Aug 21, 2010

'ARI ZAIDI,KASI ZAIDI NA NGUVU ZAIDI-PAMOJA TUTASHINDA'KAULI MBIU ILIYOZINDULIWA RASMI HAPO JANA

Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM),Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwahutubia wanachama wa CCM na wapenzi wa Chama hicho waliofika leo katika Viwanja vya Jangwani Jijini Dar wakati wa uzinduzi wa Kampeni kwa ajili ya uchaguzi mkuu 2010.
Mgombea Mwenza wa Rais Jakaya Kikwete,Dr. Mohamed Gharib Bilal akiwahutubia wanaCCM wa Dar es Salaam waliofika katika Viwanja vya Jangwani leo.
Makamu Mwenyekiti CCM (Visiwani) na Rais wa Zanzibar anaemaliza muda wake,Rais Aman Abeid Karume nae aliongea machache na wanaCCM wa Dar es Salaam na mikoa ya jirani waliojitokeza leo katika viwanja vya Jangwani,jijini Dar wakati Chama Cha Mapinduzi kilipozindua rasmi kampeni za uchaguzi mkuu 2010.
Makamu Mwenyekiti CCM (Bara),Mh. Pius Msekwa akiteja jambo na Katibu Mkuu wa CCM,Mh. Yussuf Makamba wakati wa mkutano wa ufunnguzi wa kampeni za uchaguzi mkuu zililofanyika leo katika viwanja vya Jangwani jijini Dar.
Rais Mstaafu,Alhaj Ally Hassan Mwinyi akiteja jambo na Rais wa Zanzibar,Mh. Aman Karume na huku wakisikilizwa na wake zao na wadau wengine.Kushoto ni Makamu Mwenyekiti CCM (Bara),Mh. Pius Msekwa.
Rais Kikwete akiwapungia wanaCCM wakati akiondoka.
Jukwaa Kuu.
Orijino Komedi wakifanya vitu vyao.
T.O.T wakifan ya vitu vyao huku wakiongozwa na Mh. John Komba.
Wazee wa kazi wakila mzigo.
Marlaw akiwabembeleza wanaCCM leo.
Marlaw na timu yake.Vijana wa Kiumeni wakikamua.
umati mkubwa wa wanaCCM waliofika katika viwanja vya Jangwani leo.

LIBENEKE JIPYA LA JK HILI HAPA!

Libeneke rasmi la JK na Dk. M. Gharib Bilal sasa lipo hewani:

www.kikwete2010.co.tz

Libeneke hili maalumu la Mgombea Uraisi na Mgombea Mwenza kwa tiketi ya CCM mwaka 2010 limesheheni habari mbalimbali kama:

· Wasifu wa Wagombea – Mhe. Jakaya M. Kikwete na Dr. Mohammed Gharib Bilal.
· Mafanikio katika sekta mbalimbali.
· Sera na Malengo 2010 – 2015.
· Ratiba za kampeni.
· Hotuba maalumu.
· Matoleo ya Habari.
· Video na picha.
· Mitandao ya Facebook,Twitter na Youtube.
Kupitia tovuti hii na mitandao yake utaweza kupata taarifa mbalimbali na kutoa maoni yako.

“ PAMOJA TUZIDI KUSONGA MBELE”

SIMBA YAIBANJUA AFRICA LYON 2-0, YANGA YAIPA ADABU POLISI DODOMA 1-0!!

Timu ya Simba leo imeibanjua timu ya Africa Lyon magoli mawili kwa bila kwenye uwanja wa Uhuru katika uzinduzi wa ligi kuu ya Vodacom iliyoanza leo jijini Dar es salaam, timu hiyo ilifanya umafia huo huku mashabiki mwake wakiishangilia kwa nguvu kwenmye uwanja huo. Alikuwa ni mchezaji mpya wa timu hiyo aliyetokea kwa watani wao wa jadi timu ya Young African ya mtaa wa Jangwani jijini Dar es salaam Amir Maftaha wakati alipoandika goli la kwanza katika dakika ya kumi na nne ya mchezo huo katika kipindi cha kwanza cha mchezo huo. Mpaka mapumziko Simba ndiyo ilikuwa ikiongoza goli 1-0 katika mchezo huo uliofungua pazia la ligi kuu ya Vodacom huku mahasimu wao wakuu timu ya Yanga ikiifunga timu ya Polisi Dodoma goli 1-0 kwenye uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma. Katika kipindi cha pili Amir Maftaha tena alifunga goli la pili katika dakika ya sitini na nne ya mchezo na kuifanya timu ya Simba kuibuka na magoli 2-0 hivyo kuifanya timu ya Africa Lyon kuondoka uwanjani ikiambulia patupu, ushindi huo wa timu ya Simba unaipa pointi tatu za mwanzo katika ligi hiyo.

