Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akiwanadi wagombea wa CCM jimbo la Bairadi Magharibi Andrew Chenge (kushoto) na Mgombea Bariadi Mashariki Martine Makondo wakati alipofanya ziara na kuongea na wanachama wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) katika kuwahamasisha na kuwaelezea juu ya umuhimu wa kupiga kura ili wajitokeze kwa wingi katika uchaguzi mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani unaotarajiwa kufanyika Oktoba 31 mwaka huu nchini kote (Picha zote na Mwanakombo Jumaa wa Maelezo Dar es salaam)
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akizungumza na wanachama wa UWT jimbo la Maswa mkoani Shinyanga pamoja na kuwaombea kura za Rais , Wabunge na Madiwani wa CCM ili waweze kupata kura kwa wingi katika Uchaguzi Mkuu Oktoba 31 mwaka huu.
Nimevutiwa na uzalendo wa mwanafunzi huyu wa shule ya msingi jimbo la Meatu ambaye sikuweza kumpata jina lake,kwani nilikuwa katika msafara ila jicho lilivutiwa naye jinsi alivyopata hamasa na kuvaa kichwani mwake.kama anvyoonekana akitoka shuleni.
Wanachama wa UWT Jimbo la Maswa na Kisesa wakimsikiliza Mke wa Rais Mama Salma Kikwete katika mkutano wa ndani wa kampeni na kuwanadi wagombea wa CCM ili waweze kushinda wa kishindo katika Uchaguzi Mkuu ujao Oktoba 31 mwaka huu. Picha zote na Mwanakombo Jumaa.
No comments:
Post a Comment