchini namibia

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk Amani Abeid Karume,akiwa ni miongoni mwa Viongozi wa Nchi za SADC akimuakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Jakaya Mrisho Kikwete katika Mkutano wa siku mbili unaohusu masuala mbali mbali ya Kiuchumi na Kijamii,uliofanyika katika ukumbi wa Safari Court Hotel nchini Namibia,(kushoto) Rais wa Afrika Kusini
Jacob Gedleyihlekisa Zuma.
Rais wa Malawi Prof Bingu Wa Mutharika akimkabidhi zawadi Mwenyekiti wa Umoja wa Afrika,Rais wa Nchini Congo Joseph Kabila,wakati wa Mkutano wa siku mbil9i kwa Nchi za SADC pia uandhimisha miaka 30 tokea kuundwa kwa jumuiya hiyo.
Rais wa Nchini Malawi Prof Bingu Wa Mutharika akitoa hutuba yake wakati wa mkutano wa siku mbili Nchi za SADC,unaoendelea Nchini Namibia,mkutano huo pia unaadhimisha miaka 30 tokea kuundwa kwa jumuiya hiyo.
Marais wa Nchi Mbali mbali wakiisimama wkati wa Wimbo wa Taifa za Nchi kbla ya kuanz kwa mkutao wa Jumuiya ya SADC,uliofanyika Nchini Namibia pia mkutno huo unaadhimisha miaka 30 tkea kuundwa kwa jumuiya hiyo.
Mke wa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mama Shadya Karume,akisalimiana na Rais Mstaafu wa Namibia Sam Nujoma,wakati wa Mkutano wa Nchi za, SADC Uliofanyika Nchini Namibia.
Waziri Nchi Afisi ya Rais anaeshuhulikia Fedha na Uchumi,Zanzibar Mwinyihaji Makame,akiteta jambo na Waziri wa Ushirikiano wa Afrika ya Mashariki Mohammed Aboud,wakati wa Mkutano wa siku mbili kwa Nchi za SADC,uliofanyika Nchini Namibia.
Washiriki wa Mkutano wa siku mbili wa Nchi mbali mbali za SADC wakisikiliza kwa makini harakati na matukio katika mkutano huo,liofanyika Nchini Namibia,katika ukumbi wa Safari Court Hotel pia mkutano huo unadhimisha miaka 30 tokea kuanzishwa jumuiya hiyo .
Wake za Marais wa Nchi za Jumuiya ya SADC,pamoja na Marais wastaafu wa Jumuiya hiyo kwa pamoja na washiriki wengine wa Mkutano wa siku mbili wa jumuiya hiyo,wakifuatilia kwa makini,matukio mbali mbali yanayoendelea katika ukumbi wa Safari Court Hotel.
Marais wastaafu wa Jumuiya hiyo kwa pamoja na washiriki wengine wa Mkutano wa siku mbili wa jumuiya hiyo,wakifuatilia kwa makini,matukio mbali mbali yanayoendelea katika ukumbi wa Safari Court Hotel.
Wake za Marais wa Nchi za Jumuiya ya SADC,pamoja na Marais wastaafu wa Jumuiya hiyo kwa pamoja na washiriki wengine wa Mkutano wa siku mbili wa jumuiya hiyo,wakifuatilia kwa makini,matukio mbali mbali yanayoendelea katika ukumbi wa Safari Court Hotel.
Wanafunzi wa Secondary School walioshinda Insha zinazoelezea masula a ya SADC,wakia na vyeti vyao baada ya kukabidhia na Rais Kabil,(kushoto) ni Chresencia Stephen Marwa kutoka Tanzania na Incinon Adaiano Ganga kutoka Angola wakiwa katika ukumbi wa Mkutano wa SADC,Safari Court Hotel.

Mwenyekiti Mpya wa SADC,Rais wa Namibia Hifikepunye Pohamba akitoa hutuba yake baada ya kuwa Mwenyekiti Mpya wa Jumuiya hiyo,katika Ukumbi wa Mkutano wa siku mbili,uliofanyika Safari Court Hotel,Nchini Nambia,pia mkutano huo unadhimisha miaka 30 tokea kuanzishwa kwa jumuiya hiyo.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk Amani Abeid Karume,akiwa katika Picha ya pamoja na Viongozi wakuu wa Nchi za SADC walioshiriki Mkutano wa Siku mbili uliofanyika Nchini Namibia,katika Ukumbi wa Mikutano wa Safari Court Hotel,Nchini Namibia,Rais karume anamuwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Jakaya Mrisho Kikwete.