WAREMBO VODACOM MISS TANZANIA WATOA MSAADA WA VYANDARUA MOSHI!!

Baadhi ya warembo wanaoshiriki mashindano ya Vodacom Miss Tanzania 2010 wakimpatia chandarua ya kujizuia na mbu Miriam Joseph ambaye amelazwa Marangu ikiwa ni kutekeleza kwa vitendo kauli mbiu ya Malaria Haikubaliki. kampeni iliyoanzishwa na rais Jakaya Mrisho Kikwete
Baadhi ya warembo wanaoshiriki shindano la Vodacom Miss Tanzania 2010 wakimpatia chandarua cha kujizuia na mbu Herieth masawe ambaye amelazwa hospitani hapo ikiwa ni kutekeleza kauli mbiu ya Malaria Haikubaliki.

Katibu wa hospital ya Marangu, Godrick Njau akikapokea vyandarua toka kwa Mkurugenzi wa Vodacom kanda ya kaskazini Nguvu Kamando mara baada ya kutembelea hospitalini hapo wakiwa wameambatana na warembo wanaoshiriki mashindano ya Vodacom Miss Tanzania.

Mchungaji Mtikila Aenguliwa Katika Uchaguzi Mkuu 2010

Mwenyekiti wa Chama cha Democratic (DP),Mchungaji Christopher Mtikila.

Na Mwandishi Wetu

WAKATI kampeni za uchaguzi mkuu zikifunguliwa rasmi leo hii, Tume ya Taifa ya Uchaguzi nchini (NEC) imemuengua aliyekuwa mgombea urais kupitia Chama cha Democratic (DP), Mchungaji Christopher Mtikila, kutokana na kutotimiza masharti yaliyowekwa kwa wagombea urais.

Mtikila aliyefika jana katika ofisi za NEC akiwa na mgombea mwenza wake Kibwana Said Kibwana, alienguliwa mara baada ya tume kubahini kwamba hakuwa ametimiza idadi ya wadhamini waliojitokeza kumdhamini.

Jaji Lewis Makame alisema kwamba NEC imefikia uamuzi wa kukitoa chama cha DP, baada ya Mtikila kupata wadhamini

mikoa 10, ingawa kati ya mikoa hiyo katika Mkoa wa Pwani wamepatikana wadhamini 220 wakiwamo 25 wenye kasoro.

Pia Jaji Makame alisema kwamba Mtikila pia alipata wadhamini 220 katika mkoa wa Kilimanjaro kati ya hao 27 wakiwa na kasoro.

Alisema kwamba katika Mkoa wa Dodoma kati ya wadhamini 220, wadhamini 29 walionekana kuwa na kasoro jambo liloifanya tume kuona kuwa Mtikial ahakukidhi vigezo vya kuwania urais.

Si Mtikila pekee ambaye alienguliwa, mgombea mwingine ambaye naye alikutwa na yaliyomkuta Mtikila ni Paul Kyara wa chama cha Sauti ya Umma (SAU) aliyeenguliwa baada ya kutokidhi idadi ya mikoa kumi ambayo mgombea urais anatakiwa kupata udhamini.

Baada ya kuenguliwa, Mtikila alikiri kuwa hasikitiki wala kuhudhunika kutokana na kutolewa huko, kwamadai kwamba hakuwa ameweka uhai wake katika kinyang’anyiro cha kugombea urais.

Alisema kwamba atapitia kwa makini nakala za fomu zake pamoja na viambatanisho vya udhamini, hili aweze kujua

kama atachukua hatua gani.

Vyama vingine vya Demokrasia Makini, Jahazi Asilia na NRA, vilijitoa vyenyewe baada ya kushindwa kufika leo hii katika ofisi za NEC kwaajili ya kurudisha fomu.

