Oct 18, 2010

JAKAYA KIKWETE ALIPOITEKA KAWE

-Kaongozana na Juma Othman Juma

- Waiaga CUF na kuchukua kadi za CCM

- Waahidi wengi zaidi wanakuja nyuma yao visiwani humo

Wakongwe wawili wa siasa za vyama vingi visiwani Zanzibar Mheshimiwa Fatma Maghimbi na Juma Othman Juma wamerudisha kadi zao za CUF na kuchukua za CCM leo jimboni Kawe jijini Dar es salaam na kuahidi wenzao wengi watafuata nyayo zao kutoka CUF.

Akielezea sababu zake za kurudi CCM, Juma Othman Juma amesema ameguswa kwa kazi kubwa aliyofanya Mheshimiwa Kikwete Tanzania Bara na Visiwani hususan aliporejesha amani na utulivu visiwani Unguja na Pemba kipindi cha uchaguzi mkuu wa mwaka huu.

Alisema tangu historia ya vyama vingi ianze Tanzania, kila wakati wa uchaguzi wananchi wengi wa visiwa vya Unguja na Pemba hulazimika kukimbia visiwani humo kwa kuhofia hali ya kutokuwa na usalama katika kipindi hicho.

"Lakini sasa napenda kumshukuru sana Mheshimiwa Kikwete kwa kurudisha heshima ya nchi yetu duniani kwani mwaka huu wa kampeni, hakuna hata mmoja aliyehama visiwani humo kukimbia uchaguzi" alimaliza Juma Othman akishangiliwa na umati mkubwa wa wana CCM waliojitokeza kwenye mkutano huo wa kampeni.

Mama Fatma Maghimbi amewahi kuwa waziri kivuli wa Katiba na Sheria ndani ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akiwa kama mbunge wa Chama Cha Wananchi CUF. Naye Juma Othman Juma amewahi kuwa muanzilishi wa Chama Cha Siasa visiwani kabla ya kujiunga na Chama cha Wananchi CUF.

Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama cha Mapinduzi CCM Mh. Jakaya Kikwete akimnadi Mama Kizigha, mgombea ubunge wa CCM jimbo la kawe leo kwenye mkutano wa kampeni uliofanyika kwenye viwanja vya Tanganyika Parkers jijini Dar es salaam.
Uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge, na Madiwani unatarajiwa kufanyika Oktoba 31 mwaka huu nchini kote. (Picha na Muhidin Issa Michuzi)
Bw. Juma Othman Juma akiwa na Mama Fatma Maghimbi baada ya kurejesha kadi za CUF na kupewa za CCM leo.
Msanii wa Bongo Fleva Diamond akitumbuiza leo Kawe kwenye mkutano wa kampeni wa Jakaya Kikwete
Nyomi uwanja wa Tanganyika Packers kwenye mkutano wa kampeni wa Jjakaya Kikwete leo.
sehemu ya nyomi uwanja wa Tanganyika Packers, Kawe, jijini Dar leo

Oct 17, 2010

CHAMA CHA MAWAKILI TANZANIA KUSHIRIKI UANGALIZI UCHAGUZI MKUU OKTOBA 31 2010

Tume ya Taifa ya Uchaguzi imekitunuku Chama Cha Mawakili cha Tanzania Bara kwa kifupi "CHAMA" hadhi ya uangalizi wa uchaguzi mkuu ujao, kwa mara ya kwanzachama kitasambaza wanachama wake katika mikoa kumi ya Tanzania bara yote ili kushiriki katika uangalizi wa vituo vya uchaguzi, pia kufuatilia mchakato mzima wa kampeni za uchaguzi. Chama hiki ni chama cha Wanasheria wa Tanzania Bara kama jukumu lake chama kinatetea mfumo wa jamiiambapo haki na sheriavinaheshimiwa shabaha kuu ya chama kipindi kinachoelekea uchaguzi mkuu ni kwamba uchaguzi ufanyika kwa utaratibu unaokidhi utawala wa sheria na unaoshabihiana na viwango bora na uzoefu wa kimataifa. Kwa usemi wa rais wa chama Bwna Felix George Kibodya ni msimamo wetu kwamba matakwa ya wananchi yawe msingi wa mamlaka ya serikali Jambo hili ndiyo mwanzo na hatima ya usimamizi wetu wa uchaguzi mkuu ujao. Kwa lengo hili chama kimeanda Ilani ya uchaguzi inayofafanua shabaha na mchango wa chama chetu kwa ajili ya uchaguzi mkuu ujao wa Rais, Wabunge na Madiwani utakaofanyika tarehe 31 Oktoba 2010 nchini kote, Shabaha zinazotajwa zitaweka misingi ya mchakato wetu wa ufuatiliaji na uangalizi. Siku ya Uchaguzi kila mwanaglizi atafuatilia shughuli zinjavyoendelea katika vituo vya uchaguzi hususan atafuatilia matukio ya ukiukaji wa taratibu za upigaji kura, usalama na hujuma kwa makasha ya kura, Hitirafu za kuhesabu kura na uandishi wa matokeao. Wanachama wetu watasambazwa Tanzania Bara katika mikoa 10 yaani Tanga, Arusha, Tabora, Mwanza, Tanga, Dodoma, Dar es salaam, Mbeya, Mtwara,Kilimanjaro na Mara, Bw. Felix Kibodya amesema chama hicho pia kitapokea taarifa mbalimbali kutoka kwa wananchi zinazohusiana na uchaguzi kupitia ujumbe utakaotumwa kwa nja ya simu za mkononi katika mitandao yote ya simu wakituma kwa kuandika neno Tufumbue acha nafasi kisha wataandika ujumbe na kuutuma katika namba 15540 gharama ikiwa ni shilingi 150 kwa ujumbe mmoja. Baada ya kumaliza uangalizi wake chama kitatangaza tathmini wiki mbili baadae mara baada ya uchaguzi na matokeo kutangazwa.

