Sep 21, 2010

FM ACADEMIA KUTAMBULISHA VUTA NIKUVUTE MBAGALA KUU!!

BENDI ya muziki wa dansi ya FM Academia Wazee wa
Ngweasuma' Ijumaa Septemba 24 watafanya utambulisho
maalum wa albamu yao mpya ya Vutanikuvute kwenye Ukumbi
wa Nawina Resort Mbagala Kuu.
Mratibu wa Onesho hilo Zahor Said, alisema kuwa usiku huo
maalum wa Ngwasuma utakuwa na burudani mbalimbali ambazo
zitausindikiza utambulisho huo.
Said alisema watafanya utambulisho huo kwa kusindikizwa na
vikundi vya unenguaji vya kiduku.
Alisema utambulisho huo wa albamu ya Vuta nikuvute utakuwa
chini ya Rais waNyoshi El Saadat watapiga nyimbo zote 11
zilizopo kwenye Albamu hiyo ikiwa ni pamoja na nyimbo za
zamani.
Nyimbo zilizobeba albamu hiyo kuwa ni Heshima kwa
Wanawake ambayo ilipata tunzo mwaka jana,Mwili wangu,
Usiku wa juma tano na Jasmini.
Nyimbo zingine ni Angalia shida yangu,Mgeni,Heiken
Ngwasuma,Moses Katumbi,Fadhila kwa mama Intro Ngwasuma
Mathematics na vuta ni kuvute ambayo imebeba jina la albam.
Usiku huo umedhaminiwa na Henkein Bear, Kampuni ya Inoch,
Blog za JaneJohn5, Mamapipiro na Full Shangwe.
Mwisho

No comments:

THE DON HIMSELF

Karibuni sana kwenye blog hii ya kijamii iliyosheheni makila kitu kuanzia siasa uchumi afya na burudani kwa ujumla wake.uingiapo kwenye blog hii ni mengi ambayo utapata nafasi ya kukutana nayo,kumbuka mawazo yako ndo hasa yanayojenga na kunifanya niwe na ufanisi zaidi.kariiiiiiibuuuuuuuuuuuu saaaaaaaaaaaaaaanaaaaaaaaaa.(THE DJ HIMSELF-JIWE)

Followers

BLOG ZA MARAFIKI

Search This Blog

ZILIZOPITA

DUNIA MUZIMA