Aug 17, 2012

MAGAZETI YA LEO TRH 17/08/12

.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.

RAISI JAKAYA MRISHO MRISHO KIKWETE ASEMA AHADI YAKE YA KUILETA REAL MADRID IPO PALE PALE

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amesema kuwa bado ni dhamira ya Serikali yake kuileta moja ya timu za Ligi Kuu ya Soka ya Hispania (La Liga) kutembelea Tanzania na amemtaka Balozi mpya wa Hispania katika Tanzania kusaidia kufanikisha dhamira hiyo.

Aidha, Rais Kikwete ameipongeza Hispania kwa kutetea ubingwa wa Kombe la Mataifa ya Ulaya (Euro) 2012 katika mashindano yaliyomalizika mwezi uliopita nchini Poland na Ukraine.

Akizungumza na Balozi mpya wa Hispania, Mheshimiwa Luis Manuel Cuesta Civis mara baada ya kupokea hati yake ya utambulisho katika hafla fupi iliyofanyika jana Ikulu jijini Dar es Salaam leo, Rais alisema: “Wananchi wa Tanzania, ambako timu za Hispania, zina washabiki na wafuasi wengi, bado wanasubiri kwa hamu ziara ya moja ya timu kubwa za Ligi Kuu ya Soka ya Hispania. Tunataka ije hapa, icheze mechi moja ama mbili na itembelee mbunga zetu maarufu za wanyama,” alisema Rais Kikwete na kuongeza:

“Kama utakavyokuja kuthibitisha mwenyewe, Watanzania ni watu wanaopenda michezo na hasa soka na ni wafuatiliaji wakubwa wa Ligi Kuu ya Hispania ambako timu zenye mvuto zaidi ni Real Madrid na Barcelona.”

Rais Kikwete pia aliipongeza Hispania kwa kutetea ubingwa wake wa Ulaya.

“Tunawapongeza sana kwa kuweka historia. Kwanza mlishinda Kombe la Mataifa ya Ulaya, kisha mkashinda Kombe la Dunia. Sasa mmeweza kutetea Kombe la Ulaya. Hili halijapata kutokea kwa nchi moja kushikilia vikombe vyote viwili vikubwa vya soka duniani kwa wakati mmoja ama nchi kutetea Kombe la Ulaya.”

DULLY 'MTOTO WA KARIAKOO' OFFICIAL VIDEO ...teentz.com

PICHA 11 ZA RVP AKIWA KWENYE SIKU YA KWANZA YA MAZOEZI NA MAN UTD!












RATIBA KAMILI YA FIESTA 2012, MSIMU NDIO HUU USHAANZA, JIPANGEE, BHAAAASSIIIIIIIIII.

Aug 16, 2012

KITU ALICHOKIFANYA RAIS MUSEVEN KWA MGANDA ALIESHINDA OLYMPIC, HII NDIO NYUMBA ALIYOKUA AKIISHI..


.
Baada ya kurudi home, Maelfu ya waganda wamempokea Stephen Kiprotich mshindi wa medali ya dhahabu kwenye riadha ya Olympic 2012 ambapo ameifanya Uganda itangazwe mshindi wa medali hiyo baada ya miaka 40.
Kiprotich ambae ni askari magereza alieshinda kwenye mbio za wanaume jumapili iliyopita ndani ya Olypic 2012, amezawadiwa cheki ya dola za kimarekani elfu 80 ambazo zimetolewa na Rais Yoweri Museveni ambae pia amempandisha cheo mara tisa kwenye kazi yake ya uaskari Magereza.
Standard Media wameripoti kwamba mzigo ulikua mzito manake watu walipanga foleni kumpokea Stephen huko Entebbe akiwa amebebwa kwenye gari ambalo lilikua na plate namba iliyoandikwa UG GOLD.
Hii ndio nyumba aliyokua akiishi Stephen.
Watu walikua wengi mpaka waliziba njia ambapo magari yaliyokua kwenye msafara yalikosa pa kupita wakati yakielekea ikulukumpeleka Stephen kunywa chai asubuhi na Rais Museveni.
Baada ya Kiprotich kupewa cheki yake ya dola elfu 80, alimuomba rais Museveni kuwajengea wazazi wake nyumba kaskazini mashariki mwa Uganda ambapo rais Museveni amekubali kujenga hiyo nyumba ya vyumba vitatu.
Kwenye line nyingine ni kwamba rais Museven ameahidi kwamba katika muda ujao, mwanamichezo yoyote wa Uganda atakaeshinda medali ya kimataifa, atakua analipwa shilingi shilingi milioni moja za Uganda kila mwezi.(SOURCE:www.millardayo.com)

MAGAZETI YA LEO TRH 16/08/12


.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.

MRISHO NGASSA AIOKOA STARS NA KIPIGO BOTSWANA - YATOKA SARE YA 3-3



Taifa Stars imetoka sare ya mabao 3-3 na wenyeji Botswana (Zebras) katika moja kati ya mechi kadhaa za kirafiki za kalenda ya Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) zilizochezwa leo (Agosti 15 mwaka huu) usiku.
 
Hadi mapumziko kwenye mechi hiyo iliyochezwa Uwanja wa Molepolole ulioko Kilometa 40 nje ya Jiji la Gaborone, timu hizo zilikuwa zimefungana mabao 2-2. Stars ndiyo iliyokuwa ya kwanza kupata bao dakika ya 17 lililofungwa kwa penalti na beki Erasto Nyoni.
 
Mwamuzi Lekgotia Johannes Stars alitoa adhabu hiyo baada ya beki Oscar Obuile Ncenga wa Zebras kumuangusha ndani ya eneo la hatari mshambuliaji Mrisho Ngasa aliyekuwa akimkabili kipa Mompoloki Sephekolo.
 
