Sep 10, 2010

Rais Kikwete katika swala ya eid mkoani tanga leo


Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na baadhi ya waumini wa dini ya kiislamu muda mfupi baada ya kumalizika kwa swalla ya Iddi iliyoswaliwa katika Msikiti Mkuu wa Riyadh mjini Tanga leo asubuhi
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akipeana mkono wa Iddi na Rais Mstaafu wa awamu ya pili Mzee Ali Hassan Mwinyi wakati wa Swalla ya Iddi iliyoswaliwa katika Msikiti mkuu wa Riyadh mjini Tanga.Mzee Mwinyi ndiye mgeni Rasmi katika baraza la Iddi litakalofanyika kitaifa mjini Tanga.
Rais Mstaafu awamu ya pili Mzee Ali Hassan Mwinyi akisalimiana na Mufti Mkuu sheikh Issa Shaaban Simba wakati wa Swalla ya Iddi iliyoswaliwa mjini Tanga leo.Katikati anayeangalia ni Rais Jakaya Mrisho Kikwete
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiteta jambo na Mufti Mkuu wa Tanzania Sheikh Issa Shaaban Simba wakati wa swalla ya Idd iliyoswaliwa kwenye Msikiti Mkuu wa Riyadh mjini Tanga leo asubuhi (picha na Freddy Maro)

EID MUBARAK


Blogu ya JIWE THE DJ inapenda kuwatakia Eid Mubarak waislam woote popote pale walipo katika dunia hii.

vodacom foundation yasaidia watoto yatima kisiwani zanzibar


Mkurugenzi wa Mahusiano wa Vodacom Foundation Mwamvita Makamba akiwakabidhi Mbuzi watoto yatima na wanaoishi katika mazingira magumu wa mjini Unguja Zanzibar kwenye hafla ya futari iliyoandaliwa na Vodacom Foundation na kutoa misaada ya vyakula,madafutari pamoja na mbuzi 12 kwa ajili ya sikukuu ya Eid el Fitr,Vyote vikiwa na thamani ya Shilingi Milioni 2.
Naibu Khadhi Mkuu wa Zanzibar Shekhe Khamis Haji Khamis akiwakabidhi akiwakabidhi Mafuta ya kula watoto yatima na wanaoishi katika mazingira magumu wa mjini Unguja Zanzibar mara baada ya kukabidhiwa rasmi na Mkurugenzi wa Mahusiano wa Vodacom Foundation kwenye hafla ya futari iliyoandaliwa na Vodacom Foundation na kutoa misaada ya vyakula, mafuta ya kula,madafutari pamoja na mbuzi 12 kwa ajili ya sikukuu ya Eid el Fitr,Vyote vikiwa na thamani ya Shilingi Milioni 2.
Watoto yatima na waishio katika mazingira hatarishi wa mjini Unguja Zanzibar wakiwa wamepokea mbuzi wao mara baada ya kukabidhiwa na Mkurugenzi wa Mahusiano wa Vodacom Foundation Mwamvita Makamba kwenye hafla ya futari iliyoandaliwa na Vodacom Foundation na kutoa misaada ya vyakula,mafuta ya kula,madafutari pamoja na mbuzi 12 kwa ajili ya sikukuu ya Eid el Fitr,Vyote vikiwa na thamani ya Shilingi Milioni 2.
Mtoto yatima Sharifa Khamis wakidato cha tatu(10) akimuonyesha uhodari wa kuandika Mkurugenzi wa Mahusiano wa Vodacom Foundation Mwamvita Makamba kwenye hafla ya futari iliyoandaliwa Unguja Zanzibar , Vodacom Foundation walitoa misaada ya vyakula,mafuta ya kula,madafutari pamoja na mbuzi 12 kwa ajili ya sikukuu ya Eid el Fitr,Vyote vikiwa na thamani ya Shilingi Milioni 2.

