Ni globu ya kijamii inayojihusisha na mambo yote ya kijamii,natumaini jamii yangu ya kitanzania itafaidika sana pindi ichukuapo fursa ya kuperuzi kwenye globu hii,dhamira yangu ni kufikisha ujumbe pamoja na kuiburudisha jamii yangu na furaha yangu ni kuona natimiza dhamira yangu kwako.natumaini kuwa wewe utaniunga mkono kwa kile ambacho nataka kukifanya kwa ajili ya jamii yangu ya kitanzania.NASHUKURU KWA KUNIELEWA.
Aug 12, 2010
WAZIRI WA KAZI PROF.KAPUYA AZINDUA MWAKA WA VIJANA!!
Mikoko ya Vodacom kukuza uchumi kwa washindi!!
Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii yakabidhi vifaa Tiba Dodoma!!
BLOOD DIAMONDS - A TRAGEDY OF HISTORIC PROPORTION!!
MWENYEKITI WA (YUNA) HAPA NCHINI AWAPA CHANGAMOTO VIJANA!!
Wajumbe mbalimbali wakimsikiliza mwenyekiti wa Asasi ya Vijana ya Umoja wa Mataifa hapa nchini YUNA Bw. Benny Kikove wakati alipokuwa akiongea na wajumbe wa konamano hilo asubuhi hii.
TAIFA STARS NA HARAMBEE STARS NGUVU SAWA!!
Precision Air yaleta ndege mpya!!
WAGOMBEA UBUNGE WA CUF (W) ILALA WAJITAMBULISHA!!
MAOFISA HABARI WAKUTANA LEO JIJINI DAR.
Aug 11, 2010
BASATA KUYAPA MENO RASMI MASHIRIKISHO YA SANAA
Mchakato huo utakaodumu kwa siku nne hadi Ijumaa umeanza kwa Shirikisho la Wasanii wa Sanaa za Ufundi kuchagua viongozi wao wa muda ambao watasimamia kikamilifu utayarishaji wa kanuni za kuliongoza shirikisho hilo na baadaye kuitisha uchaguzi utakaowaweka viongozi wa kikatiba.
Katika uchaguzi huo uliosimamiwa na Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Utamaduni Kutoka Wizara ya Habari Utamaduni na Michezo Bi.Angela Ngowi, Bw.Adrian Nyangamale ambaye ni Rais wa Chama cha Wasanii wachoraji alichaguliwa kuwa Rais wa Muda wa Shirikisho hilo baada ya kupata kura 12 kati ya 21 zilizopigwa na kuwabwaga wenzake ambao ni Gwalugano Lyimo na Focus Senya.
Kwa upande wa Makamu wa Rais,Mwanamitindo maarufu nchini,Khadija Mwanamboka aliibuka kidedea baada ya kupata ushindi wa kishindo wa kura 18 kati ya 21.Nafasi ya Katibu ilikwenda kwa Godfrey Ndimbo huku mweka hazina akichaguliwa Rashidi Mbogo.
Wajumbe walioteuliwa kuliongoza jahazi la shirikisho hili ni pamoja na Rashidi Munyana,Basil Nyambele na Gwalugano Ayoub.
Akizungumza baada ya Uchaguzi,Msimamizi wa uchaguzi Bi.Ngowi alisema kwamba,huo ni mwanzo wa wasanii kujisimamia na kujipanga kwa ajili ya kutetea maslahi yao na kuhakikisha wanalinda haki ya kazi zao na kutafuta masoko kwa ajili ya kazi zao.
Aliongeza kwamba,viongozi waliochaguliwa lazima wahakikishe wanasimamia kikamilifu katiba na kutafuta fursa na mbinu za kupenya kwenye soko la pamoja la Afrika Mashariki.
Kwa upande wake Katibu Mtendaji wa BASATA,Ghonche Materego alisema kwamba, lengo la Baraza ni kuona wasanii wanakuwa na umoja wa kitaifa na Kutoka kwenye makucha ya utegemezi na kupambana mmojammoja.Aliongeza kwamba, wakati umefika kwa wasanii kuonesha usasa na kuachana na ufanyaji kazi za sanaa wakiwa katika mazingira yasiyo rasmi na ya kulalamika tu bila kuwa watendaji na watekelezaji.
Mlezi wa Wasanii wa Sanaa za Ufundi,Rashid Masimbi ambaye pia ni Mjumbe wa Bodi ya BASATA alisema kwamba, kazi iiyopo mbele ni kwa viongozi waliochaguliwa kuja na mipango ya muda mfupi na mrefu katika kulikuza shirikisho, kutafuta wanachama wapya na kuandaa kanuni za kuliendesha shirikisho hilo.
