Oct 13, 2010

ZIARA YA MAMA SALMA KIKWETE,MEATU,BARIADI NA MASWA MKOANI SHINYANGA.

Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akiwanadi wagombea wa CCM jimbo la Bairadi Magharibi Andrew Chenge (kushoto) na Mgombea Bariadi Mashariki Martine Makondo wakati alipofanya ziara na kuongea na wanachama wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) katika kuwahamasisha na kuwaelezea juu ya umuhimu wa kupiga kura ili wajitokeze kwa wingi katika uchaguzi mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani unaotarajiwa kufanyika Oktoba 31 mwaka huu nchini kote (Picha zote na Mwanakombo Jumaa wa Maelezo Dar es salaam)
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akizungumza na wanachama wa UWT jimbo la Maswa mkoani Shinyanga pamoja na kuwaombea kura za Rais , Wabunge na Madiwani wa CCM ili waweze kupata kura kwa wingi katika Uchaguzi Mkuu Oktoba 31 mwaka huu.
Nimevutiwa na uzalendo wa mwanafunzi huyu wa shule ya msingi jimbo la Meatu ambaye sikuweza kumpata jina lake,kwani nilikuwa katika msafara ila jicho lilivutiwa naye jinsi alivyopata hamasa na kuvaa kichwani mwake.kama anvyoonekana akitoka shuleni.
Wanachama wa UWT Jimbo la Maswa na Kisesa wakimsikiliza Mke wa Rais Mama Salma Kikwete katika mkutano wa ndani wa kampeni na kuwanadi wagombea wa CCM ili waweze kushinda wa kishindo katika Uchaguzi Mkuu ujao Oktoba 31 mwaka huu. Picha zote na Mwanakombo Jumaa.
Wanachama wa UWT jimbo la Bariadi Mashariki na Magharibi wakimshangiria Mke wa Rais Mama Salma Kikwete (hayupo pichani) alipokutana nao kwenye mkutano wa ndani kuhusu umuhimu wa kujitokeza kwa wingi kupiga kura katika Uchaguzi Mkuu Oktoba 31 mwaka huu.

No comments:

THE DON HIMSELF

Karibuni sana kwenye blog hii ya kijamii iliyosheheni makila kitu kuanzia siasa uchumi afya na burudani kwa ujumla wake.uingiapo kwenye blog hii ni mengi ambayo utapata nafasi ya kukutana nayo,kumbuka mawazo yako ndo hasa yanayojenga na kunifanya niwe na ufanisi zaidi.kariiiiiiibuuuuuuuuuuuu saaaaaaaaaaaaaaanaaaaaaaaaa.(THE DJ HIMSELF-JIWE)

Followers

BLOG ZA MARAFIKI

Search This Blog

ZILIZOPITA

DUNIA MUZIMA