VINJARI NA CAMERA YA JIWE!!!

anajulikana kama SHAMIMU MLACHA ama SHANEY ni mmoja kati ya wanaounda jopo la Flava zone toka hapa 106.5fm Radio Mlimani ya chuo kikuu cha dar es salaam akiwa kwenye pozi tofauti(sa haya si ndo makirikiri ya idd aisee)
















Sep 9, 2010

MRISHO MPOTO ADONDOKA NA ADELA

Msanii mwenye mistari yenye ujumbe mzuri na kumfikia mtu kwa haraka ujumbe wake Mrisho Mpoto, ametoa wimbo wake mpya kama wiki na nusu sasa unaoitwa Adela akiwa amemshirikisha msanii Ismail aliyeimba kiitikio cha wimbo huu.
Wimbo huu Mpoto anamzungumzia Adela kwamba anyooshe kidole na hana nia mbaya yakumrudisha darasani, Studio ya Fishcrab chini ya Producer Lamar ndio umeutengeneza wimbo huu.
Ufuatilie wimbo huu mpya wa Mpoto ili upate na wewe ujumbe uliopo ndani ya wimbo huu wa Adela.

BODI YA KOROSHO YAZINDUA UNUNUZI WA KOROSHO NCHINI!!

Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Korosho Tanzania Hemed Mkali(katikati) akitangaza leo jijini Dar es salaam ufunguzi wa ununuzi wa korosho hapa nchini kwa msimu wa 2010/2011. Wengine ni Mkurugenzi wa Huduma za Masoko wa Bodi hiyo Mohamed Hassan Hanga (kushoto) na Meneja Tawi wa Bodi Tawi la Dar es salaam Martin Malifedha.

NA ZAHRA MAJID- MAELEZO.

MSIMU wa ununuzi wa korosho kwa mwaka 2010/2011 nchini unatarajiwa kuanza Jumatano ya wiki.

Ununuzi huo unatarajia kutumia Mfumo wa Stakabadhi ghalani ambapo Vyama vya Ushirika vitapeleka korosho kwenye maghala ya Serikali ambapo ndipo mnada utafanyikia.

Hayo yalisemwa jana jijini Dar-es-salaam na Makamu Mwenyekiti wa Bodi hiyo Hemedi Mkali wakati wa mkutano na waandishi wa habari katika ukumbi wa Idara ya Habari ( MAELEZO).

Alisema kuwa korosho zitauzwa kwa mnada utakaofanyika katika Bodi ya Korosho na katika Ofisi za Bodi katika mikoani Tanga, Mtwara, Pwani, Dar-es salaam, Morogoro, Ruvuma na Wilaya za Kyela na Ludewa Tunduru.

Mkali alisema kuwa korosho zitakazouzwa ni zile tu zitakazokuwa kwenye magulio yaliyosajiliwa na Serikali na kuongeza uuzaji wa korosho kinyume cha utaratibu huo , wahusika watachukuliwa hatua kwa mujibu wa Sheria namba 12 ya mwaka 2009.

“ Wanunuzi wa korosho wanaombwa wafuate taratibu hizi za ununuzi kwani watakaojaribu kukiuka taratibu hizi za ununuzi basi wajue Sheria hii inayohusu sekta ya korosho itachukua mkondo wake” Mkali alisema.

Mkali alizitaja kuwa timu zitakazoendesha mnada huo kuwa na wawakilishi toka Bodi ya Korosho,Vyama vya Ushirika Benki ya CRDB na NMB, Bodi ya Leseni za maghala Tanzania, Maafisa Ushirika watakaoteuliwa kama waalikwa na wengine wanaohitaji kushuhudia watafuata utaratibu maalum wa minada hiyo.

Halikadhalika, alisema kuwa,katika mfumo wa stakabadhi za mazao maghalani, kwa niaba ya wakulima korosho zitakusanywa na chama cha ushirika cha msingi katika magulio yaliyosajiliwa kwa kuwalipa wakulima asilimia 70 ya bei dira kwa korosho daraja la kwanza.

Mkali alisema kuwa watalipwa malipo ya pili asilimia 30 baada ya korosho kuuzwa mnadani.

“Aidha watalipwa malipo ya tatu (ya majaliwa) kutokana na bei itakayopatikana kwenye mauzo mnadani” Aliongeza Mkali.

Mkali alitaja viwango vya bei za korosho kuwa ni Tshs. 800 kwa kilo moja kwa daraja la kwanza(STD) na Tshs. 640 kwa kilo moja kwa daraja la pili(UG).

