Aug 21, 2012

FIESTA BHAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAS ISHANOGA ASEE


Njiani kuelekea Moshi Kilimanjaro kwa ajili ya Fiesta 2012 tutakayo enjoy pamoja Ijumaa august 24 tukiwashuhudia wakali kibao kwenye stage kama CMB Prezzo, Shetta na wengine kibao.
Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro Leonidas Gama kwenye interview na Clouds Fm na Clouds Tv nyumbani kwake ambapo yeye ndio atafungua rasmi Serengeti Fiesta 2012 kwenye mkoa wake ukiwa mkoa wa kwanza kuanza na Fiesta mwaka huu.
Simon Simalenga wa Clouds Media Group na mkuu wa mkoa Leonidas Gama.
Team Clouds ikiwa na mkuu wa mkoa.
Producer Erick Kusaga na mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro Leonidas Gama.
Millard Ayo na Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro Leonidas Gama.
.
.
.
.
.
.

PICHA TISA ZA BALAA ZA BARABARANI KUTOKA DAR MPAKA MOSHI.


Hizi picha nimezipiga kwenye safari ya kutokea Dar mpaka Moshi, hii ajali ya kwanza ilitokea karibu na Mlandizi ambapo hili lori la nyuma ndio lililigonga la mbele.
.
.
Hapa ni kwenye moja kati ya kona za mto wami.
Kwenye kituo cha polisi Wami, haya ni magari ya Wakenya waliopoteza maisha kwenye ajali Tanga wakati wakisafiri kwenda Dar es salaam.
.
Hii ni karibu na Segera.
Hili lori la njano lilishindwa kuendelea na safari baada ya kukwama kwenye matope.
kwa hisani ya www.millardayo.com

MAGAZETINI LEO 21/08/12


.
.
.





























REKODI ZA MBWANA SAMATTA ZAMPANDISHA THAMANI MARA 3 ZAIDIYA SIMBA WALIYOPEWA NA TP: KTK MECHI 7 AFUNGA MABAO 5, MANNE YA KICHWA.



Mbwana Ally Samatta anazidi kung'ara kwenye soka la anga ya kimataifa akiwa na klabu yake ya TP Mazembe.

Mbwana Samatta ambaye tayari anatimiza mwaka mmoja tangu ajiunge na timu yake hiyo ya Kinshasa Congo akitokea klabu bingwa ya Tanzania bara Simba Sports Club, amekuwa mmoja ya wafungaji bora na tegemeo kabisa kwenye timu hiyo inayomilikiwa na tajiri Moise Katumbi.

Kwa takwimu zilizo sahihi kabisa za Mbwana Samatta katika msimu huu 2011/12 upande wa Ligi ya mabingwa wa Afrika amecheza mechi 7 tu.

Katika mechi hizo saba Samatta "Golden Boy" amefunga mabao 5. Katika magoli hayo matano, kichwa chake kimeweka kambani mabao 4 na moja amefunga kwa guu lake la kulia.

Mabao hayo matano ya Samatta kwenye Africa Champions league amezifunga timu za Power Dynamo akiwa Ugenini, Akafunga bao lingine dhidi ya Al Merreikh aTP wakiwa nyumbani kabla ya kuja kuwafunga tena Wasudan hao nyumbani kwao Khartoum. Alhly wakawa majeruhi wengine wa Mbwana Samatta baada ya kuwaumiza wakiwa kwao Misri. TP Mazembe wakiwa uwanja wao nyumbani Tanzania Golden Boy akatupia bao moja kwenye mechi dhidi ya Berekum Chelsea. Ikafika zamu ya waarabu Zamalek ambaye akawafunga bao moja moja nyumbani na Ugenini na kutimiza mabao matano.

Dakika ambazo Mbwana Samatta anafunga sana magoli ni kuanzia kati ya dakika ya 16-30 ambapo hapo amefunga mabao mawili. kuanzia dk ya 31 mpaka 42 amafunga goli moja tu, huku akionekana kuwa hatari zaidi kwenye dakika ya 75 ya mchezo kwani tayari ameshafunga mabao mawili kwenye dakika hiyo.