YANGA WATUA DAR KWA SHANGWE

Beki mahiri wa timu ya Yanga na timu ya Taifa Taifa Stars Nadir Haroub (Cannavaro) akihojiwa na vyombo mbalimbali vya habari kwenye uwanja wa ndege wa Mwalimu J.K.Nyerere leo mara baada ya timu hiyo kuwasili ikitokea mkoani Mwanza ambako ilicheza mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom kati yake na watani wao wa jadi timu ya Simba zote za jijini Dar es salaam. Katika mchezo huo Mchezaji Jerrison Tegete ndiye aliyefunga goli katika dakika ya 71 kipindi cha pili ambapo kwa mujibu wa mtangazaji wa TBCEnock Bwigane aliyekuwa akitangaza mchezo huo Jerry Tegete akiwa na mpira alimuita golikipa wa Simba Juma K. Juma na kumwambia "Poooooooooooooooooooooo!!!!" wakati kaseja akishanga jina hilo ndipo tegete akafunga goli safi lililoipa ushindi timu hiyo ya Jangwani na matokeo kuwa Yanga 1-Simba 0.
Nadir Haroub Cannavaro akisindikizwa na mashabiki wa timu hiyo mara baada ya kuwasili kwenye uwanja wa ndege wa J.K.Nyerere leo.
Kiungo wa timu ya Yanga Nurdin Bakari naye alikuwemo klatika msafara huo.
Mchezaji Athman Idd (Chuji ) akitoka kwenye uwanja wa ndege wa Mwalimu J.K.Nyerere huku akiongea na simu mara baada ya timu hiyo kuwasili jijini Dar es salaam leo.

Oct 16, 2010

DK BILAL ALIPOUNGURUMA BABATI, MBULU NA KARATU


Mgombea Mwenza wa Urais wa CCM, Dk. Mohamed Gharib Bilal akiwahutubia wananchi wa Kijiji cha Lukumanda Kata ya Ufana Wilaya ya Babati Vijijini, wakati wa mkutano wa kampeni uliofanyika jana.
Mgombea Mwenza wa Urais wa CCM, Dk. Mohamed Gharib Bilal akimnadi mgombea Ubunge wa Jimbo la Mbulu, Philp Marmo wakati wa mkutano wa kampeni uliofanyika Wilaya ya Mbulu jana.
Mgombea Mwenza wa Urais wa CCM, DK. Mohamed Gharib Bilal akipokea kadi ya aliyekuwa Mwenyekiti wa Tawi la NCCR Mageuzi Kijiji cha Guse, Lucas Albin aliyerejesha kadi ya chama chake na kujiunga na CCM wakati wa mkutano wa kampeni uliofanyika katika kijiji cha Lukumanda Wilaya ya Babati Vijijini Mkoa wa Manyara jana.
Mgombea Mwenza wa Urais wa CCM, Dk. Mohamed Gharib Bilal, akitoka katika uwanja wa mkutano wa Kijiji cha Lukumanda baada ya kumaliza mkutano wa kampeni jana
Wananchi wa Kijiji cha Endabash Kata ya Endabash Wilaya ya Karatu, wakimsikiliza mgombea Mwenza wa urais wa CCM, Dk Mohamed Gharib Bilal, wakati alipofanya mkutano wa kwanza wa kampeni katika Wilaya hiyo jana.Picha na Muhidin Sufiani.

