Timu ya Simba leo imeibanjua timu ya Africa Lyon magoli mawili kwa bila kwenye uwanja wa Uhuru katika uzinduzi wa ligi kuu ya Vodacom iliyoanza leo jijini Dar es salaam, timu hiyo ilifanya umafia huo huku mashabiki mwake wakiishangilia kwa nguvu kwenmye uwanja huo. Alikuwa ni mchezaji mpya wa timu hiyo aliyetokea kwa watani wao wa jadi timu ya Young African ya mtaa wa Jangwani jijini Dar es salaam Amir Maftaha wakati alipoandika goli la kwanza katika dakika ya kumi na nne ya mchezo huo katika kipindi cha kwanza cha mchezo huo. Mpaka mapumziko Simba ndiyo ilikuwa ikiongoza goli 1-0 katika mchezo huo uliofungua pazia la ligi kuu ya Vodacom huku mahasimu wao wakuu timu ya Yanga ikiifunga timu ya Polisi Dodoma goli 1-0 kwenye uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma. Katika kipindi cha pili Amir Maftaha tena alifunga goli la pili katika dakika ya sitini na nne ya mchezo na kuifanya timu ya Simba kuibuka na magoli 2-0 hivyo kuifanya timu ya Africa Lyon kuondoka uwanjani ikiambulia patupu, ushindi huo wa timu ya Simba unaipa pointi tatu za mwanzo katika ligi hiyo.
Ni globu ya kijamii inayojihusisha na mambo yote ya kijamii,natumaini jamii yangu ya kitanzania itafaidika sana pindi ichukuapo fursa ya kuperuzi kwenye globu hii,dhamira yangu ni kufikisha ujumbe pamoja na kuiburudisha jamii yangu na furaha yangu ni kuona natimiza dhamira yangu kwako.natumaini kuwa wewe utaniunga mkono kwa kile ambacho nataka kukifanya kwa ajili ya jamii yangu ya kitanzania.NASHUKURU KWA KUNIELEWA.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
ME MYSELF & I
THE DON HIMSELF
Karibuni sana kwenye blog hii ya kijamii iliyosheheni makila kitu kuanzia siasa uchumi afya na burudani kwa ujumla wake.uingiapo kwenye blog hii ni mengi ambayo utapata nafasi ya kukutana nayo,kumbuka mawazo yako ndo hasa yanayojenga na kunifanya niwe na ufanisi zaidi.kariiiiiiibuuuuuuuuuuuu saaaaaaaaaaaaaaanaaaaaaaaaa.(THE DJ HIMSELF-JIWE)
No comments:
Post a Comment