mkuu wa udhamini vodacom george rwehumbiza na katibu wa yanga mwalusako wakionyesha jezi ya yanga
nyange kaburu na mkuu wa udhamini vodacom george rwehumbiza wakionyesha jezi ya simba
Raurence Mwalusako katibu mkuu yanga akipokea vifaa vya michezo
Wadhamini wa ligi kuu Tanzania bara kampuni ya simu za mikononi ya VODACOM itatumia kiasi shilingi milioni 35 kwaajili ya mchezo wa ngao ya hisani baina ya SIMBA NA yanga utakaochezea kesho kutwa jumatano katika uwanja wa taifa.
Mkuu wa udhamini wa vodacom GEORGE RWEHUMBIZA amesema wamefanya hivyo kwaajili ya kutambua umuhimu wa mchezo huo na kukabidhi jezi zitakazotumiwa siku hiyo .
Wakipokea vifaa hivyo katibu mkuu wa YANGA Raurence Mwalusako na makamu mwenyekiti wa SIMBA GEOFREY NYANGE wakisema mchezo huo utaonyesha ishara njema kwao kwenye msimu huu
Mchezo huo wa ngao ya HISANI utachezwa majira ya saa kumi jioni tofauti na hapo awali ambapo kulikuwa na taarifa kuwa mchezo huo ungechezwa usiku.
No comments:
Post a Comment