Mshindi wa Tuzo ya UEFA ya Mchezaji Bora
Ulaya kwa Msimu wa 2011/12 atajulikana hapo Agosti 30 baada ya leo
Listi ya Wachezaji 32 kuchujwa na kubakizwa watatu ambao wametangazwa na
UEFA kuwa ni Lionel Messi na Iniesta wa Barcelona, na Ronaldo wa Real
Madrid.
Tuzo hii ilifufuliwa upya na Rais wa
UEFA, Michel Platini, na kwa mara ya kwanza alitunukiwa Lionel Messi
Mwezi Agosti Mwaka jana.
Mshindi wa Tuzo hii atapewa Tuzo yake hapo Agosti 30 huko Monaco.
Kama ilivyokuwa Mwaka jana, Jopo la
Wanahabari toka kila Nchi Wanachama wa UEFA, Nchi 53, ndilo lilichagua
hao watatu kwa kura kutoka Listi ya Wachezaji hao 32 wa mwanzoni.
Wachezaji hawa watatu waliobakishwa watapigiwa kura ‘laivu’ Agosti 30 na Wanahabari hao hao toka Nchi 53 Wanachama wa UEFA.
LISTI AWALI YA WACHEZAJI 32:
Sergio Agüero (ARG) – Manchester City FC
Xabi Alonso (ESP) – Real Madrid CF
Mario Balotelli (ITA) – Manchester City FC
Jakub Błaszczykowski (POL) – Borussia Dortmund
Gianluigi Buffon (ITA) – Juventus
Iker Casillas (ESP) – Real Madrid CF
Petr Čech (CZE) – Chelsea FC
Fábio Coentrão (POR) – Real Madrid CF
Leslie Davies (WAL) – Bangor City FC
Didier Drogba (CIV) – Chelsea FC (Amehamia Shanghai Shenhua FC)
Cesc Fàbregas (ESP) – FC Barcelona
Falcao (COL) – Club Atlético de Madrid
Joe Hart (ENG) – Manchester City FC
Zlatan Ibrahimović (SWE) – AC Milan
Andrés Iniesta (ESP) – FC Barcelona
Shinji Kagawa (JPN) – Borussia Dortmund (Amehamia Manchester United FC)
Vincent Kompany (BEL) – Manchester City FC
Frank Lampard (ENG) – Chelsea FC
Lionel Messi (ARG) – FC Barcelona
Luka Modrić (CRO) – Tottenham Hotspur FC
Mesut Özil (GER) – Real Madrid CF
Pepe (POR) – Real Madrid CF
Andrea Pirlo (ITA) – Juventus
Sergio Ramos (ESP) – Real Madrid CF
Raúl González (ESP) – FC Schalke 04 (Amehamia Al-Sadd Sports Club)
Cristiano Ronaldo (POR) – Real Madrid CF
Wayne Rooney (ENG) – Manchester United FC
David Silva (ESP) – Manchester City FC
Fernando Torres (ESP) – Chelsea FC
Yaya Touré (CIV) – Manchester City FC
Robin van Persie (NED) – Arsenal FC
Xavi Hernández (ESP) – FC Barcelona
No comments:
Post a Comment