VODACOM MISS TANZANIA KUMEKUCHA!!

Hizi ndiyo picha za warembo 30 wanaotarajiwa kupanda jukwaani Septemba 11 kwenye ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es salaam katika shindano la kumsaka Vodacom Miss Tanzania jumamosi ijayo.

TOM & JENNY IN TANZANIA in BOOKSHOP!

A novel Idea Slipway, A novel Idea Seacliff Village, A novel Idea Steers, A novel Idea Shoppers Plaza, Scholastic Bookshop Mlimani City, Salamander Bookshop, Shrijee Supermarket Morogoro Store, Triniti Bar & Restaurant, TPH Bookshop, At the Green Bookshop, Mtindilo General Enterprise, TIC Shop Seacliff, Mchilavula Bookshop, JM Mall Supermarket, Airport Internet Café, Safari Boutique, Cliffton Supermarket, Treasure of Africa, La Petite Galerie, African Art, Alliance Francaise, Epis d’or, Zawadi Southern Sun, Mbalamwezi, Water Front Slipway, Muzu Art Galery, Namanga News Stand, St Peter News Stand, Palm Beach News Stand, IST News Stand, Kall Kwik Bookshop, Out of Africa, Airport Bookshop, Kipepeo Beach Resort, Cultural Heritage Cliffton Plaza Village Walk ALSO available at Novel Idea Arusha, Novel Idea Iringa, Bagamoyo Beach Resort -Bagamoyo, Memories of Zanzibar-Zanzibar, Morogoro, Mombasa, Belgium.

YOU CAN AS WELL GET A COPY DIRRECTLY FROM US, NO MINIMUM ORDER!

For wholesale and interested Distributers and for more details contact:-

Tel: 0713 471 371

Ziara ya Mwenyekiti wa WAMA Mama Salma Kikwete-Mkoa wa DSM!!

Mwenyekiti wa Taasisi ya Maendeleo ya Wanawake (WAMA) Mama Salma Kikwete Sept,8,2010 jijini Dar es salaam(kulia) akimtambulisha Mbunge mtarajiwa wa Jimbo la Kigamboni Wilaya ya Temeke Mkoa wa Dar es Salaam kupitia CCM Dr.Faustine Ndugulile katika mkutano wa uhamasishaji kwa wanachama wa UWT katika Uchaguzi Mkuu ujao (Picha na (Mwanakombo Jumaa)
Mwanachama wa UWT wa Wilaya ya Temeke pamoja mtoto wake nao hawakukosa kuhudhuria mkutano huo wa uhamasishaji wa umuhimu wa kupiga kura katika Uchaguzi mkuu ujao,jijini Dar es Salaam Sept.8,2010, kwani mama huyo ijapokuwa ana mtoto mdogo lakini anahaki ya kufahamu umuhimu wa kupata elimu ya kupiga kura.Mkutano huo ulihudhuriwa na Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maenedeleo (WAMA) Mama Salma Kikwete hayupo pichani. (Picha na Mwanakombo Jumaa)
Aliyekuwa mshindani mkubwa wa Jimbo la Temeke Salim Chikago (kushoto) akipongezana na mshindi wa kura za maoni katika jimbo hilo Abbas Mtemvu katika mkutano huo jijini Sept.8,2010.ambao ulihudhuriwa na Mwenyekiti wa Taasisi ya WAMA Mama Salma Kikwete (hayupo pichani)

Sep 4, 2010

UJUMBE WA LEO TOKA BLOG JIRANI!!!




Mtanzania yeyote Mzalendo wa kweli, mwenye akili timamu, asiye na mtindio wa ubongo, wala mtumwa wa hila chafu, wala udumavu wa kiakili, tena asiye na utando wa buibui wala tongotongo za ufisadi machoni, wala asiye mzembe wa kufikiri, anaalikwa asome kwa uangalifu na azingatie makala hii na awashirikishe ndugu, jamaa na marafiki zake popote pale walipo..