Aug 20, 2010

BAADHI YA WAREMBO WANAO WANIA TAJI LA MISS TANZANIA MWAKA HUU

Wilhemina Etami (Kanda ya Kati)
Alice Lushiku (Kanda ya Kinondoni)
Bahati Chando (Ilala)
Flora Martin (Elimu ya Juu)
Fatma Ibrahim (Kanda ya Ziwa)
Salma Mwakalukwa(Ilala)
Buduri Ibrahim(Kanda ya Ziwa)
Amisuu Malick (Kinondoni)
Britnery Urassa (Temeke) Irene Hezron (Kinondoni)
Genevieve Emmanuel (Teneke) Vodacom Miss Tanzania anayemaliza muda Miriam Gerald akiwa katika kubarizi hkambini hapo.
Vodacom Miss Tanzania katika picha ya pamoja. Moja ya sehemu ya vivutio vilivyopo katika hoteli ya Giraffe View Dar es Salam.
Baadhi ya warembo.
Mlezi wa Miss Tanzania ambaye pia ni Mkurugenzi wa Kituo Cha Uwekezaji nchini (TIC) Emmanuel Ole Naiko,alipowatembelea jana na kambini kwao hoteli ya Giraffe View, Dar es Salaam.

FOMU ZA KUGOMBE URAIS ZARUDISHWA RASMI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akiwashukuru jana jijini Dar es salaam, wanachama wa CCM waliojitokeza kumpongeza kwa hatua ya kurejesha fomu katika Ofisi za Tume ya Uchaguzi na pia kukubaliwa kama Mgombea halali wa CCM katika uchaguzi ujao. Picha na Tiganya Vincent-Dar es salaam
Mgombea Mwenza wa Rais Jakaya Mrisho Kikwete Dkt Mohamed Gharib Bilal akiwashukuru wanachama wa CCM na wapenzi waliofika jana katika viwanja vya Ofisi Ndogo ya CCM jijini Dar es salaam kwa ajili ya kuwapongeza kwa kukubaliwa bila na Tume ya Uchaguzi ya Tanzania kuwa wagombea kwa tiketi ya CCM katika uchaguzi ujao.
Katibu Mkuu wa CCM Yusuph Makamba (kushoto) akiteta na Mwenyekiti wa CCM Dkt Jakaya Kikwete jana nje ya Ofisi Ndogo za CCM jijini Dar es salaam mara baada kurejea kutoka Tume ya Uchaguzi alipokuwa amerudisha Fomu ya kuwania Urais wa Tanzania katika uchaguzi Mkuu ujao.
Msaani Ummy Wenceslaus (Dokii) akitumbuiza jana jijini Dar es salaam baadhi ya wanachama waliofika katika Ofisi Ndogo za CCM kuwalaki wagombea wao mara baada ya Rais Kikwete na Mgombea Mweza Dkt Bilal kurejea kutoka Tume ya Uchaguzi ambapo alikuwa amerudisha fomu kuwania Urais wa Tanzania katika uchaguzi Mkuu ujao.
Wanachama wa Chama Cha Mapinduzi wakiwasikiliza wagombea wao wakati walipokuwa wakihutubia maelfu wa wanachama wao katika ofisi ndogo ya chama CCM Lumumba.

Wagombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha CHADEMA Dr. Wilbroad Slaa kushoto na Mgombea Mwenza Khamis Hamad Khamis mara baada ya kurejesha fomu zao katika ofisi za tume hiyo leo jijini Dar es salaam. Tume ya Taifa ya Uchaguzi ilipanga kuwa Wagombea wote wanatakiwa kuwa wamerudisha fomu leo Agost 19 na kesho Agosti 20 ndiyo kampeni zinaanza rasmi kwa vyama vyote ambapo uchaguzi mkuu unatarajiwa kufanyika Oktoba 31 mwaka huu.
Wanachama wa Chama CHADEMA wakishangilia nje ya ofisi za Tume ya Uchaguzi ya Taifa wakati walipomsindikiza wagombea wa urais kupitia chama hicho wakati waliporejesha fomu katika Tume hiyo leo jijini Dar es salaam.
Mwenyekiti wa NCCR Mageuzi James Mbatia akiwa katika msafara nawanachama wa chama hicho katika maeneo ya Moroco Konondoni jijini Dar es salaam mara baada ya kurejesha fomu ya kugombea ubunge jimbo la Kawe leo.
Wanachama wa chama cha NCCR Mageuzi wakiwa katika msafara katika maeneo ya Moroco Kinondoni mara baada ya mgombea wao wa ubunge jimbo la kawe kurejesha fomu za kugombea ubunge kawe leo.

Wagombea Urais kupitia Chama Cha Wananchi CUF Prof. Ibrahim Lipumba kushoto na Mgombea mwenza Duni Haji Duni wakipunga mikono yao mara baada ya kurejesha fomu zao katika Ofisi za Tume ya Taifa ya Uchaguzi Jijini Dar es salaam leo ambapo wagombea kutoka vyama vyote vyote wanatarajia kuanza kampeni kesho nchini kote.
Viongozi wa Chama Wanachi CUF wakinyanyua juu mikono yao kuwapungia wanachama wa Chama hicho waliowasindikiza wagombea wao wakati waliporejesha fomu leo jijini Dar es salaam.
Wanachama wa chama cha CUF wakishangilia katika ofisi za Tume ya Uchaguzi leo wakati wagombea urais wa chama chao waliporejesha fomu Tume ya Uchaguzi leo.