BASATA liko kwenye mkakati kabambe wa kujenga umoja wa wasanii kupitia mashirikisho ambapo sasa wasanii nchi nzima watakuwa na fursa ya kuwa na sauti moja pia kupanga misimamo yao itakayoheshimika kitaifa na kimataifa.
Mashirikisho ambayo yameundwa na sasa uongozi wake unatafutwa ni yale ya Sanaa za Ufundi,Sanaa za Muziki,Sanaa Jongevu (Filamu) na Sanaa za Maonesho.
Baraza linawataka wasanii wote, kuhakikisha wamejisajili na kujiunga na mashirikisho hayo kwa ajili ya kuanza mkakati wa kutetea maslahi yao.
RATIBA KAMILI YA CHAGUZI KATIKA MASHIRIKISHO
1. Jumatano,Agosti 11, 2010-Shirikisho la Muziki Tanzania,Kwenye Ukumbi wa BASATA kuanzia saa 4.00.Asubuhi.
2. Alhamisi,Agosti 12,2010-Shirikisho la Sanaa za Maonesho,Ukumbi wa BASATA kuanzia Saa 4.00 Kamili.
3. Ijumaa Agosti 13, 2010-Ahirikisho la Sanaa za Jongevu (Filamu) Tanzania, Ukumbi wa BASATA kuanzia saa 4.00.
Matokeo yatatangazwa kwnye vyombo vya habari,
WADAU WOTE MNAKARIBISHWA,
Habari na Alistide Kwizela,Afisa Habari wa BASATA.
Ukweli Kuhusu Haruna Moshi ‘ Boban’ : Alikosa Namba Gavle IF
TWIGA STARS RECEIVED BY WASHINGTON GOVERNOR CHRISTINE GREGOIRE!
Aug 10, 2010
KENYA WAJIFUA NA MAZOEZI KATIKA UWANJA WA KARUME KUJIANDAA NA MCHEZO DHIDI YA STARS KESHO KATIKA UWANJA WA UHURU JIJINI DSM
Rais Kikwete azindua Ujenzi wa Miundombinu ya Mfumo wa Mabasi yaendayo Haraka Dar es Salaam!!
BIG BROTHER ALL STARS MUNYA OR TATIANA – AFRICA MUST DECIDE!
O’NEILL AIMUA KUSEPA ASTON VILLA……!!!!
Martin O’Neill.
Kocha huyo amechukua hatua hiyo baada ya kuwa na sintoelewana kati yake na mmiliki wa klabu hiyo ajulikanae kwa jina la Randy Lerner na kikubwa ni kutokana na kuzwa kwa kiungo James Milner kwa Man city na kama angeweza kutumia kitita cha mauzo hayo kununua wachezaji wengine.
Lakini yaonekana kocha huyo alivumilia sana uzwaji wa wachezaji wake tegemeo kama Gareth Barry nae kwenda Man city.
Timu hiyo imemteuwa Kevin Macdonald kuwa mrithi wa mda mfupi nae akikabiliwa na kibarua kigumu cha mechi kati yao na West ham utd siku ya jumamosi
TUIGE MFANO KAMA WA AKINA USHER RAYMOND…!!!
Usher,Bill Clinton & Ciara on the stage.
Usher brought out some of his celebrity friends, including Justin Bieber, former president Bill Clinton, Ciara and Young Money rapper Lil Twist to help him take part in his New Look Foundation’s first annual World Leadership Awards, held Friday night (Aug 6) in Atlanta, GA at the Cobb Energy Performing Arts Center.
Ciara later joined Usher on-stage to perform a duet to John Lennon’s “Imagine,” while Usher’s young protege Justin Bieber hit the stage solo for his own performance set. Usher himself even treated the crowd to a few performances, including his #1 hit single “OMG.”
Ciara na Justin Bieber
Bill Clinton na Usher Raymond wakiwa Back stage.
Usher and His New Look Foundation Host First Annual World Leadership Awards in Atlanta.
Blog team: Wote tunakubali ya kuwa wanamuziki na wacheza filamu wanachukuliwa kama kioo cha jamii hapa nchini kupitia kazi zao wanazo zifanya. kutokana na hadhi hiyo wanayo nafasi kubwa ya kufanya mambo ya muhimu yanayo lenga kuisaidia jamii inayo wazunguka si tu kwa kuingia katika siasa bali kuanzisha taasisi zinazo gusa nyanja mbalimbali za jamii na hata katika kuleta ufanisi wa kazi wa sekta mbalimbali za kiserikali. Na hii si kwa wao tu hata watangazaji wa redio na televisheni ambao wamekuwa wakionekana na kusikika nchi nzima.