Dr Slaa yes we can! Huyu ni mtanzania wa pili baada ya Nyerere kuchukia ufisadi kwa vitendo. Ni mtanzania wa pili kuchukia umaskini wa watanzania kwa vitendo. Ni Dr. Slaa aliyesimama na kutaja majina ya wala rushwa na mafisadi. Akataka wale wanaopinga wampeleke mahakamani. Hakuna aliyethubutu kujitokeza kumpeleka mahakamani.

Ni Dr. Slaa aliyesimama bungeni kuomba posho za wabunge kupungzwa kuzielekeza zaidi kwa watanzania maskini. Ni Dr Slaa aliyesimama bila woga kunyosha vidole kwa matumizi mabaya ya ofisi za umma. Ni Dr Slaa amekuwa mtanzania baada ya Nyerere kutoa hoja za nguvu zinazomlenga kumkomboa mtanzania maskini. Maisha bora kwa kila mtanzania yako wapi? Ajira milioni moja ziko wapi? Hebu mwenye mbavu za kujibu swali hili ajibu bila unafiki!

Ni Dr Slaa anayeweza kudhibiti matumizi mabaya ya ofisi za umma. Ni Dr Slaa anayeweza kuwapa elimu ya bure watoto wetu pale mlimani. Achana na longolongo za CCM kuwatoza ushuru watoto. Waulizeni majukwaani wao Nyerere aliwatoza ada? Kama si kutaka watanzania waendelee kuwa mambumbumbu ni nini? kama si kutaka watanzania tuendeleee kuwa watumwa ni nini?

Ni Dr. Slaa anayeongelea treni ya umeme kwenda Kigoma, Dodoma, Tabora, na Mwanza. Waulize mpango wao ccm kama si kuwapa wahindi wanaoleta mabehewa ambayo mababu zetu walitumia wakati wa ukoloni. Sasa wahindi wanabaki kutudanganya na bajaji wakati vyuma chakavu vya reli sasa vinatumika kujenga vyoo. Hawa hawatutakii mema. Hawana tofauti na akina Carl Peters.

Ni Dr Slaa anayeongelea mfumko wa bei -nani hajajua dola leo hii ni sawa na tsh 1500. Uchumi unadidimia kwa kasi. Ahadi nyingine za uongo lukuki zinatolewa tena, wakati zile tulizoahidiwa mwaka 2005, hata moja haijatekelezwa. Watanzania walio wengi na hasa wa vijijini, wamelala usingizi. Wanafumbuliwa macho, lakini wamesinzia bado! Wanatabasamu, wanachekelea na kuridhika na vitisheti vya kijani na vikofia za njano. Wamekwishazoea shida kiasi kwamba wanadhani ni sehemu ya maisha yao. Ee mwenyezi Mungu, tunusuru na hili balaa..

Ni Dr.Slaa anaweza kuzuia wizi wa matrilion ya pesa kutoka migodi yetu ya Buzwagi, Geita, Bulyankulu, Buhemba, Nyamongo, Tulawaka, Nzega na Tanzanite. CCM wameshindwa kwa sababu ni washirka wakubwa na wameruhusu wizi huo. Ni Dr Slaa anaeweza kuwalipa wafanyakazi zaidi ya shilingi 350.000 achana na CCM ambayo imeshindwa kusimamia maliasili ambazo zingeliwapa wafanyakazi kima cha chini kinachokidhi mahitaji yao.

Ni Dr.Slaa anayeweza kusimamia mashirika ya umma kuleta tija achana na CCM wanaofyonza michango yetu kule, kwani haya mashirika yameshindwa nini kuwajengea nyumba wanachama wake? Mbona kwingine yameweza? Ni Dr.Slaa anayeweza kuongoza nchi bila woga, kwa utawala wa kweli wa sheria bila kuwaonea watu wala bila kulipiza visasi.

Ni Dr. Slaa ambaye amepanga kubadili katiba ili Rais afuate matakwa ya walio mwajiri ambao ni wananchi. Waulize CCM hata kama mtu kaiba anapewa mda arudishe pesa. Hivi inaingia akilini kweli? Utawala wa sheria uko wapi? Naomba niwape heko ITV kwa kuturejeshe kwenye hotuba za mwalimu. Katika hotuba yake moja alisema waziri mmoja kule uingereza aliandikwa kidogo tu gazetini juu ya kashfa, yule waziri alijiuzulu na waziri mkuu hata hakumjibu bali aliteua mtu mwingine.