Orodha ya wagombea ubunge na uwakilishi katika uchaguzi mkuu wa Tanzania 2010 ya chama cha CUF

Katibu Mkuu wa CUF Maalim Seif Shariff Hamad

Dar es Salaam

Tanga

Hussein Siyovelwa (Ilala);
Kimangale Mussa (Segerea);
Heko Pori (Ukonga);
Shaban Mapeyo (Kawe);
Shabaan Nassor (Kinondoni)
Mustafa Mungwe (Kigamboni)

Mussa Mbarouk (Tanga Mjini);

Remmy Shundi (Handeni);
Bakar Mbega (Mkinga);
Abubakar Bakari (Muheza);
Gogola Gogola (Mlalo);
Fabi Sozi (Bumbuli);
Abassy Mkankamghanga (Lushoto),
Jumaa Magogo (Korogwe Mjini);

Mohamed Asiu (Korogwe Vijijini)

Omar Masomaso (Pangani)

Kilimanjaro

Awadh Mwarabu (Same Magharibi).
Mtwara ni Hassan Abdallah (Mtwara Mjini);
Katani Katani (Tandahimba);
Clara Mwatuka (Masasi);
Mtikita Mtikita (Lulindi);
Hakika Maarifa (Newala)
Chikamba Wanainuka (Mtwara Vijijini)

Lindi

Salum Barwany (Lindi Mjini);
Ayubu Nassor (Mchinga),
Khalfan Mandanje (Mtama);
Madaraka Beyi (Liwale),
Nanjase Nanjase (Nachingwea),
Abubakary Kondo (Ruangwa),
Seleman Bungara (Kilwa Kusini)
Said Manoro (Kilwa Kaskazini).

Tabora

Edward Zombwe (Urambo Mashariki),
Kirungi Kirungi (Urambo Magharibi),
Hassan Mwigwayasila (Igalula),
David Kassoga (Tabora Kaskazini),
Kidumla Kidumla (Bukene),
Dominic Kizwalo (Nzega)
Abdallah Katala (Sikonge)

Kagera

Christina Kasimbazi (Bukoba Vijijini),
Nicolaus Batalingaya (Karagwe),
Twaha Taslima (Bukoba Vijijini),
Hamida Issa (Biharamulo Magharibi),
David Tibanywana (Chato)
Yahya Ndyema (Nkenge)

Arusha

Ghariby Baalawy (Arusha Mjini),
John Pallangyo (Arumeru Mashariki),
Adella Kileo (Arumeru Magharibi)
Navaya Ndaskoi (Monduli)

Mara

Mustafa Wandwi (Musoma Mjini),
Vedastus Msita (Mwibara)
Wilegi Songambele (Bunda)
Pwani ni Jafar Ndende (Mkuranga),
Seif Porwe (Kibiti),
Ali Kihambwe (Rufiji),
Wahabi Twalut (Mafia),
Adui Kondo (Kisarawe),
Zahoro Vuai (Bagamoyo)
Miraj Mtibwiliko (Chalinze)

Shinyanga

Mwalimu Mbukuzi (Shinyanga Mjini),
Khanipha Ruhinda (Maswa Mashariki),
Seif Baya (Maswa Magharibi),
Jackson Deodatus (Bukombe),
Shashu Lugeye (Solwa),
Sauda Kasiga (Msalala),
Hamisi Makapa (Kahama),
Creoface Magere (Mbogwe)
James Matinde (Kisesa)

Kigoma

Fatma Kinguti (Kigoma Mjini),
Salum Kajanja (Buyungu),
Athumani Hamisi (Muhambwe),
Rashid Kaduguda (Kasulu Magharibi)
Ibrahim Magara (Buhigwe)

Mbeya

Ezekia Mtafya (Ileje),
Asukile Kabango (Mbozi Magharibi),
Nkuyuntila Siwale (Mbozi Mashariki),
Yusuf Said (Kyela)
Shaweji Salinyambo (Mbarali)

Iringa

Mussa Fufumbe (Isimani),
Godfrey Hongele (Njombe Kaskazini),
Stanley Fwila (Njombe Kusini)
Jacob Mhanga (Njombe Magharibi)

Manyara

Rashid Mgaya (Babati Mjini),

Juma Nyeresa (Kiteto)

Eliseus Amedeus (Mbulu)

Ruvuma

Mazee Mazee (Tunduru Kaskazini),
Mohammed Mambo(Tunduru Kusini)
Hassan Mtwangambati (Namtumbo)

Morogoro

Willy Dikundile (Kilosa Kati),
Abeid Mlapakolo (Morogoro Mjini)
Blandina Mwasabwite (Morogoro Kusini Mashariki)