WAZIRI MKUU MIZENGO PINDA ATEMBELEA HOSPITALI ZA MUHIMBILI NA OCEAN ROAD.

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akimtazama Winter Isaac (3) ambaye ni mmoja wa watoto waliolazwa kwenye Taasisi ya Saratani ya Ocean Road jijini Dar es salaam wakati alipotembelea Taasisi hiyo Oktoba 15, 2010. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akisalimiana na waganga na wauguzi wa wodi ya watoto kwenye hospitali ya taifa ya Muhimbili pamja na baadhi ya watumishi wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii wakati alipotembelea hospitali hiyo kukagua wodi ya wazazi na watoto Oktoba 15, 2010. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akisalimiana na watumishi wa Taasisi ya Saratani ya Ocean Road jijini Dar es salaam wakati alipoitembelea, Oktoba 15, 2010 . (picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

MAPACHA WA3 WAZINDUA "JASHO LA MTU" KWA MBWEMBWE TRAVELTINE!

Mkurugenzi wa ASET Asha Baraka ambaye alikuwa mgeni rasmi akizindua rasmi albam ya kundi la Mapacha WA3 inayoitwa Jasho la Mtu katika uzinduzi wa nguzu uliofanyika kwenye hoteli ya Traveltine Magomeni jijini Dar es salaam, kundi la Mapacha WA3 linaundwa na Mwanamuziki Josse Marra kutoka FM Academia, Kalala Junior na Harid Chokoraa. Katika picha kulia ni Bw. Ahmed Magoma na kushoto mwisho ni Bw. Bitusi Mkurugenzi wa B2C Transport katikati ni Masoud Wanani Mkurugenzi wa CDS wakishuhudia uzinduzi huo.
Mwimbaji Harid Chokoraa akionyesha uwezo wake katika kucheza wakati wa onesho la uzinduzi wa albam yao inayoitwa Jasho la Mtu kundi hilo la Mapacha wa3 lilikonga nyoyo za mashabiki na kuwakuna vilivyo usiku wa kuamkia leo kwenye hoteli ya Travltine Magomeni jijini Dar es salaam kulia ni Kalala Junio na kushoto ni Josse Marra.
Mzee Yusuf mwimbaji wa muziki wa Taarab na Kiongozi wa bendi ya taarab ya Jahazi Molden Taarab akiimba huku akiwa amezungukwa na vimwana jukwaani wakati aliposhiriki katika uzinduzi wa albam ya Mapacha wa3 inayoitwa Jasho la Mtu.
Queen Suzy kichaa wa Jukwaani mnenguaji wa bendi ya Frican Stars akifunika na shoo yake matata.
Mamaa Monica kushoto naye akajimwaga stejini na rafiki yake huku mzee akiwa jukwaani akifanya mambo makubwa.
Sasa ni zamu ya wanenguaji hawa hebu wacheki mdau kazi kwako.
Vijana Twende Kazi! Mwanamuziki wa FM Academia Josse Mara akiongoza wanenguaji pamoja na wanamuziki wenzake wanaounda kundi la Mapacha wa3 katika kuzindua albam yao ya Jasho la Mtu ulifanyika usiku wa kuamkia leo kwenye hoteli ya Traveltine Magomeni jijini Dar es salaam ukisindikizwa na bendi ya African Stars na Mzee Yusuf kutoka Jahazi Molden Taarab.
Huyu alikuwa mjamzito lakini yeye akaamua kuja kwenye onesho la mapacha watatu na hatimaye akawazaa mapacha watatu palepale Traveltine Magomeni ambao ni Josse Mara wa FM Academia, Harid Chokoraa na Kalala Jujior ambao jana walizindua albam yao ya Jasho la Mtu.
Rapa wa bendi ya Frican Stars anayeitwa Furgason akicheza na mmoja wa wanenguaji wa bendi ya African Stars jana usiki wakati wa onesho la uzinduzi wa albam ya Jasho la Mtu.
Mamaa Lwiza Mbutu Kiongozi wa bendi ya African Stars kulia akiongoza wanamuziki wenzaka katika kucheza shoo ya nguvu kwenye uzinduzi wa albam ya Jasho la Mtu ya Mapacha wa3.
Mwanamuziki mkongwe Mafumu Bilal Bombenga akijilipua kwa shoo kali jukwaani wakati wa onesho la uzinduzi wa Albam ya Mapacha wa3 inayoitwa "Jasho la Mtu" kwenye ukumbi wa Traveltine Magomeni.