CCM hawawezi hayo? Eti wanataka ushahidi. Nani kawambia rushwa tule wawili harafu tutoe vielelezo? Tunaiona rushwa kwa matokeo yake. Matengenezo ya barabara ya bilion 200, baada ya siku mbili imeharibika. Kwanini usimfukuze waziri na katibu wake wa wizara kwanza? CCM hawawezi! eti wanataka vielelezo!

Ni Dr Slaa anayeweza kufanya hayo. Si tumeona mnazi mmoja alivyowataja mafisadi wote! hapo akiwa ni mbunge tu! Je akiwa rais si watakimbia nchi? Jamani nawambia tumpe miaka mitano tu awakurupushe muone moto utakavyowaka.. Tutapata dawa, tutapata shule za bure, tutapata madawati. Jamani hivi kweli karne ya leo watoto wanasoma wamekaa chini? we must be serious! Hivi kweli dunia ya leo watu wanavuliwa nguo njiani kwenda Mwanza, Shinyanaga, Tabora, Kigoma, Mbeya, Lindi na Mtwara kwa sababu ya usafiri wa malori?

Nani asiye jua madaktari wetu wengi bingwa wapo botswana kwa sababu ya maisha duni Tanzania na hivi kwenda kutafuta maisha bora wakati hapa kwetu wananchi maskini wanakufa bila madawa? Nani asiyejua matatizo ya umeme, maji, makazi, maradhi, yanavyotutesa? Nani asiyejua wakulima wetu wasivyokuwa na masoko ya mazao yao? Nani asiejua asilimia 85 ya watanzania wanatumia vibatari au makoroboi kama mwanga? nani asiejua tunavyonyonywa na hawa wakoloni waliokuja kuchukua kila kitu??

Jamani wafanyakazi, wakulima, na wanafunzi, kwa nini mnalala usingizi? Kwa nini mnapiga miayo ya njaa wakati maghala yetu yamejaa nafaka? Ni akili gani hii? Nchi yetu inazo raslimali za kututosha, lakini wanaozifaidi ni vibaka wachache. Mtalala hadi lini?

Ni Dr Slaa mzalendo wa kweli, na sio kwa ajili ya sifa, anaweza kutuvusha tulipo. Nchi hii ni maskini na umaskini wenyewe ni wa kujitakia. Tanzania ni tajiri tuna kila kitu - mito, maziwa, national parks, migodi, mazao ya misitu, na kila aina ya utajiri. Lakini tuko maskini wa kutupwa! Naona huruma na umaskini wa kifikra wa watanzania.

Hivi kuna mtu hajui mapolisi wanalala kwenye vibanda vya mabati? Hivi kuna ambao hawajui mapolisi watendaji wanalipwa laki moja? Wamekosa nini hawa? Ni ajabu! pamoja na laki yao moja utakuta bado wanatumika kuwanyanyasa watetezi wao. Hata maaskari amkeni hiyo laki moja yenu haina tija hadi mrubuniwe kuwanyanyasa wapinzani ambao kimsingi wanawatetea ninyi! Hivi maaskari mnayo macho ya kuona? Jamani tuache woga inawezekana! Mbona Kenya wameweza? Mbona malawi wameweza?Mbona zimbabwe wameweza? Mbona Ghana wameweza? Kufanya mabadiliko sahihi, inawezakana na nafasi ni hii tuitumie.

Tumtume Dr Slaa atukurupushie wezi wote na atuwekee katiba sawa. Huo ndio msingi wa yote. Ni Dr. Slaa asiyeogopa kuwepo na mgombea binafsi. CCM hili hawaliwezi. Wamelipinga hadi mahakamani. Wanataka wao tu ndio waendelee kututawala na kutunyonya.

