Jumatano
Agosti 15 ni Siku ya Kalenda ya FIFA iliyowekwa mahsusi kwa ajili ya
Mechi za Kimataifa za Kirafiki na Nchi nyingi Duniani zimeandaa Mechi za
kujipima ikiwemo Tanzania ambayo Timu yake, Taifa Stars, itakwenda huko
Gaborone kucheza na Wenyeji wao Botswana.
Huko Barani Ulaya, ambako Nchi zake
zitaanza Mwezi ujao kinyang’anyiro cha Mechi za Mchujo za kuwania kufuzu
kucheza Fainali za Kombe la Dunia za Mwaka 2014 huko Brazil, zipo Mechi
nyingi na zinazohusisha Timu kubwa.
Mabingwa wa Dunia na Ulaya, Spain,
watarudi tena dimbani kwa mara ya kwanza tangu watwae EURO 2012 hapo
Julai 1 kwa kucheza na Puerto Rico Siku ya Jumatano ikiwa ni matayarisho
ya Mechi yao ya Kundi I la Kombe la Dunia 2014 dhidi ya Georgia hapo
Septemba 11, Kundi ambalo pia wapo France, Belarus na Finland.
Italy wao watacheza Kirafiki na England
hapo Jumatano huko Berne, Uswisi huku Timu zote hizi pia zikikabiliwa na
Mechi za Makundi yao Kombe la Dunia Mwezi Septemba ambapo Italy
watacheza na Bulgaria na England watakipiga na Moldova hapo Septemba 7.
France, wakiwa chini ya Kocha mpya
Didier Deschamps, watacheza Mechi ya Kirafiki na Uruguay huku wakiwa na
Kikosi chenye mabadiliko ambacho hakina Wachezaji maarufu kina Hatem Ben
Arfa, Philippe Mexès, Adil Rami, Yohan Cabaye, Alou Diarra, Florent
Malouda na Yann M'Vila ambao wote wametemwa.
Na Russia nao watacheza na Ivory Coast wakiwa chini ya Kocha wao mpya Fabio Capello.
Mechi ya Kirafiki ya kusisimua itakuwa
ni ile kati ya Netherlands na Belgium ambayo ina Wachezaji wakubwa
wanaotamba hivi sasa kina Vincent Kompany, Jan Vertonghen, Thomas
Vermaelen, Eden Hazard, Axel Witsel, Moussa Dembélé na Marouane
Fellaini.
Vigogo wa Soka Duniani, Brazil, wao watacheza kirafiki na Sweden.
RATIBA BAADHI YA MECHI
Jumatano, Agosti15
Mechi za Kimataifa za Kirafiki
Botswana v Tanzania
Costa Rica v Peru
Ecuador v Chile
El Salvador v Jamaica
Mexico v USA [Saa 9 usiku]
Albania v Moldova [Saa 7 mchana]
Japan v Venezuela [Saa 7 na nusu mchana]
South Korea v Zambia [Saa 8 mchana]
China PR v Ghana [Saa 8 Dak 35 mchana]
Puerto Rico v Spain [Saa 12 jioni]
Russia v Ivory Coast Saa 12 jioni]
Armenia v Belarus [Saa 1 usiku]
Azerbaijan v Bahrain [Saa 1 usiku]
Croatia v Switzerland [Saa 2 na robo usiku]
Bulgaria v Cyprus [Saa 3 usiku]
Luxembourg v Georgia [Saa 3 usiku]
Norway v Greece [Saa 3 usiku]
Sweden v Brazil [Saa 3 usiku]
Ukraine v Czech Republic [Saa 3 usiku]
Denmark v Slovakia [Saa 3 na robo usiku]
Austria v Turkey [Saa 3 na nusu usiku]
Hungary v Israel [Saa 3 na nusu usiku]
Montenegro v Latvia [Saa 3 na nusu usiku]
Belgium v Netherlands, 19:45
Estonia v Poland [Saa 3 Dak 45 usiku]
Germany v Argentina [Saa 3 Dak 45 usiku]
Macedonia v Lithuania [Saa 3 Dak 45 usiku]
Northern Ireland v Finland [Saa 3 Dak 45 usiku]
Serbia v Rep of Ireland [Saa 3 Dak 45 usiku]
Slovenia v Romania [Saa 3 Dak 45 usiku]
Wales v Bosnia-Hercegovina [Saa 3 Dak 45 usiku]
England v Italy [Saa 5 usiku]
France v Uruguay [Saa 5 usiku]
Scotland v Australia [Saa 5 usiku]
Iceland v Faroe Islands [Saa 5 Dak 45 usiku]
Portugal v Panama [Saa 6 Usiku]
Paraguay v Guatemala [Saa 6 usiku]
Alhamisi, Agosti 16
Canada v Trinidad and Tobago [Saa 9 usiku]
Costa Rica v Peru [Saa 9 usiku]
Ecuador v Chile [Saa 9 usiku]
El Salvador v Jamaica [Saa 9 usiku]