Mwanza

Komanya Athanas (Buchosa),

Mbaraka Chiru (Sengerema),
Peter Malebo (Geita),
Oscar Ndalahwa (Busanda),
Andrea Mkanga (Nyang’hwale),
Abdallah Mtina (Misungwi),
Omar Mbalamwezi (Nyamagana),
Mtebe Msita (Ukerewe),
Ligawa Ndalahwa (Kwimba)
Julius Samamba (Sumve)

Katavi

Aram Ndimubenya (Mpanda Mjini),

Athumani Kababende (Mpanda Vijijini)

Abbas Ally (Katavi)

Singida

Rashid Mindicar (Singida Mjini),
Sizimwe Kanyota (Singida Kaskazini)
Dalfina Patric (Singida Magharibi)

Dodoma

Ngomoka Joseph (Mtera),
Ngomoka William (Chilonwa),
Yahya Deni (Kondoa Kaskazini),
Hassan Missanya (Kondoa Kusini)

Tabora

Kapasha Kapasha (Tabora Mjini)

Zanzibar

Faki Haji Makame (Mtoni),

Rashid Soud Khamis (Bububu),

Hassan Omar Issa (Mfenesini),
Khamis Msabaha Mzee (Dole),
Khatib Haji Ali (Fuoni),
Ussi Juma Hassan (Mwanakwerekwe),
Hamad Ali Hamad (Magogoni),
Hemed Said Nassor (Dimani),
Seif Suleiman Kombo (Amani)
Khamisi Ali Khamisi (Kwamtipura)
Ali Juma Khamisi (Chumbuni),
Khamisi Mussa Haji (Kwahani),
Idarous Habib Mohamed (Kikwajuni),
Khalid Rajab Mghanah (Rahaleo),
Suleiman Khamis Ally (Mpendae),
Muhammad Ibrahim Sanya (Mji Mkongwe),
Mohamed Yussuf Maalim (Jang’ombe)
Ahmed Khamis Hamad (Magomeni)
Ramadhan Ali Mbarouk (Bumbwini),
Ali Rashid Ali (Kitope),
Othman Habibu Juma (Donge),
Ali Mati Wadi (Matemwe),
Yussuf Haji Khamis (Nungwi),
Rashid Khamis Rashid (Tumbatu),

Khamisi Suleiman Kombo (Chaani),
Hassan Omar Nahodha (Mkwajuni),
Abdi Mohamed Adeyoum (Uzini),
Ali Khamis Ame (Chwaka)
Shabaan Iddi Ame (Koani)
Mohamed Kombo Ali (Makunduchi),
Vuai Issa Haji (Muyuni),
Mussa Haji Kombo (Chakechake),
Ahmed Juma Ngwali (Ziwani),
Hamad Rashid Mohammed (Wawi),
Haji Khatib Kai (Micheweni)

Rashid Ali Abdalla (Tumbe),

Khatib Said Haji (Konde),
Kombo Khamisi Kombo (Mgogoni),
Mbaruk Salum Ali (Wete),
Khalifa Suleiman Khalifa (Gando),
Said Suleiman Said (Mtambwe),
Rajab Mbarouk Mohamed (Ole),
Rashid Ali Omar (Kojani),
Salim Hemed Khamis (Chambani),
Mohamed Habib Mnyaa (Mkanyageni),
Masoud Abdalla Salim (Mtambile),
Abdalla Haji Ali (Kiwani)
Ali Khamisi Seif (Mkoani)

Watakaowania uwakilishi katika Baraza la Wawakilishi

Nassor Ahmed Mazrui (Mtoni),
Bakar Haji Muhammad (Bububu),
Masoud Nassor Seif (Mfenesini),

Hasne Abdalla Abeid (Dole),

Asha Ali Fakih (Fuoni),
Idrisa Hamad (Mwanakwerekwe),
Abdilah Jihad Hassan (Magogoni)
Manzi Ibrahim Juma (Kiembesamaki)
Ali Juma Ali (Dimani),
Khamis Rashid Abeid (Amani),
Dk. Majaliwa Juma Seif (Kwamtipura),
Maulid Suleiman Juma (Chumbuni),
Hassan Juma Hassan (Kwahani)
Bakar Hassan Bark (Kikwajuni).
Omar Mussa Makame (Rahaleo),
Maharouk Abdalla Suleiman (Mpendae),
Ismail Jussa Ladhu (Mji Mkongwe),
Haji Ameir Muhunzi (Jang’ombe),
Zainab Omar Mzee (Magomeni),
Zahran Juma Mshamba (Bumbwini),
Hassan Khatib Kheri (Kitope),
Machano Omar Masanja (Donge)
Shauri Makame Mkadam (Matemwe)
Haji Mwadini Makame (Nungwi),
Makame Hamad Makame (Tumbatu),