Jamani 2010 hakuna kudanganyika! enough is enough. Acheni kudanganyika. Wakati ndio huu. Watanzania msipoamua sasa, mtamlaumu nani tena? Nawatamani watu wa kule Mara -hakuna kura inaibiwa. Zote zinasimamiwa. Tukibadilika inawezekana, tena ni rahisi. Peleke ujumbe huu kwa marafiki, ndugu, jamaa, babu na bibi yako kule kijiji ambako wanadhani bado Nyerere ndiye rais wa nchi hii. Peleka ujumbe huu haraka kwa simu kama ipo, au kwa njia ya posta, mradi tu wale jamaa waliochoka kuishi wasiikwapue barua wakidhani ni hela..

Mh. Kikwete Akubalika Mkoani Morogoro

Mgombea Urais kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM),Mh. Dr. Jakaya Kikwete akionesha ilani za uchaguzi za CCM. Shoto ni ilani ya mwaka 2005 na kuume ni ilani ya uchaguzi mpya ambayo ni nene zaidiMh. Dr. Jakaya Kikwete akimnadi mgombea Ubunge wa jimbo la Morogoro Mjini, bw. Abdulaziz Abood wakati akiendelea na kampeni zake mkoani Morogoro leo.

Mh. Kikwete akiwasalimia wananchi wa Mkoa wa Morogoro waliofurika katika uwanja wa Jamhuri mjini humo.

Mgombea Urais kwa tiketi ya CCM,Mh. Dr. Jakaya Kikwete akiwahutubia wanachama wa CCM pamoja na wapenzi wa chama hicho waliofika leo katika uwanja wa Jamhuri,mjini Morogoro.

Vuvuzela asilia likipuliwa na mmoja wa wakazi wa Morogogo.

Baadhi ya wazee wa mji wa Ngerengere wakimsikiliza mgomea urais kwa tiketi ya CCM,Mh. Dr. Jakaya Kikwete leo.

maandamano ya pikipiki wakatika wa kumlaki Mh. Kikwete mkoani Morogoro leo.

Kepteni John Komba akiwa sambamba na TOT wakitumbuiza katika uwanja wa Jamhuri,mjini Morogoro leo.

wengi walijitokeza kumsikiliza Mh. Kikwete leo.

Moja ya mabango ya Kampeni ya Mh. Kikwete.

Umati mkubwa wa wakazi wa Morogoro walijitokeza kumsikiliza mgombea urais kwa tiketi ya CCM, Mh. Dr. Jakaya Kikwete alipokuwa akihutubia leo katika Uwanja wa Jamhuri na maeneo mwengine ya mkoa wa Morogoro

BREAKING NEWZ-KEISHA AJICHOMOA TIP TOP


kuna taarifa ambazo nimezisikia katika moja ya radio za hapa nyumbani tanzania kuwa yule msanii nguli toka katika kundi la TIP TOP CONNECTION khadija shaabani aka KEISHA ameamua kujiondoa katika kundi hilo kwa kile alichodai madai yaliyopitiliza dhidi ya meneja wake anayejulikana kama BABU TALE.sijapata uhakika sana juu ya hili ila naahidi alhamisi ya wiki ijayo kila kitu kitakuwa tayari na ukweli utaupata hapa hapa bloguni kwako.

ZIARA YA MAMA SALMA KIKWETE MKOANI MANYARA!!

Wanachama wa UWT Wilayani Babati Mkoa wa Manyara wakimkaribisha kwa salamu Mwenyekiti wa Taasisi yaWanawake na Maendeleo (WAMA) Mama Salma Kikwete pichani Sept.2.2010,alipofanya ziara mkoani humo na kufanya mkutano wa kuwahamasisha kuhusu Uchaguzi Mkuu hapo Oktoba 30,2010. Picha zote na Mwanakombo Jumaa-MAELEZO.
Muwakilishi wa UWT Wilaya ya Kiteto Mkoani Manyara (shoto) akimvisha nguo ya vazi la asili pamoja na viatu Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA) Mama Salma Kikwete alipokuwa katika ziara ya kuwahamasisha wanawake wa mkoa huo Sept.2,2010 kuhusu umuhimu wa kupiga kura na katiak Uchaguzi ujao.Mama Kikwete amemaliza ziara yake na kurejea leo Dar es salaam.
Akina mama wa UWT wa Mkoa wa Manyara wakimshangilia mama Salma Kikwete wakati alipowatembelea karibuni

HII NDIYO VODACOM MISS TANZANIA SPORTS DAY INAYOFANYIKA JANGWANI SEA BREEZE!!