Zitto Kabwe asks for your contributions

Dear Friends,

I would like to express my heartfelt gratitude for all your support.
Today we mark the start of a new journey.

This morning I submitted my nominations forms for re-election for the Kigoma North parliamentary seat ready to serve again the people of Kigoma North and my country TANZANIA.In order to make it happen am humbly asking for your support; if you would like to see Zitto back in Parliament and serving our nation I ask for your support.
I am ready to serve you once again.

DONATE:
Help Zitto keep fighting for our future and our country. Join the campaign by making a donation today.
Your contribution and support will help us in our campaign.

To donate, please:Make a Deposit to Our Campaign Account:

NAME: ZITTO KABWE ZUBERI
BANK: CRDB BANK
ACCOUNT NUMBER: 01J2082022500

Contact Details:
Contact Person: Mhonga Ruhwanya
Mobile Number: +255 0758 000 111
E-mail Address: zitto2010@gmail.com
FACEBOOK: http://www.facebook.com/zittokabwe
Blog: http://www.zittokabwe.wordpress.com/
Follow me on my Twitter Account: http://www.twitter.com/zittokabwe
On FLICKER(PICTURES): http://www.flickr.com/photos/zittokabwe

ZITTO KABWE CAMPAIGN

Aug 18, 2010

UJUMBE WA SAJNA KWA MAFANZ WAKE


Hello, asante sana kwa mchango wako wa aina yoyote uliotupatia katika kuifanikisha album ya Sajna mpaka kukamilika na sasa ikiwa tayari kuingia sokoni Alhamisi hii tarehe 19 Agosti 2010, ASANTE SANA..


ALBUM TITLE: IVETA
ARTIST: SAJNA
RELEASE DATE: 19TH AUGUST 2010
EXECUTIVE PRODUCER: KID BWOY
DISTRIBUTOR: GMC & UMOJA AUDIO VISUAL
ALBUM DETAILS:
Album ya IVETA ya msanii SAJNA ina jumla ya nyimbo 10, ambayo ilianza kutengenezwa Mwezi January 2010 na kukamilika mwezi July 2010. Wasanii waliopata nafasi ya kushirikishwa katika album hii ni Belle 9, Linah wa THT, Josefly kutoka Musoma Mara pamoja na Pipi. Lengo la kutoshirikisha wasanii wengi sana ni kutaka kuonesha uwezo wake na kuthibitisha kwamba msanii mchanga si lazima atoke kwa kupitia mgongo wa wasanii wakubwa.
Studio na producers waliohusika kutengeneza nyimbo katika album hii ni pamoja na TETEMESHA RECORDZ chini ya KID BWOY, AB RECORDS chini ya AMBA, A2P chini ya SAM TIMBER, IMMORTAL MUSIC chini ya TRIS na M LAB chini ya DUKE.
Single ya pili kutoka bado haijaamuliwa ila ni kati ya SITAKI KUUMIZWA na MBALAMWEZI, moja kati ya hizo itakayopendekezwa na wadau wengi ndio itakayofuata baada ya IVETA.

Song list as appeared on Cd cover
1. IVETA
2. Sitaki Kuumizwa ft. Linah
3. Binadamu
4. Mbalamwezi
5. Udehule
6. Mganga ft. Josefly
7. Nadhifa
8. Roho Mbaya ft. Belle 9 & Pipi
9. Subira
10.Ishara ya Msalaba
ALBUM ITATOKA KATIKA CD NA AUDIO CASSETTE

Regardz
Executive Producer
Kid bwoy
Tetemesha Recordz

THE DON HIMSELF

Karibuni sana kwenye blog hii ya kijamii iliyosheheni makila kitu kuanzia siasa uchumi afya na burudani kwa ujumla wake.uingiapo kwenye blog hii ni mengi ambayo utapata nafasi ya kukutana nayo,kumbuka mawazo yako ndo hasa yanayojenga na kunifanya niwe na ufanisi zaidi.kariiiiiiibuuuuuuuuuuuu saaaaaaaaaaaaaaanaaaaaaaaaa.(THE DJ HIMSELF-JIWE)

Followers

BLOG ZA MARAFIKI

Search This Blog

ZILIZOPITA

DUNIA MUZIMA