Oct 15, 2010

uzinduzi wa filamu za ulaya wafana sana leo jijini dar


Balozi wa Umoja wa Ulaya nchini Tanzania,Tim Clarke akizungumza katika uzinduzi wa filamu za Ulaya uliofanyika New World Cinema,Mwenge jijini Dar usiku huu.
Mmoja wa watengeneza filamu kutoka nchini Ujerumani,Matthias Luthardt akitoa maelezo ya filamu yake aliyoitengeneza,kwenye uzinduzi wa filamu za Ulaya uliofanyika jioni hii katika ukumbi wa New World Cinema,Mwenge jijini Dar.
wadau pia walikuwepo.
Balozi wa Ufaransa nchini,Jaque Champagne de Labriolle (kushoto) akiwa katika mazungumzo na mmoja wa wageni waliofika katika uzinduzi huo.
Balozi wa Umoja wa Ulaya nchini,Tim Clarke akibadilishana mawazo na baadhi ya wageni waalikwa waliofika katika uzinduzi huo wa filamu uliofanyika jioni hii katika ukumbi wa New World Cinema,Mwenge jijini Dar.
Tayana Tibenda (shoto) kutoka 1 plus,akifanya mahojiano na mmoja wa watengeneza filamu kutoka nchini Ujerumani,Matthias Luthardt katika uzinduzi wa filamu za Ulaya uliofanyika jioni hii katika ukumbi wa New World Cinema,Mwenge jijini Dar.
Mkuu wa Kitengo cha Habari ofisi ya Umoja wa Ulaya Tom Vens (kushoto) akiwa katika mazungumzo na mmoja wa waakilishi wa balozi za umoja wa Ulaya.
wageni waalikwa wakibadilishana mawazo.
kucheza na nyoka
vijawa wa Wanne Star wakicheza na Nyoka katika uzinduzi wa Filamu za Ulaya uliofanyika jioni hii katika ukumbi wa New World Cinema,Mwenge jijini Dar.
maongezi ya hapa na pale yalitawala kwa mabalozi wa jumuiya ya Ulaya waliofika katika uzinduzi huo wa Filamu za Ulaya.
Balozi wa Umoja wa Ulaya,Tim Clarke (katikati) akiwa katika mazungumzo na Mkuu wa Kitengo cha Habari ofisi ya Umoja wa Ulaya Tom Vens (kushoto) na Mkurugenzi wa 1Plus,Fina Mango
Balozi wa Ufaransa nchini,Jaque Champagne de Labriolle akicheza na Nyoka.
Balozi wa Umoja wa Ulaya,Tim Crarke (pili kulia) akimwangalia Ofisa Habari wa Umoja wa Ulaya nchini,Henry Lyimo (kulia).wengine ni mchezea Nyoka hiyo na mmoja wa wageni waalikwa.
wageni mbali mbali walikuwepo.
Balozi wa Umoja wa Ulaya nchini,Tim Clarke akizungumza katika uzinduzi huo.
furaha ilitawala katika uzinduzi huo.

wageni waalikwa wakibadilishana mawazo.

Rais Jakaya Kikwete ahitimisha mbio za mwenge Kigoma.

kiongozi wa mbio za mwenge kitaifa mwaka huu 2010 Dr.Nassoro Ally Matuzya akimkabidhi mwenge wa Uhuru Rais Dr.Jakaya Mrisho Kikwete wakati wa sherehe za kilele cha mbio hizo kilichofanyika katika uwanja wa michezo wa Lake Tanganyika mjini Kigoma leo mchana.
Kiongozi wa mbio za mwenge kitaifa mwaka huu 2010 Dr.Nassoro Ally Matuzya akikabidhi risala za utii kwa Rais Dr.Jakaya Mrisho Kikwete wakati wa cherehe za kilele cha mbio za mwenge zilizofanyika katika uwanja wa michezo wa Lake Tanganyika mjini Kigoma leo mchana.
Rais Dr.Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na timu ya viongozi wa mbio za
mwenge wa Uhuru mwaka huu wakati wa sherehe za kilele cha mbio hizo
zilizofanyika katika uwanja wa michezo wa Lake Tanganyika mjini Kigoma leo(Picha na Freddy Maro)

THE DON HIMSELF

Karibuni sana kwenye blog hii ya kijamii iliyosheheni makila kitu kuanzia siasa uchumi afya na burudani kwa ujumla wake.uingiapo kwenye blog hii ni mengi ambayo utapata nafasi ya kukutana nayo,kumbuka mawazo yako ndo hasa yanayojenga na kunifanya niwe na ufanisi zaidi.kariiiiiiibuuuuuuuuuuuu saaaaaaaaaaaaaaanaaaaaaaaaa.(THE DJ HIMSELF-JIWE)

Followers

BLOG ZA MARAFIKI

Search This Blog

ZILIZOPITA

DUNIA MUZIMA