Baadhi ya warembo wanaoshiriki katika shindano la Vodacom Miss Tanzania wakianza mbio za magunia wakati wa michezo ya Miss Tanzania Sports Day inayofanyika kwenye ufukwe wa Jangwani Sea Breeze Kunduchi shindano hilo litafanyika Septemba 11 katika ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es salaam.
Baadhi ya Warembo wakikimbia na magunia katika michezo ya Miss Tanzania Sports Day inayofanyika leo kwenye ufukwe wa Jangwani Sea Breeze.
Albert Makoye Mkuu wa Itifaki Kamati ya Miss Tanzania akiwapa warembo utaratibu wa kujisajili kwa ajili ya michezo ya Vodacom Miss Tanzania Sports Day.
Warembo wakiwa wamekaa tayari kwa kurekodi kipindi maalum kwa ajili ya shindano hilo leo kwenye ufukwe wa Jangwani Seabreeze.
Kutoka kushoto Grace,Jenny, Matina,Biduga, Grace na Rashid wakishuhudia na kushiriki katika michezo mbalimbali iliyoshirikisha warembo wanaoshiriki katika shindano la Vodacom Miss Tanzania.
Kutoka kulia ni Wadau kutoka Vodacom Tanzania Rashid, Eric, Edwin,Faidhal na rafiki yao kati.

PONGEZI ZA MOHAMMED G. DEWJI KWENDA KWA TIMU YA TAIFA STARS!!

Mimi kama mwenyekiti wa kamati ya ushindi kwa timu yetu ya Taifa (Taifa Stars) ninayofuraha kubwa kuwapa pongezi uongozi mzima wa timu yetu ya Taifa pamoja na wachezaji wetu kwa ushujaa waliouonyesha katika mechi yao dhidi ya Timu ya Taifa ya Algeria iliyochezwa siku ya Ijumaa tarehe 3/9/2010 ikawa ni kampeni za kuelekea katika kombe la mataifa ya Afrika.

Kwa nini nasema ni ushujaa? Ni kwa sababu ya kuweza kuonyesha mchezo safi ile hali kukiwa na uonevu ulioonekana wazi ukiwa na lengo la kukandamiza timu yetu isipate ushindi. Hakuna mtu yoyote ambaye aliyeshuhudia mechi hiyo atapingana nami eti kulikwa hakuna uonevu! Lakini matokeo tuliyoyapa yamedhihirisha ukomavu wetu katika soka la kimataifa, Pongezi zangu za dhati zimfikie kocha mkuu wa Jean Paulsen kwa kuweza kuwataarisha wachezaji kiakili ili kukabiliana vilivyo na hali hiyo ya uonevu na pia nitakuwa mchoyo wa fadhila kama sitampa pongezi nyingi Abdi Kassim (Babi) kwa goli zuri alilolifunga katika kipindi cha kwanza cha mchezo.

Vilevile tukumbuke haya yote ni matunda ya mheshimiwa Rais Jakaya Mrisho Kikwete baada ya kuamua kuweka nguvu kubwa katika mchezo wa soka nchini naye pia nampa pongezi kubwa na ninafahamu naye anasheherekea pamoja nasi matokeo haya popote pale alipo.

INTERVIEW YA C PWAAA NDANI YA STUDIO ZA MLIMANI TV LEO

INTERVIEW YA SAM WA UKWELI STUDIO ZA MLIMANI TV LEO

THE DON HIMSELF

Karibuni sana kwenye blog hii ya kijamii iliyosheheni makila kitu kuanzia siasa uchumi afya na burudani kwa ujumla wake.uingiapo kwenye blog hii ni mengi ambayo utapata nafasi ya kukutana nayo,kumbuka mawazo yako ndo hasa yanayojenga na kunifanya niwe na ufanisi zaidi.kariiiiiiibuuuuuuuuuuuu saaaaaaaaaaaaaaanaaaaaaaaaa.(THE DJ HIMSELF-JIWE)

Followers

BLOG ZA MARAFIKI

Search This Blog

ZILIZOPITA

DUNIA MUZIMA