NDIVYO ILIVYOKUWA KWENYE USAILI WA BBS
Washiriki wa BONGO STAR SEARCH 2010 wakiandikisha majina yao kwa ajili ya Usaili wa Kushiriki kinyang’anyiro hicho.
Baunsa akiwapanga Vijana waliojitokeza kwa ajili ya Kushiriki kwenye Audition za BSS 2010 zilizoanza leo asubuhi katika Ufukwe wa COCO BEACH.
Askari wa Kampuni ya ULTIMATE Security akiwatuliza washiriki waliokuwa wakileta fujo kuogmbania namba kwa ajili ya kuingia kwenye usaili.
Kikundi cha Vijana wanaoishi Keko walikutwa na Camera ya THE DJwakifanya mazoezi ya kuimba nje ya Ukumbi wa Coco beach kabla ya kufanyiwa usaili.
Washiriki wakiwa kwenye foleni kwa ajili ya kuandikisha namba zao.
Pichani ni mshiriki Angela Batazari (22) mkazi wa mtoni Kijichi akitoa maoni yake mbele ya Camera ya THE DJ juu ya mchakato mzima wa BSS 2010 alisema kwamba kutakuwa na ushindani mkubwa tofauti na mwaka jana kwa sababu watu wamejitambua kuwa wana vipaji vya kuimba ili waweze kupata ajiri kutokana na Tasnia ya Muziki hasa wa Bongo FlavaJAJI MKUU AWAPANDISHA VYEO MAHAKIMU SINGIDA,DODOMA..!!!
Na Hillary Shoo,
Singida.
JAJI mkuu wa mahakama ya Tanzania,Augustino Ramadhan, amewaagiza wafanyakazi wa mahakama nchini,kuhakikisha wanajiendeleza kielimu ili kujijengea mazingira mazuri ya kuweza kumudu vema majukumu yao ya kila siku.
Jaji Ramadhan ametoa wito huo jana (9/8/2010) muda mfupi baada ya kuwaapisha mahakimu watatu kuwa mahakimu wa mahakama ya hakimu mkazi.Hafla hiyo ilifanyika kwenye ofisi ya hakimu wa mahakama ya hakimu mkazi mjini hapa.
Alisema katika dunia ya sasa mambo mengi yanabadilika kwa kasi yakiwemo ya kisheria,kanuni na taratibu na hivyo,ili hakimu au mfanyakazi wa mahakama aweze kumudu kutekeleza wajibu wake vizuri, hana budi kujiendeleza kielimu.
Aidha, aliwataka kujiwekea mikakati ya kujiendeleza wenyewe au kutafuta misaada mbalimbali kwa madai kwamba wakisubiri mafungu ya fedha za serikali,wanaweza kuchelewa kujiendeleza kielimu. ”Binafsi nawapongeza sana ninyi kwa juhudi zenu binafsi za kujiendeleza kielimu,ninyi ni mfano mzuri wa kuigwa na wafanyakazi wengine wa mahakama nchini na hata sekta zingine”alisema.
Katika hatua nyingine, Jaji Ramadhan aliwaagiza mahakimu hao kwenda kutekeleza wajibu wao kwa kuzingatia sheria,kanuni na taratibu zilizowekwa na si vinginevyo. ”Nendeni mkafanye kazi kwa uadilifu mkubwa,msiige mambo yasiyofaa.Sheria,kanuni na taratibu ndio ziwaongoze katika kutekeleza majukumu yenu.Serikali inawalipa mishahara mizuri kwa lengo la kuwaokoa msijiingize kwenye matatizo”alifafanua.
Mahakimu walioapishwa jana, ni Fedinard Vugingi ambaye alikuwa hakimu wa mahakama ya mwanzo Kondoa mkoani Dodoma na sasa anakuwa hakimu mfawidhi wa mahakama ya wilaya ya Kondoa. Aziza Hassan Mbadjo aliyekuwa karani katika mahakama kuu ya ardhi Dar-es-salaam,sasa amekuwa hakimu katika mahakama ya hakimu mkazi mjini hapa.
Naye Terrysophia Cornelio Tesha aliyekuwa hakimu wa mahakama ya mwanzo Ipembe,sasa anakuwa hakimu katika mahakama ya hakimu mkazi Singida mjini.
Mahakimu wote hao watatu, wamejiendeleza kwa nguvu zao wenyewe. Jaji Ramadhan na msafara wake wameondoka Singida mjini leo (jana) asubuhi kuelekea mkoani Shinyanga.