Meneja Udhamini wa Vodacom Tanzania Rukia Mtingwa akionyesha nembo ya Mashindano ya baiskeli ya Vodacom Mwanza Cycle Challenge yanayotarajiwa kufanyika Mkoani Mwanza Mwezi ujao wanaoshuhdia katikati ni Mkuu wa Udhamini Vodacom Tanzania George Rwehumbiza na kulia ni Nazir Manji Mwenyekiti wa Chama cha Baiskeli CHABATA.
Mkuu wa Udhamini Vodacom Tanzania Bw. George Rwehumbiza akizungumza na waandishi wa habari kwenye ukumbi wa Idara ya Habari Maelezo leo wakati alipotangaza rasmi kufanyika kwa mashindano ya Baiskeli yanayojulikana kama Vodacom Mwanza Cycle Challenge yanayotarajiwa kufanyika tarehe 12 na 13 mwezi ujao mkoani Mwanza. Akielezea zaidi George Rwehumbiza amesema mashindano hayo yatakuwa katika mbio za kilomita 196 kwa wanaume, kilomita 80 kwa wanawake na mbio mbio hizo pia zitawahusisha walemavu ambapo zitafanyika mbio za kilomita 15 kwa walemavu wanaume na kilomita 10 kwa walemavi wanawake. Ameongeza kuwa zawadi zimeboreshwa zaidi kwa mwaka huu na zitatangazwa hapo baadae mara baada ya mambo yote kukamilika. Amefafanua kwa mba mashindano ya Vodacom Mwanza Cycle Challenge yanaandaliwa na kampuni ya simu za mkononi Vodacom Tanzania kwa miaka 5 sasa na kwa mwaka huu yanadhaminiwa pia na kampuni za Alphatel, TBL, Knight Support na SBC. Vodacom Tanzania imekuwa ikidhamini michezo mbalimbali kama vile Soka, Riadha, Kuogelea, Mashindano ya Boti, Mashindano ya Mbuzi, Vodacom Miss Tanzania, Tenisi michezo mingine mini, mwingine aliyepo kwenye picha ni Rukia Mtingwa Meneja Udhamini Vodacom Tanzania.
No comments:
Post a Comment