Bao hilo halikudumu muda mrefu, kwani Zebras walisawazisha dakika ya 26 baada ya shuti kali lililopigwa na
Lemponye Tshireletso nje ya eneo la hatari kumshinda nahodha wa Taifa Stars, Juma Kaseja. Dakika tano baadaye kiungo mshambuliaji Mwinyi Kazimoto aliifungia Stars bao la pili kwa shuti la mbali.
 
Tshireletso aliisawazishia tena Zebras dakika ya 37. Mfungaji alifunga bao hilo kwa kichwa akiunganisha mpira wa krosi kutoka wingi ya kushoto uliopigwa na Tebogo Sembowa ambaye kabla alimtoka beki Aggrey Morris.
 
Kipindi cha pili kilianza kwa Kocha Kim Poulsen wa Stars kuwatoa Frank Domayo na Salum Abubakar na nafasi
zao kuchukuliwa na Shabani Nditi na Athuman Idd. Safari hii Zebras ndiyo walioanza kufunga dakika ya 69 ambapo kiungo Michael Mogaladi aliifungia bao la tatu kwa kichwa akiunganisha krosi fupi iliyotokana na mpira wa kurusha.
 
Dakika 13 za mwisho Stars walicheza pungufu baada ya beki Erasto Nyoni kutolewa nje kwa kadi nyekundu kutokana na kumchezea rafu mshambuliaji Lovemore Murirwa.
 
Mrisho Ngasa ambaye alikuwa nyota kwenye mchezo huo aliisawazishia Stars dakika ya 84 baada ya kugongeana one-two na mshambuliaji Simon Msuva aliyetokea benchi kuchukua nafasi ya Haruna Moshi.
 
"Licha ya timu kucheza vizuri, tatizo kubwa lilikuwa kwenye safu ya ulinzi ambapo mabeki waliruhusu mipira mingi ya krosi na kuwaacha washambuliaji wa Botswana wakifunga bila bughudha. Mabeki hawatakiwi kuruhusu mipira ya krosi, wakiruhusu ni lazima wahakikishe wanawadhibiti washambuliaji wa timu pinzani.
 
"Kwa upande wa washambuliaji, Said Bahanuzi alikuwa akicheza mechi yake ya kwanza ya kimataifa akiwa na Stars tangu nilipomjumuisha kwenye timu kwa mara ya kwanza. Kuna makosa madogo madogo ambayo niliyatarajia, hivyo nitamrekebisha polepole," alisema Kocha Poulsen mara baada ya mechi hiyo.
 
Stars; Juma Kaseja, Erasto Nyoni, Amir Maftah, Aggrey Morris, Kelvin Yondani, Frank Domayo/Shabani Nditi,
Mrisho Ngasa, Salum Abubakar/Athuman Idd, Said Bahanuzi/Simon Msuva, Haruna Moshi/Ramadhan Singano na Mwinyi Kazimoto.
 
Zebras; Mompoloki Sephekolo, Tshepo Motlhabankwe/Tshepo Maikano, Edwin Olerile, Oscar Obuile Ncenganye, Mompati Thuma, Patrick Motsepe/Jackie Mothatego, Lemponye Tshireletso, Michael Mogaladi, Tebogo Sembowa, Ntesang Simanyana na Galabgwe Moyana/Lovemore Murirwa.
 
Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager inarejea nyumbani kesho (Agosti 16 mwaka huu) ambapo itawasili Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) saa 1.20 usiku kwa ndege ya Kenya Airways.(www.shaffihdauda.com)

ROBIN VAN PERSIE NA CESC FABREGAS - WALIVYOFANYA TAREHE 15 AUGUST KUWA MBAYA KATIKA HISTORIA YA ARSENAL




Tarehe 15 ya August itaendelea kuwa tarehe ya maumivu kwa washabiki wa Arsenal milele.
Kwanini?


Kwanini?

Msimu uliopita mnamo tarehe 15, mwezi kama huu yaani August, Arsenal walimuuza nahodha wao na kiungo wa kutegemewa Cesc Fabregas waliomsajili na kukaa nae kwa takribani miaka 8. 


Pia tarehe kama ya leo (15th August) Arsenal wanakubaliana ada ya uhamisho na mahasimu wao Manchester United kwa ajili ya nahodha na mshambuliaji wao wa kutumainiwa Robin van Persie kujiunga na Mashetani wekundu.



Kwa maana hiyo Cesc Fabregas na Van Persie ambaye nae amekaa Arsenal kwa miaka nane toka 2004-2012 wanaifanya tarehe hii (15th August) kuwa kumbukumbu mbaya kwa mashabiki wa klabu yao ya zamani - Arsenal.


UFANANO WAO
1: Wote wemakaa Arsenal kwa miaka nane, Fabregas kutoka 2003 - 2011, Van Persie 2004-2012.

2: Wote walikuwa manahodha wa Arsenal mpaka wakati wanauzwa.

3: Wote wameondoka Arsenal katika tareheh moja. 

R.I.P TO ARSENAL - RVP MANCHESTER UNITED

By Aidan Seif Charlie

THE DON HIMSELF

Karibuni sana kwenye blog hii ya kijamii iliyosheheni makila kitu kuanzia siasa uchumi afya na burudani kwa ujumla wake.uingiapo kwenye blog hii ni mengi ambayo utapata nafasi ya kukutana nayo,kumbuka mawazo yako ndo hasa yanayojenga na kunifanya niwe na ufanisi zaidi.kariiiiiiibuuuuuuuuuuuu saaaaaaaaaaaaaaanaaaaaaaaaa.(THE DJ HIMSELF-JIWE)

Followers

BLOG ZA MARAFIKI

Search This Blog

ZILIZOPITA

DUNIA MUZIMA