Uzinduzi wa ndege hiyo uliongozwa na Mwenyekiti wa IPP media Bw. Reginald Mengi kama mgeni rasmi na kuhudhuriwa pia na mabalozi, wadau wa biashara wa Precision Air pamoja na wafanyakazi wa shirika la ndege hilo.
Mkurugenzi Mkuu na Meneja
Mwendeshaji wa Precision Air, Bw. Alfonse Kioko alisema, “Mpango wetu wa kuongeza idadi za ndege ni mkakati madhubuti kabisa katika ukuaji wa kampuni na kutimiza huduma iliyo bora kwa wateja.”
Aliendelea: “Kutimia kwa ndege hizi mpya saba ni kuongezea nguvu ndege zetu tatu za zamani, kitu ambacho itatuwezesha kufanya kazi kwa ufanisi zaidi na kuweza kutimiza mahitaji ya wateja wetu kwa gharama nafuu zaidi. Hii ni kwa manufaa yetu sote, sisi na wateja wetu.”
Ndege hii mpya iliwasili tarehe 18 Septemba 2010 kutokea Toulouse-Ufaransa ambapo makao makuu ya ATR na kiwanda cha ndege kilipo. Ndege hizi aina ya ATR zimetengenezwa mahususi kabisa kwa namna ambayo madhara yake kwa mazingira na ya hali ya hewa ni mfinyu mno, kwa maana utoaji wake wa gesi aina ya kaboni ni mdogo. Hakika hii ni hatua na chaguo la kipekee kabisa kwa Precision Air kujali mazingira.
Ndege hiyo yenye usajili nambari 5H-PWG imepewa jina la Kilimanjaro, na imetengenezwa ikiwa na vifaa vya kisasa vya burudani kwa ajili ya wasafiri kuangalia sinema na kusikiliza muziki watakapokuwa wakisafiri. Ndege hiyo ina uwezo wa kubeba abiria 66 tu ili iweze kutoa pia nafasi zaidi kwaajili ya mizigo ya abiria.
“Ndege hii imepewa jina la Kilimanjaro kwa sababu tofauti; Mosi, ni kwa heshima ya mchango mkubwa wa kibiashara ambao Precision inapata kutoka kwa watu wa Kilimanjaro, pili, kila sehemu ambayo ndege hii itakwenda, itatangaza kivutio cha utalii wa mlima mrefu kuliko yote Afrika, na ya mwisho, kama tu jinsi jina lake lilivyo, lengo letu ni kuwa shirika la ndege liliyojuu kuliko yote barani Afrika,” alisema Bw. Kioko.
No comments:
Post a Comment