Aug 17, 2010

rais karume amwakilisha rais kikwete mkutano wa sadc nchini namibia

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk Amani Abeid Karume,akiwa ni miongoni mwa Viongozi wa Nchi za SADC akimuakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Jakaya Mrisho Kikwete katika Mkutano wa siku mbili unaohusu masuala mbali mbali ya Kiuchumi na Kijamii,uliofanyika katika ukumbi wa Safari Court Hotel nchini Namibia,(kushoto) Rais wa Afrika Kusini
Jacob Gedleyihlekisa Zuma.
Rais wa Malawi Prof Bingu Wa Mutharika akimkabidhi zawadi Mwenyekiti wa Umoja wa Afrika,Rais wa Nchini Congo Joseph Kabila,wakati wa Mkutano wa siku mbil9i kwa Nchi za SADC pia uandhimisha miaka 30 tokea kuundwa kwa jumuiya hiyo.
Rais wa Nchini Malawi Prof Bingu Wa Mutharika akitoa hutuba yake wakati wa mkutano wa siku mbili Nchi za SADC,unaoendelea Nchini Namibia,mkutano huo pia unaadhimisha miaka 30 tokea kuundwa kwa jumuiya hiyo.
Marais wa Nchi Mbali mbali wakiisimama wkati wa Wimbo wa Taifa za Nchi kbla ya kuanz kwa mkutao wa Jumuiya ya SADC,uliofanyika Nchini Namibia pia mkutno huo unaadhimisha miaka 30 tkea kuundwa kwa jumuiya hiyo.
Mke wa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mama Shadya Karume,akisalimiana na Rais Mstaafu wa Namibia Sam Nujoma,wakati wa Mkutano wa Nchi za, SADC Uliofanyika Nchini Namibia.
Waziri Nchi Afisi ya Rais anaeshuhulikia Fedha na Uchumi,Zanzibar Mwinyihaji Makame,akiteta jambo na Waziri wa Ushirikiano wa Afrika ya Mashariki Mohammed Aboud,wakati wa Mkutano wa siku mbili kwa Nchi za SADC,uliofanyika Nchini Namibia.
Washiriki wa Mkutano wa siku mbili wa Nchi mbali mbali za SADC wakisikiliza kwa makini harakati na matukio katika mkutano huo,liofanyika Nchini Namibia,katika ukumbi wa Safari Court Hotel pia mkutano huo unadhimisha miaka 30 tokea kuanzishwa jumuiya hiyo .
Wake za Marais wa Nchi za Jumuiya ya SADC,pamoja na Marais wastaafu wa Jumuiya hiyo kwa pamoja na washiriki wengine wa Mkutano wa siku mbili wa jumuiya hiyo,wakifuatilia kwa makini,matukio mbali mbali yanayoendelea katika ukumbi wa Safari Court Hotel.
Marais wastaafu wa Jumuiya hiyo kwa pamoja na washiriki wengine wa Mkutano wa siku mbili wa jumuiya hiyo,wakifuatilia kwa makini,matukio mbali mbali yanayoendelea katika ukumbi wa Safari Court Hotel.
Wake za Marais wa Nchi za Jumuiya ya SADC,pamoja na Marais wastaafu wa Jumuiya hiyo kwa pamoja na washiriki wengine wa Mkutano wa siku mbili wa jumuiya hiyo,wakifuatilia kwa makini,matukio mbali mbali yanayoendelea katika ukumbi wa Safari Court Hotel.
Wanafunzi wa Secondary School walioshinda Insha zinazoelezea masula a ya SADC,wakia na vyeti vyao baada ya kukabidhia na Rais Kabil,(kushoto) ni Chresencia Stephen Marwa kutoka Tanzania na Incinon Adaiano Ganga kutoka Angola wakiwa katika ukumbi wa Mkutano wa SADC,Safari Court Hotel.

Mwenyekiti Mpya wa SADC,Rais wa Namibia Hifikepunye Pohamba akitoa hutuba yake baada ya kuwa Mwenyekiti Mpya wa Jumuiya hiyo,katika Ukumbi wa Mkutano wa siku mbili,uliofanyika Safari Court Hotel,Nchini Nambia,pia mkutano huo unadhimisha miaka 30 tokea kuanzishwa kwa jumuiya hiyo.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk Amani Abeid Karume,akiwa katika Picha ya pamoja na Viongozi wakuu wa Nchi za SADC walioshiriki Mkutano wa Siku mbili uliofanyika Nchini Namibia,katika Ukumbi wa Mikutano wa Safari Court Hotel,Nchini Namibia,Rais karume anamuwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Jakaya Mrisho Kikwete.

No comments:

THE DON HIMSELF

Karibuni sana kwenye blog hii ya kijamii iliyosheheni makila kitu kuanzia siasa uchumi afya na burudani kwa ujumla wake.uingiapo kwenye blog hii ni mengi ambayo utapata nafasi ya kukutana nayo,kumbuka mawazo yako ndo hasa yanayojenga na kunifanya niwe na ufanisi zaidi.kariiiiiiibuuuuuuuuuuuu saaaaaaaaaaaaaaanaaaaaaaaaa.(THE DJ HIMSELF-JIWE)

Followers

BLOG ZA MARAFIKI

Search This Blog

ZILIZOPITA

DUNIA MUZIMA