Ni globu ya kijamii inayojihusisha na mambo yote ya kijamii,natumaini jamii yangu ya kitanzania itafaidika sana pindi ichukuapo fursa ya kuperuzi kwenye globu hii,dhamira yangu ni kufikisha ujumbe pamoja na kuiburudisha jamii yangu na furaha yangu ni kuona natimiza dhamira yangu kwako.natumaini kuwa wewe utaniunga mkono kwa kile ambacho nataka kukifanya kwa ajili ya jamii yangu ya kitanzania.NASHUKURU KWA KUNIELEWA.
Aug 16, 2012
ROBIN VAN PERSIE NA CESC FABREGAS - WALIVYOFANYA TAREHE 15 AUGUST KUWA MBAYA KATIKA HISTORIA YA ARSENAL
Tarehe 15 ya August itaendelea kuwa tarehe ya maumivu kwa washabiki wa Arsenal milele.
Kwanini?
Kwanini?
Msimu uliopita mnamo tarehe 15, mwezi kama huu yaani August, Arsenal walimuuza nahodha wao na kiungo wa kutegemewa Cesc Fabregas waliomsajili na kukaa nae kwa takribani miaka 8.
Pia tarehe kama ya leo (15th August) Arsenal wanakubaliana ada ya uhamisho na mahasimu wao Manchester United kwa ajili ya nahodha na mshambuliaji wao wa kutumainiwa Robin van Persie kujiunga na Mashetani wekundu.
Kwa maana hiyo Cesc Fabregas na Van Persie ambaye nae amekaa Arsenal kwa miaka nane toka 2004-2012 wanaifanya tarehe hii (15th August) kuwa kumbukumbu mbaya kwa mashabiki wa klabu yao ya zamani - Arsenal.
UFANANO WAO
1: Wote wemakaa Arsenal kwa miaka nane, Fabregas kutoka 2003 - 2011, Van Persie 2004-2012.
2: Wote walikuwa manahodha wa Arsenal mpaka wakati wanauzwa.
3: Wote wameondoka Arsenal katika tareheh moja.
R.I.P TO ARSENAL - RVP MANCHESTER UNITED
By Aidan Seif Charlie
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
ME MYSELF & I
THE DON HIMSELF
Karibuni sana kwenye blog hii ya kijamii iliyosheheni makila kitu kuanzia siasa uchumi afya na burudani kwa ujumla wake.uingiapo kwenye blog hii ni mengi ambayo utapata nafasi ya kukutana nayo,kumbuka mawazo yako ndo hasa yanayojenga na kunifanya niwe na ufanisi zaidi.kariiiiiiibuuuuuuuuuuuu saaaaaaaaaaaaaaanaaaaaaaaaa.(THE DJ HIMSELF-JIWE)
No comments:
Post a Comment