Khamis Amour Vuai (Chaani),

Vuai Kona Haji (Mkwajuni),
Salma Hussein Zaral (Uzini),
Ali Mrisho Haji (Chwaka),
Khamis Malik Khamis (Koani)
Ameir Mussa Ameir (Makunduchi)
Suleiman Hassan Suha (Muyuni),
Omar Ali Shehe (Chakechake),

Rashid Seif Suleiman (Ziwani),
Saleh Nassor Juma (Wawi),
Abdalla Juma Abdalla (Chonga),
Subeti Khamis Faki (Michweweni),
Rufai Said Rufai (Tumbe),
Suleiman Hemed Khamis (Konde),
Abubakar Khamis Bakary (Mgogoni)
Asaa Othman Hamad (Wete)
Said Ali Mbarouk (Gando),
Salim Abdalla Hamad (Mtambwe),
Hamad Masoud Hamad (Ole),
Omar Ally Jadi (Kojani),
Mohammed Mbwana Hamad (Chambani),
Haji Faki Shaali (Mkanyageni),
Muhamed Haji Khalid (Mtambile),
Haji Hassan Hija (Kiwani)
Abdalla Mohamed Ali (Mkoani)

IMETOLEWA NA CUF MAKAO MAKUU

warembo wa miss tanzania waingia kambini leo

warembo wa Miss Tanzania wanaoingia kambini leo hii,wakiwa katika usafiri wao tayari kwa safari ya kuelekea Kambini.
wakiingia katika usafiri wao.
walinzi wa warembo (Mabaunsa)

Warembo waliofanikiwa kuingia Fainali ya Taifa ya Mashindano ya Urembo ya VODACOM MISS TANZANIA 2010, leo wameingia kambini kwa ajili ya kuanza mchakato wa kumrithi mrembo anayemaliza muda wake, Miriam Gerald.

Akizungumza na waandishi wa habari Jijini Dar es Salaam leo mchana kabla ya warembo hao kuelekea Kambini, Mkurugenzi wa Kamati ya Miss Tanzania, Hashim Lundenga, alisema kuwa “Warembo hao Wakiwa kambini watakuwa na ratiba mbali mbali ikiwa ni pamoja na kufanya kazi za kijamii na kutembelea sehemu mbali mbali za vivutio vya kitalii”

Alizitaja sehemu hizo kuwa siku ya Tarehe 17 / 08 / 2010 warembo watapewa semina maalumu na viongozi wa kamati ya Miss Tanzania pamoja na kusaini mikataba kati yao na waandaaji.

Tarehe 19 / 08 / 2010 waandishi wa habari wote watapata nafasi ya kuongea na washiriki na kupata maoni yao na jinsi walivyojiandaa katika kunyakuwa taji la VODACOM MISS TANZANIA 2010

Mwishoni mwa wiki warembo wote wakiambatana na baadhi ya viongozi wa kamati watasafiri kwenda katika mikoa ya kanda ya kaskazini “KILIMANJARO: na “ARUSHA” kwa ajiri ya kutembelea vivutio vya utalii ili kuvitangaza na kuwahamasisha watanzania ili wajenge utamaduni wa kutembelea, kuvilinda na kuvithamini vivutio vyetu.

Huu ni mpango tunaoshirikiana na taasisi za serikali yaani ,BODI YA UTALII, TANAPA na NGORONGORO CONCERVATION AREA AUTHORITY.

Huu ni mwaka wa pili taasisi yetu “Miss Tanzania” kushirikiana na taasisi za serikali kuhamasisha watanzania kuthamini na kutembelea vivutio vilivyopo nchini kwetu.

Tunategemea kwenda mbele zaidi kwa kuvitembelea vivutio vya kusini mwa Tanzania, SELOUS, RUAHA NATIONAL PARK, MIKUMI na UDIZUNGWA, katika siku za usoni.

THE DON HIMSELF

Karibuni sana kwenye blog hii ya kijamii iliyosheheni makila kitu kuanzia siasa uchumi afya na burudani kwa ujumla wake.uingiapo kwenye blog hii ni mengi ambayo utapata nafasi ya kukutana nayo,kumbuka mawazo yako ndo hasa yanayojenga na kunifanya niwe na ufanisi zaidi.kariiiiiiibuuuuuuuuuuuu saaaaaaaaaaaaaaanaaaaaaaaaa.(THE DJ HIMSELF-JIWE)

Followers

BLOG ZA MARAFIKI

Search This Blog

ZILIZOPITA

DUNIA MUZIMA