Aug 14, 2012

MITANANGE YA KIRAFIKI KESHO

FIFA-logo-300Jumatano Agosti 15 ni Siku ya Kalenda ya FIFA iliyowekwa mahsusi kwa ajili ya Mechi za Kimataifa za Kirafiki na Nchi nyingi Duniani zimeandaa Mechi za kujipima ikiwemo Tanzania ambayo Timu yake, Taifa Stars, itakwenda huko Gaborone kucheza na Wenyeji wao Botswana.
Huko Barani Ulaya, ambako Nchi zake zitaanza Mwezi ujao kinyang’anyiro cha Mechi za Mchujo za kuwania kufuzu kucheza Fainali za Kombe la Dunia za Mwaka 2014 huko Brazil, zipo Mechi nyingi na zinazohusisha Timu kubwa.
Mabingwa wa Dunia na Ulaya, Spain, watarudi tena dimbani kwa mara ya kwanza tangu watwae EURO 2012 hapo Julai 1 kwa kucheza na Puerto Rico Siku ya Jumatano ikiwa ni matayarisho ya Mechi yao ya Kundi I la Kombe la Dunia 2014 dhidi ya Georgia hapo Septemba 11, Kundi ambalo pia wapo France, Belarus na Finland.
Italy wao watacheza Kirafiki na England hapo Jumatano huko Berne, Uswisi huku Timu zote hizi pia zikikabiliwa na Mechi za Makundi yao Kombe la Dunia Mwezi Septemba ambapo Italy watacheza na Bulgaria na England watakipiga na Moldova hapo Septemba 7.
France, wakiwa chini ya Kocha mpya Didier Deschamps, watacheza Mechi ya Kirafiki na Uruguay huku wakiwa na Kikosi chenye mabadiliko ambacho hakina Wachezaji maarufu kina Hatem Ben Arfa, Philippe Mexès, Adil Rami, Yohan Cabaye, Alou Diarra, Florent Malouda na Yann M'Vila ambao wote wametemwa.
Na Russia nao watacheza na Ivory Coast wakiwa chini ya Kocha wao mpya Fabio Capello.
Mechi ya Kirafiki ya kusisimua itakuwa ni ile kati ya Netherlands na Belgium ambayo ina Wachezaji wakubwa wanaotamba hivi sasa kina Vincent Kompany, Jan Vertonghen, Thomas Vermaelen, Eden Hazard, Axel Witsel, Moussa Dembélé na Marouane Fellaini.
Vigogo wa Soka Duniani, Brazil, wao watacheza kirafiki na Sweden.
RATIBA BAADHI YA MECHI
Jumatano, Agosti15
Mechi za Kimataifa za Kirafiki
Botswana v Tanzania
Costa Rica v Peru
Ecuador v Chile
El Salvador v Jamaica
Mexico v USA [Saa 9 usiku]
Albania v Moldova [Saa 7 mchana]
Japan v Venezuela [Saa 7 na nusu mchana]
South Korea v Zambia [Saa 8 mchana]
China PR v Ghana [Saa 8 Dak 35 mchana]
Puerto Rico v Spain [Saa 12 jioni]
Russia v Ivory Coast Saa 12 jioni]
Armenia v Belarus [Saa 1 usiku]
Azerbaijan v Bahrain [Saa 1 usiku]
Croatia v Switzerland [Saa 2 na robo usiku]
Bulgaria v Cyprus [Saa 3 usiku]
Luxembourg v Georgia [Saa 3 usiku]
Norway v Greece [Saa 3 usiku]
Sweden v Brazil [Saa 3 usiku]
Ukraine v Czech Republic [Saa 3 usiku]
Denmark v Slovakia [Saa 3 na robo usiku]
Austria v Turkey  [Saa 3 na nusu usiku]
Hungary v Israel [Saa 3 na nusu usiku]
Montenegro v Latvia [Saa 3 na nusu usiku]
Belgium v Netherlands, 19:45
Estonia v Poland [Saa 3 Dak 45 usiku]
Germany v Argentina [Saa 3 Dak 45 usiku]
Macedonia v Lithuania  [Saa 3 Dak 45 usiku]
Northern Ireland v Finland  [Saa 3 Dak 45 usiku]
Serbia v Rep of Ireland [Saa 3 Dak 45 usiku]
Slovenia v Romania [Saa 3 Dak 45 usiku]
Wales v Bosnia-Hercegovina [Saa 3 Dak 45 usiku]
England v Italy [Saa 5 usiku]
France v Uruguay [Saa 5 usiku]
Scotland v Australia [Saa 5 usiku]
Iceland v Faroe Islands [Saa 5 Dak 45 usiku]
Portugal v Panama [Saa 6 Usiku]
Paraguay v Guatemala [Saa 6 usiku]
Alhamisi, Agosti 16
Canada v Trinidad and Tobago [Saa 9 usiku]
Costa Rica v Peru [Saa 9 usiku]
Ecuador v Chile [Saa 9 usiku]
El Salvador v Jamaica [Saa 9 usiku]

No comments:

THE DON HIMSELF

Karibuni sana kwenye blog hii ya kijamii iliyosheheni makila kitu kuanzia siasa uchumi afya na burudani kwa ujumla wake.uingiapo kwenye blog hii ni mengi ambayo utapata nafasi ya kukutana nayo,kumbuka mawazo yako ndo hasa yanayojenga na kunifanya niwe na ufanisi zaidi.kariiiiiiibuuuuuuuuuuuu saaaaaaaaaaaaaaanaaaaaaaaaa.(THE DJ HIMSELF-JIWE)

Followers

BLOG ZA MARAFIKI

Search This Blog

ZILIZOPITA

DUNIA MUZIMA