HASHIM LUNDENGA MWAANDAAJI WA MISS TANZANIA.
Mashindano ya urembo ya VODACOM miss TANZANIA 2010 yatafanyika Septemba 11 mwaka huu Jijini DSM huku warembo thelathini na moja waliochaguliwa katika kanda zote zilizoandaa mashindano hayo wanatarajia kuingia kambini .
Akizungumza Jijini DSM mkurugenzi wa miss TANZANIA HASHIM LUNDENGA amesema kuwa shindano la mwaka huu litakuwa la aina yake na litaandaliwa tafauti na miaka ya nyuma
LUNDENGA amesema kuwa mwaka huu kumekuwa na ushindani mzuri katika ngazi mbali mbali za mashindano hayo hivyo wanatarajia katika fainali atapatikanana mrembo ambaye ataweza kuwakilisha nchi vyema katika mashindano ya dunia.
Amesema licha ya kuingia kambini katika kipindi cha mfungo wa ramadhani lakini warembo hao wataweza kuendeela na ibada zao kama kawaida
No comments:
Post a Comment