Aug 18, 2010

Mwakalebela ajisalimisha, asomewa mashitaka, yuko nje kwa dhamana

Na www.wavuti.com

Frederick Mwakalebela na mkewe, Celina, kizimbani Iringa

Aliyekuwa mshindi wa kura za maoni jimbo la Iringa mjini Bw Frederick Mwakalebela na (suti nyeusi ) akiwa na mkewe (suti nyeupe) wakisindikizwa na marafiki kuingia mahakamani.

Umati mkubwa wa wananchi wa mji wa Iringa na vitongoji vyake ulifurika kusikiliza kesi ya tuhuma za rushwa iliyofunguliwa na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa, TAKUKURU, dhidi ya aliyekuwa mgombea wa Ubunge wa Jimbo la Iringa Mjini kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi, CCM, bwana Frederick Mwakalebela.

Kesi hiyo ndivyo iliyotamkwa na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM kuwa Kamati Kuu ya Chama Cha Mapinduzi, NEC-CCM kama kigezo kikuu cha kuliengua jina la Frederick Mwakalebela katika nafasi hiyo hata ikiwa alishinda katika kura ya maoni, na badala yake nafasi hiyo kupewa mbunge aliyemaliza muda wake na anayewania tena nafasi hiyo, bi Monica Mbega.

Inasimuliwa na Francis Godwin kupitia blogu yake kuwa umati mkubwa wa wananchi wa jimbo la Iringa waliacha shughuli zao na kufika kusikiliza kesi ya Mwakalebela kiasi cha watu kukosa nafasi za kuketi ndani na hivyo kuifuatilia kesi hiyo wakiwa nje ya chumba cha Mahakama ilikokuwa ikiendelea kesi hiyo.

Anasema kuwa baadhi ya wananchi walikuwa na barua zao tayari kwa ajili ya kumdhamini bwana Mwakalebela endapo ingehitajika kufanya hivyo, vile vile, “…mahakimu wasema haijapata kutokea toka kuanzishwa kwa mahakama hiyo umati mkubwa kama huo kuja mahakamani kusikiliza kesi”.

Mwalalebela, ambaye alikuwa kajiandaa kikamilifu, alipataa dhamana iliyosainiwa ya shilingi Milioni 5 na wadhamini wawili.

Mwakalebela akisubiri kusomewa shitaka mahakamani Iringa

No comments:

THE DON HIMSELF

Karibuni sana kwenye blog hii ya kijamii iliyosheheni makila kitu kuanzia siasa uchumi afya na burudani kwa ujumla wake.uingiapo kwenye blog hii ni mengi ambayo utapata nafasi ya kukutana nayo,kumbuka mawazo yako ndo hasa yanayojenga na kunifanya niwe na ufanisi zaidi.kariiiiiiibuuuuuuuuuuuu saaaaaaaaaaaaaaanaaaaaaaaaa.(THE DJ HIMSELF-JIWE)

Followers

BLOG ZA MARAFIKI

Search This Blog

ZILIZOPITA

DUNIA MUZIMA