Mafanikio hayo ya Samatta kwenye michuano mbalimbali TP Mazembe inayoshiriki yamezidi kumuongezea thamani kwenye soko la usajili duniani, kutoka kuuzwa kwa dola 100,000 na Simba kwenda TP Mazembe mpaka sasa anakadiriwa kuwa na thamani ya £175,000 ambayo ni mara 3 ya zaidi TP waliilipa Simba kumsaini Samatta.(www.shaffihdauda.com)

MVIVU, MCHELEWAJI MAZOEZINI NA UTOVU WA NIDHAMU VYAMUONDOA ALEX SONG ARSENAL - ATAMBULISHWA RASMI BARCA





Wakati baadhi ya mashabiki wa Arsenal wakiwa wana maumivu ya kuondokewa na mchezaji wao muhimu wa pili ndani ya wiki moja, Alex Song, taarifa zainasema kwamba kocha wa klabu hiyo Arsene Wenger amemuachia kiurahisi mcameroon huyo baada ya kuchoswa na utovu wa nidhamu wa mchezaji huyo, uchelewaji wa kwenye mazoezi na uvivu alionao. Kutokana na tabia zake hizo Wenger hakusita hata mara moja ilipokuja ofa ya Barcelona ya kumsajili Song kwani ilikuwa ni kumuondolea mzigo alioubeba bila kupenda katika kipindi kirefu kilichopita, kuondoka kwa Song kumefungua njia kwa Arsenal kuweza kushinda mbio za usajili wa mkopo wa Nuri Sahin kutoka Real Madrid.

Wakati Wenger akisema cha nini - Barcelona walikuwa wanasema watakipata lini. Pichani Alexander Song akiwa anatambulishwa rasmi baada ya kujiunga na klabu yake mpya ya Barcelona.(kwa hisani ya shaffihdauda.com)

Aug 17, 2012

NDUGU ZANGU WA ARSENAL, HIKI NDICHO ALICHOSEMA KOCHA WENU KUHUSU KUMSAJILI WA KUZIBA NAFASI YA VAN PERSIE!


.
Kwanza poleni sana katika kipindi hiki kigumu cha kuchukuliwa mkali Robin van Persie ambae ameingia kwenye familia ya Alex Ferguson.
Ninachotaka kuwaambia ni ripoti ya gazeti la The Sun Uingereza kuandika kwamba kocha Arsene Wenger wa Arsenal amesisitiza kwamba hatonunua striker mwingine ili kuchukua nafasi ya Robin Van Persie.
Yani kasema washambuliaji Olivier Giroud na Lukas Podolski wanatosha kabisa kuziba nafasi ya Van Persie na muda wote wawili hao walikua wakiandaliwa kuchukua hiyo nafasi.
.
Kocha huyo Mfaransa mwenye miaka 62 toka aletwe duniani, amesema japo inauma kupoteza mchezaji kama Van Persie kulikua hakuna njia yoyote isipokua kumuuza tu.
Kwenye line nyingine ni kwamba kocha wa Manchester United amesema anaamini jumatatu Van Persie atacheza kwenye mechi dhidi ya Everton.
August 15 2012 usiku ndio ilithibitisha kumchukua Van Persie ambapo Fergie alithibitisha kwamba mkali huyo alitarajiwa kufika Old Traford August 16 jioni kuonana na madaktari wa club hiyo na ana imani yote yaliyobakia yatamalizika kabla ya mechi ya jumatatu.
Kwa kumalizia amefananisha uwepo wa Wyne Rooney, Van Persie, Chicharito na Danny Welbeck kama ilivyokua 1999 kwa uwepo wa vichwa vikali kama Yorke, Cole, Sheringham and Solskjaer — the four best strikers in Europe.(www.millardayo.com)

THE DON HIMSELF

Karibuni sana kwenye blog hii ya kijamii iliyosheheni makila kitu kuanzia siasa uchumi afya na burudani kwa ujumla wake.uingiapo kwenye blog hii ni mengi ambayo utapata nafasi ya kukutana nayo,kumbuka mawazo yako ndo hasa yanayojenga na kunifanya niwe na ufanisi zaidi.kariiiiiiibuuuuuuuuuuuu saaaaaaaaaaaaaaanaaaaaaaaaa.(THE DJ HIMSELF-JIWE)

Followers

BLOG ZA MARAFIKI

Search This Blog

ZILIZOPITA

DUNIA MUZIMA